Re: NENO LA LEO

142 views
Skip to first unread message

Bahati Mashimba

unread,
Nov 11, 2015, 5:46:52 AM11/11/15
to YourTrueVine, eliezer.mwangosi, Mgedzi Deborah
Amina.Palipo na Upendo pana umoja , amani na maendeleo

Ubarikiwe sana na Mungu


On 11/8/15, eliezer.mwangosi <eliezer....@yahoo.com> wrote:
> NENO LA LEO - USHAURI KWA WATU WA MUNGU BAADA YA UCHAGUZI
> Mathayo 5:44-45 "Lakini mimi nawaambia, wapendeni ADUI zenu, waombeeni
> WANAOWAUDHI; ili mpate kuwa wana wa Baba yenu aliye mbinguni....."
>
> Nilipokuwa nafuatilia post za wapendwa wengi na wakati mwingine kusikiliza
> wakiongea juu ya matokeo ya uchaguzi hasa wa Uraisi, nimesikitika kugundua
> kwamba wapendwa wengi wameghafilika na kutanga mbali na misingi ya wokovu
> wetu. Wengi wameruhusu shina la uchungu lichipuke ndani ya mioyo yao na
> hatimaye kuwatia unajisi (Soma Waebrania 12:14-15), roho za visasi na uadui
> zimetawala kuwasumbua wengi.
>
> Katika somo langu la 30.08.2015, nilitoa somo lililosema: WATU WA MUNGU NA
> SIASA / UCHAGUZI, likitoa mwanga jinsi Mungu anavyohusika na tawala za
> jamii, na watu wa Mungu wanachopaswa kukifanya na namna ya kuyapokea
> matokeo. Baada ya matokeo nimegundua watu wa Mungu wengi hawajui jinsi Mungu
> anavyotenda kazi hasa katika michakato ya kupata watawala wa serikali
> inayojumuisha WAOVU NA WEMA, mawazo ya Mungu yako tofauti sana na mawazo
> yetu. Hivyo tunapoona mambo hayako sawa, tunapaswa kutulia na kutafuta
> hekima yake.
>
> Neno linasema "Mpende Adui na Kumuombea", Jihoji Kama Mcha Mungu, baada ya
> matokeo ya uchaguzi na Raisi kuapishwa, iwe ni kwa haki au laa, umechukuwa
> hatua gani? Siku moja kabla ya Raisi kuapishwa nilisikia malalamiko mengi
> tena yenye uchungu na wengine kufikia kuombea Mabalaa yatokee ili
> asiapishwe. Hadi leo hii kuna wapendwa wengi wanaombea mabaya yatokee kwa
> Raisi aliye madarakani, ikiwa ni adhabu kutoka kwa Mungu. Kumbukeni Chama au
> Serikali haina Dini, ila ndani yake kuna wacha Mungu na Waovu. Kumbukeni
> Taifa la Israeli lilipigwa na kuhujumiwa haki na mataifa maovu kwa sababu tu
> ya maovu ya watu wachache.
>
> KWA WATANZANIA: Wale wanaoamini kuwa wameporwa haki yao Kupitia mchakato wa
> uchaguzi, ni wakati wa kukaa na Mungu ili awape hekima ya kufanya maamuzi
> sahihi bila kutenda UOVU, wajichunguze na kujihoji, wakiona kuna uovu ndani
> yao juu ya jamii watubu na kuungama, ili Mungu ajidhihirishe juu yao kwa
> wakati. Waombeeni walioko madarakani kwa wakati huu, ili Mungu awape hekima
> na ufahamu wa kutenda mambo kwa HAKI. Kusudi la Mungu ni KUOKOA sio kupoteza
> roho, ombea waokolewe, wawe na hofu ya Mungu, ndipo mtapandishwa juu ya
> Vilima kwa wakati uliokubalika.
>
> KWA WATANZANIA: Wanaoamini wameshinda kwenye uchaguzi; kwa hakika Mungu
> ndiye anayejua, kama ni kwa uhalali au laa. Kama nilivyotangulia kusema,
> ndani ya vyama na serikali kuna WAOVU na WEMA. Ikitokea Mungu ameruhusu
> mafanikio kwa njia isiyo halali, sio kwamba anakubaliana na uovu, ila kuna
> neema inamtafuta mmoja atubu, ili aokolewe. Huu ni wakati wa mpito wa
> kupimwa tena katika mizania ya Mungu. Kama kuna Uovu wowote ni wakati wa
> Kutubu ili Mungu awafanikishe katika HAKI. Kumbukeni hakuna AMANI Kwa Waovu
> (Isaya 48:22).
>
> Kama ushindi ulikuwa ni wa halali, bado mnatakiwa kunyenyekea chini ya Mkono
> wa Mungu, ili azidi kuwakweza na kuwafikisha katika vilele. Bila Mungu
> hekima ya Mwanadamu ni patupu, shetani atawashinda na kuwa na hali mbaya
> kuliko matazamio ya watanzania. 1Petro 5:6-7.
>
> HITIMISHO: Bwana Mungu anasema "Maana mawazo yangu si mawazo yenu, wala njia
> zenu si njia zangu; asema BWANA" Isaya 55:8. Watu wa Mungu tunahitaji kuwa
> makini na kuomba hekima kwa Mungu, hasa tunapojihusisha na mambo ya Vyama
> vya siasa ambavyo havina misingi ya Dini. Sisi tunatazama kwa macho ili
> kutimiza makusudi na mapenzi ya mioyo yetu, lakini Mungu hayuko hivyo.
> Usishindwe na Ubaya, bali uushinde ubaya kwa wema 'Warumi 12:21'.
>
> Watu wa Mungu tunaoishi katika kazazi hiki kiovu, tunapaswa kuwa chachu ya
> kuleta AMANI, tukiwaombea waovu waokolewe, kuchukia UOVU sio kulipa visasi
> na kuombea mabaya, hizo ni roho za yule adui. Waovu wanaonywa kwa upendo,
> wanashauriwa, wanaombewa, wakiendelea na uovu unaotudhuru tutatumia vyombo
> vya sheria na kutafuta haki. Ni agizo la Mungu kuzitii Mamlaka zozote
> zilizowekwa katika Jamii - Warumi 13:1-7. Mwenye Mamlaka ya mwisho juu ya
> Kuziweka na Kuziangusha Mamlaka ni Mungu, kwa njia zozote mwanadamu hawezi
> bila Mungu.
>
> MUNGU BARIKI TANZANIA - TIMIZA KUSUDI LAKO KWA WATANZANIA - KATUONDOLEE UOVU
> - KILA ALIYESHIKA MAMLAKA UKAMTIISHE AKAWE CHINI YA MAMLAKA YAKO - VIONGOZI
> WOTE UWABARIKI NA KUWAPA HEKIMA YA KUONGOZA TAIFA LA TANZANIA KWA WAKATI
> ULIO AMRIWA.
>
> Na Ev. Eliezer Mwangosi - Tel. 0767210299 - Email.
> eliezer....@yahoo.com.
>
>
>
>
> Sent from Samsung tablet

Mashimba

unread,
Nov 18, 2015, 8:22:34 AM11/18/15
to eliezer mwangosi@yahoo. com, yourtruevine@googlegroups com
Amina.

"eliezer.mwangosi" <eliezer....@yahoo.com> wrote:

NENO LA LEO - HITAJI KUU LA ULIMWENGU
Tafakari: Mathayo 6:33 "Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo mtazidishiwa".

Kila kunapokucha maisha ya mwanadamu yanazidi kukutana na changamoto za kukatisha tamaa. Kuanzia maisha ya mtu binafsi, familia, taifa hadi mataifa n.k. Kila siku zinaibuka changamoto mpya zinazoumiza vichwa. 

Bila kujali; uzuri wa maumbile, hali ya kifedha, elimu waliyonayo, mali wanazomiliki, demokrasia walizonazo, uwe katika ndoa au laa, uwe na mchumba au katika mahusiano yoyote, mwanadamu awe na hali yoyote ile, ni hakika anayo changamoto, na kama kwa sasa hana; atakuwa amaisha ipitia au ziko mbele zinakuja. 

Sikiliza; Watu wanatafuta AMANI, lakini Kila leo amani inazidi kupotea, wengi wanatembea wakiwa na maumivu moyoni, kila mmoja akiwa amejeruhiwa na jambo fulani. Hata siku hii leo wengi wana mizigo mizito, hawajui mwisho wake. Vijana wana changamoto, watu wazima ndio usiseme, viongozi wa mataifa makubwa kwa madogo hawalali. 

Hitaji letu kuu ili kupita salama katika dhoruba hizi za ulimwengu ni kumrudia Mungu, kuutafuta ufalme wake kwanza, adha zote tunazozipata ni mishale ya adui shetani, inayotupata kwa HILA. Amani ya kweli na ya kudumu bila Mungu, ni kujilisha upepo. Wanaodai wana amani bila Mungu, hiyo ni ya kitambo tu. 

Ayubu 22:21 inasema "Mjue sana Mungu, ili uwe na AMANI; ndivyo MEMA yatavyokujia". Hakuna njia ya mkato ya kupata Amani ya kweli nje ya kutoa maisha yetu kwa Kristo, aliyekuja kumuokoa mwanadamu, na kumuweka huru na mishale ya Adui shetani, ambayo ni dhambi na matunda yake. 

MUNGU ATAWALE NIA YA KILA MMOJA WATU ILI TUPATE USHINDI MILELE. 

NAWATAKIA WOTE SIKU NJEMA YENYE AMANI NA BARAKA TELE.

Na Ev. Eliezer Mwangosi.






Sent from Samsung tablet

Mtoka James

unread,
Nov 18, 2015, 9:38:06 AM11/18/15
to yourtr...@googlegroups.com, eliezer mwangosi@yahoo. com

Amen

--
Mimi ni mzabibu ninyi ni matawi, akaaye ndani yangu nami ndani yake, huyo huzaa sana; maana pasipo mimi ninyi hamwezi kufanya neno lolote.Yohana 15:5
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "YourTrueVine" group.
To post to this group, send email to yourtr...@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

Mashimba

unread,
Nov 19, 2015, 12:41:18 AM11/19/15
to eliezer mwangosi@yahoo. com, yourtruevine@googlegroups com, Mgedzi Deborah
Amina.Ubarikiwe sana mpendwa kwa ujumbe unaogusa maisha ya kila mkristo.Watu wengi hawajaweza kuifahamu kuwa kutokusamehe na kusahau makosa ya watu ni dhambi kama ilivyo dhambi ya kuiba,kuua,ufisadi,nk .Imendikwa Kwa maana mkiwasamehe watu makosa yao, na Baba yenu wa mbinguni atawasamehe ninyi.Bali msipowasamehe watu makosa yao, wala Baba yenu hatawasamehe ninyi makosa yenu .Mathayo 6:14-15

"eliezer.mwangosi" <eliezer....@yahoo.com> wrote:

NENO LA LEO - DHAMBI ILIYOWASHINDA WENGI
Tafakari: Marko 11:25 "Nanyi, kila msimamapo na kusali, sameheni, mkiwa na neno juu ya mtu; ili na Baba yenu aliye mbinguni awasamehe na ninyi makosa yenu".

Kama kuna dhambi itakayowapeleka wengi motoni,  ni hii ya kutosamehe. Ingelikuwa mtu anapewa kuona yaliyo ndani ya mioyo ya watu; tungeshuhudia majeraha makubwa yasiyopona, yaliyotokana na kuumizwa na ndugu au jamaa na wakati mwingine wapenzi wao. Japokuwa hatuwezi kuona, maneno ya manung'uniko na malalamiko yanafunua mizigo ilioko ndani japo kwa sehemu ndogo. 

Wengi utasikia wanasema "nimemsamehe ila sitasahau" huyo bado anamaumivu hajasamehe. Wengi wanaenda majumba ya Ibada, wanaimba, wanahubiri, wanatoa zaka na sadaka, huku wakiwa bado wana mafukuto ya chuki kwa waliowakosea. Utakuta mtu anajisifia akisema "mimi  hata simsalimii" au "nikimuona nakereka", ndivyo wengi walivyo hata kama hawasemi. Jiulize ukimuona yule mbaya wako unajisikiaje? Kila mmoja analo jibu. 

Haijalishi umeumizwa kiasi gani; iwe ni kazini, iwe kwenye ndoa au mahusiano, au katika mazingira yoyote; unapaswa kusamehe kabisa, na kuachilia roho za kulipa kisasi, manung'uniko, malalamiko, chuki, hasira na harara. Hayo yote yakidumu moyoni yanafunga kabisa milango ya mbinguni.

Yesu alirudia kufundisha jambo hili akiwa anawafundisha wanafunzi wake kuomba akisema - Mathayo 6:12 "utusamehe deni (makosa) yetu, kama sisi nasi tuwasemehevyo wadeni (waliotukosea) wetu". Kwa maneno hayo, tunajifunga kitanzi au kuwa huru, kwa kusamehe au kutosamehe. 

Wapendwa katika hali ya ubinadamu jambo hili la msamaha ni gumu, hivyo linahitaji kutoa maisha yetu kwa Yesu Kristo ili atupatie uwezo wa kutenda yale tusiyoweza, atupatie tabia ya Upendo wa kuwapenda wabaya na kuwaombea. Msamaha ni mojawapo ya vipimo kama kweli tunaongozwa na Roho mtakatifu au bado tuko chini ya kongwa la utumwa. 

NAWATAKIA WOTE SIKU NJEMA YENYE NURU YA MAFANIKIO NA BARAKA TELE. 

By: Ev. Eliezer Mwangosi - 0767 210 299. 




Sent from Samsung tablet

Mashimba

unread,
Nov 26, 2015, 4:14:13 AM11/26/15
to eliezer mwangosi@yahoo. com, yourtruevine@googlegroups com, Mgedzi Deborah
Amina.Asante kwa ujumbe mzuri unaotufundisha na na tunavyoweza kuisho kwa kuyatakasa macho na masikio yetu.
Bwana azidi kukupa neema katika kila kazi njema

"eliezer.mwangosi" <eliezer....@yahoo.com> wrote:

WAKATI UNAOFAA KUWA KIPOFU NA KIZIWI
Ni nani aliye kipofu, ila mtumishi wangu? au aliye kiziwi, kama mjumbe wangu nimtumaye? Ni nani aliye kipofu, kama yeye aliye na amani [mkamilifu]? naam, kipofu kama mtumishi wa BWANA? Unaona mambo mengi, lakini huyatii moyoni; masikio yake ya wazi, lakini hasikii. Isaya 42:19,20 [KJV].

Ni upofu gani huu? Ni upofu ambao hautayaruhusu macho yetu kutazama sana maovu. Hautayaruhusu macho yetu kutulia juu ya maovu. Hautayashika mambo yale yanayoonekana na kuupoteza umilele katika kumbukumbu zake.... Tunataka kuona ipasavyo, tunataka kuona kama vile aonavyo Mungu; maana Shetani anajaribu daima kuyageuza mambo yale ambayo macho yetu yanayaangalia sana ili tupate kuyaona kwa njia yake aliyoichagua....

Mtumishi wa Mungu aliye hai anaona akiwa na kusudi fulani. Macho hutakaswa na masikio nayo hutakaswa, na wale watakaofumba macho na masikio yao wasiyaangalie maovu watabadilika. Lakini endapo watawasikiliza wale wanaozungumza nao na wanaojaribu kuyaongoza mawazo yao mbali na Mungu na mbali na mambo yao yale ya milele, basi, hapo ndipo fahamu zao zote zitapotolewa kutokana na kile macho yao yanachokiangalia sana. Yesu asema, "Basi... jicho lako likiwa safi, mwili wako wote utakuwa na nuru. Lakini jicho lako likiwa bovu, mwili wako wote utakuwa na giza." Mathayo 6:22,23.

Inaleta tofauti kubwa juu ya kile tunachoilisha mioyo yetu na roho zetu. Tunaweza kuiacha mioyo yetu kutafakari sana hadithi zile za mahaba na ndoto zisizowezekana, je! hayo yatatufanyia nini sisi? Yatatuangamiza, mwili na roho.... Twataka kuwa na nguvu ile itakayotuwezesha kuyafumba macho yetu kwa mandhari [picha] zile zisizokuwa nzuri; zisizotuadilisha tabia zetu, zile ambazo hazitatutakasa na kutufanya kuwa waungwana; na kuziba masikio yetu kwa kila kitu kilichokatazwa katika Neno la Mungu. Anatukataza kuwaza maovu, kusema maovu, na hata kutafakari maovu....

Ndani ya Yesu mimi naona kila kitu kilicho chema, kila kitu kilicho kitakatifu, kila kitu kinachotia moyo na kilicho safi. Basi, kwa nini mimi nipende kuyafumbua macho yangu sana ili kuangalia kila kitu kinachochukiza? Kwa kutazama tunabadilishwa. Na tumtazame Yesu na kuutafakari uzuri wa tabia yake, na kwa kutazama tutabadilishwa tupate kufanana na sura yake.

BWANA AWAPATIE SIKU NJEMA YENYE AMANI NA BARAKA TELE




Sent from Samsung tablet

Mashimba

unread,
Nov 27, 2015, 1:15:43 AM11/27/15
to eliezer mwangosi@yahoo. com, yourtruevine@googlegroups com, Mgedzi Deborah
Amina.Bwana akubariki

"eliezer.mwangosi" <eliezer....@yahoo.com> wrote:

NENO LA LEO - JE SILAHA ZAKO ZINA UWEZO?

Tafakari: 2Wakorintho 10:3-5
 "Maana ingawa tunaenenda katika mwili, hatufanyi vita kwa jinsi ya mwili; maana Silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina UWEZO KATIKA MUNGU hata kuangusha Ngome; tukiangusha Mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu;  na tukiteka nyara kila FIKIRA ipate KUMTII Kristo". 

Nakumbuka usemi wa marehemu Baba wa Taifa Mwalimu JK Nyerere, wakati Raisi wa Uganda Idd Amini alipoivamia Tanzania, Baba wa Taifa alisema "Nia tunayo, Sababu tunayo na Uwezo wa kumpiga tunao". Ndipo akatoa Amri ya Kumpiga na Kuivunjilia mbali ngome yake katika nchi yake.

Katika ulimwengu wetu huu uliotekwa na Adui shetani, ni jambo la kawaida kusikia Watu wanajiita ni Wakristo, wengine wanajiita wacha Mungu, wengine wameokoka n.k. Wanauwezo mkubwa hata wa kuimba nyimbo za dini kwa hisia kubwa, lakini jambo la kushangaza, asilimia kubwa unawakuta bado ni watumwa wa yule Adui. 

Mbali na kuonekana watu wema au wacha Mungu machoni pa watu, ndani ya Mawazo yao au Fikira zao, kumejaa Visasi, Uadui, Kutosamehe, Husuda, Wivu. Wakati mawazo, maneno na matendo ya Ngono na Mapenzi yakiendelea kukamata akili za Vijana kwa Wazee, wakipigwa upofu wasione kuwa ni dhambi; Mungu anazidi kutoa wito wa Kushinda vita. 

Wapendwa Ngome kuu za Shetani ziko katika MAWAZO au FIKIRA, huko ndiko zinatakiwa zivunjiliwe mbali, hatimaye mawazo yetu yaunganishwe na Kristo. Hayo yanawezekana tu kwa watu ambao wameruhusu utawala wa Ufalme wa Mungu kuwa ndani yao, kwa njia ya Roho mtakatifu. 

Ni wakati wa kila mmoja kujipima, kuwa je; ni kweli amezivaa Silaha zenye Uwezo wa Mungu? Mawazo na Fikira Je zinapatana na Mungu au zimejaa Uchafu wa yule Adui shetani? Yesu Kristo alikuja kwa ajili ya kutuokoa kutoka katika mateka ya dhambi, na huu ndio uhuru wa Kweli.

NAWATAKIA WOTE SIKU NJEMA YENYE BARAKA TELE NA MAFANIKIO KATIKA MWILI NA ROHO.

Na: Ev. Eliezer Mwangosi - 0767 210 299.




Sent from Samsung tablet

Bahati Mashimba

unread,
Dec 4, 2015, 3:59:27 AM12/4/15
to eliezer.mwangosi, YourTrueVine, Mgedzi Deborah
Amina .BWANA akubariki mpendwa katika Yesu

On 12/4/15, eliezer.mwangosi <eliezer....@yahoo.com> wrote:
> NENO LA LEO - TAHADHARI KWA WATU WA MUNGU
> Tafakari:- Yuda 1:3 "Wapenzi, nilipokuwa nikifanya bidii sana kuwaandikia
> habari ya wokovu ambao ni wetu sisi sote, naliona imenilazimu kuwaandikia,
> ili niwaonye kwamba mwishindanie imani waliokabidhiwa watakatifu mara moja
> tu."
>
> Kama kuna wakati wa hatari kwa watu wa Mungu, ni huu tulionao sasa. Mtume
> paulo alitoa tahadhari juu ya wengi kupokea wokovu bandia kutoka kwa
> watumishi au manabii wasiotumwa na Bwana, wanaochanganya ukweli na uongo, na
> watu wasio na ujuzi wa neno la Mungu wanapotea pasipo kujua.
>
> Mtume paulo anasema "Kwa maana kuna watu waliojiingiza kwa siri, watu
> walioandikiwa tangu zamani hukumu hii, makafiri wabadilio neema ya Mungu
> wetu kuwa ufisadi, nao humkana yeye aliye peke yake Mola, na Bwana wetu Yesu
> Kristo." Yuda 1:4. Wapendwa, kuna uasi mwingi unaendelea katikati ya
> wanaojiita watu wa Mungu, na ndio unaoleta laana nyingi katika kizazi
> chetu.
>
> Wakati umefika wa kila mmoja kuamka kiroho, na kuhakikisha juu ya msingi wa
> Imani aliyonayo. Jiulize kama kweli umeishindania Imani waliyokabidhiwa
> watakatifu mara moja tu, linganisha mafundisho unayoshika kama ni sawa na
> mafundisho ya Mitume wa Yesu. Kumbuka, watakatifu ni wale wazishikao AMRI za
> Mungu na Imani ya Yesu - Ufunuo 14:12.
>
> Kama kawaida Shetani anawaongoza watu kutojifunza na kutii Amri za Mungu,
> huku akiwaondoa wasijue kazi ya Neema ya Kristo inavyotenda kazi kumuokoa
> mdhambi na kumuweka huru. Vita hii ya Kiroho yampasa kila mtu aielewe vizuri
> ili asimame kama mtakatifu siku ile ya hukumu. Ufunuo 12:17. Kumbuka, Amri
> za Mungu zinaosha dhambi, ni sawa na kioo kinachoonyesha uchafu, wakati
> Neema ya Yesu, kupitia mauti ya Msalaba, inatupatia Msamaha, ondoleo na
> ushindi wa dhambi kwa anayetubu.
>
> NEEMA YA MUNGU IKAWE JUU YA KILA MMOJA WETU ILI TUSIMAME TUKIWA WASHINDI
> MILELE ZOTE.
>
>
>
> Sent from Samsung tablet

Mtoka James

unread,
Dec 4, 2015, 5:19:56 AM12/4/15
to yourtr...@googlegroups.com, Mgedzi Deborah, eliezer mwangosi@yahoo. com

Amen  mubarikiwe

--
Mimi ni mzabibu  ninyi ni matawi,  akaaye ndani yangu  nami ndani yake, huyo huzaa sana; maana pasipo mimi  ninyi  hamwezi kufanya   neno lolote.Yohana 15:5
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "YourTrueVine" group.
To post to this group, send an email to yourtr...@googlegroups.com.

Mashimba

unread,
Dec 9, 2015, 12:31:56 AM12/9/15
to eliezer mwangosi@yahoo. com, yourtruevine@googlegroups com, Mgedzi Deborah
Amina mtumishi katika shamba la Bwana

"eliezer.mwangosi" <eliezer....@yahoo.com> wrote:

NENO LA LEO - CHECHE ZA UASI NA CHANZO CHAKE
➡Basi,  wapenzi mkitangulia kujua hayo, jilindeni nafsi zenu, msije mkachukuliwa na kosa la hao wahalifu mkaanguka na kuuacha uthibitifu wenu. 2 Petro 3:17.

1⃣ Katika  siku hizi za mwisho, maovu yanapozidi kuongezeka, na upendo wa wengi unavyozidi kupoa, Mungu atakuwa na watu wake watakaolitukuza jina lake, na kusimama kama wakaripiaji wa dhambi. Wanatakiwa kuwa "watu wa pekee," ambao watakuwa waaminifu kwa sheria ya Mungu [Amri Kumi], wakati ulimwengu utakapojaribu kuzitangua amri zake; na wakati uweza wa Mungu unaoongoa utakapofanya kazi ndani ya watumishi wake, majeshi yale ya giza yatajipanga na kutoa upinzani mkali sana, uliodhamiriwa. Shetani atafanya kazi yake kwa "uwezo wote, na ishara na ajabu za uongo, na katika madanganyo yote ya udhalimu kwa hao wanaopotea." Atatumia kila mbinu ya udanganyifu kuishawishi mioyo ya wanadamu....

2⃣ Kazi  hiyo ya uasi huanzia katika maasi fulani ya kisirisiri ndani ya moyo wa mtu dhidi ya matakwa ya Sheria ya Mungu. Tamaa chafu, tamaa isiyo halali ya kupenda makuu, hutunzwa na kuendekezwa moyoni, na mashaka na giza humtenga mtu huyo mbali na Mungu. Tusipoyashinda maovu hayo, yatatushinda.

3⃣ Watu  ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakisonga mbele katika njia ile ya kweli, watajaribiwa kwa maonjo na majaribu. Wale wanaosikiliza mashauri ya Shetani, na kukengeuka kutoka katika unyofu wao, wataanza kwenda katika njia ile inayoshuka chini, na jaribu fulani lililoandaliwa [na Shetani] kwa werevu sana litawaharakisha kwenda kwenye njia ile ya uasi, mpaka kushuka kwao kutaonekana dhahiri na kunakuwa kwa kasi sana. Dhambi zile zilizokuwa za kuchukiza mno kwao hapo kwanza, [sasa] zinakuwa  za kuvutia sana, nazo hukaribishwa na kutendwa na wale waliotupilia mbali kicho chao kwa Mungu pamoja na utiifu wao kwa sheria yake. Lakini furaha yao nyingi sana mwanzoni mwa uasi wao, itaishia katika majonzi, kujivunjia heshima [aibu], na maangamizi.

4⃣ Tunahitaji kuwa macho daima, kukesha na kuomba ili tusije tukaingia majaribuni. Kujiendekeza kuwa na kiburi cha kiroho, tamaa mbaya, mawazo machafu, na cho chote kile kinachotutenga mbali na ushirika wetu wa karibu sana, ulio mtakatifu, pamoja na Yesu, huziweka roho zetu katika hatari kubwa. Yatupasa kuwa na imani iliyo hai kwa Mungu.... Kama wazo hilo la uasi linawasikitisha ninyi, nanyi hamtaki kuwa maadui wa ile kweli,... basi, "lichukieni lililo ovu, mkiambatana na lililo jema." Warumi 12:9.

BARAKA ZA BWANA ZIAMBATANE NA KILA MMOJA WETU KATIKA SIKU YA LEO.




Sent from Samsung tablet

Mtoka James

unread,
Dec 9, 2015, 12:57:26 AM12/9/15
to yourtr...@googlegroups.com, Mgedzi Deborah, eliezer mwangosi@yahoo. com

Amen  ubarikiwe  kwa ujumbe  huu  wakutujenga  kidogo.

--
Mimi ni mzabibu ninyi ni matawi, akaaye ndani yangu nami ndani yake, huyo huzaa sana; maana pasipo mimi ninyi hamwezi kufanya neno lolote.Yohana 15:5
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "YourTrueVine" group.
To post to this group, send email to yourtr...@googlegroups.com.

Mashimba

unread,
Dec 14, 2015, 4:47:17 AM12/14/15
to eliezer mwangosi@yahoo. com, yourtruevine@googlegroups com, Mgedzi Deborah
Amina.Bwana wa majeshi azidi kukubariki

"eliezer.mwangosi" <eliezer....@yahoo.com> wrote:

TAFAKARI: JE! UTAUFUNGUA MLANGO?
Tazama,  nasimama mlangoni, nabisha; mtu akiisikia sauti yangu, na kuufungua mlango nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye pamoja nami. Ufunuo 3:20.

1⃣ Yesu  asema, "Tazama, nasimama mlangoni, nabisha." Je! tutamfungulia? Yeye asingependa kutuona sisi tukisimama wakati huu, katikati ya hatari kubwa za siku za mwisho, kwa nguvu zetu wenyewe za kibinadamu.... Ni haki yetu kutembea katika mwanga wa jua wa kuwapo kwake, na kufuma katika tabia zetu tunazozijenga kamba zile za dhahabu za uchangamfu, shukrani, uvumilivu, na upendo. Kwa njia hiyo tunaweza kuonyesha uwezo wa neema ya Mungu, na kuakisi [kuiangaza] nuru ile itokayo mbinguni katikati ya wasiwasi na maudhi yanayotujia siku kwa siku.... Basi, mbona tunatembea kwa kujikwaa katika njia yetu bila kuwa na nuru hiyo?

2⃣Kila  onyo, kila karipio, na kila ombi katika Neno la Mungu, au kupitia kwa wajumbe wake aliowatuma, ni kubisha [kugonga] mlangoni pa moyo wako; ni sauti yake Yesu, ikiomba kuingia ndani yako. Kila bisho [kugonga] unalolidharau, huifanya azma yako ya kutaka kufungua kufifia zaidi na zaidi. Kama sauti hiyo ya Yesu haisikilizwi mara moja, basi, itachanganyika pamoja na sauti zingine nyingi katika moyo wako, yaani, masumbufu ya dunia na shughuli zake, mambo hayo yatachota mawazo yako yote, na hisia hiyo [ya kusikia sauti ya Yesu] itatoweka [moyoni mwako]. Moyo wako utaguswa kidogo tu, na kuishia katika hali ile ya hatari ya kupoteza uwezo wake wa kutambua hata usiweze kujua ufupi wa wakati ulio nao, na umilele ulioko ng'ambo ile ya pili.

3⃣ Wengi  wanazo takataka nyingi sana walizozilundika mlangoni pa moyo wao hata hawawezi  kumruhusu Yesu kuingia ndani. Wengine wana matatizo kati yao na ndugu zao ambayo hayana budi kuondolew [kusuluhishwa], wengine wana hasira mbaya, kiburi, uchoyo; kwa wengine ni kule kuipenda dunia kunakoweka kizuizi mlangoni pao. Vyote hivyo ni lazima viondolewe, kabla hawajaweza kufungua mlango na kumkaribisha ndani Mwokozi wao. 

4⃣Ni ya thamani jinsi gani ahadi hii, "nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye pamoja nami." Lo! ni pendo lililoje, pendo la ajabu la Mungu kwetu sisi! Baada ya sisi kuwa na uvuguvugu wote huu na dhambi tulizo nazo, yeye anatuambia, Nirudieni, nami itawarudieni, nami nitawaponya na kurudi nyuma kwenu kote.

5⃣  Kazi  yetu sisi ni kuufungua mlango wa moyo wetu na kumkaribisha Yesu ndani. Anabisha [Anagonga] akitaka kuingia ndani yako.... Je! utaufungua mlango? Yesu anasimama nje ya mlango wa moyo wako. Mkaribishe ndani, Mgeni wako huyo wa mbinguni.

NEEMA YA MUNGU WETU IKATAWALE MAISHANI MWETU DAIMA - NAWATAKIA SIKU NJEMA




Sent from Samsung tablet

Mashimba

unread,
Dec 23, 2015, 3:33:06 AM12/23/15
to eliezer mwangosi@yahoo. com, yourtruevine@googlegroups com, Mgedzi Deborah
Amina mtumishi

"eliezer.mwangosi" <eliezer....@yahoo.com> wrote:

NENO LA LEO - SIMAMA; BADO KUNA TUMAINI
Zaburi 40:1-2 "Nalimgoja Bwana kwa saburi, akaniinamia akakisikia kilio changu. Akanipandisha toka shimo la uharibifu, toka udongo wa utelezi; Akaisimamisha miguu yangu mwambani, akaziimarisha hatua zangu."

Ni jambo la kawaida katika kizazi chetu kushudia watu wengi wakipitia maisha ya kukatisha tamaa na kuvunjika moyo, mwanadamu amezungukwa na kila aina ya mitego, ambayo wengi huishia kunasa kwenye matope ya utelezi na hatimaye kushindwa kujinasua. 

Maisha ya Daudi ni mfano wa maisha ya watu wengi wa kizazi hiki, bila kujali wanajiita watu wa Mungu au laa, wengi wanapitiwa na mishale ya yule adui, na hatimaye kupitia changamoto za maisha yenye majeraha na uchungu mioyoni. 

Bila kujali hatua za miguu yako iliposimama, iwe ni kwenye utelezi wa dhambi; au shimo refu la matatizo, Mungu yuko tayari kukutoa na kukupandisha juu na hatimaye kukupatia ushindi kama alivyompatia Daudi. 

Yesu Kristo alikufa msalabani ili kutuokoa kutoka katika kila mitengo na tanzi za adui shetani. Ni wakati uliokubalika kupokea wokovu na kusimama katika tumaini la ushindi daima. 

UPENDO WA MUNGU UKATAMALAKI KWA KILA MMOJA WETU - NAWATAKIA SIKU NJEMA. 

Na: Ev. Eliezer Mwangosi
Simu: 0767210299





Sent from Samsung tablet

Mashimba

unread,
Dec 25, 2015, 12:47:14 PM12/25/15
to eliezer mwangosi@yahoo. com, yourtruevine@googlegroups com, Mgedzi Deborah
Haleluya mtumishi.Asante kwa neno la uzima

"eliezer.mwangosi" <eliezer....@yahoo.com> wrote:

NENO LA LEO - SALAMU ZA SIKUKUU YA KRISMASI
Tafakari: Mathayo 1:20-21 "Basi alipokuwa akifikiri hayo, tazama, malaika wa Bwana alimtokea katika ndoto, akisema, Yusufu, mwana wa Daudi, usihofu kumchukua Mariamu mkeo, maana mimba yake ni kwa uweza wa Roho Mtakatifu. Naye atazaa mwana, nawe utamwita jina lake Yesu, maana, yeye ndiye atakayewaokoa watu wake na dhambi zao".

Ingawa kuna wakristo wasiosherehekea Krismasi na wanaosherehekea, ujumbe huu unawafaa wote, ili mradi wanaamini kuwa Yesu alizaliwa kwa kusudi la ukombozi. Kwa walioniuliza maswali juu ya Krismasi, nimeandaa na ku post somo maalumu linaloeleza Ukweli juu ya sikukuu ya Krismasi 25 Desemba, wanaotafuta UKWELI naamini limewasaidia. 

Wakati ulimwengu wa kikristo asilimia kubwa wanajumuika katika kusherehekea sikukuu ya KRISMASI, wakimanisha kusherehekea kuzaliwa kwa Mwokozi wetu Yesu Kristo, ndivyo tunashuhudia vyombo vya usalama, wakijizatiti kupambana na uovu wa kila namna unaoweza kujitokeza. 

Ni mambo ya kusikitisha, kuona jinsi shetani anavyoweza kuharibu akili za watu hata wasijue wanachokifanya. Siku ambayo watu walipaswa wauone muujiza wa Mungu wa kugeuza mioyo ya vijana kwa wazee, itengane na dhambi na kuunganishwa na mbingu,  tunashuhudia uovu mwingi ukipangwa kutekelezwa siku hii ya Desemba 25. Kuna watu wameenda kwenye mkesha, au usiku mtulivu wakiwa na miadi na wapenzi wao kwenda kuvunja amri za Mungu. 

Mpendwa, hebu jiulize mipango yako katika siku hii ya Krismasi, ni kweli inampatia utukufu Mungu? ni kweli Yesu anazaliwa moyoni na kung'oa mizizi ya Dhambi? Unakwenda kusali! Huko kwenye friji kuna kreti za soda au vileo? Ingelikuwa malaika wanaonyesha message zote za kwenye simu za wanaojiita wasafiri wa mbinguni,  wengi wangeona aibu, na wewe Je?. 

Hebu wote wanaosherehekea sikukuu hii kwa Imani ya kuzaliwa Yesu Kristo, wapokee Nuru kwa kuruhusu Yesu kuzaliwa upya ndani ya mioyo yao, na kuleta wokovu kwa  kila dhambi. Mipango ya Nyumba za wageni kwa ajili ya uasherati, vilabu vya pombe, wanaoiba wake na waume za watu, na kila aina ya mipango ya Uovu, ikashindwe kwa Mamlaka ya Jina la Yesu Kristo.

NEEMA YA BWANA IKAAMBATANE KILA MMOJA WETU KATIKA KIPINDI HIKI CHA SIKUKUU. 

Na: Ev. Eliezer Mwangosi .... Tel. 0767210299 




Sent from Samsung tablet

Mashimba

unread,
Dec 31, 2015, 1:56:57 PM12/31/15
to eliezer mwangosi@yahoo. com, yourtruevine@googlegroups com, Mgedzi Deborah
Amina.Nawatakia Baraka mwaka 2016

"eliezer.mwangosi" <eliezer....@yahoo.com> wrote:

NENO LA LEO - CAMERA INAYONASA MAWAZO YA WATU
Tafakari: Mhubiri 12:14 "Hii ndiyo jumla ya maneno; yote yamekwisha sikiwa; Mche Mungu, nawe uzishike AMRI zake, maana kwa ujumla ndiyo impasayo mtu. Kwa maana Mungu ataleta hukumuni kila kazi, pamoja na kila NENO LA SIRI, likiwa jema au baya".

Pamoja na maendeleo ya digitali tuliyofikia, bado kuna mambo ambayo yanafanyika kwa siri, na wengine wasiyajue kabisa. Kuna wanaume wanakufa bila wake zao kujua mali zingine zilipo. Wengi wanajeruhiwa kwa kuvunja mahusiano kwa siri na kuja kudhihirika baadaye, binti mmoja alishangaa kusikia tangazo la ndoa kati ya mchumba wake na binti mwingine ambaye hakuwahi kusikia kama walikuwa na mahusiano, ilikuwa ni SIRI. 

Ikitokea simu zote zikusanywe bila taarifa na kuanza kusomwa jumbe zilizomo hadharani, utashangaa watu wakitokwa na jasho, na kushuhudia mahusiano ya wachumba na wanandoa kufikia mwisho. Uovu mwingi na wa kutisha unapangwa kwa siri, mauaji, ujambazi, uzinifu na uasherati, chuki, visasi, wivu, ulevi, nk, watu wanajitahidi kuvifanya kwa siri. Utasikia mtu anasema, tutafanya iwe SIRI asijue mtu, na kweli kibinadamu wanafanikiwa kwa wakati fulani, lakini utashangaa siku ikifika yote yanakuwa wazi. 

Rafiki; kwa Mungu hakuna SIRI, camera yake inanasa hadi mawazo ambayo bado kuingizwa kwenye matendo, na yanatunzwa kwenye kumbukumbu zisizofutika kwa ajili ya kuonyeshwa hadharani siku ya HUKUMU. Kumbuka wapendwa watashuhudia walivyosalitiwa kwa siri.... ndipo kila mtu atakiri kuwa "Hukumu za Mungu ni za kweli na za haki". Wengi wanajitahidi kufuta jumbe kwenye simu ili wasione wenzi wao, jumbe hizo zote hazifutiki kwenye kamera ya Mungu, zitaletwa zote. 

Tunapomalizia masaa ya mwaka 2015 kwa kalenda ya kibinadamu, hebu kila mmoja wetu achukue hatua ya kusimama upande salama, adhamirie kuishi maisha ya kumcha Mungu. Ni kwa kusalimisha maisha yetu kwa Kristo, mwenye uwezo wa kutakasa mawazo machafu kwa njia ya Roho mtakatifu. Ukristo ni kuunganishwa fikra zetu na nia zetu na Yesu Kristo, huko ndiko kuzaliwa upya. 

Wale wote waliompokea Kristo wanafanyika watoto wa Mungu, wanaoishi wakitii Amri za Mungu kwa uwezo wa Roho mtakatifu, wako huru na dhambi (uasi wa sheria). Soma: 1Yohana 3:4-9. Watoto wa Mungu, dhambi zao zinafutwa, na watakuwa na Mungu wakishiriki katika kazi ya kuwahukumu wadhambi waliokataa kuokolewa. Soma: 1korintho 6:1-3. Kufikia muda huu tukiwa hai, ni FULSA isiyopaswa kuipuuzwa, hebu kila mmoja afanye maamuzi ya kuondokana na AIBU NA KUDHALILISHWA katika siku isiyojulikana. 

NAWATAKIA MWAKA MPYA MWEMA WENYE MAFANIKIO NA BARAKA TELE. 

Na Ev. Eliezer Mwangosi - Simu: 0767210299.




Sent from Samsung tablet

Mashimba

unread,
Jan 3, 2016, 11:35:21 PM1/3/16
to eliezer mwangosi@yahoo. com, yourtruevine@googlegroups com, Mgedzi Deborah
Amina mtumishi.Tuenende katika hali ya upya

"eliezer.mwangosi" <eliezer....@yahoo.com> wrote:

NENO LA LEO - ANZA UPYA NA BWANA
Tafakari: 2 Wakorintho 5:17. "Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita ; tazama! yamekuwa mapya".

Kila mtu akipewa nafasi ya kuelezea hali ya maisha aliyoipitia ndani ya mwaka mzima wa 2015, kuna mengi tungeyasikia, mengine yatakuwa ya kufurahisha, mengine ya kusikitisha, mengine ya kukatisha tamaa n.k. Kila mtu amepitia hali fulani iliyo tofauti na mwenzie. Hata hivyo kwa neema ya Mungu yeyeto aliyefanikiwa kuusoma ujumbe huu, hana budi kumshukuru Mungu kwa kupatiwa nafasi tena kuuona mwaka 2016. 

Kuna watu mwaka 2015 umepita kama wako peponi, kila waliyoyapanga yalienda salama na afya zao zikiwa bila migogoro. Wengine hali zao zilikuwa nusu nusu, mara wako peponi mara majonzi. Kuna wengine mwaka mzima umekuwa majanga matupu, machungu yamekuwa mazito kiasi cha kutoona mazuri. Kuna watu wamejeruhiwa na kubaki mioyo yao ikiwa imejaa majeraha ambayo hawana matumaini ya kupona. 

Mpendwa; haijalishi umepitia maisha gani mwaka ulioisha, iwe ni furaha na baraka tele au maumivu ya kukatisha tamaa, haijalishi hali ya machungu ilipita au inaendelea, ziwe ni changamoto za magonjwa, iwe ni kuporomoka kwa biashara, iwe ni upweke, iwe ukata wa pesa, iwe ni kukosa ada ya shule au chuo, iwe ni kusalitiwa na umpendaye, iwe ni changamoto ya kisiasa kukosa cheo, iwe ni kuonewa, iwe ni kupitiwa na mikasa ya Rushwa n.k. Neno la leo linasema ANZA UPYA NA BWANA. 

Siri ya mafanikio na kuwa na maisha yenye matumaini milele, ni kuwa mikononi mwa Mungu. Hata dhoruba za maisha zikivuma, ndani ya Kristo ni salama. Kumbuka rafiki, maisha bila Mungu ni kujilisha upepo, utajiri na ukuu wa dunia hii bila Yesu ni maisha ya kubahatisha.

Amua sasa kuanza upya na Bwana, na hatimaye ukiri na kusema - YA KALE YAMEPITA, TAZAMA YAMEKUWA MAPYA. 

NAWATAKIA MWAKA MPYA WENYE BARAKA TELE ZA MUNGU NA MAISHA YENYE MATUMAINI. 

Na. Ev. Eliezer Mwangosi - Simu: 0767210299.




Sent from Samsung tablet

Mashimba

unread,
Jan 12, 2016, 1:06:04 AM1/12/16
to eliezer mwangosi@yahoo. com, yourtruevine@googlegroups com, Mgedzi Deborah
Amina mtumwa wa Bwana

"eliezer.mwangosi" <eliezer....@yahoo.com> wrote:

NENO LA LEO - ATHARI ZA MITANDAO KATIKA KIZAZI CHETU
Tafakari: Waefeso 6:11 "Vaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kuzipinga hila za Shetani".

Neno hila linaweza kueleweka vizuri kwa kutumia mfano wa wavuvi wa samaki, ambao wakitaka kumnasa samaki mkubwa kwa kutumia ndoano, wanaweka dagaa kwenye ndoano au wegine wanatumia vibati vidogo vinavyong'aa kwenye maji na kuonekana kama samaki mdogo. Mara zote samaki wakubwa wamenasa kwenye ndoano wakiwa wanameza samaki mdogo ambaye kwa ndani kuna ndoano. Mvuvi ametumia HILA kumnasa samaki kwa ulaghai wa kuweka doano ndani dagaa ili kumnasa samaki mkubwa.

Mtandao ni moja ya mtego hatari ambao shetani anautumia siku hizi kuwanasa vijana kwa wazee, wengi wamekuwa ni marehemu, waliokufa kiroho kwa sababu ya mitandao. Nakumbuka zamani wazazi wenye maadili walikuwa wanawakataza vijana wao wasiende kwenye majumba ya dansi na sinema, kwa kuogopa kuharibika tabia, katika kizazi hiki, majumba ya dansi na video hadi za ngono ziko mikononi na majumbani.

Siku hizi mahusiano mengi, hadi ya uchumba huanzia kwenye mtandao, udanganyifu mwingi unatendeka kwenye mitandao na wengi wananasa bila kujua, mvulana mmoja alipoteza muda mwingi wa uchumba na bibi kizee wa miaka 70 aliyekuwa ameweka picha yake ya urembo akiwa msichana kwenye Facebook. Wee kazana tu ku type "cuteee" mara "Sweetee" kumbe ni mwanaume kaweka picha na jina la mrembo kwenye profile yake, mtadanganywa hadi lini?.

Uchumba hadi ndoa vinavunjika kutokana na vijana wengi kuharibikiwa akili kwa sababu ya mazoea machafu kupitia mitadao. Utakuta vijana wanajisifia kwa kufanya ngono za mtandaoni (sex online), na wapenzi wao wanaofahamiana kwa picha, shetani ametega nyavu kwenye mtandao, roho chafu za mahaba zinawaunganisha wanaume kwa wanawake, ili wote wachafuliwe akili na kupagawa na mapepo ya Ngono. Mitandao imekuwa ni bahari yenye kubeba uchafu wa kila namna unaoifunika dunia yetu.

Vijana wengi wanapoteza muda kwa ku chat, mara FB, WhatsApp, twitter, instagram, imo, etc, ukifuatilia anachokifanya ni ku like ujumbe hata bila kuusoma na kuangalia picha au video. Kizazi hiki kinaendelea kujeruhiwa kwa vijana kutokuwa makini na masomo bila kusahau uzembe kazini. Muda mwingi unapotea ukitumika ku peruzi mambo yasiyo na tija katika maisha, wengi wanapoteza muda na mwisho inawagharimu.

Hata hivyo kwa upande mwingine mtandao ukitumika vizuri, una faida kubwa sana kwa maisha ya binadamu, neno la leo lisingewafikia wengi na kwa haraka pasingekuwepo mtandao. Ndio maana tafakari ya leo, inatujulisha jambo la kufanya ili mtandao uwe na faida kwetu kuliko hasara ambayo wengi wanaipata. Tunapaswa kuvaa silaha za Mungu ili tuweze kuzipinga HILA ZA SHETANI za kwenye mitandao. Silaha za Mungu ni kuruhusu uongozi wa Roho mtakatifu kutawala akili zetu daima.

MUNGU ATUJALIE HEKIMA NA MACHO YA KUONA MITEGO YA SHETANI KUPITIA MITANDAO.

NAWATAKIA SIKU NJEMA YENYE KUJAA MAFANIKIO NA BARAKA TELE

Na Ev. Eliezer Mwangosi - Simu: +255(0)767210299




Sent from Samsung tablet

Mashimba

unread,
Jan 13, 2016, 2:56:49 AM1/13/16
to eliezer mwangosi@yahoo. com, yourtruevine@googlegroups com, Mgedzi Deborah
Amina.Pia this hike kweli katika upendo

"eliezer.mwangosi" <eliezer....@yahoo.com> wrote:

NENO LA LEO - UWE MWAMINIFU HATA KUFA
Tafakari: Ufunuo 2:10 "Usiogope mambo yatakayokupata; tazama, huyo ibilisi atawatupa baadhi yenu gerezani ili mjaribiwe, nanyi mtakuwa na dhiki siku kumi. UWE MWAMINIFU HATA KUFA, nami nitakupa taji ya uzima".

Unabii huo ulikuwa juu ya kanisa la Kristo amgbalo katika nyakati mabalimbali limepitia mateso, hadi wengine kufikia kifo kwa ajiri ya Kristo. Hata leo tunashuhudia shetani akiwaangusha wengi katika majaribu na vitisho, na wengi wanaishia kuanguka na hatimaye kufa bila tumaini la uzima wa milele.

Je ni wangapi wapo tayari kupata hasara ya maisha haya kwa ajili ya msimamo wao kwa Mungu? Mara nyingi shetani anageuza mambo, anawaletea vijana wa kike na wa kiume, na watu wazima, mambo ambayo yanaonekana yanafaida katika maisha haya, wakati kwa vipimo vya Mbinguni ni Uovu unaoleta majuto milele. 

Nilisikia binti aliyekuwa amefumaniwa na mume wa mtu, akidai hawezi kumuacha, kwa sababu hana njia nyingine ya kuishi. Na wengine utasikia, "wanaume wa siku hizi hawaoi bila kukujua kimwili - zinaa", hata hivyo ndio kwanza tunashuhudia wachumba wanabwagwa kila kukicha. 

Vijana kwa wazee wanazidi kujeruhiwa na muovu shetani kwa udanganyifu wa kupata faida katika maisha ya dhambi, na mwisho wa yote wanaishia kutengwa na Mungu wao. Hata viongozi wa Dini wengi wanaishia kupotea kwa kujitafutia makundi kwa njia hata ya undanganyifu ili wapate fedha za kuendeshea maisha. Uizi, udanganyifu, utapeli, uongo ni tabia za kawaida maofisini, katika mahusiano, kwenye biashara, vyuoni n.k. Watu sio WAAMINIFU.

MUNGU ATUSAIDIE TUWE WAAMINIFU DAIMA, TUWE TAYARI KUFA KULIKO KUMKOSEA MUNGU.

MUNGU AWAPATIE SIKU NJEMA YENYE BARAKA TELE

Ev. Eliezer Mwangosi - Simu: 0767210299




Sent from Samsung tablet

Mashimba

unread,
Jan 21, 2016, 2:51:08 AM1/21/16
to eliezer mwangosi@yahoo. com, yourtruevine@googlegroups com, Mgedzi Deborah
Amina .Asante sana kwa kutukumbusha juu ya maisha ya ndoa namna Mungu anavyochukia wana ndoa wanapoishi nje ya utaratibu wake .Ndoa ni jambo la heshima kwa wana ndoa na watu wote.Tuziheshimu ndoa kama neno la Mungu linavyosema "Ndoa na iheshimiwe na watu wote,na malazi yawe safi kwa maana waasherati na wazinzi Mungu atawahukumia adhabu .Waebrania13:4"

Bwana akubariki


"eliezer.mwangosi" <eliezer....@yahoo.com> wrote:

NENO LA LEO - MUNGU ANACHUKIA KUACHANA
Tafakari: Malaki 2:15-16 "..... Kwa hiyo jihadharini roho zenu; mtu awaye yote asimtende mke wa ujana wake mambo ya hiana. Maana mimi nakuchukia kuachana, asema BWANA...."

Hili ni agizo la Bwana kwa wote walio Katika NDOA, walio katika fungate la Uchumba, wanaotafuta wachumba, na wale ambao tayari wameachana. Kuachana ni dhambi inayomchukiza Mungu, kizazi chetu kimejaa wahanga wa dhoruba hii ya kuachana kwa sababu ya Ndoa nyingi kuanzishwa katika misingi mibovu. Sababu nyingine ni wanandoa kutojisalimisha kwa Mungu ili atawale muungano wao. 

Ndoa ni taasisi iliyoanzishwa na Mungu kabla ya dhambi,  ipo kwa ajili ya utukufu wa Mungu, ndoa kwa asili ni muungano wa kiroho kati ya watu wawili, kwa ajili ya kuwa mawakili wa Mungu. Ndio maana shetani anapiga vita, na kurusha mishale yenye sumu za kila namna, kuhakikisha ndoa zinakuwa ndoano, au zisitimize kusudi la Mungu. 

Ninawaasa vijana, mruhusu Mungu awaongoze na kuwapatia wenzi wema, acheni kurukia rukia, na kudakwa dakwa kama mipila, acheni kuwa na wachumba mnawaowakubali huku mnao wengine, acheni udanganyifu, UPENDO na uwe wa kweli uliojengwa na Mungu. 

Wenye ndoa, bila kujali mwanzo wenu, salimisheni ndoa zenu kwa Mungu, ili azilinde na mishale ya Adui. Wale wanaopanga kuwasaliti wenzi wao, kwasababu zozote zile wasifanye hivyo. Mruhusu Mungu aingilie kati kila changamoto, kwake yote yanawezekana. 

Walio watelekeza wenzi wao na kujiegesha kwa vijumba hasara, bila kusahau ma suger mam, wanao hujumu ndoa zao kwa kufuga vi serengeti boys,  waache mara moja kabla hasira ya Bwana kuwaka juu yao na kulipa kisasi. 

NAWATAKIA WOTE SIKU NJEMA YENYE MAFANIKIO NA BARAKA TELE. 

Na. Ev. Eliezer Mwangosi - 0767210299. 




Sent from Samsung tablet

Mtoka James

unread,
Jan 21, 2016, 3:11:12 AM1/21/16
to yourtr...@googlegroups.com

Amen  mubarikiwe

--
Reply all
Reply to author
Forward
0 new messages