--- On Fri, 12/30/11, The Kingdom News: Maombi. <theking...@yahoo.com> wrote:
From: The Kingdom News: Maombi. <theking...@yahoo.com> Subject: Asante Yesu kwa 2011, Nakuamini kwa 2012 To: "The Kingdom News: Maombi. Member" <patmy...@yahoo.com> Date: Friday, December 30, 2011, 9:36 PM
--Damu ya Yesu--
|
The Kingdom News
Kanisa la Mtandaoni.
|
Huduma ya
Maombi. |
|
Asante Yesu kwa mwaka
2011, Ninakuamini Wewe kwa mwaka 2012.
"Mshukuruni
Bwana kwa kuwa ni mwema, na kwa maana fadhili zake zadumu hata milele"
Bwana Yesu asifiwe
daima!
Ninaamini unaendelea vyema na unatambua na kumshukuru Mungu kwa matendo makubwa
anayoyafanya katika maisha yako, kama Neno la Mungu lisemavyo,
"Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema, na kwa maana fadhili zake zadumu hata
milele" (Zaburi 107:1)
Ninayo furaha kuulete ujumbe
huu kwako, ikiwa ni siku ya mwisho kabisa ya mwaka 2011, na napenda
tutafakari kidogo kuhusu kuingia kwetu mwaka 2012.
Tulipokuwa tunakumbushana kujiandaa kwa mwaka 2011 (kwa wale walikowa wamejiunga
na Huduma hii tayari), nilifundisha kwamba ni muhimu kila mtu aandike mipango
yake ya mwaka mzima wa 2011 na kumwomba Mungu juu ya mipango hiyo na kuweka
mikakati ya kuitimiza. Wakati huu tunapoelekea mwisho wa mwaka, ni wakati mzuri
wa kila mmoja wetu kupima ni kwa kiasi gani umefanikiwa kuitimiza mipango yako
ya mwaka huu. Umefanikiwa na kushindwa kwa kiasi gani? Ni sababu gani
zimekufanya ushindwe kwa kiasi hicho? na kisha utazame ni namna gani unaweza
kufanikiwa zaidi katika mwaka ujao.
Jambo lingine la muhimu sana nililofundisha lilikuwa ni kumwomba Mungu akupe
Neno la kukuongoza kwa kipindi kizima cha mwaka 2011, Je, ulimwomba Mungu hili?
Je umeona uhusiano wowote wa Neno hilo na maisha yako kwa mwaka 2011?
Kama bado, basi tunapoingia mwaka 2012, ni vyema sasa kukaa faragha na Mungu na
kumwomba Mungu kuhusu maisha yako/familia yako kwa kipindi cha mwaka mzima wa
2012. Mwombe Roho Mtakatifu wa Mungu akupe ushauri/hekima ya kujipanga kwa ajili
ya 2012. Ni mambo gani unatamani kuyatenda ndani ya mwaka 2012?
•Ni mambo gani unatamani kumfanyia Mungu mwaka 2012?
•Ni mambo gani unatamani Mungu akufanyie 2012?
•Ni mambo gani utamani Mungu aifanyie familia yako mwaka 2012?
•Ni mambo gani kwenye maisha yako ambayo hutaki yajirudie tena?
Kwa maneno mengine, kaa chini uandike malengo yako kwa mwaka 2012, ni mambo gani
unatamani kuyafanikisha kwa msaada wa Mungu? Yaandike katika karatasi na
uyatunze vizuri. Jumuisha pia kama kuna mambo yoyote ya kitabia au yahusuyo
nafsi yako ambayo unataka kuyabadilisha ndani ya mwaka 2012. Kisha, weka
mikakati ya namna utakavyoyatimiza mambo hayo utakayopanga, na ukishafanya hivyo,
basi andika vizuri mipango hiyo na kisha anza kumwomba Mungu ili akusaidie
kuyafanikisha hayo yote yanayompendeza.("Moyo
wa mtu hufikiri njia yake, bali BWANA huelekeza hatua zake",
Mithali 16:9)
Mwombe Mungu akupe Neno lake la kukuongoza kwa mwaka mzima wa 2012, hili
litakusaidia sana kujua Mungu anataka uishi vipi 2012 na namna
utakavyoyashuhulikia mambo yatakayojitokeza mwaka huo. Hitimisha maombi yako kwa
kupeleka sadaka Kanisani unaposali na umweleze Mungu kuwa unaambatanisha sadaka
yako na maombi yako kwa ajili ya mwaka 2012. Karatasi uliyoandika mipango na
mikakati yako ya mwaka 2012 itunze ili uwe unaipitia kila baada ya muda fulani
kutathmini utekelezaji wake.
Usiache mwaka 2012 ukukute hujajiandaa kuupokea, jiandae vizuri kuuingia mwaka
huo, kumbuka "Aonavyo mtu
nafsini mwake ndivyo alivyo" (Mithali 23:7a, tafrisi kutoka KJV)
Mwaka 2012 utakuwa mwaka mwema kwetu sote.
Tuombe...
Mungu Baba, ninakuja mbele zako kwa Damu ya Yesu Kristo. Ninakushukuru sana kwa
ajili ya baraka zako kwangu katika mwaka mzima wa 2011. Baba, ninakuamini Wewe
tena kwa ajili ya mwaka mpya wa 2012. Ninakushukuru sana kwa ajili ya yale yote
ambayo umeniwezesha kuyatimiza kwa mwaka 2011, ninaomba unisamehe kwa yale
niliyoshindwa kuyatimiza kwa mwaka huu. Ninaomba unipe nuru yako kuhusu mwaka
2012, nifundishe namna ya kufanikiwa katika mwaka 2012. Ninakiri kuwa mwaka 2012
utakuwa ni mwaka wa mimi kuwekwa huru na kufanikiwa sana. Nimeomba na kuamini
haya kwa Jina la Yesu Kristo, Amen.
Katika kipindi hiki tunapoelekea mwaka mpya, ni jambo la faida sana nikiweza
kupata maoni kutoka kwako kuhusu Huduma hii. Ninawabariki wale wote ambao tayari
wameanza kunitumia maoni yao, nimeyaona na ninayazingatia. Kama bado, tafadhali
nipatie maoni yako kwa
kubonyeza hapa
na kujaza fomu fupi ya maoni.
Nakutakia kila la heri katika
mwaka 2012.
Yesu Kristo ni Yeye yule,jana leo na hata milele;
(Maandiko ya Biblia niliyotumia katika ujumbe huu ni kutoka tafsiri ya NENO
BIBLIA, isipokuwa pale nilipoonesha tofauti)
|
|
|
|
|
Mungu aibariki sana kampuni ya Digital
Brain (www.digitalbraintz.com)
kwa kuendelea kudhamini huduma hii ya kwenye mtandao. Mungu Aliye
juu Mbinguni na awabariki sana na kuwapa neema ya kukua na kufanikiwa
ulimwenguni pote, Amen.
|
|
|
Unapokea ujumbe huu wa Neno la
Mungu
baada ya kujiunga au kuunganishwa na mwenzako katika Huduma hii ya Kanisa la
Mtandaoni la Kingdom News. Kama umepokea Ujumbe huu baada ya rafiki yako ku-forward kwako,
basi unaweza kujiunga mwenyewe katika huduma hii kwa kutembelea
www.TheKingdomNews.org ili uendelee
kupokea ujumbe katika email yako.
Tafadhali wafahamishe wengine kuhusuhuduma hii na ubarikiwe na Bwana.
Kwa maswali/mahitaji yoyote kuhusu Huduma hii, wasiliana nami:
email:
thekingdomnews@yahoo.com
Ubarikiwe na
Bwana.
Hizi ni taarifa muhimu kuhusu namna
ulivyounganishwa na Huduma hii ya Mtandaoni:
Umeunganishwa katika huduma ya:
The Kingdom News: Maombi.
Umeunganishwa kwa kutumia email :
|