TAFUTA KWANZA UFALME WA MUNGU

637 views
Skip to first unread message

Bahati Mashimba

unread,
Apr 16, 2012, 3:19:00 AM4/16/12
to yourtr...@googlegroups.com

Bali, zingatieni kwanza Ufalme wa Mungu na matakwa yake, na hayo mengine yote mtapewa kwa ziada. Mathayo 6:33


Yesu aliwaambia wanafunzi wake wasiwe na wasiwasi juu ya mahitaji  ya miili yao ya kwamba wale nini,wanywe nini,wavae nini. Mungu anajua kabisa  kwamba tunahitaji kuvaa, kula, kusoma,kuoa na kuolewa, nyumba, pesa, kuponywa magonjwa, ulinzi.Hayo yote  na meningine Mungu anayajua  na  hutupa nguvu na njia ya kuyapata.

Hata hivyo Mungu anataka tumjue yeye kwanza matakwa yake .Kwa kumjua yeye tupata muda wa kumtumikia, kusali, kusoma na kujifunza neno lake, kumtolea dhabihu ya miili yetu, kuhudhuria ibada na semina za neo lake, na kushika sheria zake.Unapoenda kazini nenda kazini kutafuta kwanza ufalme wake na pesa zitafuata maana Mungu anajua ili uwe napesa unahitaji ufanye kazi.Unapotaka kuoa au kuolewa tafuta kwanza ufalme wake na ndoa itafuata maana Mungu anajua muda wako wa kuoa na kuoelewa ukifika ni lazima uoe au uolewe.


Ndiyo maana watu wengi wanasumbuliwa sana na mioyo yao kutosheka,na hawaridhiki.Kile  wanachopata kila siku kwao hakitoshi. Ukiomba upate ubunge moyo utataka upate na uwaziri, ukiomba upate kazi yenye pesa nzuri, ukiipata kazi hiyo moyo utataka kazi nyingine yenye pesa  zaidi. Hitaji la  moyo  wa  mtu asiyezaliwa mara  ya  pili  huwa  halitosheki siku zote. Kama  mkristo  hajampa Mungu   nafasi  ya   kwanza  katika  maisha  yake  tatizo  hili  lazima limsumbue.Tunaona taifa letu watu wachache walio wakristo  na wasiomjua Kristo wenye nafasi serikalini wanavyojilimbikizia mali  kwa njia isiyo halali kwa sababu mioyo yao inatafuta kile ambacho hakiwezi kukidhi  haja za utajiri, ndiyo maana hawatosheki na wanachokipata.

Mpendwa tukitafuta kwanza ufalme wa Mungu na matakwa yake atatuwezesha kutupa moyo wa imani wa kumtumainia  yeye na atatupa yote tunayohitaji. Lazima tutambue kwamba  hofu ya Mungu husaidia mtu kupata baraka za Mungu kila siku.

Tunapoanza kuhangaikia mahitaji  yetu bila kumtafuta
Mungu,kujua  ukuu na uwezo wake  tunafananishwa na watu wasiomjua Mungu maana nao wanahangaikia kutafuta maisha kwa njia  kama wanavyofanya wanaomjua Mungu (Maana hayo yote yanahangaikiwa na watu wasiomjua Mungu. Baba yenu wa mbinguni anajua kwamba mnahitaji vitu hivyo vyote Mathayo 6:32)

Wapendwa  yatupasa tuanze siku na Mungu kwa kuomba ufalme wake utawale mahali pote tutakapokuwa kwa siku hiyo na kumkabidhi moyo na fikira zetu ili aweze kutupitisha katika njia iliyosalama na  kukuzidishia yote tunayohitaji.

Nawatakia baraka za Bwana na tuishi katika kuutafuta ufalme wa Mungu.
 


MaryGlady Heri

unread,
Apr 16, 2012, 3:59:26 AM4/16/12
to yourtr...@googlegroups.com
Asante sana Bahati,ni kweli uliyoyasema,Mungu azidi kukubariki kwa kutoa neno zuri sana!

2012/4/16 Bahati Mashimba <bahat...@yahoo.com>

--
Mkikaa ndani yangu na maneno yangu yakikaa ndani yenu basi ombeni chochote mtakacho nanyi mtapewa.Yohana15:7

Bahati Mashimba

unread,
Apr 16, 2012, 12:01:19 PM4/16/12
to yourtr...@googlegroups.com
Asante na Mungu akubariki
--
Hata niwapo taabuni napata kitulizo maana ahadi yako yanipa uhai.Zaburi119:50


Reply all
Reply to author
Forward
0 new messages