NENO LA LEO

117 views
Skip to first unread message

eliezer.mwangosi

unread,
Jan 21, 2018, 11:27:00 PM1/21/18
to
NENO LA LEO - KUJILISHA UPEPO. 

Muhubiri 2:11 "Kisha nikaziangalia kazi zote zilizofanywa kwa mikono yangu, na taabu yote niliyotaabika katika kuzitenda; na tazama, yote ni ubatili na kujilisha upepo, wala faida hakuna chini ya jua."

Nakumbuka kisa cha Baba mmoja tajiri, aliyekuwa na uwezo wa kufanya lolote kwa sababu ya mali alizokuwa nazo. Alikuwa akiambiwa habari za Mungu, anasema "Mungu anatafutwa na maskini na wazee, umesikia wapi matajiri wanahangaika na Mungu, ili viweje?".

Katika wakati asioudhania, akaugua ugonjwa ambao tiba yake ilikuwa ni pamoja na mashariti haya; asile chakula kilichoungwa chumvi, asile vyakula vya nyama, chakula kisipikwe kwa mafuta, asitumie sukari wala aina yoyote ya soda au juice za viwandani, asitumie kileo cha aina yoyote n.k. Siku moja akiwa kitandani hajiwezi alisikika akisema "KWELI MAISHA NI UPEPO".

Rafiki sikiliza, kuna watu ni matajiri, lakini wanaziangalia mali zao kwa macho, wanafaidi wengine. Elimu, uzuri, mali, vyeo, vipaji, bila Mungu ni kujilisha Upepo, dunia inapita tena haraka, hakuna anayejua mwisho wake ila ni Mungu pekee anayejua.

Kuna watu wananyanyua mabega na kunyanyasa wenzao kwa sababu tu ya nafasi au maisha na mali walizo nazo, lakini jiulize wanamzidi Sulemani hata kwa lolote? Mwingine utakuta ana mke mmoja, nyumba ndogo mbili na makahaba hawazidi 10, anajiona ndio mwenyewe, uliza Sulemani alikuwa nao wangapi?  .... Bado akaona maisha Mungu ni Kujilisha UPEPO. 

Jambo ambalo ni la hakika ni hili, watu wote wanapopitia changamoto wanamhitaji na wanamtafuta Mungu, hapo ndipo wengi wanakuwa wamechelewa, wengi wanalala mauti bila matumaini. Neno la leo linatuongoza kumtafuta Mungu sasa kabla ulimwengu haujageuka. 

Kwa wale wanaopitia dhoruba fulani sasa, bado neema ya Mungu ipo, inua macho yako juu mtazame Mwokozi wako, ahadi hii itatimia kwako, "Mathayo 11:28 Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha."

NAKUTAKIA JUMATATU NJEMA YENYE BARAKA TELE

Na: Ev. Eliezer Mwangosi





Sent from Samsung tablet

Bahati Mashimba

unread,
Jan 22, 2018, 9:55:21 AM1/22/18
to eliezer.mwangosi, YourTrueVine
Amina mtumwa wa BWANA.

eliezer.mwangosi

unread,
Jan 23, 2018, 10:11:38 PM1/23/18
to
NENO LA LEO - TAHADHARI YA KUITUMIA NEEMA VIBAYA

Tito 2:11-12 "Maana neema ya Mungu iwaokoayo wanadamu wote imefunuliwa; nayo yatufundisha kukataa ubaya na tamaa za kidunia; tupate kuishi kwa kiasi, na haki, na utauwa, katika ulimwengu huu wa sasa;"

Ni kawaida ya wanadamu kupindua mambo na kutumia fulsa vibaya. Ni jambo la kawaida kusikia "Isingelikuwa NEEMA tungeisha wote", uovu unazidi kuongezeka kati ya watu wanaojiita watu wa Mungu, wakidai wako chini ya neema ya Kristo, na wengi wanajifariji wakijua wako salama, wakiendelea na dhambi za siri au wazi huku wakidumu katika huduma za Ibada.

Ni jambo la kawaida kusikia mwalimu wa Kwaya anatembea na fulani, au kiongonzi fulani anatembea na mpendwa fulani, na hao wanadumu katika huduma. Tunashuhudia tabia hizi za, chuki, wivu, visasi, uzushi, uongo, ubinafsi, kugombania vyeo, Dharau, uonevu, dhuruma, uzinifu, ULEVI, uchawi, utapeli n.k. zikidumu kwa wanaojiita wasafiri, hiyo yote ni kwa sababu ya NEEMA, ingelikuwa enzi za Torati wangeadhibiwa na wengine kuuwawa.

Wakati shetani anawakusanya watu na kuwaandaa kwa ajili ya hukumu, huku wengine akiwajeruhi na kukatisha maisha yao kwa vifo vya ghafla wangali ni waovu, kwa mwamvuli wa NEEMA, neno la leo linatoa tahadhari kwa wote ili asiwepo wa kupotea. Ndio maana mtume Paulo aliuliza; "Tuseme nini basi? Tudumu katika dhambi ili neema izidi kuwa nyingi?" Warumi 6:1.

Mpendwa, neema ya Mungu kupitia kifo cha Yesu Kristo, imetolewa kwetu ili KUTUOKOA na kutuweka huru mbali na dhambi, inatupatia nguvu ya kutii mapenzi au amri au maagizo ya Mungu, inatupatanisha na Mungu, inatupatia msamaha wa dhambi, neema inatupatia HAKI ya kuwa watoto wa Mungu kwa Imani.

Mungu anashangaa kuona wanaokiri kuwa ni watu wake, waliokombolewa wakidumu kuishi maisha yaliyo kinyume na tabia ya Kristo, wakifikiri wako salama. Mwisho anawauliza swali hili - Warumi 2:4 "Au waudharau wingi wa wema wake na ustahimili wake na uvumilivu wake, usijue ya kuwa wema wa Mungu wakuvuta upate kutubu?".

Neema ya Mungu izidi kuwa juu ya kila mmoja, ili tuishi maisha matakatifu, katika zama hizi za UOVU, na tuwe tayari kupokea baraka zake na kuurithi uzima wa milele.

NAWATAKIA WOTE SIKU NJEMA YENYE KUJAA BARAKA ZA BWANA.

Na:Ev. Eliezer Mwangosi
Simu: 0767210299 - Kwa wenye mahitaji ya Kiroho.




Sent from Samsung tablet

eliezer.mwangosi

unread,
Jan 24, 2018, 10:36:56 PM1/24/18
to aak...@hq.bot-tz.org, ester...@yahoo.com, annie...@yahoo.com, cella...@yahoo.co.uk, emie...@yahoo.com, Arusha Reception, bmas...@gmail.com, elijahc...@yahoo.com, bngan...@yahoo.com, evam...@yahoo.co.uk, devon...@yahoo.com, ckiiz...@yahoo.com, emmy...@yahoo.com, Andyni...@yahoo.com, benson...@yahoo.com, emba...@yahoo.com, damar...@ymail.com, epiphania...@yahoo.com, bmt...@gmail.com, elig...@yahoo.co.uk, Erick...@hotmail.com, Dat...@scitz.com, Buhatwa Ladislaus, berna...@gmail.com, weddym...@gmail.com, csend...@yahoo.com, Emmyk...@gmail.com, answ...@yahoo.co.uk, alfredb...@yahoo.com, annas...@yahoo.com, ana...@hotmail.co.uk, debok...@yahoo.com, emap...@yahoo.co.uk, chec...@yahoo.co.uk, dai...@diamondtrust.co.tz, yourtr...@googlegroups.com, deri...@yahoo.com, anne...@hotmail.com, deoma...@yahoo.com, ant...@gmail.com, elyta...@yahoo.com, Edesia Kahyarara, apbw...@yahoo.co.uk, Evel...@gmail.com, bar...@yahoo.com, cjk...@yahoo.co.uk, Dorah....@tigo.co.tz, zaina...@yahoo.com, ema...@serena.co.tz, ymt...@hotmail.com
NENO LA LEO - WEMA WA BWANA NI WA MILELE

Zaburi 118:29 "Mshukuruni BWANA kwa kuwa ni mwema, Kwa maana fadhili zake ni za milele."

Katika ulimwengu huu uliojaa masumbufu ya maisha, akili za wanadamu zimejaa matatizo, zimejaa kutoridhika, midomo imejaa kutamka shida na mapito. Hivyo hata anapomgeukia Mungu, akili yote inakuwa ni kupeleka mizigo ya matatizo aliyo nayo.

Neno la leo linatukumbusha kutazama wema wa Bwana na Fadili zake alizotutendea, halafu tumshukuru. Ukifuatilia, maombi mengi ya watu na tamaa za mioyo yao ni kutimiziwa mahitaji yao, hebu leo kila mmoja atafakari yale Bwana aliyomtendea ktk maisha yake yote aliyopitia.

Kuna watu wa umri wako wamesha lala mauti, kuna watu ni vichaa, kuna watu hivi leo hawajitambui wako mahututi, kuna watu wako maporini hawana pa kulala kwa sababu ya vita, kuna watu wanakufa kwa njaa, hebu angalia wahitaji wengine wanaoteseka, utagundua wema wa Mungu kwako.

Hebu kila mtu apige picha ya maisha yake yote ya nyuma, atagundua kuna mkono wa Bwana uliomfikisha hai siku ya leo, wengi wamepitia vipindi vigumu, lakini leo maisha yanaendelea. Katika hali yoyote uliyonayo, bila kujali ukubwa wa tatizo unalopitia, wema wa Mungu uko pamoja nawe.

Mtume Paulo anasema, "Msijisumbue kwa neno lo lote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu." Wafilipi 4:6. Shukrani zetu zinaonyesha tunatambua wema tunaotendewa na Mungu.

NAWATAKIA SIKU NJEMA YENYE MAFANIKIO TELE KATIKA KILA JAMBO

Na: Ev. Eliezer Mwangosi.

Simu: 0767 210 299 - Kwa wenye wahitaji.
Sent from my Samsung Galaxy smartphone.

eliezer.mwangosi

unread,
Jan 24, 2018, 10:48:59 PM1/24/18
to
Sent from Samsung tablet

eliezer.mwangosi

unread,
Jan 25, 2018, 9:57:33 PM1/25/18
to
NENO LA LEO - KUUSHINDA UBAYA KWA WEMA

Warumi 12:21 "Usishindwe na ubaya, bali uushinde ubaya kwa WEMA".

Katika ulimwengu tunaoishi, ni kawaida kukutana na changamoto za wawili wapendanao kukosana kwa sababu mbalimbali, na mara nyingi tumeshuhudia watu wakilipa visasi, yaani kulipa ubaya kwa ubaya (UBAYA UBAYA TU). Lakini ukifuatilia sana utagundua kuwa, kila visasi na chuki vilipojitokeza matokeo yake yalikuwa ni maumivu makubwa kuliko mwanzo. Utakuta wapendanao wanavunja mahusiano, ndoa na uchumba vinasambaratika, hata marafiki pete na kidole wanaachana tena kwa uchungu mkubwa. 

Kupitia neno la leo, Mungu ajuaye siri za vyanzo na sababu za kutokea kutoelewana katika jamii,  anashauri kuwa " Tuushinde Ubaya kwa WEMA", maana yake,  tuwe na msamaha, na Mungu atusaidie kurudisha amani kwa kuwatendea mema waliotukosea. Huwezi kujua kwa nini jambo fulani limetokea, ambalo kwa kweli unaona limekuumiza,  lakini Mungu huwa anajua chanzo chake. Kumtendea wema aliyekukosea kibinadamu ni vigumu, lakini kwa Mungu yote yanawezekana. 

Kumbukeni tunaishi katika uwanja wa maisha ambayo kwa asili, adui shetani amepanda mbegu ya uovu, shetani ana chukia akiona katika jamii kuna Upendo, Furaha na Amani, hivyo anatumia kila njia kwa hila kuleta tofauti, wenye kutoka juu ndio wanaweza kulijua hili, ndio maana Yesu alisema "Wasameheni wanao waudhi na Kuwaombea). Ukimsamehe na kumuombea adui yako, unampalia makaa kichwani, akiendelea kwa ujeuri Bwana atamtandika, jua kisasi ni cha Bwana. 

Mungu atusaidie tuushinde kila UBAYA kwa kutenda WEMA kwa kila mtu. 

NAWATAKIA SIKU YENYE MAFANIKIO NA BARAKA TELE

### Sambaza ujumbe huu kwa wengine au nipatie email au namba zao niwe nawatumia kwa WhatsApp###

Na. Ev. Eliezer Mwangosi




Sent from Samsung tablet




Sent from Samsung tablet

Bahati Mashimba

unread,
Feb 1, 2018, 4:01:51 AM2/1/18
to yourtr...@googlegroups.com
Amina.Ubarikiwe sana mtumwa wa BWANA

On 1/26/18, 'eliezer.mwangosi' via YourTrueVine
> --
> Mimi ni mzabibu ninyi ni matawi, akaaye ndani yangu nami ndani yake, huyo
> huzaa sana; maana pasipo mimi ninyi hamwezi kufanya neno lolote.Yohana
> 15:5
> ---
> You received this message because you are subscribed to the Google Groups
> "YourTrueVine" group.
> To post to this group, send an email to yourtr...@googlegroups.com.
> For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
>

eliezer.mwangosi

unread,
Feb 4, 2018, 10:29:50 PM2/4/18
to
NENO LA LEO - IPOKEE AMANI YA KWELI

Yohana 14:27 "Amani nawaachieni; amani yangu nawapa; niwapavyo mimi sivyo kama ulimwengu utoavyo. Msifadhaike mioyoni mwenu, wala msiwe na woga."

Pamoja na watu wengi kuwa na mapumziko ya siku mbili kwa wiki, yaani kutofanya kazi siku ya Jumamosi na Jumapili, bado siku ya Jumatatu kwa wengi inakuwa ni siku ya misongo, hali hiyo ni kutokana na adha mbalimbali zinazojitokeza.

Ulimwengu tunaoishi neno AMANI linazidi kuwa msamiati kwa wengi, wengi wanaenda maofisini, au kwenye biashara, au mashambani n.k. wakiwa wamejawa na mawazo juu ya kuzivuka changamoto zinazowakabili, bila kujali Vyuma vimekaza, watoto wanadai kwenda shule, ada na mahitaji mengine yanatakiwa, wakati vipato vimeishia kwenye madeni.

Jambo la kushangaza hata matajiri, ukiwafuatilia ndani ya mioyo yao, wengi wanapitia changamoto fulani, isiyojali pesa au vyeo walivyonavyo. Kuna magonjwa, vurugu za ndoa na mahusiano, kuonewa, upweke, kudaiwa, mafarakano ya ndugu, kusumbuliwa na uchawi n.k. Hayo yanaweza kuifanya Jumatatu yako isiwe ya AMANI.

Sikiliza; unaweza kuianza Jumatatu yako vizuri na wiki nzima ikapita salama ukiamini na kuipokea ahadi ya Yesu, ni yeye pekee awezaye kukupitisha SALAMA katika kila dhoruba ya moyo wako. Unaona nini mbele yako? Yesu anasema, USIFADHAIKE WALA USIWE NA WOGA .... ATAKUSHINDIA.

NAKUTAKIA JUMATATU NJEMA YENYE KUJAA AMANI TELE.

Na: Ev. Eliezer Mwangosi
Simu: 0767 210 299 - Kwa Ushauri zaidi.




Sent from Samsung tablet

Mtoka James

unread,
Feb 5, 2018, 5:50:33 AM2/5/18
to yourtruevine
Amen  barikiwa  mtumishi

--
Mimi ni mzabibu ninyi ni matawi, akaaye ndani yangu nami ndani yake, huyo huzaa sana; maana pasipo mimi ninyi hamwezi kufanya neno lolote.Yohana 15:5
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "YourTrueVine" group.
To post to this group, send email to yourtr...@googlegroups.com.

eliezer.mwangosi

unread,
Feb 7, 2018, 2:01:38 PM2/7/18
to
NENO LA LEO - MIZANIA YA KIROHO

Luka 21:34 "Basi, jiangalieni, mioyo yenu isije ikalemewa na ulafi, na ulevi, na masumbufu ya maisha haya; siku ile ikawajia ghafula, kama mtego unasavyo."

Kama kuna mtego ambao shetani amefanikiwa kuwanasa wengi, basi huu wa MIOYO KULEMEWA NA MASUMBUFU YA MAISHA unaongoza. Hata asilimia kubwa ya wanaokesha kwenye majumba ya Ibada ni kwa sababu ya KULEMEWA, wanatafuta msaada.

Hata ujumbe huu naufupisha kwa sababu watu hawasomi, wakidai ujumbe mrefu unachosha kusoma, sasa waulize mioyo yao inapenda nini? Muda wanautumia kwa kitu gani? Asilimia kubwa ya akili ya mwanadamu inatumika kwa MASUMBUFU YA MAISHA HAYA.

AKILI ZIMETEKWA, utakuta ujumbe wa neno la leo, unasomwa kichwa na akijitahidi sana fungu, halafu anaenda anabofya LIKE au anaandika AMEEEE, wakati Ujumbe halisi ambao Mungu alikusudia aupate ameukosa. Cha kushangaza anaweza kuchat mambo ya kidunia masaa mengi hadi kukesha.

Wapendwa, wacha Mungu, wenye hofu ya Mungu, wanazidi kutoweka katika Kizazi chetu, huku WASANII WA KIROHO na wenye dini za mtindo na watafuta maisha, wakiendelea kujazana kwenye Ibada za leo. Shetani ameteka mioyo ya wengi, UOVU haukomi japo waabuduo wanaongezeka. HIZO NDIZO HILA ZA SHETANI.

Huu ni wakati wa kukataa wokovu bandia, wokovu wa kutafuta mali, wokovu wa kusaka wachumba n.k. Mungu anatafuta wanaomtafuta yeye kwa bidii ili abadilishe maisha yao, na mengine yafuate kama matokeo.

Enyi Vijana, wako wapi akina Yusufu wa leo, wako wapi akina Danieli wa leo? Wengi wameishia kwenye mitandao wakijeruhi na kujeruhiwa mioyo yao, hawana muda wa Kufunga wakiomba na kuutafuta uso wa Bwana kwa ajili ya UTAKASO, wengi wamebaki ni miti mikavu, imekauka kama sio kuoza.

Muda mwingi unatumika kwa mambo ya mwili, kutafuta pesa, kusaka mahusiano, kuviringisha viuno kwenye majumba ya starehe, kukodolea macho tamthilia usiku kucha, kupiga umbea kwenye vijiwe, kushinda kwa waganga n.k. Hayo yote ndiyo yanapewa nafasi kubwa, wengi WAMENASA.

UTAFUTENI KWANZA UFALME WA MUNGU NA MWENGINE YOTE MTAZIDISHIWA.

NAWATAKIA SIKU NJEMA YENYE MIANZO MIPYA YA BARAKA.


Na: Ev. Eliezer Mwangosi
Simu: 0767210299




Sent from Samsung tablet

Bahati Mashimba

unread,
Feb 7, 2018, 2:17:01 PM2/7/18
to 'eliezer.mwangosi' via YourTrueVine
Amen.Asante sana mtumwa wa Bwana kwa huduma ya neno la Mungu.Bwana akubariki


--

eliezer.mwangosi

unread,
Feb 8, 2018, 10:55:53 PM2/8/18
to
NENO LA LEO - AHADI KWA WASAFIRI

Kutoka 23:25-27 "Nanyi mtamtumikia BWANA, Mungu wenu, naye atakibarikia chakula chako, na maji yako; nami nitakuondolea ugonjwa kati yako. Hapatakuwa na mwenye kuharibu mimba, wala aliye tasa, katika nchi yako; na hesabu ya siku zako nitaitimiza. Nitatuma utisho wangu utangulie mbele yako, nami nitawafadhaisha watu wote utakaowafikilia..........."

Maneno hayo ni ahadi aliyoitoa Mungu kwa taifa lake la Israeli baada ya kuwatoa utumwani misri, wakiwa safarini kuelekea inchi ya ahadi. Safari yao ilikuwa ngumu, ilikutana na vikwazo vingi, walipitia uzoefu usio wa kawaida, lakini walishuhudia mkono wa Mungu ukitenda makuu hadi kufanya njia pasipo njia.

Neno la leo, limekuja kwetu kutukumbusha ahadi za Bwana kwa watu wake, wewe na mimi tuko safarini, na safari yetu haiko salama, misongo, hofu, huzuni, kuvunjika mioyo, kukata tamaa, kukosa amani, kukosa matumaini, fadhaa, manung'uniko n.k. ni hali zinazozidi kutanda katika mioyo ya wengi. Hayo yote yanatokana na hali halisi ya maisha katika dunia yetu iliyojaa uovu na kila aina ya laana. 

Rafiki; haijalishi uwe umepitia au unaptia changamoto ngumu kiasi gani, Bwana ameahidi kutuondolea hayo, na zaidi ameahidi kutuma UTISHO wake ututangulie mbele yetu, je kuna jambo la kumshinda Bwana? Hebu tuimarishe Imani zetu Kwake, tumtumaini yeye daima,  naye atalitimiza neno lake Kwa wakati uliokubalika. 

NAWATAKIA SIKU NJEMA YENYE MIBARAKA TELE

Na: Ev. Eliezer Mwangosi
Simu: 0767 210 299.





Sent from Samsung tablet

eliezer.mwangosi

unread,
Feb 13, 2018, 10:49:25 PM2/13/18
to aak...@hq.bot-tz.org, ester...@yahoo.com, annie...@yahoo.com, cella...@yahoo.co.uk, emie...@yahoo.com, Arusha Reception, bmas...@gmail.com, elijahc...@yahoo.com, bngan...@yahoo.com, evam...@yahoo.co.uk, devon...@yahoo.com, ckiiz...@yahoo.com, emmy...@yahoo.com, Andyni...@yahoo.com, benson...@yahoo.com, emba...@yahoo.com, damar...@ymail.com, epiphania...@yahoo.com, bmt...@gmail.com, elig...@yahoo.co.uk, Erick...@hotmail.com, Dat...@scitz.com, Buhatwa Ladislaus, berna...@gmail.com, weddym...@gmail.com, csend...@yahoo.com, Emmyk...@gmail.com, answ...@yahoo.co.uk, alfredb...@yahoo.com, annas...@yahoo.com, ana...@hotmail.co.uk, debok...@yahoo.com, emap...@yahoo.co.uk, chec...@yahoo.co.uk, dai...@diamondtrust.co.tz, yourtr...@googlegroups.com, deri...@yahoo.com, anne...@hotmail.com, deoma...@yahoo.com, ant...@gmail.com, elyta...@yahoo.com, Edesia Kahyarara, apbw...@yahoo.co.uk, Evel...@gmail.com, bar...@yahoo.com, cjk...@yahoo.co.uk, Dorah....@tigo.co.tz, zaina...@yahoo.com, ema...@serena.co.tz, ymt...@hotmail.com
NENO LA LEO: UHAKIKA WA KUVUKA SALAMA

Zaburi 107:28-30 "Wakamlilia Bwana katika dhiki zao, akawaponya na shida zao. Huituliza dhoruba, ikawa shwari, mawibi yake yakanyamaza. Ndipo walipofurahi kwa kuwa yametulia, naye huwaleta mpaka bandari waliyoitamani".

Katika zama zote, baada ulimwengu kuingia katika pambano kati ya wema na ubaya, tumeshuhudia watu wema kwa waovu wakipitia dhoruba mbalimbali za maisha. Visa vingi vimeandikwa katika biblia, vikionyesha jinsi Mungu alivyowatendea watu wake waliokuwa wanapitia Dhiki na Taabu za maisha.

Haijalishi tunapitia dhoruba gani za maisha haya, Mungu yuko makini akiangalia, wale watakao dumu kuyainua macho yao wakimtazama kwa Imani, wakidai ahadi zilizofunuliwa katika neno lake, wamehakikishiwa kufika ng'ambo salama. 

Kila mwanadamu aliyezaliwa katika ulimwengu huu wa dhambi, anapitia namna fulani ya changamoto, japo zinatofautiana, hata hivyo wote tumepewa fulsa ya kupata msaada kutoka kwa Mwokozi wetu. Kadri tunavyomkaribia Mungu wetu kwa kusoma neno lake na kuomba kwa Imani, tunakuwa na uhakika wa ushindi kwa kila jaribu. 

Tafakari ya leo itusaidie kusimama kwa Imani iwe wakati wa dhoruba au shwari .... mwisho ni tumaini na ushindi. Kila mtu kuna jambo anatamani litendeke, kuna sehemu anatamani afike, kuna kitu anatamani akipate, kuna hali anatamani aifikie, sikiliza; ukimtumaini Mungu uatafanikiwa ili mradi ni kwa utukufu wake. 

WEMA WA MUNGU UZIDI KUMFUNIKA KILA MWENYE MATUMAINI HAYA.

NAWATAKIA SIKU NJEMA YENYE KUJAA BARAKA ....

Na. EV. Eliezer Mwangosi
Simu: 0767 210 299



eliezer.mwangosi

unread,
Feb 13, 2018, 10:50:18 PM2/13/18
to aak...@hq.bot-tz.org, ester...@yahoo.com, annie...@yahoo.com, cella...@yahoo.co.uk, emie...@yahoo.com, Arusha Reception, bmas...@gmail.com, elijahc...@yahoo.com, bngan...@yahoo.com, evam...@yahoo.co.uk, devon...@yahoo.com, ckiiz...@yahoo.com, emmy...@yahoo.com, Andyni...@yahoo.com, benson...@yahoo.com, emba...@yahoo.com, damar...@ymail.com, epiphania...@yahoo.com, bmt...@gmail.com, elig...@yahoo.co.uk, Erick...@hotmail.com, Dat...@scitz.com, Buhatwa Ladislaus, berna...@gmail.com, weddym...@gmail.com, csend...@yahoo.com, Emmyk...@gmail.com, answ...@yahoo.co.uk, alfredb...@yahoo.com, annas...@yahoo.com, ana...@hotmail.co.uk, debok...@yahoo.com, emap...@yahoo.co.uk, chec...@yahoo.co.uk, dai...@diamondtrust.co.tz, yourtr...@googlegroups.com, deri...@yahoo.com, anne...@hotmail.com, deoma...@yahoo.com, ant...@gmail.com, elyta...@yahoo.com, Edesia Kahyarara, apbw...@yahoo.co.uk, Evel...@gmail.com, bar...@yahoo.com, cjk...@yahoo.co.uk, Dorah....@tigo.co.tz, zaina...@yahoo.com, ema...@serena.co.tz, ymt...@hotmail.com

Bahati Mashimba

unread,
Feb 15, 2018, 1:59:30 PM2/15/18
to aak...@hq.bot-tz.org, ester...@yahoo.com, annie...@yahoo.com, cella...@yahoo.co.uk, emie...@yahoo.com, Arusha Reception, bmas...@gmail.com, elijahc...@yahoo.com, bngan...@yahoo.com, evam...@yahoo.co.uk, devon...@yahoo.com, ckiiz...@yahoo.com, emmy...@yahoo.com, Andyni...@yahoo.com, benson...@yahoo.com, emba...@yahoo.com, damar...@ymail.com, epiphania...@yahoo.com, bmt...@gmail.com, elig...@yahoo.co.uk, Erick...@hotmail.com, Dat...@scitz.com, Buhatwa Ladislaus, berna...@gmail.com, weddym...@gmail.com, csend...@yahoo.com, Emmyk...@gmail.com, answ...@yahoo.co.uk, alfredb...@yahoo.com, annas...@yahoo.com, ana...@hotmail.co.uk, debok...@yahoo.com, emap...@yahoo.co.uk, chec...@yahoo.co.uk, dai...@diamondtrust.co.tz, yourtr...@googlegroups.com, deri...@yahoo.com, anne...@hotmail.com, deoma...@yahoo.com, ant...@gmail.com, elyta...@yahoo.com, Edesia Kahyarara, apbw...@yahoo.co.uk, Evel...@gmail.com, bar...@yahoo.com, cjk...@yahoo.co.uk, Dorah....@tigo.co.tz, zaina...@yahoo.com, ema...@serena.co.tz, ymt...@hotmail.com, eliezer.mwangosi
Amen.Barikiwa na Bwana

--
Reply all
Reply to author
Forward
0 new messages