On 11/19/12, Warema S.Senzia <
gwa...@yahoo.com> wrote:
> Bahati asante kwa somo zuri la Sabato.
> Kwa bahati mbaya Wakristo wengi sana wamekuwa wakifundisha Biblia bila
> kufundisha somo la Sabato. Binafsi nilijiuliza kwa nini Wakristo wengi
> hawatunzi Sabato ili hali imeandikwa katika Biblia? nikajifunza sababu ya
> kuwa na siku tofauti na Sabato, katika kujifunza nikasoma vitabu vya
> historia vikionesha kama Mfalm ( Emperor) Constantine Mkuu ndio alibadili
> agizo hilo kutoka Sabato kwenda jumapili na huo ulikuwa wakati kanisa likiwa
> dogo linakuwa sasa kanisa likakuwa likiwa na mafundisho ya kibinadamu kama
> siku tofauti na Sabato na ubatizo wa maji machache n.k. na kwa kua
> Constantine akiwa Mfalme wa Rumi na Rumi ilitawala seheu kubwa ya Dunia basi
> watu wengi wakajikuta wakifuata Ukristo usio kamili. Kanisa la wakati huo
> lilizuia wakristo kusoma Biblia na hivyo kuwafanya wengi kutojua mafundisho
> sahihi ya Biblia.
> Zama za kuzuiwa kusoma Biblia zikapita, lakini watu wengi wakawa tena
> hawataki kubadili mazoea yao hata kama wakiona ni tofauti za mafundisho ya
> Biblia.
>
> Katika kujifunza siku sabato nilikutana na video kadhaa, ninaweza kuweka
> kama kuna watu wanahitaji kujifunza nami pia. Nyingi zipo kwa kiingereza.
>
> Asante na sote tubarikiwe tukijifunza kuhusu Sabato takatifu ya MUNGU.
> "...Surely goodness and love will follow me
> all the days of my life, and I'll dwell in the house of the LORD forever"
>
>
>