Fw: Fwd: [Injili] Somo: Mambo 7 unayohitaji kuyajua juu ya mpango wa Mungu alionao kwa ajili ya maisha yako

2,756 views
Skip to first unread message

Deborah Mgedzi

unread,
Mar 16, 2012, 7:48:15 AM3/16/12
to Bahati Mashimba, Rev. George Fupe, Rev. George Fihavango, csend...@yahoo.com, ecac...@yahoo.com, semz...@yahoo.co.uk, lugano ross, Fred Kiangio, cathy sanga, eligreta mnzava, Elikira Ndossi, Kumbwaeli Salewi, Mathias kavugha, happiness nkya, Nkundwe Mwakyusa, neema Kibona, Nana Temu, Violet Minja, anna nswilla, Eva Muro

----- Forwarded Message -----
From: Grace Jengo <grace...@yahoo.co.uk>
To: Deborah Mgedzi <debora...@yahoo.com>; Oscar Kaitaba <ocka...@yahoo.com>; Edward Kirumbi <ekir...@yahoo.com>; Dr. Edith Ngirwamungu <ed...@trachoma.or.tz>; Bernard Kilembe <bcki...@trachoma.or.tz>; Peter Kilima <kil...@trachoma.or.tz>; Eva Muro <mu...@tz.afro.who.int>; Karoli Malley <kdma...@sightsavers.or.tz>; Pius Blubo <pbmt...@yahoo.com>; elisifa kinasha <eli...@hotmail.com>; Nicholas Kinabo <niki...@mail.com>; Milka Mafwiri <mmaf...@yahoo.com>; anna sanyiwa <annas...@yahoo.com>; adeline saguti <adelin...@yahoo.com>; maria saguti <maria...@yahoo.com>; Mariam Ally <mariam...@yahoo.com>; Immanuel Jengo <im...@chamberofmines.org>; Emmanuel Furahini <efur...@hotmail.com>; Rachel Bertha Ramadhani <rachelr...@yahoo.com>; Nkundwe Mwakyusa <tuk...@yahoo.com>; Agnes Kisanga <nka...@hotmail.com>; Kisa Kapichi <kkap...@sightsavers.or.tz>; meje...@yahoo.com; Christina Jengo <chris...@yahoo.com>; joanne simon <lc_ba...@hotmail.com>; Elias Jengo <elia...@yahoo.com>; Rose Jengo <rose...@yahoo.com>; ZAWADI MWITULA <zemw...@hq.bot-tz.org>; Zawadi Richard <zappi...@yahoo.co.uk>; mama Mwinge <smw...@yahoo.com>; Upendo Mwingira <umwi...@yahoo.com>
Sent: Thursday, June 1, 2006 7:11 PM
Subject: Fwd: [Injili] Somo: Mambo 7 unayohitaji kuyajua juu ya mpango wa Mungu alionao kwa ajili ya maisha yako

----- Forwarded Message -----

Ndugu zangu ya leo nikukumbushana tu! Mungu atusaidie hekima yake katika kusoma somo hili.

Note: forwarded message attached.

Dr Grace E.B.Saguti MMed Oph.
Coordinator
National Eye Care/Onchocerciasis Control Program
Ministry of Health
P.O.Box 9083
Dar Es Salaam.
Tel 0255222130009, mob 0744287875.
Fax 0255222130009
MAMBO 7 UNAYOHITAJI KUYAJUA JUU YA MPANGO WA MUNGU ALIONAO
KWA AJILI YA MAISHA YAKO
Utangulizi:
“Mwaka 1986 nilipata msukumo ndani yangu mkubwa sana wa kutaka kumtumikia Mungu. Wakati huo nilikuwa nafikiri ukitaka kumtumikia Mungu ni lazima uwe mchungaji. Kwa hiyo nikaamua kutafuta chuo cha Biblia ili nipate kusomea uchungaji. Nikapata chuo cha Biblia cha kusomea uchungaji, na nikapata pia mtu aliyekuwa tayari kunisomesha mpaka niweze kuhitimu. Lakini siku moja mchana Roho Mtakatifu alisema nami wazi wazi moyoni mwangu ya kuwa sijaitwa kuwa mchungaji kwa hiyo nisiende kusomea uchungaji.
Ikabidi niwaombe radhi wale waliokuwa tayari kunisaidia kusomea uchungaji ya kuwa nilikuwa hapo mwanzoni sijasikia sauti ya Mungu vizuri. Na kwamba sitaweza kwenda tena kusomea uchungaji, maana Roho Mtakatifu ameniambia sijaitwa kufanya huduma hiyo.
Karibu kipindi hicho hicho nilipata kitabu cha mhubiri mmoja wa Marekani ambaye alieleza juu ya wito wake ulivyo, na kile ambacho Yesu alisema naye. Anasema alifanya kazi ya uchungaji miaka 12 lakini hakuwa na amani ndani yake, ingawa kazi ya Mungu ilikuwa inaendelea vizuri, watu walikuwa wanaokoka, wanapona magonjwa yao, na pia kujazwa Roho Mtakatifu.
Pamoja na mafanikio hayo bado ndani yake hakuwa na amani. Anasema moyoni mwake alikuwa anajisika kama vile mtu ajisikiavyo anaponawa miguu yake huku amevaa soksi! Kuona hivyo akaamua kuacha kufanya kazi ya kichungaji; na akaanza kufundisha semina mbalimbali za neno la Mungu. Ndani ya moyo wake akapata amani ambayo alikuwa hajawahi kuipata katika muda wote ule wa miaka 12 aliyohudumu kama mchungaji. Pia, wakati huo Yesu akamtokea katika maono na akamwambia ya kuwa alipoanza kufundisha ndipo alipoanza awamu ya kwanza ya huduma aliyoitiwa! Na kwamba miaka 12 ya uchungaji haikuhesabiwa, kwa sababu huo haukuwa wito wake! Yule mhubiri alishangaa sana na akamuuliza Yesu ni kwa nini basi alikuwa anambariki katika huo uchungaji? Yesu akamwambia alikuwa hambariki yeye kama mhubiri, bali alikuwa anabariki neno la Mungu alilokuwa analihubiri!
          Nilipotafakari ushuhuda huu wa mhubiri wa Marekani; na pia nilipokumbuka nilivyozuiwa kwenda kusomea uchungaji; nilijikuta nimeingia katika maombi mazito na ya muda mrefu nikitaka nijue wito wangu toka kwa Mungu.
          Nikiwa naendelea na maombi hayo nikaongozwa kusoma mstari huu wa Yeremia 29:11 unaosema “ Maana nayajua mawazo ninayowawazia ninyi, asema Bwana, ni mawazo ya amani, wala si ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za mwisho?” Niliposoma mstari huu kwenye tafsiri mojawapo ya kiingereza niliona ikisema “ Maana najua mipango niliyowapangia ninyi, asema Bwana, ni mipango ya kuwapa mafanikio, wala si ya kuwafanya msifanikiwe, ili niwape maisha mazuri ya baadaye…..”
          Ndani ya mstari huu, Mungu alituongoza mimi na mke wangu kujua wito tulioitiwa na kuanza kutembea katika mpango aliotupangia katika maisha yetu pamoja.
          Katika barua hii fupi tunataka tukushirikishe mambo 7 muhimu ambayo unapaswa kuyajua juu ya mpango wa Mungu alionao kwa ajili ya maisha yako. Kutokana na mambo haya saba yanazaliwa mambo mengi yaliyo muhimu sana kwa kila mtu kuyajua kufuatana na mpango ambao amepangiwa. Sisi tunayaweka mambo haya kwa muhtasari tu, lakini tunaamini Roho Mtakatifu atakufunulia na kukufundisha mengi zaidi.
Jambo la Kwanza:
          Lijue kwanza kusudi la Mungu juu ya maisha yako, kabla ya kuujua mpango wa Mungu juu yako! Kwa sababu mpango upo tu kwa ajili ya kutekeleza hatua na njia ya kuhakikisha ya kuwa kilichokusudiwa kimefikiwa. Bila kulijua kusudi, mpango wa utekelezaji  unakosa msukumo na unakosa mwelekeo! Bila kulijua kusudi la Mungu kukuweka duniani wakati huu, mpango wo wote unaotekeleza ili kufanikisha maisha yako, unakosa msukumo na unakosa mwelekeo. Matokeo yake ni mipango yako kutofanikiwa, na ikifanikiwa mafanikio hayo yanakuwa ni ya muda mfupi tu.
          Imeandikwa katika Mithali 19:21 “Mna hila nyingi (au mipango mingi) moyoni mwa mtu; lakini shauri (au kusudi) la Bwana ndilo litakalosimama (au ndilo litakalofanikiwa)”. Pia, ukisoma katika kitabu cha Isaya 46:10 Mungu anasema; “ Nitangazaye mwisho tangu mwanzo, na tangu zamani za kale mambo yasiyotendeka bado; nikisema, Shauri (au kusudi) langu litasimama (au litafanikiwa), nami nitatenda mapenzi yangu yote”.
          Kwa kutafakari mistari hii utajua ya kuwa: kusudi la Mungu halibadiliki na limewekwa ili kufanikiwa na kumfanikisha kila mtu anayelitekeleza. Mipango ya kutekeleza kusudi inaweza kubadilika, lakini kusudi lenyewe la Mungu huwezi kulibadilisha.
          Kwa mfano, kusudi la Mungu mojawapo lilikuwa ni kuwa na wanadamu wenye sura yake. Mpango wa kuwapata ilikuwa ni kwa njia ya ndoa. Lakini dhambi ilipoingia, Mungu akabadilisha mpango, na kuamua kutumia njia ya kuhubiri neno ili watu wazaliwe mara ya pili, ili kusudi lake la kuwa na wanadamu wenye sura yake lipate kutimia!
          Mfano mwingine, ni wa kusudi la Mungu la kuwafikisha nchi ya Kaanani, wana wa Israeli baada ya kuwatoa Misri. Mpango wa Mungu ilikuwa ni kumtumia nabii Musa lakini Musa hakuweza na badala yake Mungu akamwinua Yoshua ili kumalizia utekelezaji wa mpango huu!
          Fahamu hili; wewe ni sehemu ya mpango wa Mungu katika kutekeleza kusudi lake alilonalo. Ukivuruga maisha yako, na usipotaka kutubu; na hata kama ukitubu lakini usifuate mpango wa Mungu, kuna uwezekano mkubwa wa Mungu kuinua mtu mwingine ili atekeleze hilo Mungu analotaka! Kwa Kiingereza chepesi tunaweza kusema: A plan of God is a set of coordinated steps which are implementable within a specified time in  order to accomplish an identified purpose of God. Na neno hili Purpose of God lina maana ya: God’s motivation behind a vision you pursue; A reason God has in creating a thing or a person, An end result God expects out of a particular plan; A destination God wants you to reach on your journey He has led you to take.
          Kiswahili chepesi cha neno kusudi kinachotumika na wengi ni Neno ‘Lengo.’ Kusudi au lengo la watu wengi linalowafanya wafanye biashara ni ili kupata utajiri. Lakini kibiblia utajiri siyo mwisho wa safari bali ni sehemu ya mpango wa Mungu wa kuimarisha utekelezaji wa agano lake duniani. Hii ni kufuatana na mstari wa Kumbukumbu ya Torati 1:18.
Jambo la Pili:
          Mpango wa Mungu juu yako si wa kuutafuta; upo tayari maana uliandaliwa kabla hujazaliwa! Ile tu kwamba umezaliwa na unaishi, ina maana kuna mpango ambao Mungu ameuandaa unaohitaji mtu kama wewe kuutekeleza – kiumbo, kimwili, kiakili na kiroho! Wazo hili tumelipata kutokana na kusoma mistari hii ya Waefeso 1: 3- 5, na Waefeso 2:10.
          Kwa hiyo ni muhimu sana ujizoeze kumwomba Mungu akuwezeshe kujua jinsi anavyosema na watu wake; lakini pia akupe hekima na ufunuo wa kutafsiri na kuelewa anachokuambia. Pia usisahau kuomba Neema ya kukitekeleza.
          Kama umesoma vizuri na kulielewa jambo la kwanza tulilokuambia juu ya kulijua kusudi la Mungu kabla ya mpango wake; utakuwa umejua ya kuwa kusudi ni kubwa ki-umuhimu kuliko mpango. Ndiyo maana Mungu hawezi kubadilisha kusudi lake ili kukidhi mipango yetu ya kibinadamu.
          Tena utakuwa umepata picha moyoni mwako ya kuwa wewe ni sehemu tu ya watu wengi ambao Mungu anao na amewaweka ili kuhakikisha mipango Yake inafanikiwa ili kusudi lake alilolikusudia lisimame.
          We are not designed to work alone or implement His plans alone! Hatukuumbwa ili tufanye kazi peke yetu, au hatukuumbwa ili tutekeleze mipango ya Mungu peke yetu. Kufanikiwa kwa mtu mmoja kunategemea mafanikio ya mtu mwingine. Mnayeshirikiana naye akifanikiwa na wewe pia unafanikiwa! Au kama unashirikiana na mashine au chombo Fulani – kufanikiwa kwako kunategemea pia mafanikio ya utendaji wa mashine hiyo au chombo hicho.
Jambo la Tatu:
          Mungu ametenga muda maalumu wa kutekeleza kusudi lake na mipango yake! Maana katika Mhubiri 3:1,17 tunasoma ya kuwa , “Kwa kila jambo kuna majira yake, na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu ….. Nikasema moyoni mwangu, Mungu atawahukumu wenye haki na wasio haki; kwa kuwa kuna wakati huko kwa kila kusudi na kwa kila kazi”.
          Tunataka ujue ya kuwa mipango ya leo inaweza isifae kesho. Kilichofanikiwa mwaka uliopita kinaweza kisifanikiwe kikitekelezwa mwaka huu. Lazima kujifunza kwenda na wakati wa Mungu na kujua tunachojua kukifanya ndani yake.
          Kufuatana na kitabu cha 1 Mambo ya Nyakati 12:32, wana wa Israeli walijua siri hii wakati Daudi akiwa mfalme wao. Na hii ni kwa sababu Mfalme Daudi alikuwa analitumikia kusudi la Mungu na wala si kusudi lake mwenyewe wala la wana wa Israeli (Matendo ya Mitume 13:36)
          Umuhimu wa kujua nyakati za Mungu tunauona pia tunaposoma katika Matendo ya Mitume 17:26 na kuelewa ya kuwa kabla mwanadamu hajaumbwa, Mungu aliweka kwanza nyakati kwa ajili ya utekelezaji wa kusudi na mipango Yake akimtumia mwanadamu huyo.
Jambo la Nne:
          Mungu anapoweka wazo ndani yako juu ya mpango wake anaotaka uutekeleze, ujue basi katika mawazo ya Mungu mpango huo tayari umekwishatekelezwa na kumalizika.
          Kwa mfano; mara kwa mara tunawaambia wenzetu waliomo katika kamati za semina tunazoandaa sehemu mbali mbali ya kuwa – katika mawazo ya Mungu semina hizi tayari zimekwisha fanyika na Mungu ameona matokeo yake.
          Watu wengine wakitusikia tukisema namna hii huwa hawatuelewi. Lakini sisi tunaamini kabisa ya kuwa pale Mungu anapotupa wazo la kuifanya semina mahali Fulani, kwake Mungu semina hiyo ameitekeleza na kufika mwisho, na ndipo anapotuambia.
          Kazi yetu inabaki kuomba Mungu atuwezeshe kuyajua na kuyatekeleza anayotaka tuyafanye, ili kusudi la kuwepo semina hiyo lifikiwe. Ndiyo maana katika Isaya 46:10 Mungu anasema; “nitangazaye mwisho tangu mwanzo, ….. mambo yasiyotendeka bado; nikisema, shauri langu litasimama, nami nitatenda mapenzi yangu yote”.
          Kwa hiyo basi ina maana Mungu anatangaza mambo yasiyotendeka bado jambo hilo likiwa ndiyo linaanza tu! Pia, hawezi akautangaza mwisho wa jambo likiwa ndiyo tu linaanza kama hajauona huo mwisho wake utakavyokuwa! Na kama anaujua mwisho wake, jambo likiwa tu ndiyo linaanza,ina maana hatua zilizopo kati ya mwisho na mwanzo unazotakiwa kuzifanya anazijua na yuko tayari kukuongoza ili uweze kulifikisha jambo hilo katika mwisho wake mzuri uliokusudiwa na Mungu.
          Ndiyo maana katika Yeremia 29:11 anasema; “ Maana nayajua, mawazo ninayowawazia ninyi, asema Bwana, ni mawazo ya amani, wala si ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za mwisho”.
          Tulipojua hili, ndani ya mioyo yetu tulipata utulivu mkubwa sana wa kuwa na uhakika wa kuwa Mungu anaweza kutuongoza katika mipango anayotupa, kwa mfanikio toka mwanzo hadi mwisho wa mipango hiyo. Tunataka na wewe ujue hili ya kuwa Mungu hawezi kukupa jambo la kufanya ambalo hajui mwisho wake utakuwaje! Ukijua hili litakusukuma kuwa karibu na Mungu ili umjue zaidi kwa namna ambavyo akikupa mpango wa kuutekeleza, atakuongoza pia katika utekelezaji wake hatua kwa hatua hadi ufike katika mwisho ule ambao ulikusudiwa.
Jambo la Tano:
          Upo upako wa Roho Mtakatifu wa kukusaidia kuanza mpango ambao Mungu amekupa uutekeleze, na ule wa kukusaidia uweze kuumalizia huo mpango vizuri.
          Upako ni uwezo wa Mungu au nguvu za Mungu ndani ya Roho Mtakatifu ili kutusaidia kuyatimiza makusudi ya Mungu katika maisha yetu.
          Ndiyo maana Yesu Kristo anamwita Roho Mtakatifu ya kuwa ni “msaidizi”. Soma Yohana 14:16,17, 26 na Yohana 16:7 -15. Kumbuka msaada unapelekwa pale panapohitaji msaada. Roho Mtakatifu hawezi kukulazimisha kukupa msaada usioutaka – labda mtu mwingine amwombe Mungu kwa ajili yako.
          Yesu Kristo maana yake Yesu ‘mpakwa mafuta’. Kwa kuwa neno ‘Kristo’ maana yake ni ‘masihi’ au ‘mpakwa mafuta’. Kwa hiyo anapojiita Yeye ni Alfa na Omega (Ufunuo wa Yohana 1:8), ana maana ndani yake unapatikana upako wa kuanzia (Upako wa Alfa), na pia ano upako wa kutusaidia kumalizia jambo vizuri hadi mwisho (Upako wa Omega).
          Ndiyo maana biblia inamtaja Yesu kama mwanzilishi (Alfa) na mkamilishaji (Omega) wa imani yetu! (Waebrania 12:2). Kwa hiyo kama una jambo ambalo Mungu ameliweka ndani yako na hujui namna ya kuanza kulitekeleza, basi ni vizuri umwombe Mungu akupe upako wa Alfa ili ukusaidie kuanza. Na kama umeanza kulifanya jambo alilokupa Mungu kufanya, lakini hujui namna ya kumalizia, basi ni vizuri umwombe akupe upako wa Omega ili akusaidie namna ya kulimazia jambo hilo vizuri.
Jambo la Sita:
          Uwe mwangalifu sana na uhusiano unaokuwa nao na watu mbalimbali; - maana unaweza kukwamisha au kufanikisha mpango wa Mungu juu yako!
          Tunaamini unakumbuka jinsi ambavyo Mtume Petro alimkataza Yesu huku akimkemea baada ya Kristo kuelezea mpango wa Mungu juu yake wa kwenda Yerusalemu kusulubiwa. Yesu na Petro walikuwa marafiki, lakini shetani alimtumia Petro ili amkatishe tamaa asiendelee na mpango wa kwenda Yerusalemu kusulubiwa. Yesu akamkemea Petro akisema; “ Nenda nyuma yangu, shetani; u kikwazo kwangu; maana huyawazi yaliyo ya Mungu, bali ya wanadamu”.
          Hata ikiwa mbele yako kuna mapambano na majaribu ya namna gani, unahitaji marafiki wanaokutia moyo kusonga mbele, na si rafiki anayekutia moyo ili urudi nyuma na kuuacha mpango wa Mungu.
          Ukisoma Kutoka 32:1-8, 21-26 utaona jinsi ambavyo Haruni alivyoshindwa kuwasaidia wana wa Israeli walipokuwa wamechoka na kukata tamaa katika kumsubiri Musa atoke mlimani alikokwenda kuongea na Mungu. Kufuatana na Yoshua 1:6 na 2Mambo ya Nyakati 20:20 kuna watumishi ambao ndani yao ameweka neno kwa ajili yako ili likusaidie ufanikiwe.
          Kwa hiyo uwe mwangalifu ndani ya moyo wako ili ujue unampa nafasi mtumishi wa Mungu wa namna gani na nafasi ya namna gani. Soma 2 Wakorintho 7:2! Je! Ushauri anaokupa unakukwamisha zaidi au unakufanikisha? Je! ushauri anaokupa unakufanya uwe huru zaidi ndani ya Kristo au unajikuta unapoteza uhuru wako? Je! akikukuta umekwama kwenye dhambi au kwenye majaribu anakupa neno la namna gani? – je, linakusaidia utoke katika hali hizo na ushindi wa Yesu au neno hilo analokupa linakufanya ujihukumu na kujilaumu zaidi?
Jambo la Saba:
          Mpe Mungu utukufu na kumrudishia sifa anazostahili kwa Mungu kukutumia na ukafanikiwa katika kutekeleza mpango wake juu ya maisha yako!
          Ukifanya hili siku zote itakuwa ishara toka kwako ya kuonyesha ya kuwa umefanikiwa si kwa uwezo wala nguvu zako bali kwa Roho wa Mungu. Hili ndilo wazo la Zekaria 4:6.
          Lakini pia ukiwa na nia na moyo huu ndani yako Yesu Kristo atainuliwa katika mipango yako; na itakuwa rahisi watu wanaokuzunguka kumwona Mungu katika maisha yako. Yesu alisema; “ Nami nikiinuliwa juu ya nchi, nitawavuta wote kwangu” (Yohana 12:32).
          Je! mipango unayofanya ambayo unasema Mungu amekuongoza kuifanya, huwa inampa Mungu utukufu kwa kiasi gani? Je! umewahi kulifikiria hili? Ni muhimu kufikiria hili kila wakati maana imeandikwa: “Na kila mfanyalo, kwa neno au kwa tendo, fanyeni yote katika jina la Bwana Yesu, mkimshukuru Baba kwa yeye” (Wakolosai 3:17) “…… mtendapo neno lo lote, fanyeni yote kwa utukufu wa Mungu” (1 Wakorintho 10:31)
Tuzidi kuombeana!
Ni sisi katika utumishi wa Kristo,
Christopher na Diana Mwakasege


Eliezer Mwangosi

unread,
Mar 16, 2012, 7:58:24 AM3/16/12
to yourtr...@googlegroups.com

Amen,

 

BE BLESSED AND HAVE A NICE WEEK END

 

 

Eliezer Mwangosi

--
Mkikaa ndani yangu na maneno yangu yakikaa ndani yenu basi ombeni chochote mtakacho nanyi mtapewa.Yohana15:7

 

Important Notice:

The National Bank of Commerce Limited is a registered Commercial Bank in the United Republic of Tanzania.

This e-mail and any files transmitted with it are confidential and intended for the use of the individual or entity to whom they are addressed.

Please note that there are terms and conditions and some important restrictions, qualifications and disclaimers ("the Disclaimer") that apply to this email. To read this click on the following address or copy into your Internet browser:

http://www.nbctz.com/disclaimer/email

The Disclaimer forms part of the content of this email.

 

Reply all
Reply to author
Forward
0 new messages