NENO LA LEO:SIMAMA IMARA KATIKA WOKOVU

2,184 views
Skip to first unread message

Bahati Mashimba

unread,
Apr 25, 2017, 3:40:14 AM4/25/17
to YourTrueVine
NENO LA TAFAKARI: SIMAMA IMARA KATIKA WOKOVU

WAFILIPI 2:12 Basi wapendwa wangu kama vile mlivyotii sikuzote si
wakati mimi nilipokuwapo tu, bali sasa zaidi sana mimi nisipokuwapo,
UTIMIZENI WOKOVU WENU wenyewe kwa kuogopa na kutetemeka..

Wapendwa tunaishi nyakati zilizojaa changamoto mbalimbali za maisha,
wapo waliokosa furaha kwa sababu ya dhiki,magonjwa,uchumi kuyumba na
wengine wamekata tamaa kutokana na kukosa amani katika jamii
wanayoishi,ndoa, kazi, na hata katika hali ya umaskini ,kisiasa.

Lakini pia wapo wanaosumbukia maisha katika kutafuta kiasi kwamba
wameacha wokovu kwasababu zao za utafutaji.Haijalishi tunakazi zipi;
nilazima tutimize wokovu katika Kristo na kuwa na hofu ya Mungu si tu
tunapokuwa kwenye jamii inayotufahamu au watumishi wanaotujua bali
mahali popote tunapokuwa tuonakane tuna Yesu ndani yetu.

Mtume Paulo anatusihi Wakristo wote pamoja na Maaskofu ,Mashemasi ya
kuwa ni lazima tusimame imara katika wokovu uliowathamani sana bila
kujali changamoto za maisha tunazokutana nazo kwa kuwa tunaye Bwana
ambaye yeye ni kila kitu katika maisha yetu na tena ni furaha yetu
ambaye hututia nguvu na kutuwezesha katika mambo yote.

Ili tuweze Kusimama Imara katika Wokovu ni lazima:

1.Kujihadhari na mafundisho ya uongo Wafilipi 3:1-2

2.Kuacha kuutumainia mwili Wafilipi 3:3-7

3.Kuwa na shauku ya kumjua zaidi Yesu Wafilip 3:8-11

4.Kuwa na hamu ya kufikia lengo la imani Wafilipi 3:12-16

5.Kujiepusha na maadui wa msalaba Wafilipi 3:17-2

Bwana atubariki na neema yake iwe pamoja nasi sote,

MUNGU AZIDI KUTULINDA NA NGUVU ZAKE ILI TUSIACHE WOKOVU KWA SABABU YOYOTE ILE

Hussein Allan

unread,
Apr 25, 2017, 4:39:11 AM4/25/17
to YourTrueVine, Bahati
> --
> Mimi ni mzabibu  ninyi ni matawi,  akaaye ndani yangu  nami ndani yake, huyo huzaa sana; maana pasipo mimi  ninyi  hamwezi kufanya   neno lolote.Yohana 15:5
> ---
> You received this message because you are subscribed to the Google Groups "YourTrueVine" group.
> To post to this group, send an email to yourtr...@googlegroups.com.
> For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

Eliezer....@nbctz.com

unread,
Apr 25, 2017, 4:40:59 AM4/25/17
to yourtr...@googlegroups.com
Amen,
Barikiwa kwa neno lenye nguvu ya kutusimamisha Imara kataika safari ya wokovu.

.

Important Notice:

The National Bank of Commerce Limited is a registered Commercial Bank in the United Republic of Tanzania.

This e-mail and any files transmitted with it are confidential and intended for the use of the individual or entity to whom they are addressed.

Please note that there are terms and conditions and some important restrictions, qualifications and disclaimers ("the Disclaimer") that apply to this email. To read this click on the following address or copy into your Internet browser:

http://www.nbctz.com/emaildisclaimer.asp

The Disclaimer forms part of the content of this email.
Reply all
Reply to author
Forward
0 new messages