NENO LA LEO

64 views
Skip to first unread message

eliezer.mwangosi

unread,
Jun 7, 2016, 10:05:51 PM6/7/16
to
NENO LA LEO 👉 KUBALI YESU APINDUE MEZA

Mathayo 21:12-13 "Yesu akaingia ndani ya hekalu, akawafukuza wote waliokuwa wakiuza na kununua hekaluni, akazipindua meza za wabadili fedha, na viti vyao waliokuwa wakiuza njiwa; akawaambia, Imeandikwa, Nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala; bali ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang'anyi".

Katika nyakati hizi za upofu mkubwa wa kiroho, ni rahisi sana kutotambua na kutofautisha mambo matakatifu na mambo ya kawaida. Wayahudi walienda mbali zaidi, wakageuza hekalu la Mungu kuwa nyumba ya kufanyia biashara, ketendo ambacho Yesu alikemea na kuchukua hatua ya kuwafukuza na kuziondoa biashara zao, hatimaye Hekalu likarudishiwa hadhi ya kuwa Nyumba ya kumwabudu Mungu.

Kama ilivyokuwa kwa hekalu la Mungu, kutumika visivyo, ndivyo ilivyo katika maisha ya wengi kuitumia miili yao kuwa pango la wanyang'anyi. Wengi wamekuwa vipofu, hawatofautishi mambo ya Mungu na mambo ya Kidunia. Hawajui kuwa miili yao ni MAHEKALU ya Roho mtakatifu.

Mungu kwa kinywa cha mtume Paulo anasema: 1Wakorintho 6:19 "Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni HEKALU la Roho mtakatifu aliye ndani yenu mliyepewa na Mungu? Wala ninyi si Mali yenu wenyewe; maana mlinunuliwa kwa thamani. Sasa basi, mtukuzeni Mungu katika miili yenu."

Hebu kila anayejiita Mkristo au mtu wa Mungu ajiulize; mwili wake anautumiaje? Tabia yoyote iliyo nje ya mapenzi ya Mungu ni BIASHARA ndani ya hekalu la Mungu. Iwe ni Uongo, wivu, uchochezi, rushwa, uonevu, kupendelea, uchoyo, wizi kwa aina zote, ulaghai, masengenyo, ulevi wa pombe na sumu za madawa, kuingilia ndoa za watu, vitendo vya Uzinifu na Uasherati, kutingisha viuno kwenye madisco, na mambo yanayofanana na hayo ni Biashara chafu katika hekalu la Mungu.

Ni Yesu pekee anayeweza kurudisha hadhi ya UTAKAYIFU wa hekalu, ili lifae kwa Kazi takatifu ya kumfanyia Mungu Ibada ya kweli, kwa kuwapo Roho Mtakatifu. Huu ni wakati muafaka wa kila mmoja kujihoji na kuchukua uamuzi wa Kumruhusu Yesu kuingia ndani ya Moyo na Kufanya Kazi ya KUZIPINDUA MEZA na kutoa nje kila uchafu wa Mawazo kwa ajili ya Utukufu wa YEHOVA.

NAWATAKIA WOTE SIKU NJEMA NA YENYE BARAKA TELE.

Na: Ev. Eliezer Mwangosi.
Simu: 0767210299.




Sent from Samsung tablet

Mtoka James

unread,
Jun 8, 2016, 2:21:10 PM6/8/16
to yourtr...@googlegroups.com

Amen mubarikiwe nyote

--
Mimi ni mzabibu ninyi ni matawi, akaaye ndani yangu nami ndani yake, huyo huzaa sana; maana pasipo mimi ninyi hamwezi kufanya neno lolote.Yohana 15:5
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "YourTrueVine" group.
To post to this group, send email to yourtr...@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

eliezer.mwangosi

unread,
Jun 14, 2016, 9:09:47 PM6/14/16
to
NENO LA LEO - TOKENI KWAKE ENYI WATU WANGU
Ufunuo 18:4 "Kisha nikasikia sauti nyingine kutoka Mbinguni, ikisema, TOKENI KWAKE, ENYI WATU WANGU, msishiriki dhambi zake, wala msipokee mapigo yake".

Wakati dunia yetu ikiwa inazidi kupunga mkono wa KWAHERI, ikiaga taratibu lakini kwa uhakika, ikifikia mwisho kutokana na kikombe cha uovu kujaa, kama ilivyokuwa wakati wa Nuhu na Miji ya Sodoma na Gomola; Mungu anatoa onyo la Mwisho. Mwenye masikio na asikie.

Shetani na mawakala zake, wakiwemo viongozi wa dini mbalimbali na manabii watendao kazi ya Injili kwa Hila, wameijaza Dunia kila namna ya uchafu, na wengi bila kujua wanaandaliwa hukumu ya mwisho. Dunia hii iko chini ya Laana kubwa, japo masikio ya wanadamu yametiwa pamba, na macho yao yametiwa upofu, wasiweze kuipambanua Dhambi. Dini zimekuwa za mtindo na nadharia tu, hofu ya dhambi haipo tena.

Nabii Isaya alitabiri: Isaya 24:4-6 " Dunia inaomboleza, inazimia; ulimwengu unadhoofika, unazimia; watu wakuu wa dunia wanadhoofika. Tena dunia imetiwa unajisi kwa watu wanaoikaa; kwa maana WAMEZIASI SHERIA, WAMEIBADIRI AMRI, WAMELIVUNJA AGANO LA MILELE. Ndiyo sababu LAANA imeila Dunia hii, na hao wanaoikaa wameonekana kuwa na HATIA ......". Viongozi wa Dini waliohusika kubadili Amri za Mungu na wale wanaoendelea kufundisha Amri tofauti na NENO la Mungu, ndio wanaendelea kukijaza kikombe cha UOVU na kuilemea Dunia. 

Kuna watu ambao walisha chagua kupotea na kuwa Kuni katika moto wa Jehanamu, lakini kwa bahati mbaya sana, kuna watu wa Mungu wazuri, ambao wamedhamiria kupata uzima wa milele, ila adui shetani amewapotosha kwa njia ya Manabii na Viongozi wa dini walio amua kupotosha kweli ya Mungu. DHAMBI ni UASI wa sheria za Mungu, leo hii SHERIA za Mungu zimekuwa kitu kigeni kwa watu wa Dini, unashangaa watu wanabishana juu ya Utii wa Sheria za Mungu na kuzua Uongo kuwa Yesu aliziondoa, wakati Yesu alikuja kutuokoa, yaani kutupatia msamaha na USHINDI wa dhambi.

Dhambi za Ushoga, Usagaji, na mbaya zaidi kujibadili Jinsia, na uzazi wa chupa wa kununua mayai ya kiume na kupandikizwa tumboni mwa mwanamke, ili kupata mtoto nje ya tendo la ndoa, ni UCHAFU uliokijaza kikombe cha uovu dunia yetu, na kuiamsha hasira ya Bwana. LAANA zote hizi ni matokeo ya kutiwa giza, Katika kuipambanua na kuitii sheria ya Bwana.

Rafiki; huu ni wakati wa kumwambia Bwana akupatie macho ya kuiona sheria ya Bwana kama alivyoitoa, ruhusu Yesu akupatie uwezo wa Roho mtakatifu ili uweze kutembea katika utii na ushindi na hatimaye kuwa kati watakatifu, hao wazishikao Amri za Mungu na Imani ya Yesu - Ufunuo 14:12 "Hapa ndipo penye subira ya watakatifu, hao wazishikao Amri za Mungu, na Imani ya Yesu".

WITO: TOKENI KWAKE ENYI WATU WANGU .... MPINGENI SHETANI ..... MTIINI MUNGU.
Hebu kila mmoja ajifunze Amri za Mungu na kuruhusu Roho mtakatifu atawale maisha yetu, ili tuishi maisha matakatifu bila kuhukumiwa. Wokovu halisi ni maisha ya utii wa Amri za Mungu ndani ya Kristo. Hebu tafakari: Zaburi 119:155 "Wokovu u mbali na wasio haki, kwa maana hawajifunzi Amri zako".

WEMA WA MUNGI UKAWE JUU YA KILA MMOJA MWENYE KUISIKIA SAUTI YA WITO HUU MKUU. NAWATAKIA SIKU NJEMA.

Na: Ev. Eliezer Mwangosi - Simu: 0767 210 299.




Sent from Samsung tablet

eliezer.mwangosi

unread,
Jun 23, 2016, 11:09:55 PM6/23/16
to
NENO LA LEO - MTAZAME ALIYE KARIBU NAWE

Zaburi:34:18 "Bwana yu karibu nao waliovunjika moyo, Na waliopondeka roho huwaokoa".

Ni jambo la kawaida kuona watu wakihangaika kutafuta msaada juu ya changamoto zinazo wapata. Ndivyo tunashuhudia wengine wanachukua maamuzi magumu hata ya kujiua, baada ya kushindwa kupata msaada. Hebu kila mmoja apige picha, tatizo linapotokea, nani anakuwa wa kwanza kumwendea ili kupata msaada? Wengi watakuambia, ni wazazi, au mume, au mke, au Rafiki, au daktari bingwa, au Mchungaji n.k. kutokana na aina ya tatizo.

Neno la leo linatukumbusha kuwa; mbali na kumtegemea mtu fulani mwenye uwezo wa kukusaidia unapopitia machungu katika maisha haya, Karibu yako yupo Mungu mwenye uwezo zaidi ya wote wanaoweza kutegemewa. Mara nyingi shetani ametudanganya na kututenga na Upendo wa Mungu, na hatimaye akitujeruhi, tunakosa ujasiri wa kuutegemea mkono wa Mungu, macho huwa hayaoni, giza la machungu na simanzi huujaza moyo, na hatimaye wengine, huamua kujiua, wengine huishia kuugua vidonda vya tumbo na shinikizo la damu.

Kumbuka, mwanadamu yeyote sio wa kutegemewa, wakati wowote anaweza kugeuka au hali ikabadilika, wengi wamejeruhiwa na wenzi wao waliokuwa wameijaza mioyo yao, na wameishia kuathirika kwa namna fulani, katika hali kama hiyo ni Mungu pekee aliye Karibu sana na kila mmoja, anaweza kukuokoa katika hali ya kuvunjika moyo.

Unapojeruhiwa na kuumizwa moyo, iwe kwa magonjwa, iwe kwa kuteswa na nguvu za uchawi au majini, iwe kwa kukosa ajira, iwe kwa kushindwa masomo, iwe kwa umaskini, iwe kwa kufiwa na mwenzi, iwe kwa biashara kuporomoka, iwe kuonewa kazini, iwe kwa kukosa mchumba, iwe kwa mwenzi wa ndoa kukutesa kimahusiano, iwe ni kutengwa na marafiki, iwe ni kuonewa na ndugu, iwe ni changamoto yoyote inayo kuumiza na kujeruhi moyo wako; Mungu yuko Karibu nawe KUKUOKOA, mtazame yeye utakuwa salama. Yesu alikufa kwa ajili yetu, ili tuokolewe na kupatanishwa na Mungu Baba, mtazame yeye Uokolewe.

WEMA WA MUNGU NA UPENDO WAKE UKAONEKANE KWA KILA MMOJA WETU DAIMA.

NAWATAKIA SIKU NJEMA YENYE BARAKA NA MAFANIKIO TELE.

Na. Ev. Eliezer Mwangosi.
Simu: 0767 210 299




Sent from Samsung tablet

eliezer.mwangosi

unread,
Jun 29, 2016, 11:09:55 PM6/29/16
to
NENO LA LEO - SIRI YA KUPATA AMANI YA KWELI

Yohana:14:27 "Amani nawaachieni; amani yangu nawapa; niwapavyo mimi sivyo kama ulimwengu utoavyo. Msifadhaike mioyoni mwenu, wala msiwe na woga."

Siku moja nikiwa nasafiri kwa basi, nilikaa karibu na mama mmoja, mara baada ya muda mfupi nikasikia simu yake inaita, alipoipokea akaanza kuporomosha matusi kwa kufoka, huku akifyonya. Muda haukupita nikamuona anaanza kulia. Ilibidi nitulie na kuanza kumuombea kimoyomoyo, ili Bwana atulize dhoruba iliyo katika moyo wake, make niliona akiwa na stress kubwa.

Baada ya nusu saa kipita alionekana kutulia, ndipo nikaamuliza lililomsibu, akaongea kwa jazba akasema "Si MBWA huyu anautesa moyo wangu!" Kupitia maelezo yake niligundua mume wake hakulala nyumbani, alipitia kwa Mchepuko hadi asubuhi. Mke wake alionyesha hali ya kuchoshwa na kuumizwa kwa usaliti wa mapenzi, kiasi kwamba kila siku alikuwa na stress au msongo wa mawazo.

Kadiri siku zinavyosonga, ndivyo idadi ya watu wanaoishi na misongo ya mawazo inavyozidi kuongezeka, huku wakiathirika kiafya na hata katika ufanisi wa kazi zao. Neno la leo, linatuongoza kumtegemea Yesu Kristo wakati wote tunapopitia changamoto zenye machungu na kuumiza mioyo yetu.

Wengi ni mashahidi kuwa AMANI ya kweli na ya kudumu, inapatikana kwa Mungu. Kuna waliojijengea wigo wa Amani kwa wapenzi wao, mara walishangaa wakipitia machungu baada ya kujeruhiwa na waliokuwa wanawaamini. Hakuna kitu chochote kinachoweza kutupatia AMANI ya kudumu nje ya Mungu.

Hebu kila mmoja wetu aweke Imani yake kwa Mungu, usiruhusu mwanadamu mwenzio abebe nafsi yako, wala pesa isishike nafsi yako, wala kitu chochote, hivyo vyote vinabadilika bila kutarajia. Upendo wa mwanadamu kwako unaweza kutoweka na kuhamia kwa mwingine, lakini Upendo wa Mungu kwako ni wa milele. Mwamini na Kumtegemea Mungu, naye ataujaza moyo wako Amani Kamilifu, mawimbi yakipita HUTAFADHAIKA.

AMANI YA KRISTO IKAIJAZE MIOYO YETU FURAHA NA TUMAINI DAIMA.

NAWATAKIA SIKU NJEMA YENYE BARAKA TELE.

Na: Ev. Eliezer Mwangosi
Simu: 0767 210 299. Kwa ushauri na maombi.




Sent from Samsung tablet

eliezer.mwangosi

unread,
Jul 7, 2016, 12:38:11 AM7/7/16
to
NENO LA LEO - USISUBIRI URUSHIWE JIWE

Msimamizi wa ujenzi alikuwa anamwita mjenzi chini ya jengo yeye akiwa ghorofa ya 16. Lakini kwa sababu ya kelele za nje, mjenzi pale chini hakusikia sauti hiyo.

Ili kumfanya mjenzi ashtuke, msimamizi alirusha noti ya sh elf 5, kutoka juu na ikaangukia alipo mjenzi yule. Mjenzi aliokota, akaweka mfukoni na kuendelea na shughuli zake.

Msimamizi akarusha tena noti ya elf 10 kwa mjenzi yule. Kwa nia ya kumshtua ili wawasiliane, wakati huu pia mjenzi aliokota ile elf 10, akaiweka mfukoni na kuendelea na shughuli zake.

Sasa msimamizi akaamua kuchukua kajiwe kadogo na akarusha kakampata mjenzi. Safari hii, kwa sababu kale ka jiwe  kalimuumiza, aliangalia juu ajue kalipotoka, Ndipo msimamizi alipopata nafasi ya kuwasiiana.

Hebu tafakari kwa muda. Mungu anataka mawasiliano nasi, lakini tuko busy na shughuli zetu za dunia hii.
Anatupa zawadi/ baraka kubwa na ndogo tunazichukua na kuzifurahia bila hata kujua zinatoka kwake, bila hata kushukuru. Na mara nyingi tukijisifu kuwa TUMEBAHATIKA.

Lakini pale tunapo rushiwa kajiwe kadogo, ambacho tunaita (MATATIZO), ndipo tunamkumbuka Mungu.
Hapo ndipo tunapoomba/sali na kuwasiliana na Mungu.

Mungu anatupatia vyote na kutusamehe dhambi, sisi tunapokea na kusahau, tubadilike, Mungu hafurahii.

Tusisubiri turushiwe mawe, wakati wote tumkumbuke na kumsifu Mungu.

Tufanye kumuomba,kumshukuru na kumsifu Mungu iwe sehemu ya maisha ya kila siku.

MUNGU AWABARIKI NA KUWAPATIA SIKU NJEMA.




Sent from Samsung tablet
Reply all
Reply to author
Forward
0 new messages