Asante sana James kwa ufafanuzi wako ni kweli Neno la Mungu ndio Yesu
Kristo mwenyewe na tukilishika Neno la Mungu tutakuwa tumemshika
Yesu mwenyewe na Yesu atakuwa ndani yetu kwani yeye ni mzabibu wa
kweli na sisi tu matawi ya mzabibu.
Maisha ya Kristo haya kuanza wakati alipozaliwa hapa duniani kama
mtoto mchanga kwani yeye ni Neno na alikuwako kwa Mungu na alifanyika
mwili kama tulivyoona kwenye Yohana1:1, na 14.
Kuna dini nyingi ambazo siyo wakristo zimekuwa zikijaribu kupotosha
ukweli huu.Kwahiyo mimi na wewe inabidi tuwaeleze wengine habari za
Yesu kuwa kabla ya kuja hapa duniani alikuwa kwa Mungu na hata baada
ya kufanyika mwili wa kinadamu huko Bethlehemu yeye ni Neno na ni
Mungu.
Tuone neno la mwanafunzi wa Yesu aitwaye Filipo alinena maneno haya
kwa Yesu ''BWANA,utuonyeshe Baba, yatosha.Yesu akamwambia,Mimi
nimekuwako pamoja nanyi siku hizi zote,wewe usinijue, Filipo?
Aliyeniona mimi(Yesu) mimi amemwona Baba(Mungu),basi wewe
wasemaje ,utuonyeshe Baba(Mungu)? '' Yohana 14:8 -9.Katika maneno haya
Kristo,maana ya Baba ni Mungu.Kwahiyo tunapo jua habari za Kristo
tunajua habari za Mungu.
Neno la Mungu linatuambia kwamba Mungu ni pendo.Yesu Kristo
alituonyesha upendo wa Mungu katika maisha yake.Yesu aliwapenda watu
wote,watoto,wenye dhambi,matajiri,maskini,wenyekazi,wavuvi na
wagonjwa.
James kama ulivyoeleza 'Ukristo, kwa kifupi, ni kuishi kwa kufuata
mfano na tabia za Yesu alivyokuwa hapa duniani' Ni kweli ili tuweze
kuishi maisha ya kufuata mfano na tabia za Kristo ni lazima tujifunze
maisha yake.
Wakati Yesu alipokuwa hapa duniani alituonyesha mambo mengi yaliyo
mema.Tunapokuwa na tatizo yatupasa tufikiri juu ya maisha ya Kristo
alifanya nini juu ya tatizo kama hili.
BWANA akubarikie na kukulinda.
Saimon(BEM)
On Feb 28, 3:32 pm, James Malima <
james.mal...@gmail.com> wrote:
> Naamini kabisa kwamba kwa mujibu wa Yohana, hilo ndo jibu sahihi. Hili jina
> Yesu limekuja katika agano jipya baada ya Mariamu kupata mimba kwa uweza wa
> Roho Mtakatifu na kumzaa Yesu. Kabla ya hapo, Yesu, kama nafsi ya pili ya
> Mungu, na kabla ya kuvaa mwili, ili aweze kutukomboa kutoka katika dhambi
> zetu, alikuwa akijulikana kama Neno la Mungu.
>
> Ni muhimu sana kwa Mkristo yoyote, msingi wake kuwa ni Neno la Mungu. Kama
> jinsi Mungu alivyo, kwamba habadiliki, ukilishika Neno la Mungu, unakuwa
> umemshika Mungu mwenyewe. Watu wengi siku hizi wanavutwa na miujiza, matokeo
> yake wamejikuta kuangukia mikononi mwa Manabii wa uwongo.
>
> Neno la Mungu ndio Yesu mwenyewe, na tukilishika Neno, basi tunakuwa
> tumemshika Yesu mwenyewe. Ukristo, kwa kifupi, ni kuishi kwa kufuata mfano
> na tabia za Yesu alivyokuwa hapa duniani.
>
> Mbarikiwe sana.
>
> Malima
>
> 2011/2/28 Saimon <
bmashi...@gmail.com>
> E-mail:
James.Mal...@gmail.com
> "If you fail to plan,..... you're planning to fail"- Hide quoted text -
>
> - Show quoted text -