NENO LA LEO

174 views
Skip to first unread message

eliezer.mwangosi

unread,
Nov 5, 2017, 10:34:49 PM11/5/17
to
NENO LA LEO: SIRI YA USHINDI

Zaburi 119:9-11

9 Jinsi gani kijana aisafishe njia yake? Kwa kutii, akilifuata neno lako.

10 Kwa moyo wangu wote nimekutafuta, Usiniache nipotee mbali na maagizo yako.

11 Moyoni mwangu nimeliweka neno lako, Nisije nikakutenda dhambi.

Kila kunapokucha swala la ushindi wa dhambi kwa vijana bila kuwasahau wazee linakuwa ni kitendawili. Wengi wanakiri kushindwa na kuishi maisha yasiyopatana imani zao.

Neno la leo linatuambia kuwa sababu kubwa ya kushindwa ni kutokuwa na muda wa kumtafuta Mungu kwa kusoma na kutafakari neno lake. Wengi wamekuwa mateka wa adui kwa kukosa muda wa faragha na Mungu.

Wengi wamekuwa mateka wa mambo ya kidunia, picha za ngono, matusi, tamthilia, mipila, mabishano ya siasa, mitindo ya mavazi, miziki ya ubongo wa fleva na sengeli michano, ndiyo yameteka akili za wengi.

Hebu fikiri muda mwingi watu wana chat, jiulize wana chat mambo gani? Utashangaa ni mambo yanayoujaza ubongo matope ya dunia hii na kuwatenga na Mungu.

Vijana wengi wanazidi Kuwa vipofu na kujeruhiwa na dhambi kwa sababu hawana muda na Mungu.

Inawezekana kuishi maisha ya usafi na ushindi, na tukadumu kuwa mikononi mwa Mungu, kwa kufanya maamuzi ya kuwa na muda wa kumtafuta Mungu kila siku.

NAWATAKIA WOTE SIKU NJEMA

Na  Ev. Eliezer Mwangosi.




Sent from Samsung tablet

eliezer.mwangosi

unread,
Nov 8, 2017, 5:30:04 PM11/8/17
to
NENO LA LEO - RUDI NYUMBANI 

👉 Luka 15:17-19  "Alipozingatia Moyoni mwake, alisema, Ni watumishi wangapi wa Baba yangu wanakula chakula na kusaza, na mimi hapa ninakufa kwa njaa. Nitaondoka, nitakwenda kwa Baba yangu...."

👉 Tafakari ya leo Imejengwa katika kisa cha Mwana mpotevu, aliyeamua kutoka kwa Baba yake, kwenye Maisha ya Kifalme, akaenda kula Starehe za Kidunia, lakini mwisho wake akaishia kuwa CHOKOLAA, na kuishia kulisha Nguruwe huku akiwa na njaa. Ndivyo wengi wanavyoingizwa katika WAVU na MTEGO wa Adui, wakifikiri wamepata kumbe wamepatikana. Hata kama unalala UNAPEPEWA na Mababy, na kupata kila hitaji la Moyo, kama uko nje ya Mapenzi ya Mungu Baba, kaa Chonjo, kuna Mishale ya ADUI yenye sumu inakujia. 

👉 Wapendwa marafiki zangu; Ulimwengu wetu unazidi kuzama katika Dhoruba kubwa na ya kutisha, japo ni Taratibu lakini kwa Uhakika, vilio, kuvunjika moyo, kukosa matumiani, udanganyifu, na hata asubuhi hii kuna watu wameamka na Misongo ya mawazo, wengine hawakulala usingizi.... Kila mmoja ana changamoto inayomsibu. Tunashuhudia wengi wakidai wanakula BATA, lakini ghafla upepo unageuka wanaishia Majuto.

👉 NENO linasema "Alipozingatia Moyoni mwake..... Alisema Nitaondoka, Nitakwenda Kwa BABA yangu...". Rafiki yangu, bila kujali uzito na ukubwa wa changamoto inayokusibu, angalia kwanza usalama wa mahali ulipo. Uko nyumbani mwa Baba au Nchi ya Mbali? Bila kujali dini au dhehebu lako, ni kweli umeunganishwa na Mungu? Mara nyingi watoto wa Mfalme, wanahujumiwa na kuishia kula makombo chini ya Laana ya Dhambi. Dini zimekuwa za mtindo na Usanii, watu hawazingatii na kutii neno la Mungu. Wanasoma kweli za Mungu na kuzipa kisogo, wanapenda kuombewa Baraka, Wakati hawataki kumtii mtoa Baraka - Hilo ndilo GIZA NENE LA KIROHO. 

👉 Wakati umefika wa Kuzingatia, Kutafakari na kuamua KURUDI NYUMBANI kwa Baba yetu, mwenye wezo wa kila tatizo. Kila Tendo, Neno na Wazo la Dhambi au Kinyume na neno la Mungu, ni Tanzi inayopaswa kukatwa leo. BABA anakusubiri akiwa amenyosha mikono iliyojaa Baraka na Neema kwa ajili yako. Sema; Uongo kwaheri, wizi kwaheri, wivu kwaheri, hasira kwaheri, uchawi kwaheri, mke au mume wa mtu na nyumba ndogo na Vidumu vyote kwaheri, Roho ya visasi na kutosamehe na Kila aina UOVU Sema  KWAHERI. 

AMANI YA MUNGU IKATAWALE MIOYO YA KILA MMOJA WETU. NAWATAKIA WOTE SIKU NJEMA. 

Na: Ev. Eliezer Mwangosi
Mawasiliano: 0767210299





Sent from Samsung tablet

eliezer.mwangosi

unread,
Nov 15, 2017, 4:57:44 PM11/15/17
to
NENO LA LEO: TOKA USIMAME MLIMANI MBELE ZA BWANA. 

1Wafalme 19:11 “Akasema, Toka, usimame mlimani mbele za BWANA .....” 

Hiyo ni sauti ya BWANA ikimwambia nabii Eliya aliyekuwa amelala kwenye pango, baada ya kutembea siku arobaini bila kula wala kunywa, akikimbia kwa hofu ya kuuwawa na mfalme Ahabu chini ya ushawishi wa mkewe Yezebeli. 

Akiwa amekaa katika pango hilo, alikuwa amekata tamaa ya kuishi, alikuwa amefunikwa na hofu na giza la vitisho vya mauti, akili yake ilifikia ukomo, kila milango ya matumaini ilikuwa imefungwa, hakuona nuru ya maisha mbele yake. 

Akiwa katikati ya giza nene la mawazo ndani ya pango, ndipo akasikia sauti ya BWANA ikisema "Toka usimame mlimani mbele za Bwana". Kilichofuata, Mungu alimpandisha Eliya kwa kila hali na kumtumia kama nabii wa Israeli, jambo ambalo awali lilionekana haliwezekani. 

Sauti kama hiyo inakuja kwa kila mmoja aliye katika giza la fulani la maisha, iwe ni mawazo, huzuni, kukata tamaa, hofu, kuvunjika moyo na kukosa matumaini. Kizazi hiki kuna wengi wanaishi maisha ya hofu huku nuru ya ushindi ikiwa imetoweka, wako katika pango la mapito wamejikunyata. 

Mara zote shetani anafanya kila njia kuhakikisha tunaingia kwenye mikono yake kwa dhambi, na hatimaye kuturushia mishale, inayotuteremsha hadi chini ya viwango vya kila hali, kiroho na kimwili. Watoto wa Mungu wengi wamehujumiwa, wamebaki wanalia katika mapango ya mateso. 

Neno la leo linasema; Toka katika giza la pango hilo la majaribu unayopitia, simama MLIMANI MBELE ZA BWANA, utauona mkono wa BWANA ukikuokoa na kukuweka juu ya vilele vya maisha. Sikia sauti na kuamua kusimama mlimani kwa IMANI, nawe utashinda. 

NAWATAKIA SIKU NJEMA YENYE USHINDI NA MAFANIKIO KWA KILA JAMBO.

××× WAPELEKEE WENGINE UJUMBE HUU -UTABARIKIWA ×××

Na. Ev. Eliezer Mwangosi
Simu: 0767 210 299




Sent from Samsung tablet

eliezer.mwangosi

unread,
Nov 19, 2017, 9:58:46 PM11/19/17
to

MAHUSIANO - KIJANA NA MAISHA

*** Wazee na washauri wa Vijana pia wausome ujumbe huu na kuwapelekea ***

MADA: KWA NINI VIJINA WENGI WANAANGUKIA PUA KATIKA KUOA?

Mithali 14:12 Iko njia ionekanayo kuwa sawa machoni pa mtu, Lakini mwisho wake ni njia za mauti.

Mada hii imejikitita kuwashauri vijana wa KIUME ili kujiepusha na majanga ambayo wengi wanayapatia wanapoingia katika NDOA.

Kizazi chetu kinazidi kukumbwa na janga la kuvunjika kwa ndoa changa, kama sio ndoa kuvunjika, basi ni mioyo kujaa maneno ya "LAITI NINGEJUA NISINGEOA". Na wengine hawataki kusikia habari za KUOA, japo wanaishia kuwa na NDOA za masaa.

Zifuatazo ni baadhi tu ya sababu zinazojeruhi mahusiano ya vijana, hasa katika mchakato wa UCHUMBA na hatimaye NDOA.

1. Kujenga nyumba ya mahusiano katika Michanga au Matope.

Hii inajumuisha, mahusiano yoyote yanayoanzishwa bila kumhusisha Mungu, yanaanzishwa kwa tamaa za macho, na kuwa chini ya adui, roho ya ulimwengu huu. Ni wepesi wa Kusikia neno la Mungu, kulitamka kwa nyimbo na maombi, lakini mioyo yao kwa hila imetekwa.

Neno la Mungu linasema "...Mke mwenye Busara, mtu hupewa na BWANA" Mithali 19:14, "Bwana asipoijenga nyumba, waijengao wafanya kazi bure ..." Zaburi 127:1. Kijana!  Utawezaji kuzuia mafuriko na dhoruba zisibomoe nyumba yako uliyoijenga kwenye tope au mchanga? Huko ni sawa na kujilisha UPEPO.

2. Hawana elimu ya kutosha juu ya kujitambua katika eneo hili ya mahusiani ya Uchumba na ndoa.

Kutangaza kuwa amepata mchumba siku ya kwanza alipomwambia binti NAKUPENDA na kumjibu NAMI NAKUPENDA utafikiri ulijua! Kabla hata ya kufahamiana kwa undani. Hawajui tofauti kati ya urafiki na uchumba. Hivyo utakuta Kijana ana Wachumba zaidi ya mmoja au wengi, wote akiwa amewalengeshea.

Nilishafundisha kwa undani juu ya jambo hili, unaweza kuwa na marafiki wengi, ambao mwisho unapata mchumba mmoja ... huyo ndiye unamtamkia kuwa unata awe Mchumba wako. Hatua ya uchumba sio ya kuchunguzana.

Urafiki ni uwanja wa wazi kwa ajili ya kufahamiana kwa undani bila mkataba wowote wa kuoana. Vijana wengi wanatumia Kick ya uchumba ili ampate binti, hilo ni KOSA kubwa, anzisha mazoea ya kawaida na urafiki wa kawaida kwa ajili ya kupata ufahamu wa ndani juu ya maisha yao.

3. Tatizo lingine kubwa zaidi ni kuchanganya mambo haya mawili. Kukidhi tamaa za mwili na kutafuta mchumba mwaminifu. Anatamani Mungu ampatie MKE MWEMA, wakati huohuo amejisalimisha na amekuwa mtumwa wa roho za NGONO.

Watu hao ni rahisi kumuomba Ngono binti ambaye alishamuomba urafiki, akisisitiza kuwa, Ngono ndiyo ishara ya binti kuonyesha ukubali, HII NDIYO KONA AMBAYO WENGI WAMEJERUHIWA NA ADUI.

Sikilizeni; tendo lolote la zinaa au uashertani, ngono nje ya Ndoa HALALI, ni mshale urukao mchana na Kujeruhi. Pasipo Mungu pana upendo bandia, wa kukidhi tamaa ya mwili, kama ilivyokuwa kwa Amnoni na Tamari.

Mara nyingi mabinti waaminifu, wanaokataa kutoa ngono kwa vijana marafiki au wachumba wao, wanaachwa eti kwa sababu wanaonekana kutowajali, hivyo vijana wanaruka kama ndege kwenda kutua matawi mengine yoyote na kujenga viota.

VIJANA WANGU, Huko ni kuchanganyikiwa, hayo ni mapepo na roho za mashetani, mwisho wake ni mauti, badala ya kufurahi kumpata Binti mweye hofu ya Mungu, anayefaa kwa ajiri ya Ndoa, wewe unatafuta maloli ya jeshi, ambayo muda wote yamebeba mizigo.

4. Mambo mengine ni pesa ... vijana wengi siku hizi wanatafuta wanawake wenye PESA, huo ni ujinga, nani amekwambia pesa zinajenga NDOA? Hata hivyo wewe Mwanaume, ndiye Kichwa cha nyumba, mwanamke ni msaidizi, inakuwaje mnapoteza mwelekeo na kutafuta kuwa tegemezi?

Ukimpenda mwanamke kwa pesa yake uwe tayari kumpenda anayemuwezesha, kuna wengine wanaona binti anapendeza ana pesa bila kujua pesa anazitoa wapi. Usipende MALI itakujeruhi, wewe ni mwanaume omba Mungu atakusaidia, kubali muanze maisha na hali yoyote, Mungu amesema, ataibariki nyumba ya wenye haki.

Baadhi ya matokeo ya tabia hizo za vijana kutojitambua ni hizi:

1. Wengi wameangukia PUA kuoa wasiowatarajia, kwa kutanguliza ngono, wengi wanalazimika kuoa mabinti wajanja wanaotegeshea mimba, wanaona aibu kumtelekeza binti na mtoto.

2. Mabinti wengi wanawanasa vijana WAPIMA OIL, kwa madawa ya Kishirikina, utashangaa kijana hajielewi, anamwacha binti mcha Mungu, Bikra safi, anaenda kujiegesha katika tundu bovu.

Ndoa yoyote ikianzishwa na mivuto ya kishirikiana au mivuto yoyote ya kidunia, hilo ni tundu bovu, ibirisi ndiye mshika usukani wa mahusiano yenu. Ushirikina na Maluweluwe ya mizimu, ni nyumbani pake.

3. Vilio vya mabinti mnaowaharibu kwa hila, na baadaye kuwapiga VIBUTI, huku mkiwa mmewapotezea muda, na kuwatia hasara, Mungu anavisikia vilio vyao na masononeko yao, Mungu anawalipia visasi, majuto yao yanageuka baadaye kuwa yenu.

Mnacho watendea mabinti leo, ndicho kitakachowatokea maisheni mwenu katika ndoa. Wengi wanajiuliza na kutafuta nani analoga ndoa zao, ni vurugu tu utafikiri kuna PEPO, kumbe ni laana za vilio vya mabinti waliowatelekeza zinawafuata.

USHAURI:
Wote walio na marafiki ambao mumewatangazia au mumeonyesha kuwaoa, wakati hamjafanya maamuzi juu yao, waambieni UKWELI kuwa hamjafanya maamuzi hayo ili wasiweke tumaini, na lisijekuwa tanzi yenu baadaye.

Ombeni rehema za Mungu, mkitubu kwa yaliyopita na kusahihisha yanayoendelea. Yeye ni mwaminifu atawashindia.

MWISHO:
Iweni wakweli, Iweni waaminifu, Mtegemeeni Mungu naye atawajazi haja zenu juu ya kupata wenzi BORA wa Maisha sio BORA wenzi.

NAWATAKIA VIJANA WOTE MAFANIKIO NA BARAKA TELE

Nawakaribisha kwa maswali na ushauri ... kwa inbox.

Na. Ev. Eliezer Mwangosi
Simu: +255 0767 210 299.

UKIPATA UJUMBE HUU, MPELEKEE PIA MWENZAKO.



Sent from Samsung tablet

bmashimba

unread,
Nov 23, 2017, 1:35:43 AM11/23/17
to 'eliezer.mwangosi' via YourTrueVine

Amina .Ubarikiwe mtumishi wa Bwana

--
Mimi ni mzabibu ninyi ni matawi, akaaye ndani yangu nami ndani yake, huyo huzaa sana; maana pasipo mimi ninyi hamwezi kufanya neno lolote.Yohana 15:5
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "YourTrueVine" group.
To post to this group, send email to yourtr...@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

eliezer.mwangosi

unread,
Nov 26, 2017, 10:48:10 PM11/26/17
to
NENO LA LEO - USALAMA WAKO NI WA UHAKIKA USIHOFU

Zaburi 91:10-11 "Mabaya hayatakupata wewe,Wala tauni haitaikaribia hema yako. Kwa kuwa atakuagizia malaika zake wakulinde katika njia zako zote."

Ni jambo la kawaida watu kujawa na hofu, hasa pale inapotokea hali ya kutishia amani na usalama wa maisha. Tunashuhudia uadui unapotokea katika jamii, mambo ya kutishiana maisha yanatokea.

Iwe maofisini, kwenye biashara, majumbani na sehemu mbalimabli n.k. yanapotokea mafarakano, chuki, visasi na uhasama, watu wenye uwezo wanatishia maisha ya wengine. Mtindo wa kuendeana kwa waganga unazidi kushamiri na kuleta hofu kwa wengi.

Shetani ndiye chanzo cha kila mafarakano na hatimaye maafa kutokea katika jamii, nguvu za kichawi na umizimu zinazidi kujiinua na kuleta hofu kwa wengi. Wanganga wanaojifanya wanaweza kuzuia nguvu za Kichawi wanazidi kupata umaarufu katika kizazi chetu, wakitoa huduma za Mazindiko katika nyumba, biashara, kazi, mifugo, mashamba, ndoa n.k.

Jambo la kushangaza utakuta hadi watu wa dini wamebuni hirizi za kiroho, utakuta ana mafuta ya upako kwenye chupa ameweka kwenye kitanda, wengine maji wanamwaga kuzunguka nyumba, wengine wanalalia biblia kwenye pilo, n.k. kwa ajili ya kuzuia roho chafu au uchawi, hizo zote ni HIRIZI za Miungu, ni ubatili mtupu.

Neno leo lina ujumbe wa kumhakikishia kila mtoto wa Mungu kuwa ana ULINZI wa malaika, ambaye yupo kwa ajili ya Usalama. Hakuna uchawi wa aina yoyote unaoweza kumdhuru mtoto wa Mungu. Usiwe na HOFU ya aina yoyote, wewe mtoto wa Mfalme, una ulinzi kutoka Juu masaa 24.

Uwe na amani katika mikono salama ya Mungu, jambo la kuzingatia, ni kubaki tukiwa tumeunganishwa na Mungu, nguvu ya dhambi isipate nafasi kabisa ili kututenga na mkono wa Bwana.

NAWATAKIA SIKU NJEMA YENYE AMANI TULIVU KATIKA MKONO YA BWANA.

Na. Ev. Eliezer Mwangosi




Sent from Samsung tablet

eliezer.mwangosi

unread,
Nov 27, 2017, 11:32:23 PM11/27/17
to
NENO LA LEO - HAKUNA SABABU YA KUWA NA HATIA MOYONI.

1 Yohana 1:9 "Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote."

Kuna watu wengi wanaishi na mawazo yenye kujaa hatia, wakikumbuka dhambi walizozipitia siku za nyuma, mbali na kwamba walishaungama na kutubu, bado kuna wakati wanajisikia hatia mioyoni. Ndio maana utakuta wengine wanarudia kutubu na kutubu dhambi walizokwisha zitubu tayari.

Katika pambano kuu linaloendelea kati ya wema na uovu, adui anafanya kila njia kuzihafifisha roho zilizookolewa, na kuzitia mashaka kwa kuwaonyesha dhambi zao zilizopelekwa msalabani, kuwa bado hazijasamehewa. Mioyo yenye hatia, inaongozwa kirahisi kutoamini uweza wa Mungu na Upendo wake kwa wenye dhambi, na kuhafifisha mpango wa ukombozi kupitia kafara ya Yesu Kristo.

Neno la leo, linatoa msukumo katika utashi wa mwanadamu, kuamini ahadi za Mungu juu ya Msamaha wa dhambi kwa anayetubu na kumpatia ushindi tele. Huu ni wakati wa watoto wa Mungu kusimama kwa ujasiri wakiwa huru kabisa, huku wakizitangaza fadhili za Bwana kwa ushindi mkuu.

Hakuna dhambi kubwa zaidi ya neema ya Mungu, yeye Mungu ni mwaminifu na wa haki, ameahidi kuziondoa dhambi zote na kusafisha kabisa. Hebu pasiwepo na mtu yeyote anayebaki katika hatia ya dhambi fulani, huu ni wakati wa kuburudishwa, tukiwa katika mikono yake salama.

WITO:
Pasiwe na mtoto wa Mungu anayebaki na mashaka yoyote, akidumu katika dhambi, WOKOVU NI WA HAKIKA.

NAWATAKIA SIKU NJEMA YENYE KUJAA NEEMA NA BARAKA ZA BWANA.

Na. Ev. Eliezer Mwangosi
Simu: 0767 210 299.



Sent from Samsung tablet

eliezer.mwangosi

unread,
Nov 28, 2017, 10:44:16 PM11/28/17
to
NENO LA LEO - KATIKA UKINGO WA MTO YORDANI

Yoshua 3:5 "Joshua akawaambia watu, JITAKASENI; maana kesho BWANA atatenda mambo ya ajabu kati yenu".

👉Katika safari ya waisraeli kwenda Katika nchi ya ahadi, walikutana na vikwazo vingi njiani, hata hivyo mara zote tuliona mkono wa Mungu ukiwapatia ushindi. Leo tunaona muujiza wa kuusimamisha mto Yordani uliokuwa umefurika, na Israeli wakavuka nchi kavu, maji ya mto yakiwa yamesimamishwa upande yalikotoka. Soma Yoshua 3:14-17. 

👉Kama ilivyokuwa kwa taifa la Mungu ndivyo tunavyokutana na vikwazo katika safari ya maisha haya, bila kujali Imani zetu, wengi wamesimama katika kingo za mito ya CHANGAMOTO na MAPITO ya maisha, iliyojaa MAFURIKO, hawaoni jinsi ya KUVUKA.

👉 Hata hivyo, bila kujali ni mto wa aina gani unafurika mbele yako, bila kujali umeketi hapo kwenye ukingo kwa muda gani, bila kujali ukubwa wa mafuriko yanayopita mbele yako, huenda umeona haiwezekani kuivuka changamoto unayoipitia, leo linasema "BWANA atatenda jambo la ajabu mbele yako". Mbele yako, ng'ambo ya mto, umeandaliwa mambo makuu, Mtazame na kumsikiliza Bwana, UTAVUKA SALAMA.

👉Kabla Mungu hajatenda muujiza, aliwaambia watu wake WAJITAKASE, baada ya kujitakasa ndipo wakauona mkono wa Mungu ukifanya njia pasipo njia. Utakaso ni tendo la kuamua kuacha dhambi kwa toba na maungamo, ni uamuzi wa dhati wa kuachana na kila tunayoifahamu kuwa ni dhambi.

👉Mungu yuko tayari kutuvusha katika kila changamoto tunazopitia, ili mradi tuamue kusimama upade wake. Utakaso wa kweli unapatikana kwa njia ya kutafakari NENO la Mungu ( Yohana 17:17), ambalo linaonyesha kasoro au dhambi, na hatua ya pili ni kutoa maisha kwa Kristo, ambaye anatusamehe dhambi, anatusafisha na kutupatia haki ya kuitwa watoto wa Mungu na Mwisho kutupatia maisha yenye Ushindi dhidi ya Dhambi.

👉Leo sauti ya Mungu inasikika tena ikisema, JITAKASENI, kwa maana Bwana anaenda kutuvusha katika kila aina ya mito iliyofurika mbele zetu. Iwe ni mito ya Umaskini, Magonjwa, Kuonewa, Kusalitiwa, Kudhulumiwa, Mikosi na laana, Upweke n.k. Ukiamua kukaa mikononi mwa Bwana hakika utavuka salaama. 

WEMA WA MUNGU UWAZUNGUKE NA MUWE NA BARAKA ZA BWANA DAIMA

Na: Ev. Eliezer Mwangosi - 0767210299 - Email: eliezer....@yahoo.com.




Sent from Samsung tablet

MaryGlady Heri

unread,
Nov 29, 2017, 1:16:22 AM11/29/17
to yourtr...@googlegroups.com
Hakika kweli Bwana atafanya njia pasipo njia kwa wale waliojitakasa! labda swali moja tu mtumishi, katika hayo mapito unakuta mtu anaomba,anajitakasa lakini kadiri siku ziendavyo mbele mapigo ndio yanakuja moja baada ya jingine na yanazidi uzito, unaendelea kupambana lakini still more troubles and tribulations comes in front of you and became confused.





But he who practices the truth comes to the light, that his deeds may be manifested as having been wrought in God.” John 3:21






--

Happines Francis

unread,
Nov 29, 2017, 4:13:41 PM11/29/17
to yourtr...@googlegroups.com
Barkiwa mtumishi somo zuri sana kwa vijana

--

Bahati Mashimba

unread,
Nov 29, 2017, 5:14:39 PM11/29/17
to yourtr...@googlegroups.com
Mpendwa MaryGlady; kwa uelewa wangu Mungu hurusu majaribu kwa watu wake ili

kupima imani Mfano mzuri Ayubu ambaye alimcha Mungu na kuepukana na uovu na

alikuwa akijitakasa mara kwa mara kwa ajili ya watoto wake...Lakini
tunasoma Ayubu

alipata mapigo mengi moja baada ya jingine kwa '' kuibiwa ng'ombe
na Waseba,

kuangamizwa kwa watumishi wake, moto kuteketeza kondoo wake, ngamia

kuchukuliwa kwa nguvu na Walkadayo , pia Wanae na binti zake walikufa kwa

kuangukiwa na nyumba na bado haitoshi Ayubu alipata pigo kali la
kuugua majipu

mabaya mwili wote tangu wayo wa mguu hata utosi wa kichwa.Biblia
inaeleza katika

mapigo yote hayo Ayubu hakufanya dhambi kwa midomo yake.Pamoja na mipigo yote

hayo Ayubu hayakumfanya amuache Mungu na kutenda dhambi na Mungu alifanya

mlango wa kutokea katika majaribu hayo na mwisho wa Ayubu wa
kustahimili majaribu

ulikuwa ni baraka zaidi ya ule mwanzo wake.

Katika waraka wa Yakobo ameelezea tunapostahimili majaribu ya kila
namna hutufanya kuwa wakamilifu ''Yakobo 1:2-4 Ndugu zangu hesabuni
ya kuwa ni furaha tupu mkiangukia katka majaribu mbalimbali ,
mkifahamu ya kuwa kujaribiwa kwa imani yenu huleta saburi.Saburi na
iwe na kazi kamilifu na watmilifu bila kupungukiwa na neno''




On 11/29/17, MaryGlady Heri <mgl...@gmail.com> wrote:
> Hakika kweli Bwana atafanya njia pasipo njia kwa wale waliojitakasa! labda
> swali moja tu mtumishi, katika hayo mapito unakuta mtu anaomba,anajitakasa
> lakini kadiri siku ziendavyo mbele mapigo ndio yanakuja moja baada ya
> jingine na yanazidi uzito, unaendelea kupambana lakini still more troubles
> and tribulations comes in front of you and became confused.
>
>
>
>
>
> *But he who practices the truth comes to the light, that his deeds may be
> manifested as having been wrought in God.” John 3:21*
> To post to this group, send an email to yourtr...@googlegroups.com.

Mtoka James

unread,
Nov 30, 2017, 12:56:19 AM11/30/17
to yourtruevine

Amina  watumishi wa  mungu  mubarikiwe sana

eliezer.mwangosi

unread,
Dec 4, 2017, 10:27:09 PM12/4/17
to
NENO LA LEO: DHAMBI ILIYOWANASA WENGI

Luka 12:1 Wakati huo, makutano walipokutanika elfu elfu, hata wakakanyagana, alianza kuwaambia wanafunzi wake kwanza, Jilindeni na chachu ya Mafarisayo, ambayo ni unafiki.

Mafarisayo walionekana kwa nje kuwa ni wacha Mungu lakini ndani ya mioyo yao kulijaa chuki, fitina, wivu, husuda, Majungu, na tabia chafu, na mwisho wakahusika kupanga njama za kumuua Yesu.

Kama kuna tabia inayotumika na Ibilisi kuleta madhara kati ya ndugu, ni unafiki. Unafiki ni tabia ya mtu kujionyesha kwa nje kuwa ni mtu mwema, kumbe moyo wake umejaa, chuki, wivu, husuda. Watu hawa ni hatari, ni miiba, na mishale inayochoma kwa siri.

Ndio maana Yesu akasema; Mathayo 23:28 Vivyo hivyo ninyi nanyi, kwa nje mwaonekana na watu kuwa wenye haki, bali ndani mmejaa unafiki na maasi.

Tunashuhudia ndoa, uchumba, urafiki, mahusiano, vikivunjika kwa sababu ya watu hawa WANAFIKI, wanaojifanya marafiki wa karibu, huku wakiwa na nia ya kuharibu. Ndio maana waswahili wakaishia kusema KIKULACHO KINGUONI MWAKO.

Dhambi hii ya unafiki inazidi kufunika kila mahali, iwe majumbani, maofisini na hata makanisani na masikitini, tabia hii imejaa kila kona, watu wanachekeana, na maneno mengi ya kuonyesha kupendana na tabasamu bandia, lakini ndani wamejaa hila.

Hebu kila mmoja wetu atafakari na kuzingatia maneno yafuatayo ili asije akaendelea kutumika na adui bila kujua na mwisho kuukosa uzima wa milele.

Warumi  12:9 Pendo na lisiwe na unafiki lichukieni lililo ovu, mkiambatana na lililo jema.

1 petro 2:1 Basi, wekeni mbali uovu wote na hila yote, na unafiki na husuda na masingizio yote.

Kumbuka; Wanadamu wanaangalia sura na maneno, bali Mungu huona zaidi hadi kuusoma moyo, na ndiye anayetoa maonyo haya, na ndiye awezaye kutupatia ushindi juu ya  tabia hii.

NAWATAKIA SIKU NJEMA YENYE BARAKA TELE

Na. Ev. Eliezer Mwangosi



Sent from Samsung tablet

Bahati Mashimba

unread,
Dec 5, 2017, 6:32:36 AM12/5/17
to yourtruevine, Mtoka James
Thanks James

Happines Francis

unread,
Dec 17, 2017, 8:53:36 AM12/17/17
to yourtr...@googlegroups.com
Asante sana kwa somo nzur,kanisa la Mungu linateswa sana na unafiki .barikiwa sana mtumishi

--
Reply all
Reply to author
Forward
0 new messages