WEKEZA MAISHA YAKO KWA BWANA

427 views
Skip to first unread message

Happy Mashimba

unread,
Jan 27, 2013, 2:55:57 PM1/27/13
to yourtr...@googlegroups.com
Binadamu huenda tu huko na huko kama kivuli;Hufanya ghasia tu kwa ajili ya ubatili;Huweka akiba wala hajui ni nani atakayeichukua. Zaburi 39:6
 
Maisha ya mkristo huanzia hapa duniani kwa kuamini jina la Yesu Kristo  na mwisho wake ni kwenye mji  mtakatifu  Yerusalemu mpya.Tunaona watu wengi ambao ni wakristo walivyo busy wa kienda huko na huko kutafuta utajiri kwa njia mbalimbali ikiwa ni pamoja na njia halali na wengine wanatumia njia haramu za wizi, uaji, unyang'anyaji, ufisadi, kshirikina na njia zote mbaya  wanazoweza  kuzitumia ili waweze kupata utajiri.Utajiri wa mali  ni haki ya kila mkristo anayeishi kwa kufuata  misingi ya neno la Mungu.
 
Wapo wanaosabisha ghasia  katika  jamii, ndugu, kanisa na hata taifa kwa sababu wamebaka haki za watu kwa tamaa zao binafsi za kuwa na utajiri kwa njia haramu.Biblia inatuhimiza   hao wanaoweka akiba ya utajiri wao hapa duniani hawatajua nani atachukua mali zao na zitaendelezwaje baada ya kufa kwao.Mtu hatachukua mali zake  kwenda nazo  kaburini au  kuingia nazo kwenye ufalme wa Mungu.
 
Sisi wakristo tunapoendelea kuishi kwa neema ya BWANA,na pia namna BWANA wetu  anavyotubariki katika kazi na biashara zetu halali tukumbuke kuwekeza muda wetu, pesa zetu, mali zetu, maisha yetu kwa BWANA maana tutavuna uzima wa milele.
 
Baraka za Bwana wetu Yesu Kristo ziwe nanyi daima.
 
Happiness Mashimba
 
 

Happy Mashimba

unread,
Jan 28, 2013, 3:11:16 PM1/28/13
to yourtr...@googlegroups.com
Utakieni Yerusalemu amani.Na wafanikiwe wakupendao.Zaburi 122:6
 
Mataifa mengi kwa sababu ya siasa na dhuluma yamejitahidi sana kutaka kuona wapalestina wanakubaliwa maombi yao ya kutaka mji wa Yerusalemu  upigiwe kura ya kugawanywa ili sehemu ya eneo la mji huo liwe katika upande wa West bank wanakokaa wapalestina.
Wakristo tunajua chimbuko la makanisa ni katika mji huu wa Yerusalemu.Biblia inatuelekeza kuutakia amani mji huu ili tuweze kufanikiwa.Wakristo lazima tusimame kama mwili mmoja kwakufanya maombi ya ukombozi wa mji  huu mtakatifu usije ukagawanywa  kutokana na hila za umoja wa mataifa na waarabu.
 
Kwa kuwa ahadi za Mungu ni za kweli na kusihi mpendwa katika kristo uanze sasa  kuombea taifa la Israeli na mji wa Yerusalemu ili Mungu atimize ahadi yake katika kukubariki.Unapoomba juu ya mji huu kumbuka na kuweka  taifa lako  liweze kuwa na ushirikiano  mzuri na nchi ya Israeli ili taifa liweze  kutoka katika hali tuliyo nayo na tuweze kupata maendeleo zaidi.
 
Mungu wetu anataka  taifa , mkristo mmoja mmoja , kanisa tuupende na kuutakia amani mji wa Yerusalemu ili adui wanaotaka  kuona unapigiwa kura ya kugawanywa wanashindwa.Kila taifa linapenda mafanikio na hata sisi wakristo tunapenda mafanikio katika maisha yetu.Tusiache kuomba juu ya mji wa Yerusalemu ili BWANA  aweze kuulinda na sisi atufanikishe katika mambo yetu yote.

MaryGlady Heri

unread,
Jan 29, 2013, 3:11:52 AM1/29/13
to yourtr...@googlegroups.com
Amen asante sana Dada Hapiness kwa kutukumbusha wajibu wetu,Be blessed

2013/1/28 Happy Mashimba <hmash...@yahoo.com>

--
--
Mkikaa ndani yangu na maneno yangu yakikaa ndani yenu basi ombeni chochote mtakacho nanyi mtapewa.Yohana15:7
 
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "YourTrueVine" group.
To unsubscribe from this group, send email to yourtruevine...@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
 
 

Reply all
Reply to author
Forward
0 new messages