MOYO WAKO USIWAZE MABAYA

133 views
Skip to first unread message

Bahati Mashimba

unread,
Apr 18, 2012, 2:49:19 AM4/18/12
to yourtr...@googlegroups.com
Bwana akaona ya kuwa maovu ya mwanadamu ni makubwa duniani na kwamba kila kusudi analowaza moyoni mwake ni baya tu siku zote (Mwanzo 6:5)

Kusudi kuu la Mungu kumuumba mtu kwa mfano wa sura yake ilikuwa ni kumfanya  binadamu  aweze  kuwaza mema daima, amiliki na kutawala dunia kwa niaba ya Mungu. Adamu na Hawa hawakuwahi kuwaza mabaya kabla ya kuasi.Uwezo huo ulipotea wakati Adamu na Hawa waliposhindwa  kushika makusudi ya Mungu na kukubali jaribu la nyoka lililotoka nje ya miili yao hadi wakala tunda la mti wa ujuzi wa mema na mabaya(Mwenyezi Mungu akamuuliza (Adamu) ' Nani aliyekuambia kwamba uko uchi?Je, umekula tunda la mti nililokuamuru usile?' Mwanzo 3:11). Mungu anasikitika  na kuhuzunika sana anapoona mwanadamu kila siku anawaza mabaya na kutamani kuyatenda.

Tunapomwamini Yesu Kristo tunapewa Roho mpya inayotuwezesha kusulubisha mawazo mabaya na tamaa za dunia hii.Watu wanapokataa kumtambua Mungu na kuruhusu Roho Mtakatifu kukaa ndani yao matokeo yake ni kuruhusu fikira potuvu zilizojaa kila aina ya uovu, dhuluma, ulafi, ufisadi, wivu, uuaji,ugomvi, udanganyifu, majivuno,kutotimiza ahadi, kukosa wema wala  huruma kwa wengine na mambo mengine yote  yanayofanana na hayo.

Mwamini Yesu na ukae ndani yake  ili uelee juu ya  makusudi ya Mungu na utaokoka kama Nuhu na ndugu zake walivyoelea juu ya maji wakiwa ndani ya Safina wakati wa gharika .

Nawatakia wote neema ya Mungu iwe juu yenu.

Wale walio na Kristo wameisulubisha hali yao ya kidunia pamoja na mawazo yake mabaya na tamaa zake.Wagalatia 5:24

MaryGlady Heri

unread,
Apr 18, 2012, 3:10:46 AM4/18/12
to yourtr...@googlegroups.com
Asante sana nimebarikiwa na neno lako!

2012/4/18 Bahati Mashimba <bahat...@yahoo.com>

--
Mkikaa ndani yangu na maneno yangu yakikaa ndani yenu basi ombeni chochote mtakacho nanyi mtapewa.Yohana15:7

Maki Samy

unread,
Apr 18, 2012, 9:16:23 AM4/18/12
to yourtr...@googlegroups.com
Asante kwa neno la ufalme

Bahati Mashimba

unread,
Apr 18, 2012, 9:22:41 AM4/18/12
to yourtr...@googlegroups.com
Asanteni.Jina la Bwana lipewe sifa.


--- On Wed, 4/18/12, MaryGlady Heri <mgl...@gmail.com> wrote:
Reply all
Reply to author
Forward
0 new messages