Jeuri ya serikali na CCM ipo wapi?

6 views
Skip to first unread message

Lemburis Kivuyo

unread,
Nov 21, 2011, 1:08:21 AM11/21/11
to Wazalendo Dot Net
Muswada wa kubadili katiba umepitishwa kibabe na kwa jeuri bila ya
kuwashirikisha wadau mhumi ambao ni wananchi, wanaharakati, wanazuoni,
wanasisasa hasa CHADEMA nk huku CCM na serikali yake wakifikiri
watranzania wengi wapo nyuma yao. Uchaguzi wa 2010 ulionyesha kuwa
wanaoiunga CCM ni wachache kati ya wapiga kura Mil 19 ni mil 5 tu
wlikipigia CCM tena baada ya uchakachuaji. inawezekana kabisa CCM kwa
sasa wanasupotiwa na idadi ya watanzania wasiozidi mil 2 nchi nzima.

Sasa wao kupitisha muswada wakidhani Watanzania wengi wako nyuma yao,
ikija kuonekana kuwa Watanzania wengi wanachukuzwa na nyendoi hizo za
CCM watajifichia wapi?

Ndio maana baadhi ya watanzania waliochoka wameamua kuanza kuwatishia
viongozi wa serikali kwa kuwapa siku 100 kuondoka kwneye nyasifa zao
vinginevyo yatawapata.... Wao badala ya kujadili namna ya kubadili
tabia zao na jinsi wanavyoongoza nchi ili hasira za watanzania zipoe,
wanafikiri jeshi la polisi na ulinzi wataweza kuziba ufa
unaosababishwa na ufisadi wao.

Leo wanatishia, kesho vijana wataingia msituni na support kubwa ya
watanzania walichoka kila kitu.

Mimi hii nchi, serikali na CCM wananichosha sana

Ukimtupia raisi mawe ili kuonyesha hasira yako unaitwa mhuni
Mimba za wasichana mashuleni yanaongezeka kwa sababu ya umasikini
unaoongezeka wanaambiwa wamejitakia
Wanafunzi wakiandamana kwa sababu ya kunyanyaswa wanaambiwa wanatumiwa
na wanasiasa
Wazee wakiandamana kudai mafao yao wanaambiwa wanatumiwa na wanasiasa
Waalimu wakigoma kwa kudai masilahi yao, hadithi ni ile ile
Watanzania wakitaka kuandamana kuelezea hisia zao, yaleyale
Sasa watanzania wafanyeje?
Waendelee kuvumilia shida, na ukal;i wa maisha kama morani
anayetahiriwa
Tulidhani katiba mpya ndio itaondoa uozo huu wa chama kimoja kuwa
dikteta wa maisha yetu hata kama hatuwataki wameaza na huko
kuchakachuwa

Kazi ipo

Lembu

Reply all
Reply to author
Forward
0 new messages