NENO LA LEO - MUNGU NI KIMBILIO LETU

8,746 views
Skip to first unread message

Bahati Mashimba

unread,
Sep 28, 2011, 1:55:31 AM9/28/11
to yourtr...@googlegroups.com
From: Eliezer Mwangosi <eliezer....@gmail.com>
To:
Sent: Wednesday, September 28, 2011 5:16 AM
Subject: NENO LA UZIMA 28.09.2011 - MUNGU NI KIMBILIO LETU

Salaam,

NENO LA LEO:  ZABURI 46:1-2
“Mungu kwetu sisi ni kimbilio na Nguvu, Msaada utakaoonekana tele wakati wa mateso. Kwa hiyo hatutaogopa ijapobadilika nchi, ijapotetemeka milima moyoni mwa bahari. Maji yake yajapovuma na kuumuka, ijapopepesuka milima kwa kiburi chake”
 
TAFAKARI:
Sitasahau kisa cha mama mmoja aliyejulikana kama mcha Mungu, lakini siku moja alishikwa uchawi, baada ya kukutwa makaburini usiku akiwa uchi. Baadaye iligundulika huyo mama hakuwa mchawi, ila alienda makaburini usiku kwa mashariti ya Mganga wa Kienyeji ili kuondoa Mikosi inayofanya Ndoa yake isambaratike na kuwa kama Jela ndogo, Ndoa imegeuka kuwa Ndoano. Siku ya tukio alilia kwa uchungu, akidai Ndoa yao ni Changa, lakini haina AMANI wala Furaha.
 
Mtumishi wa Mungu Daudi ana ujumbe wa matumaini, pamoja na Dhambi  yake ya Uzinzi na mauwaji ya kutisha katika familia ya Uria, alipomwendea Mungu kwa TOBA ya Dhati, alisamehewa dhambi zake na kila mara aliokolewa na Mungu kutoka katika Mikono ya Watesi.
 
Rafiki!  japo dhoruba iliyomfano wa sumani ipite katika – Ndoa yako, Biashara yako, Kazi yako, Afya yako, Mashamba yako, au maisha yako kwa Ujumla. Usifadhaike, Mungu yupo kwa ajili yetu daima ni MSAADA NA KIMBILIO LETU, KWAKE HAKUNA LISILO WEZEKANA.
 
 
KATIKA JINA LA YESU KRISTO KILA MISHALE IKAVUNJIKE – AMANI, UPENDO NA FURAHA VIKATAWALE SAWASAWA NA AHADI ZA BWANA.
 
 
BARAKA ZA BWANA ZIAMBATANE NANYI DAIMA, NA KUWA NA SIKU NJEMA.
 
 
 
Na: Eliezer  Mwangosi
 



Warema S.Senzia

unread,
Sep 28, 2011, 2:57:41 AM9/28/11
to yourtr...@googlegroups.com
Asante sana Eliezer.
Ni kweli MUNGU ni kimbilio letu na hatatuacha kamwe.
Daudi katika zaburi ya 37:25 anasema "Nilikuwa kijana na sasa ni mzee, sijawahi kumwona mwenye haki akiachwa au watoto wake kuombaomba mikate barabara". MUNGU ni mwaminifu hatotuacha kama mtumishi wake Daudi alivosema.
Asante na MUNGU akubariki
 
Senzia.
 
"...Surely goodness and love will follow me
all the days of my life, and I'll dwell in the house of the LORD forever"
 

--
Usikubali kushindwa na ubaya bali ushinde ubaya kwa wema.Waroma12:21


Eliezer Mwangosi

unread,
Sep 28, 2011, 3:15:39 AM9/28/11
to yourtr...@googlegroups.com
Amina,

Regards
Eliezer

Important Notice:

The National Bank of Commerce Limited is a registered Commercial Bank in the United Republic of Tanzania.

This e-mail and any files transmitted with it are confidential and intended for the use of the individual or entity to whom they are addressed.

Please note that there are terms and conditions and some important restrictions, qualifications and disclaimers ("the Disclaimer") that apply to this email. To read this click on the following address or copy into your Internet browser:

http://www.nbctz.com/disclaimer/email

The Disclaimer forms part of the content of this email.

 

Bahati Mashimba

unread,
Sep 28, 2011, 3:32:24 AM9/28/11
to yourtr...@googlegroups.com
Mpendwa Eliezer Bwana akubariki sana kwa neno la leo.
Ni kweli Mungu ni msaada wetu wakati wote.Tumkabidhi yeye njia zetu na kuweka matumaini yetu kwake naye atatuokoa na dhoruba zote tunazokutana nazo katika maisha yetu.Tusilegee katika imani kwasababu ya dhiki nyepesi zilizo za muda wa kitambo tu.BWANa ametuahidi tumuite siku ya mateso naye atatuokoa...Zab50:15.
 
Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo  iwe pamoja nasi sote,
 
 
 Humble yourselves in the sight of the Lord and he shall lift you up James4:10


2011/9/28 Eliezer Mwangosi <Eliezer....@nbctz.com>

Deborah Mgedzi

unread,
Sep 28, 2011, 7:29:56 AM9/28/11
to yourtr...@googlegroups.com
Amen
Reply all
Reply to author
Forward
0 new messages