Maombi ni ushiriki wa mtu na Muumba wake.Ni hali ya kiroho zaidi ya hali ya mwili.Ni hali ya kuamini Mungu zaidi kwa kutaja mahitaji yetu.Maombi ni njia tunayopata kuungana na Mungu kwa namna ya Roho.Maombi kwa wakati mwingine yanaonekana ni kama adhabu kwa baadhi ya Wakristo na kupelekea watu kufanya sala fupi wakati wa chakula, wakati wa usiku(wanapo taka kulala), asubuhi na wakati wanapokuwa kanisani au kwenye mikutano ya dini.Tunaona waziwazi wanafunzi wake Yesu wakati Yeye akiwa anasali Bustanini Gethsemane huku wanafunzi wake wakishindwa kukesha pamoja naye katika maombi hata saa moja.Tunaposhindwa kufanya maombi ya hata muda kidogo kwa siku tunampa nafsi shetani ya kutushambulia utakatifu wetu, uchumi wetu, afya zetu na hata kutuingiza majaribuni.
Yesu aliwaambia wanafunzi wake na sisi tudumu katika maombi ili tusije tukaingia kwenye tamaa za dunia hii.Neno la Mungu linasema 'Kesheni na kusali ili msije mkaingia katika majaribu.Roho iradhi lakini mwili ni dhaifu'Mathayo 26:41
Kanuni muhimu katika kuomba kwa Mkristo yoyote kwanza ni kuomba toba kabla ya kutaja mahitaji ya kuombea na pia kuwa na imani kwamba tunachoomba Mungu atatupatia kwa mapenzi yake(Mathayo11:24-25 - Kwa hiyo nawaambieni, mnaposali na kuomba kitu aminini kwamba mnakipokea nanyi mtapewa.Mnaposimama katika kusali, msameheni kila mtu aliyewakosea chochote, ili Baba yenu aliye mbinguni awasamehe nyinyi makosa yenu).
Katika hali ya sasa Wakristo wengi wamejikuta katika hali ya kukata tamaa kimwili na kiroho pia, na hadi kusabisha neno MAOMBI kwao kuwa ni kama mzigo au kuwa hayana umuhimu kwao au maombi ni ya akina fulani tu kanisani.Na wapo Wakristo wengine hawajali kabisa kuomba.Lakini Neno la Mungu linatuambia maombi ni silaha ya Mungu ya kutuwezesha kuyapinga mashamubulizi dhidi ya jeshi ovu la ulimwengu wa roho na ya watawala wakuu wa giza.Tunasoma Neno la Mungu katika waraka wa Mtume Paulo kwa Waefeso ' Salini daima, mkiomba msaada wa Mungu.Salini kila wakati kwa nguvu ya Roho.Salini bila kuchoka mkisali kwa ajili ya watu wote wa Mungu.'Efeso 6:18
Maombi yana tusaidia kujiweka tayari kwa siku ya mwisho.Tunasoma katika maandiko matakatifu kuwa 'Mwisho wa vitu vyote umekaribia, kwa hiyo mnapaswa kuwa na utaratibu na kukesha ili muweze kusali'1Petro4:7
Maombi ni alama ya ushindi ya kuonyesha kuwa sisi tuwategemezi wa Mungu.Mfalme Daudi alimulilia BWANA (Zab22:1-4 .....Waezee wetu walikutegemea nawe ukawaokoa)
Mpendwa tuombe Mungu kwa neema yake atupe nguvu na msaada ili tudumu katika maombi na kumshukuru Mungu kwa kila jambo.Neno la Mungu linasema 'Msiwe na wasiwasi juu ya kitu chochote ila kwa kila hali mwombeni Mungu katika sala juu ya mahitaji yenu kwa shukrani'.Filipi 4:6.
Mpendwa napenda kukushirikisha kwa juma linaloanza kesho tuombe kila siku juu ya mahitaji yafuatayo.
Ikiwa njaa katika nchi, au tauni au ukosefu wa mvua, au ukungu au nzige au panzi,au ikiwa watu wako wamezingirwa na adui zao katika mji wao wowote ule au yakiwa mapingo mengine yoyote au ugonjwa wowote, tafadhali usikie maombi yoyote yaatakayoombwa na mtu yeyote au watu wako wote Israeli, watakaojua kila mtu pigo lake mwenyewe na maumivu yake mwenyewe, akinyoshea nyumba hii mikono yake basi usikie kule mbinguni, pahali unapokaa , usamehe na kurudishia kila mtu kwa kadiri ya njia zake zote, wewe unayejua moyo(Kwa sababu wewe ndiwe mwenye kujua mioyo ya wanadamu wote).Ili wakuogope wewe(watakutii), waende katika njia zako siku zote watakazoishi katika nchi ambayo uliwapa baba zetu. 2 Nyakati 6:28-31