MWABUDU MUNGU KATIKA ROHO NA KWELI

7,283 views
Skip to first unread message

Bahati Mashimba

unread,
Sep 5, 2011, 11:58:38 AM9/5/11
to yourtr...@googlegroups.com
 ‘Lakini saa inakuja, nayo saa ipo, ambayo waabuduo halisi watamwabudu Baba katika roho na kweli.Kwa maana Baba awatafuta watu kama hao wamwabudu.Mungu ni Roho nao mwabuduo yeye imewapasa Kumwabudu katika roho na kweli’ Yohana4:23-24

Makusudi ya injili ya Yohana
ni ili tupate kuamini ya kwamba Yesu ndiye Kristo, Mwana wa Mungu, na kwa kuamini tuwe na Uzima kwa jina lake (Yohana20:31)
 
Katika mazungumzo yake Yesu alimwambia mwanamke Msamaria amsaidiki yeye na kwamba saa inakuja nayo saa ipo ambayo watu hawatamwabudu Baba (Mungu) katika Mlima wala kule Yerusalemu bali watamwabudu katika roho na kweli kwa kuwa yeye ni Roho.
 
Kuabudu ni kuonyesha thamani, heshima,upendo,utii,shukrani,sifa,kuomba,kubariki,kuonyesha furaha na  unyenyekevu na moyo wa kupondeka  katika kumtumikia  na kutambua ukuu wa Mungu wetu.Tunamwabudu Mungu kwa sababu yeye ni Muumbaji wa vitu vyote, ni Mkuu, kazi zake ni za kushangaza, ni Mungu wetu aliye hai na aliyeumba vitu vyote. Na imeandikwa tumsujudie Bwana Mungu wetu na tumwabudu yeye peke yake (Luka4:8). Asili ya kumwabudu Mungu inataka tumsujudie kwa roho zetu na kweli mbele yake katika hali ya unyenyekevu na kupondeka na yeye aweze kutunyanyua.Biblia inasema katika Yakobo4:10Mujinyenyekeze mbele ya BWANA naye atawanyanyua ninyi’.
 
Mungu ni Roho
Mungu ni Roho yaani, Mungu, Baba, Mwana, na Roho Mtakatifu. Mungu ni Roho, na si mwili yeye hana mwanzo wala mwisho. Tunapokea Roho wa Mungu ndani ya roho zetu wakati tunapo amini Yesu Kristo na kuzaliwa upya katika roho zetu kwa maji na kwa Roho (Yohana3:6 – Kilichozaliwa kwa mwili ni mwili na kilichozaliwa kwa Roho ni roho).Roho Mtakatifu hufanya kazi ya kuwasiliana kati ya roho zetu na Mungu.Mungu hutupa pumzi ya uzima katika roho zetu na pia akili zetu hutokana na pumzi ya Mungu (Ayubu32:8-pia imo roho ndani ya mwanadamu na pumzi ya Mwenyezi Mungu huwapa akili). Pia sisi hatukuipokea roho ya dunia bali Roho atokaye kwa Mungu, makusudi tupate kuyajua tuliyokirimiwa na Mungu (1Korintho2:12)
 
Kumwabudu Mungu katika Roho
 Mungu ametufunulia sisi wakristo kwa Roho ili tumwabudu kutoka ndani ya roho zetu, akili zetu, nguvu zetu.Katika Waefeso Efeso1:17 inasemaMungu ametupa roho ya hekima ya ufunuo katika kumjua yeye’ na pia  Roho ndiye ashuhundiaye  kwamba tunamtumikia Mungu katika kweli yake kwa sababu Roho ndiye kweli(1Yoh5:7).
 Kuabudu kwa Roho ni lazima roho zetu na mawazo yetu, tabia na matendo yetu yabadilishwe na tuweze kumpa sifa, heshima,utukufu,kumshukuru,kuomba,kuhubiri, kutoa, na mambo yote yanayohusu kujitoa kwa ajili ya kazi ya Mungu wetu. Lengo la kumwabudu Mungu ni kuonyesha ukuu wake Mungu na tunavyo mthamini katika maisha yetu. Kuabudu kwetu lazima kuonyesha uaminifu wetu kwa Mungu kwa sababu ya neema yake katika kumtoa Mwanae Yesu Kristo ili awe Mwokozi wa maisha yetu.
 Watu wengi hukosa lengo linapokuja suala la kuabudu Mungu.Mara nyingi tumechoshwa na ibada zetu za kanisani siku ya jumpili, katikati ya wiki, nyumbani, kazini, safarini, shambani, kwenye biashara na sehemu zote ambazo tunaweza kuwa tunafanya shughuli zetu za kila siku.Wakati mwingine tumechoka kuwahi kufika kwenye ibada zetu na pia kuna wakati wa kuimba nyimbo za kusifu au kuabudu tunarudia maneno bila kujua maana. Hii yote ni kwasababu roho zinakuwa hazijatawaliwa na Roho wa Mungu.Tunapomwabudu katika Roho tunaonyesha kuwa roho zetu zinamekubali kuzaliwa upya.Neno la Mungu linasema katika Wafilipi 3:3 ‘ Maana sisi tu tohara tumwabuduo Mungu kwa Roho na kuona fahari juu ya Kristo Yesu, wala hatuutumainii mwili’.
Tunapozaliwa mara ya pili Mungu ambaye ni Roho hutufanya tuwe hekalu lake.Na kwa kuwa sisi tumekuwa hekalu la Mungu na Roho wa Mungu hukaa ndani yetu (1Korintho3:16), ni lazima roho zetu zimsifu na kumtukuza Mungu kwa roho ya upendo, furaha, uaminifu. Mungu ni mmoja ambaye ana hatima yetu ya maisha yetu katika mikono yake. Wafilipi 2:12 inatuambia, ‘utimizeni wokovu wenu wenyewe kwa kuogopa na kutetemeka.’ Wokovu wetu ni jambo kubwa sana na wala halikutokea kwa bahati mbaya. Lazima tuheshimu Mungu kwa kuogopa na kutetemeka ndani ya roho zetu tunapomwabudu na kumtumikia. Wokovu wetu unategemea juu ya kama ibada zetu ni za kumpendeza Mungu au la.
 
 Kumwabudu Mungu katika Kweli
Lazima tumwabudu Mungu katika kweli. Neno ni Mungu na neno lake ni kweli. Wakristo ni lazima kumwabudu kulingana na neno lake. Hapa Bwana anatueleza kuwa lazima neno lake tulijue ili lituweke huru na litutakase maisha yetu ya kiroho na kimwili tuwe safi. Kuabudu katika kweli ni kuamini neno la Mungu na kuwa huru kifira kwa kuondoa maneno yote yasiyo mpendeza Mungu.
 
Tumwabudu kwa kujitoa mioyo, roho na nguzu zetu kwake huku tukiwa tumetakaswa na Neno lake kwa sababu ya ile kweli tuliyokwisha kuipokea. Tunapolishika neno la Mungu linatutakasa na kutufanya tuwe safi na hapo ndipo tunaweza kumwabudu Mungu tukiwa wasafi maana yeye ni Mtakatifu. Neno la Mungu linasema katika Yoh17:17Uwatakase kwa ile kweli neno lako ndiyo kweli’. Pia neno la Mungu tunapolishika linatufanya tuifahamu kweli yake (Yohana8:32 – Tena mtaifahamu kweli nayo kweli itawaweka huru).
Kwa kuamini injili ya wokovu katika Kristo ambaye yeye ni kweli, hema ya Mungu, tunapata kuishi na Kristo ndani yetu ambaye yeye ni Mungu. Kwahiyo ni lazima tunapoabudu Mungu tuwe wa kweli katika njia zetu na wakamilifu wa nafsi kwa kujitakasa katika neno lake.Tukishika neno la Mungu litatuweka huru na kuwa mbali na dhambi.
Mungu anaona uzuri wa kuabudiwa katika namna ile, ‘kwa roho na kweli’ ndiyo maana anasema anawatafuta wanaomwabudu katika roho na kweli. Hasemi tunaweza kumwabudu Mungu kwa namna tunayotaka sisi.
 
Adui wa mkristo katika kuabudu Mungu
 
1.Shetani- Shetani ni adui yetu mkubwa na hupenda kuona watu wa dunia hii wa kimtukuza yeye kwa kuwajaribu na fahari za dunia hii na kukamata muda wao ili waone mahitaji ya mwili ni muhimu sana kuliko kumtumikia Mungu wa kweli.Tunaona namna shetani alipomjaribu Yesu kwa kumpandisha juu na kumwonyesha miliki zote za dunia  na atampa zote ikiwa atamsujudia (Luka4:6-7- Ibilisi akamwambia Nitakupa wewe Enzi hii yote na fahari yake kwa kuwa imo mikonani mwangu nami humpa ye yote kama nipendavyo.Basi wewe ukisujudu mbele yangu yote yatakuwa yako)
 
2. Mwili - Mara nyingi mwili hupingana na roho kwa kuleta vishawishi vya kufanya lile ambalo hupendi kulitenda.Ndiyo maana utakuta wakristo wengi siyo watendaji wa Neno.Mtume Paulo alilia kwa sababu ya mwili  wa mauti(Roma7:18 Kwa maana najua ya kuwa ndani yangu, yaani ndani ya mwili wangu, halikai neno jema, kwa kuwa kutaka nataka bali kutenda lililo jema sipati)
 
3.Kujivuna - Watu wengi wamejaa majivuno,viburi na njia mbovu kiasi kwamba hawana muda na hawezi kuona thamani ya kujitoa kwa Mungu aliyewaumba katika kumwabudu kwa unyenyekevu.Mungu anachukia kiburi,majivuno,uovu,kinywa cha ukaidi pia anakichukia(Mithali8:13)
 
4. Mapokeo- Kuna wakristo wengi wanendelea kuabudu mapokeo ya dini na wanashindwa kuabudu Mungu katika njia ya kweli kwa sababu ya upofu wao katika kuijua Habari Njema (1Korintho2:14) 
 
Mungu anapenda tumwabudu katika roho na kweli namna ambayo yamfaa Mungu.Maisha yetu yaonyeshe kwa mataifa kuwa tunamtegemea Mungu na kuweka imani ndani yake-kwamba yeye amefanya kila lililopendeza duniani  na mbinguni, na yeye ndiye anayestahili kuheshimiwa.Yeye ndiye nguvu yetu na msaada wetu katika maisha yetu.Tusiabudu watu,kazi,mali,dhehebu,siku,sikukuu,sanamu au chochote kile bali tumwabudu  Mungu katika roho na kweli  ambayo ni njia pekee tunayoweza kumpendeza Mungu wetu katika maisha yetu ya sasa na mwisho wake tupate uzima wa milele.
 
 
Nawapenda wale wanipendao,Na wale wanitafutao kwa bidii wataniona Mitahli8:17
 

Warema S.Senzia

unread,
Sep 5, 2011, 12:37:45 PM9/5/11
to yourtr...@googlegroups.com
Ndugu nakusalimu katika jina la KRISTO. Asante kwa waraka wako huu. Umenifunza mengi.
Napenda niongeze katika somo lako lililo jema, YESU alipomwambia mwanakme Msamaria kuwa saa yaja ambayo wamwabuduo MUNGU halisi wataabudu katika roho na kweli. Kabla ya YESU kutoa maneno au mafunzo haya mwanamke alitambua ya kuwa yeye ndiye masia lakini  anamwauliza YESU '..Babu zetu waliabudu katika milima hii ila nyie Wayahudi mwaabudu Yerusalam' mwanake anatambua historia kuwa walikua wakiabudu katika milima ya Samaria, na pale walipo ni katika kisima cha Yakobo ambaye wote wanamtambua kama babu yao, hivyo anajaribu kumshawishi YESU kua nyie Wayahudi hamtendi lililo sahihi,kwa kua wayahudi baada ya Mfalme Sulemani kujenga hekalu la Yerusalem na kuliweka wakifu, sanduku la agano likawekwa humo basi ibada zote zikawa zafanyika Yerusalemu na hata kusali kuelekea huko Yeruslameu Na ni kama ambavyo leo watu huambiana kuwa kanisa (dhehebu) lenu hamfanyi hivi na vile. Lakini YESU akamjibu kuwa waabuduo halisi hawataabudu katika Yerusalemu au milima ya Samaria au Pentecoste,au Sabato au Catholic au Lutheran n.k  ila wataabudu katika roho na kweli.
KUABUDI KATIKA ROHO.
Roho siku zote yapenda yaliyo mema ila mwili mara nyingi huwa tofauti, .... hata YESU alipokua akikaribia kikombe alisema ..Roho i radhi ila mwili ni dhaifu. Yaani mara zote roho ipo tayari kutenda yaliyo mema ila mwili huwa dhaifu. Sasa waabuduo halisi wataongozwa na matendo ya rohoni na sio matendo ya mwili. Watatenda yaliyo sahihi kama roho alivovuvia,tena hawataangalia kama ni wa mlimani au Yerusalem. Mwili ni hekalu la roho Mtakatifu, sasa kwa kufuuta matendo ya roho ni kuruhusu roho wa MUNGU akae kwako afanye hekalu na kukuongoza katika kweli yote.
 
KUABUDU KATIKA KWELI.
Biblia yasema neno langu ni kweli, alafu inasema  "... mtaifahamu kweli nayo ile kweli itawaweka huru" sasa kuabudu katika kweli ni kufuata neno la MUNGU ambalo ndio ile kweli, na hilo neno litakuweka uwe huru, utakua huru toka katika jela ya shetani, uhuru wa moyo na amani ya kweli, uhuru toka tamaduni za dini na mafundisho ya binadamu kama walivofanya Wayahudi na hata leo baadhi ya Wakristo wakifuata tamaduini na mafundisho yaliyo ya binadamu. Na unakuwa huru na dhambi kwa kuwa damu aya YESU kristo imekuweka huru.
 
Mchango wangu mdogo leo kwa mara ya kwanza, katika truevine.
 
MUNGU ABARIKI KAZI YAKE NA AREJEE ATUTWAE TWENDE NAYE KATIKA YERUSALEMU MPYA.
 
"...Surely goodness and love will follow me
all the days of my life, and I'll dwell in the house of the LORD forever"
 

From: Bahati Mashimba <bahat...@yahoo.com>
To: "yourtr...@googlegroups.com" <yourtr...@googlegroups.com>
Sent: Monday, September 5, 2011 5:58 PM
Subject: MWABUDU MUNGU KATIKA ROHO NA KWELI

 ‘Lakini saa inakuja, nayo saa ipo, ambayo waabuduo halisi watamwabudu Baba katika roho na kweli.Kwa maana Baba awatafuta watu kama hao wamwabudu.Mungu ni Roho nao mwabuduo yeye imewapasa Kumwabudu katika roho na kweli’ Yohana4:23-24

Makusudi ya injili ya Yohana
ni ili tupate kuamini ya kwamba Yesu ndiye Kristo, Mwana wa Mungu, na kwa kuamini tuwe na Uzima kwa jina lake (Yohana20:31)
 
Katika mazungumzo yake Yesu alimwambia mwanamke Msamaria amsaidiki yeye na kwamba saa inakuja nayo saa ipo ambayo watu hawatamwabudu Baba (Mungu) katika Mlima wala kule Yerusalemu bali watamwabudu katika roho na kweli kwa kuwa yeye ni Roho.
 
Kuabudu ni kuonyesha thamani, heshima,upendo,utii,shukrani,sifa,kuomba,kubariki,kuonyesha furaha na  unyenyekevu na moyo wa kupondeka  katika kumtumikia  na kutambua ukuu wa Mungu wetu.Tunamwabudu Mungu kwa sababu yeye ni Muumbaji wa vitu vyote, ni Mkuu, kazi zake ni za kushangaza, ni Mungu wetu aliye hai na aliyeumba vitu vyote. Na imeandikwa tumsujudie Bwana Mungu wetu na tumwabudu yeye peke yake (Luka4:8). Asili ya kumwabudu Mungu inataka tumsujudie kwa roho zetu na kweli mbele yake katika hali ya unyenyekevu na kupondeka na yeye aweze kutunyanyua.Biblia inasema katika Yakobo4:10Mujinyenyekeze mbele ya BWANA naye atawanyanyua ninyi’.
 
Mungu ni Roho
Mungu ni Roho yaani, Mungu, Baba, Mwana, na Roho Mtakatifu. Mungu ni Roho, na si mwili yeye hana mwanzo wala mwisho. Tunapokea Roho wa Mungu ndani ya roho zetu wakati tunapo amini Yesu Kristo na kuzaliwa upya katika roho zetu kwa maji na kwa Roho (Yohana3:6 – Kilichozaliwa kwa mwili ni mwili na kilichozaliwa kwa Roho ni roho).Roho Mtakatifu hufanya kazi ya kuwasiliana kati ya roho zetu na Mungu.Mungu hutupa pumzi ya uzima katika roho zetu na pia akili zetu hutokana na pumzi ya Mungu (Ayubu32:8-pia imo roho ndani ya mwanadamu na pumzi ya Mwenyezi Mungu huwapa akili). Pia sisi hatukuipokea roho ya dunia bali Roho atokaye kwa Mungu, makusudi tupate kuyajua tuliyokirimiwa na Mungu (1Korintho2:12)
 
Kumwabudu Mungu katika Roho
 Mungu ametufunulia sisi wakristo kwa Roho ili tumwabudu kutoka ndani ya roho zetu, akili zetu, nguvu zetu.Katika Waefeso Efeso1:17 inasemaMungu ametupa roho ya hekima ya ufunuo katika kumjua yeye’ na pia  Roho ndiye ashuhundiaye  kwamba tunamtumikia Mungu katika kweli yake kwa sababu Roho ndiye kweli(1Yoh5:7).
 Kuabudu kwa Roho ni lazima roho zetu na mawazo yetu, tabia na matendo yetu yabadilishwe na tuweze kumpa sifa, heshima,utukufu,kumshukuru,kuomba,kuhubiri, kutoa, na mambo yote yanayohusu kujitoa kwa ajili ya kazi ya Mungu wetu. Lengo la kumwabudu Mungu ni kuonyesha ukuu wake Mungu na tunavyo mthamini katika maisha yetu. Kuabudu kwetu lazima kuonyesha uaminifu wetu kwa Mungu kwa sababu ya neema yake katika kumtoa Mwanae Yesu Kristo ili awe Mwokozi wa maisha yetu.
 Watu wengi hukosa lengo linapokuja suala la kuabudu Mungu.Mara nyingi tumechoshwa na ibada zetu za kanisani siku ya jumpili, katikati ya wiki, nyumbani, kazini, safarini, shambani, kwenye biashara na sehemu zote ambazo tunaweza kuwa tunafanya shughuli zetu za kila siku.Wakati mwingine tumechoka kuwahi kufika kwenye ibada zetu na pia kuna wakati wa kuimba nyimbo za kusifu au kuabudu tunarudia maneno bila kujua maana. Hii yote ni kwasababu roho zinakuwa hazijatawaliwa na Roho wa Mungu.Tunapomwabudu katika Roho tunaonyesha kuwa roho zetu zinamekubali kuzaliwa upya.Neno la Mungu linasema katika Wafilipi 3:3 ‘ Maana sisi tu tohara tumwabuduo Mungu kwa Roho na kuona fahari juu ya Kristo Yesu, wala hatuutumainii mwili’.
Tunapozaliwa mara ya pili Mungu ambaye ni Roho hutufanya tuwe hekalu lake.Na kwa kuwa sisi tumekuwa hekalu la Mungu na Roho wa Mungu hukaa ndani yetu (1Korintho3:16), ni lazima roho zetu zimsifu na kumtukuza Mungu kwa roho ya upendo, furaha, uaminifu. Mungu ni mmoja ambaye ana hatima yetu ya maisha yetu katika mikono yake. Wafilipi 2:12 inatuambia, ‘utimizeni wokovu wenu wenyewe kwa kuogopa na kutetemeka.’ Wokovu wetu ni jambo kubwa sana na wala halikutokea kwa bahati mbaya. Lazima tuheshimu Mungu kwa kuogopa na kutetemeka ndani ya roho zetu tunapomwabudu na kumtumikia. Wokovu wetu unategemea juu ya kama ibada zetu ni za kumpendeza Mungu au la.
 
 Kumwabudu Mungu katika Kweli
Lazima tumwabudu Mungu katika kweli. Neno ni Mungu na neno lake ni kweli. Wakristo ni lazima kumwabudu kulingana na neno lake. Hapa Bwana anatueleza kuwa lazima neno lake tulijue ili lituweke huru na litutakase maisha yetu ya kiroho na kimwili tuwe safi . Kuabudu katika kweli ni kuamini neno la Mungu na kuwa huru kifira kwa kuondoa maneno yote yasiyo mpendeza Mungu.
 
Tumwabudu kwa kujitoa mioyo, roho na nguzu zetu kwake huku tukiwa tumetakaswa na Neno lake kwa sababu ya ile kweli tuliyokwisha kuipokea. Tunapolishika neno la Mungu linatutakasa na kutufanya tuwe safi na hapo ndipo tunaweza kumwabudu Mungu tukiwa wasafi maana yeye ni Mtakatifu. Neno la Mungu linasema katika Yoh17:17Uwatakase kwa ile kweli neno lako ndiyo kweli’. Pia neno la Mungu tunapolishika linatufanya tuifahamu kweli yake (Yohana8:32 – Tena mtaifahamu kweli nayo kweli itawaweka huru).
Kwa kuamini injili ya wokovu katika Kristo ambaye yeye ni kweli, hema ya Mungu, tunapata kuishi na Kristo ndani yetu ambaye yeye ni Mungu. Kwahiyo ni lazima tunapoabudu Mungu tuwe wa kweli katika njia zetu na wakamilifu wa nafsi kwa kujitakasa katika neno lake.Tukishika neno la Mungu litatuweka huru na kuwa mbali na dhambi.
Mungu anaona uzuri wa kuabudiwa katika namna ile, ‘kwa roho na kweli’ ndiyo maana anasema anawatafuta wanaomwabudu katika roho na kweli. Hasemi tunaweza kumwabudu Mungu kwa namna tunayotaka sisi.
 
Adui wa mkristo katika kuabudu Mungu
 
1.Shetani- Shetani ni adui yetu mkubwa na hupenda kuona watu wa dunia hii wa kimtukuza yeye kwa kuwajaribu na fahari za dunia hii na kukamata muda wao ili waone mahitaji ya mwili ni muhimu sana kuliko kumtumikia Mungu wa kweli.Tunaona namna shetani alipomjaribu Yesu kwa kumpandisha juu na kumwonyesha miliki zote za dunia  na atampa zote ikiwa atamsujudia (Luka4:6-7- Ibilisi akamwambia Nitakupa wewe Enzi hii yote na fahari yake kwa kuwa imo mikonani mwangu nami humpa ye yote kama nipendavyo.Basi wewe ukisujudu mbele yangu yote yatakuwa yako)
 
2. Mwili - Mara nyingi mwili hupingana na roho kwa kuleta vishawishi vya kufanya lile ambalo hupendi kulitenda.Ndiyo maana utakuta wakristo wengi siyo watendaji wa Neno.Mtume Paulo alilia kwa sababu ya mwili  wa mauti(Roma7:18 Kwa maana najua ya kuwa ndani yangu, yaani ndani ya mwili wangu, halikai neno jema, kwa kuwa kutaka nataka bali kutenda lililo jema sipati)
 
3.Kujivuna - Watu wengi wamejaa majivuno,viburi na njia mbovu kiasi kwamba hawana muda na hawezi kuona thamani ya kujitoa kwa Mungu aliyewaumba katika kumwabudu kwa unyenyekevu.Mungu anachukia kiburi,majivuno,uovu,kinywa cha ukaidi pia anakichukia(Mithali8:13)
 
4. Mapokeo- Kuna wakristo wengi wanendelea kuabudu mapokeo ya dini na wanashindwa kuabudu Mungu katika njia ya kweli kwa sababu ya upofu wao katika kuijua Habari Njema (1Korintho2:14) 
 
Mungu anapenda tumwabudu katika roho na kweli namna ambayo yamfaa Mungu.Maisha yetu yaonyeshe kwa mataifa kuwa tunamtegemea Mungu na kuweka imani ndani yake-kwamba yeye amefanya kila lililopendeza duniani  na mbinguni, na yeye ndiye anayestahili kuheshimiwa.Yeye ndiye nguvu yetu na msaada wetu katika maisha yetu.Tusiabudu watu,kazi,mali,dhehebu,siku,sikukuu,sanamu au chochote kile bali tumwabudu  Mungu katika roho na kweli  ambayo ni njia pekee tunayoweza kumpendeza Mungu wetu katika maisha yetu ya sasa na mwisho wake tupate uzima wa milele.
 
 
Nawapenda wale wanipendao,Na wale wanitafutao kwa bidii wataniona Mitahli8:17
 
--
Usikubali kushindwa na ubaya bali ushinde ubaya kwa wema.Waroma12:21


Bahati Mashimba

unread,
Sep 6, 2011, 2:58:28 AM9/6/11
to yourtr...@googlegroups.com
Amina.Warema ubarikiwe sana kwa mchango wako mkubwa katika kufafanua juu ya njia sahihi ya kumwabudu Mungu wetu.Mchango wako  naamini utabariki watu wengi na pia  utaendeleza kukuza  roho zetu.Kwa kuwa miili yetu ni hekalu la Mungu na Yesu ndiye kuhani mkuu basi tuitoe miili yetu iwe dhabihu iliyo hai takatifu ya kumpendeza Mungu.
Nakutakia siku njema na BWANA AKUBARIKI.
 
 NEEMA YA BWANA WETU YESU KRISTO NA IWE PAMOJA NA ROHO ZETU.AMINA
 Humble yourselves in the sight of the Lord and he shall lift you up James4:10

Deborah Mgedzi

unread,
Sep 6, 2011, 3:25:46 AM9/6/11
to yourtr...@googlegroups.com
Asante sana Bahati na Warema. Somo hili litanisaidia zaidi wakati wa kipindi cha fellowship na pia nimewapa na wapendwa wengine. Mmbarikiwe sana. Zawadi yangu ni kutoka Zaburi 91 - MUNGU MLINZI WETU - INAPENDEZA SANA KAMA UTASOMA ZABURI HII KILA SIKU PAMOJA NA KUMB. 6:4-13. 11:10-23. Mungu Anatubadilisha siku hadi siku ila mradi tukae katika njia Zake. Amen.

--- On Mon, 9/5/11, Bahati Mashimba <bahat...@yahoo.com> wrote:

Saimon

unread,
Sep 8, 2011, 3:57:58 AM9/8/11
to YourTrueVine
Asante pia nawe kwa zawadi nzuri ya neno la uzima. Ni kweli Mungu ni
mlinzi wetu na ndiye anayetupa baraka mbalimbali katika maisha yetu
tunachotakiwa ni kuweka matumaini yetu kwake na kushika neno lake.
Zaburi91: 2,10,11 'Nitasema BWANA ndiye kimbilio langu na ngome
yangu,Mungu wangu nitakayemtumaini.Mabaya hayatakupata wewe, wala
tauni haitaikaribia hema yako.Kwa kuwa atakuagizia malaika zake
wakulide katika njia zako zote'.
Kumb10:16,17,18 'Jitunzeni nafsi zenu,mioyo yenu isije
ikadanganywa,mkageuka na kutumikia miungu mingine na kuiabudu.Hasira
za BWANA zikawaka juu yenu naye akafunga mbingu kusiwe na mvua wala
nchi isitoe matunda yake.Kwa hiyo yawekeni maneno yangu mioyoni mwenu
na rohoni mwenu, yafungeni yawe dalili juu ya mikono yenu nayo
yatakuwa kama utepe katikati ya macho yenu.
Maneno haya tuyaweke rohoni mwetu kwa maana Roho ndiyo itiayo uzima
na mwili haufai kitu Yoh6:63.

Mungu atubariki sote na Neema iwe pamoja nasi.

On Sep 6, 9:25 am, Deborah Mgedzi <deborahmge...@yahoo.com> wrote:
> Asante sana Bahati na Warema. Somo hili litanisaidia zaidi wakati wa kipindi cha fellowship na pia nimewapa na wapendwa wengine. Mmbarikiwe sana. Zawadi yangu ni kutoka Zaburi 91 - MUNGU MLINZI WETU - INAPENDEZA SANA KAMA UTASOMA ZABURI HII KILA SIKU PAMOJA NA KUMB. 6:4-13. 11:10-23. Mungu Anatubadilisha siku hadi siku ila mradi tukae katika njia Zake. Amen.
>
> --- On Mon, 9/5/11, Bahati Mashimba <bahatie...@yahoo.com> wrote:
>
> From: Bahati Mashimba <bahatie...@yahoo.com>
> Subject: Re: MWABUDU MUNGU KATIKA ROHO NA KWELI
> To: "yourtr...@googlegroups.com" <yourtr...@googlegroups.com>
> Date: Monday, September 5, 2011, 11:58 PM
>
> Amina.Warema ubarikiwe sana kwa mchango wako mkubwa katika kufafanua juu ya njia sahihi ya kumwabudu Mungu wetu.Mchango wako  naamini utabariki watu wengi na pia  utaendeleza kukuza  roho zetu.Kwa kuwa miili yetu ni hekalu la Mungu na Yesu ndiye kuhani mkuu basi tuitoe miili yetu iwe dhabihu iliyo hai takatifu ya kumpendeza Mungu.
> Nakutakia siku njema na BWANA AKUBARIKI.
>  
>  NEEMA YA BWANA WETU YESU KRISTO NA IWE PAMOJA NA ROHO ZETU.AMINA
>
>  Humble yourselves in the sight of the Lord and he shall lift you up James4:10
>
> 1.Shetani- Shetani ni adui yetu mkubwa na hupenda kuona watu wa dunia hii wa kimtukuza yeye kwa kuwajaribu na fahari za dunia hii na kukamata muda ...
>
> read more »
Reply all
Reply to author
Forward
0 new messages