Kushuka kwa thamani ya Shilingi ya Tanzania

231 views
Skip to first unread message

Phares Magesa

unread,
Apr 29, 2015, 10:43:59 AM4/29/15
to wanataaluma TPN Group

Wanataaluma,

 

Habari za siku ndugu zangu Wazalendo !

 

Nadhani kila mmoja ameona ambavyo thamani ya fedha yetu ilivyoshuka thamani katika historia ya nchi yetu tangu tupate uhuru.

 

Kushuka kwa thamani ya fedha ya nchi yoyote haina maana ya kuonyesha moja kwa moja kuwa uchumi wa nchi husika umeshuka au umeathirika, hivyo basi  kushuka au kupanda kwa thamani ya fedha kuna faida na hasara kulingana na mfumo na mpangilio wa kiuchumi wa nchi husika. Ziko nchi hufaidika kwa kushusha thamani ya fedha zake makusudi kwa malengo ya kupandisha kiwango cha mauzo ya nje na kuuza zaidi.

 

Mengi yanasemwa kuhusu sababu za kushuka kwa thmani ya fedha yetu dhidi ya dola ya Marekenai sasa nikaribishe michango kama kuna mdau yoyote ndani ya jukwaa hili anaweza kutuelimisha zaidi.

 

Noamba tuchangie mada hii kwa lengo la kuelimishana sababu, faida na hasara na nini kifanyike,  labda kupitia jukwaa hili kuna mambo yanaweza yakachukuliwa na watunga sera wetu ambao baadhi yao ni wanchama wa mtandao huu ili kusaidia kujenga uchumi wetu.

 

Maana taarifa muhimu wananchi wasipoelimishwa vizuri kwa kupewa taarifa sahihi na kwa wakati sahihi inaweza ikasababisha wananchi kupaniki na kuleta athari zaidi kwenye uchumi , mfano ni jinsi uchumi wa dunia ulivyoyumba miaka ya 2008/2009  sababu moja ilichangiwa na wananchi wa Marekani na Uingereza kutopata taarifa sahihi kwa wakati sahihi na ikapelekea wengi wao kufanya maamuzi yasiyo sahihi ya kiuwekezaji/kifedha yaliyosababisha kuyumba kwa uchumi wote wa dunia.

 

Hivyo basi naomba nitoe wito kwa wote tuwe huru kutumia jukwaa hili na majukwaa mengine kwa lengo la kuelimishana na kupashana habari mbali mbali zilizo sahihi kwa faida yetu wote.

 

Wasalaamu.

 

Phares Magesa ,

B.Sc,PGDSE,MBA, IEng.,MIET
----------------------------

Mtaalamu na Mshauri wa TEHAMA, Menejimenti na Uongozi

 

Rais -  Mtandao wa Wanataaluma Tanzania (TPN)

www.tpntz.org

 

Cell: +255 (0784/0713/0767) 618320

 

E-mail:   mag...@tanzaniaports.com

                pma...@gmail.com

                mag...@hotmail.com

Herment Mrema

unread,
Apr 29, 2015, 1:25:22 PM4/29/15
to wana...@googlegroups.com, wanataaluma TPN Group
Magesa et al

Ninavyoelewa na kama Gavana w Benki Kuu alipokwisha kuitolea maelezo kuhusu kushuka kwa thamani ya shillingi sababu kubwa ni kukua kwa uchumi wa marekani kwa kasi kubwa labda nitoe ya kuongezea.  Kwa ujumla confidence ya public kwenye hali ya uchumi wetu ni ya chini hasa kutokana na ukweli kuwa kutakuwa na change of regime.  Hata kama Chama tawala kikiwa kitaendelea kuongoza nchi lakini inaelekea kutakuwa na mabadiliko makubwa ya msingi, kisera na strategically au kimkakati.  Hiyo inafanya wafanyabiashara wengi kuoperate uchumi kwenye kiwango kidogo. Hata production kwa ajili ya kuexport imepungua labda Benk kuu watujuze hali ya exports ikoje.  Vile vile wakati dola inapanda ni kawaida kwa dhahabu kushuka bei hivyo dola tonazopata kutokana na mauzo ya dhahabu ni chache.

Kuchelewa kwa CCM kutoa mwanga ni nani anaweza kuwa Raisi kwa kipindi kijacho nayo imechangia woga wa watu kuhusu stability ya nchi hasa kwa vile kunaonekana kuna msuguano ndani ya chama au makundi ndani ya chama.  Watu wanahisi kuwa hwenda CCM ikagawanyika kutokana na makundi kitu ambacho sio chema kwa nchi kwani CCM legelege itafanya nchi kuwa legelege.

Sababu nyingine ni kuwa mauzo yetu ya nje bado sio mengi kiasi cha kupambana na dola iliyo na nguvu.  Tungekuwa na dola nyingi kwenye soko kutokana na mauzo mengi ya bidhaa, madini na mazao mengine kungefanya dola ziwe nyingi kwenye soko kuliko mahitaji ikiwa na maana kuwa bei ingeshuka

Sababu ingine ambayo ninaifikiria na kuwa licha ya kuwa uchumi wa marekani umekuwa kwa kasi na manunuzi ya mafuta bado ni ya chini kwa upande wa Marekani labda kuna watanzania wachache wanahamisha fedha kuogopa kuwa matokeo ya uchaguzi ujao unaweza ukawaathiri kibiashara au kukawa na regime change ambayo itakuwa na policy change ambayo hawana uhakika itawalinda wenye mitaji yao nchini.

Kuna sababu nyingi lakini kwa elimu yangu ndogo ya uchumi huo ni mchango wangu

Herment A. mrema


From: mag...@hotmail.com
To: wanat...@googlegroups.com
Subject: [wanabidii] Kushuka kwa thamani ya Shilingi ya Tanzania
Date: Wed, 29 Apr 2015 08:43:57 -0600
--
Send Emails to wana...@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+...@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+...@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

Bubelwa E. Kaiza

unread,
Apr 29, 2015, 3:53:32 PM4/29/15
to wanat...@googlegroups.com, wana...@googlegroups.com

Mrema,

Umeongea kiasi fulani ila sababu za kushuka kwa Tzs. dhidi ya dola ya kimarekani ni hizi zifuatazo:-

1.  Kuvuja kwa uchumi (economc leakage)/matumizi holela ya dola kwenye mzunguko wa ndani ya nchi wa fedha. Duniani kote, kuendesha uchumi imara kunahitaji mikakati na taasisi imara za kusimamia sera, sheria na kanuni za fedha. Nchini Ufaransa, kwa mfano, hairuhusiwi kubadilisha/kununua Euro taslim zenye thamani ya zaidi ya dola 1000! Afrika ya Kusini hairuhusiwi kutumia dola/euro isipokuwa rand tu unaponunua mali au huduma yoyote (hotelini, ticket za ndage n.k). Hapa nchini kwetu hali ni shaghala baghalamamlaka zinazopaswa kusimamia uchumi wa nchi hazifanyi chochote; bureaux de change zinahamisha mauzo ya kila siku ya madukani kwenda nje ya nchi.

 

2.  Watu, hasa mafisadi, kutorosha/kuhodhi dola nje ya nchi kutokana na hofu ya uchuguzi mkuu. Hali hii inasababisha uhaba wa dola hivyo kutengeneza artificial appreciation ya dola kutokana na msingi mkuu wa uchumi wa demand vs. supply.

 

3.  Tanzania kutokuwa na dhahabu ya kuuza nje ya nchi (dhahabu inayochimbwa siyo ya kwetu bali ni ya makampuni yanayochimba (wawekezaji) na zaidi ya 90% ya mauzo ya dhahabu na madini mengine nje ya nchi hairudishwi nchini bali yanabaki huko (clauses za MDAs zinatoa fursa hizo kwa makampuniya madini) nyumbani kwao na wawekezaji. Kwa kifupi Tanzania siyo gold mining country bali ni source of gold, hivyo haimiliki madini yanayochimbwa nchini kwake bali madini husika humilikiwa na nchi mama wa makampuni ya wawekezaji.

 

4.  Kuwa na weak manufacturing, construction and professional services industries hivyo nchi kutegemea imports zaidi kuliko uwezo wa kuuza huduma na bidhaa nje ya nchi. Aidha mauzo ya mazao ya kahawa, pamba, katani na chai nje ya nchi yamepungua kufikia negligible value. Nchi isipouza bidhaa na huduma za kutosha nje ya nchi haiwezi kuwa na akiba ya kutosha ya fedha ya kigeni. Na kwa mukhtadha huu, thamani ya fedha ya nchi haiwezi kuimarishwa na pesa ya misaada au mikopo kutoka kwa wafadhali au mashirika ya Bretton Woods.

 

5.  Impact ya wizi wa pesa ya akaunti ya Tegeta Escrow (wafadhili kuzuia pesa ya misaada ya kibajeti). Zipo sababu nyingine pia zinazoathiri uchumi wa nchi (kuwa wa hovyo) kama Tanzania ambazo watu wake wengi bado hawategemei maarifa na ujuzi, bali ardhi na bidhaa, hususan kutokana na tasnia ya uziduaji.

 

Najua MNEC-CCM Magesa anatafuta hoja za ku-pacify hali mbaya inayokikabili chama chake ila ukweli ndio huo (free consultancy).

 

Kaiza      

--
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanataaluma wa Tanzania" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanataaluma...@googlegroups.com.

ymshana2003

unread,
Apr 30, 2015, 4:11:56 AM4/30/15
to wanat...@googlegroups.com
Kwa kuongezea tu...
Ile Sera ya "kujitegemea" imeloweshwa maji....basda ya wito wa "Ruksa" kujichanganya katika biashara tukasahau kujichanganya katika mambo ya"uchumi"....
BoT haitoshi katika shughuli ya "Economic Intelligence" ili kuzuia shughuli za 'Ecomic Hitmen' wanaoweza kuangusha uchumi wa nchi kirahisi tu.....hasa hasa baada ya kupata mnuso wa gas....kuna wataalam wataendelea kuja 'kutusaidia' na "kujisaidia zaidi" kwani kuna soko Tz. Usimamizi wa hao "wataalam" ingebidi uwe wa karibu zaidi kwani tunao wataalam wetu ambao Mfumo uliopo hauwahusishi vilivyo....

Naishia hapo.

Yassin Mshana

Ni hayo tu kwa leo.
Sent from Samsung Mobile

Makori Breens

unread,
Apr 30, 2015, 4:32:27 AM4/30/15
to wanat...@googlegroups.com
Je,Kenya walitupita wapi?Shilling ya Kenya ni thabiti kulingana na
yet.Dolla Moja ya Marekani nchin Kenya ni Ksh.93 ilihali hapa Tanzania
dhidi ya Tsh ni Maelfu
> - mamlaka zinazopaswa kusimamia uchumi wa nchi hazifanyi chochote; bureaux

ymshana2003

unread,
Apr 30, 2015, 4:48:39 AM4/30/15
to wanat...@googlegroups.com
Jibu la kuhusu Kenya na nchi zingine liko wazi.....kwa sababu  Wakenya wengi hawana durect link na uchumi na pesa yao......angalia tena hali ya confidence ya watu wake wa kawaida. Hawakua na Siasa kama yetu....hivyo uchumi wao umeshonana na watu wa nje siku nyingi hivyo Ksh inalindwa kuliko Naira na Malawi Kwacha isipingue thamani......ambavyo ni kinyume na Tz tunavyofanya kuachia Tsh ielee katika true value yake ambavyo ni vizuri sana..

Nimemaliza

Yassin..

Mohamed Sumar

unread,
Apr 30, 2015, 5:18:33 AM4/30/15
to wanat...@googlegroups.com

It is my opinion that this frightening devaluation of Tanzania Shillings has little, if anything, to do with

donor funds, or any other factors that might be causing the devaluation with complex social consequences

upon the poor masses of the nation. The result would be even more frightening !

Our failure to safeguard our currency is due to our absolute or complete lack seriousness in handling

the abuses we inflict upon our economy.

Past and recent financial scandals (some in newspapers and some in the ……. can provide some glimpse of

the problems.

 Mohamed Sumar.

-------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------

Bubelwa E. Kaiza

unread,
Apr 30, 2015, 6:27:41 AM4/30/15
to wanat...@googlegroups.com

Hello tujadili uchumi wa Tanzania na namna ya kuuokoa badala ya kuishia kulinganisha tu na mafanikio ya kiuchumi ya nchi nyingine. Ni vizuri wachumi wakachukua nafasi yao maana hisia na mipasho ya kisiasa haitatusaidia. Let’s talk openly.

 

Kwa taarifa ya wengine, uchumi wa Kenya umejengewa katika msingi imara wa a strong manufacturing and professional services industries. Kenya ni nchi ya tatu kwa Africa kuwa na a very strong manufacturing industry baada ya Africa Kusini na Egypt. Bajeti za kila mwaka za Serikali ya Kenya hutokana na/hutegemea kodi (hasa kutoka tasnia ya usindikaji na kilimo) na other internal pubic financing strategies such as monetary instruments kwa asilimia 95. Serikali ya Kenya huachia mashirika ya nje (BWs) kuchangia asilimia 5 tu ya bajeti na hii ni baada ya BWs kuomba kuchangia bajeti ya Serikali ili wasiwe useless/irrelevant.

 

Nakumbuka wakati wa Kibaki BWs walitaka kuleta mambo ya GBS ya hapa kwetu, kujadili michango yao ya ku-finance bajeti ya Serikali hadharani, Kibaki aliwaeleza kuwa Serikali yake haijadili mambo ya budget financing hadharani, kwamba siyo utamaduni wa Kenya na iwapo BWs wangeshindwa kuvumilia utamaduni huo wa Kenya, Serikali ilikuwa radhi kutopokea hiyo asilimia 5 yao ya nyongeza katika bajeti ya Serikali ya Kenya. BWs waliufyata mpaka leo.

 

Lakini pia sekta ya fedha ya Kenya inasimamiwa vilivyo siyo holela kama hapa kwetu. Huwezi kuona wananchi waki-transact kwa kutumia dola au euro bali Ksh. Export component ya Kenya ni kubwa na nchi ina comprehensive strategy ya uchumi, mfano tujiulize kiasi cha dola kinachoingizwa nchini humo kutokana na travel service export ya KQ. Tujiulize maduka kama ya NAKUMATI, Mabenki, manunuzi yanayofanywa na Ofisi za Umoja wa Mataifa (Giligili?) na kadhalika, yanayouza bidhaa na/au huduma nje ya Kenya yanaingiza dola/euro kiasi gani nchini humo. Kenya ina mkakati mkubwa unaotekelezwa na kila Mkenya kuhakikisha uchumi wa nchi unabaki imara.

 

Salam kwa MNEC Magesa.

 

Kaiza

Bubelwa E. Kaiza

unread,
Apr 30, 2015, 8:08:01 AM4/30/15
to wanat...@googlegroups.com

..... mwaka 2008 Serikali ya Zambia ilifuta mikataba (MDAs) yote ya uchimbaji madini iliyokuwepo baada ya kuona nchi yao hainufaiki na mauzo ya shaba nje ya nchi. Sheria mpya ya madini ilitungwa na kuachana na mambo ya MDAs (ushauri wa BWs). Kampuni zinazotaka kuwekeza nchini Zambia hufuata taratibu za kisheria za kupewa/kununua leseni za uchimbaji na kuingia kazini. Hakuna misamaa ya kodi wala ruzuku kwa makampuni ya wawekezaji kama Tanzania inavyofanya. Zambia inadhibiti mauzo yote ya shaba nje ya nchi. Leo hii nilipokwenda kununua ZKwacha hapa Lusaka nimekuta Kwacha 7 zinanunuliwa kwa dola 1.

 

Tunachojifunza kutoka Zambia ni kuwa Serikali ikifanya maamuzi sahihi na kuweka sera sahihi, uchumi wetu unaweza tena kurudi kwenye reli; hata shilling 5 kununua dola moja ya Marekani kama ilivyokuwa mwanzoni mwa miaka ya 1980.

 

Salamu kwa MNEC Magesa.

 

Kaiza  

Alex Nguluma

unread,
Apr 30, 2015, 10:14:26 AM4/30/15
to wanat...@googlegroups.com
Hi Yasin,
Naona Kali zako.
Alex  Nguluma

Sent from my iPhone

Dr Yassin Mshana

unread,
Apr 30, 2015, 11:16:24 AM4/30/15
to wanat...@googlegroups.com
Dr Nguluma,

Shukrani.

Inabidi wote tuwe wataalam wa Uchumi sasa ili kusaidiana kwani hali imebadilika ghafla kama vile TSh imetekwa,...au ni nini?

Pamoja na salaam

Y Mshana


--
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanataaluma wa Tanzania" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanataaluma...@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.



--
Independent Consultant
c/o DFID-South Africa, 255 Hill Street, Arcadia, Pretoria 0002, Republic of South Africa
Skype: yassinmshana1, Mobile:+2773 079 6267 , Fax: +27 (012) 421 7500
Do You really NEED TO PRINT THIS?
  "The illiterates of the 21st century are not those who cannot read or
 write but those who cannot learn, relearn and unlearn" Alvin Toffler

mwit...@yahoo.com

unread,
Apr 30, 2015, 11:43:35 AM4/30/15
to wanat...@googlegroups.com, <wanabidii@googlegroups.com>
I was just about to make an online remittance to Tanzania only to realise that our currency is not listed. Anyone knows why?



Sent from my iPhone

Salome Mallamia

unread,
Apr 30, 2015, 1:41:39 PM4/30/15
to wanat...@googlegroups.com, <wanabidii@googlegroups.com>

Habari zenu?

Mimi naona shilingi inaporomoka kwasababu tuna Viongozi wenye mamlaka ya kuleta mabadiliko lakini HAWAJITAMBUI na KUTEKELEZA wajibu wao. Tuna wataaluma waliosoma lakini HAWAJITAMBUI na KUTEKELEZA wajibu wao.

Nchi ni kama familia haina tofauti na Mzazi anaezaa tu watoto alafu ANAZEMBEA kutimiza wajibu wake kama Baba au Mama.

Nchi ni kama kuendelea gari highway na inaendeshwa na dereva mwenye DHARAU MJUAJI HASHAURIKI lazima utaokotwa korongoni tuu. 

Hata uwe na team nzuri kiasi gani kama HUTOI FURSA  watu kufanya mambo ya kisomi na wewe kiongozi UKAYASIMAMIA kwa maendeleo ya taifa you are doomed.

Kiongozi MBINAFSI lazima ataua uchumi kwasababu anawaza TUMBO lake tuuuu wakati kiongozi anatakiwa KUJIKANA NAFSI YAKE na KUSIMAMIA MASLAHI YA UMMA.

Kinachoendelea kwenye uchumi wetu hakijitaji rocket science Hali ya uchumi au shilingi itaimarika sio kwaajili ya kwenda seminar na makongamano bali kwa MIMI na WEWE kuacha UBINAFSI na kutenda  na kusimamia HAKI na UWAJIBIKAJI kwa manufaa ya Watanzania.

Wasalaam
Salome

Dr Yassin Mshana

unread,
Apr 30, 2015, 3:27:30 PM4/30/15
to wanat...@googlegroups.com

Mwalimu alisema, "It can be done, play your part".

Nakubaliana na mtaalam Salome..

Tuko wote jamani?

Tuokoe Shillingi yetu kwa namna mbali mbali....kuanzia hapo mtu ulipo..

Shukrani.

Yassin

Yonah Samo

unread,
Apr 30, 2015, 4:21:08 PM4/30/15
to wanat...@googlegroups.com
Kuongezea maoni mazuri ya Salome, kuna jambo linanishangaza 'kukua kwa uchumi  na kuporomoka jwa thamani ya shilingi. Very strange! Wazendo tubudi uzalisha wa bidhaa za ndani kuleta equilibrium kati ya export na import...law of supply and demand ndio inayoididimiza thamani ya hela yetu. Tunaagiza sana toka china na sehemu zingine kwa sana kuliko kuuza nje....so shilingi inafukuza dola chacha (sababu ya demand) so shilingi nyingi (less demanded) na dolar kidogo (highly demanded). Tuache kulalamika suluhi iko mikononi mwetu

Sent from my iPhone

Neema Machege

unread,
Apr 30, 2015, 4:57:31 PM4/30/15
to wanat...@googlegroups.com
Asalaam alleikoum wapendwa..
Mbona miaka iliyopita wenzetu kenya thamani vya pesa yao Ilikua sawa tu Na yetu? 
Inasikitisha kuona pesa yetu binashuka kila siku. 
Ila nafikiri tatizo ni sisi wenyewe , we're not productive enough.  Kenya wana produce Sana Na wana export sana, 
Imagine huku Europe ukienda supermarket kuna avocado , green beans , tea, coffee etc kutoka Kenya,  these guys are ambitious and hard working .. 
Hata Viatu vya ngozi vya kimasai hizo tunaita za culture just a simple thing,, ukienda kununua mtaani wauzaji wanasifia zinazotoka Kenya ni poa zaidi, 
That's a nonessential , watanzania tumezidi. Only fewer people are creative the rest ni maneno mengi, 
It's for us to wake up, make a move , be creative, and use our natural resources to backup our money. 
Na Sasa Chinese Na neighbours countries  wanavamia , tusipoangalia we'll wake up one day to find out that we're foreigners in our own country.. 
And that day will be the end of the end .. 

Let's save whatever is left before the whole ship sank completely.. 
God bless our beautiful country , and may he bring us the courage to bring some changes,
Amen 🙏

Neema Ezekiely 
--

Janet Mbene

unread,
Apr 30, 2015, 6:09:22 PM4/30/15
to wanat...@googlegroups.com
Neema asante lakini naona na wewe umelalamika bila kutoa pendekezo nini kifanyike?
Hili jambo linachangiwa na factors nyingi. lakini tuanze hapo tulipo kila mmoja azalishe kitu, kama ni ajira yake mwenyewe kama ni bidhaa ya shambani uvuvi ufugaji nk,  tulioajiririwa tutumie muda wetu kufanya kazi kuongeza tija na ufanisi na kuongeza pato la ndani. pili tuongeze thamani ya mauzo yetu ya nje ili kupata fedha ya kigeni zaidi. tatu tulegeze masharti ya uwekezaji katika viwanda vinavyoajiri watu wengi na kuchangia zaidi kwenye pato la taifa mfano nguo? ngozi maziwa na bidhaa zake, agro processing.uvuvi na ufugaji wa samaki nk. nne tuhamasishe matumizi ya bidhaa zetu hii itakuza soko la ndani na kukuza savings zitakazotumika kupanua uwekezaji na akiba na hi itawezesha kupunguza uagizaji wa bidhaa nje na kuinua thamani ya fedha yetu, mwisho tuache rushwa ili kuwe na ufanisi wa soko na kupunguza gharama za uzalishaji na kufanya bidhaa kufikika kwa wengi na kuinua maisha ya watanzania wengi.
Mwisho wasomi tuwe wa kwanza kuonyesha mfano katika yote hayo badala ya kulalama na kunyooshea wengine vidole.

MWISHO WATANZANIA TUCHUKIE MEDIOCRITY! KURIDHIKA NA SUB-STANDARD PERFORMANCE KWENYE KILA JAMBO!


TUAMKE  TUANZE KULITUMHLIA TAIFA LETU NA KUJIFM
--
Janet Z.Mbene (MP)
Deputy Minister for Industry and trade
P O BOX 9503 Dar Es Salaam
Tel:     +255 22 2127873
Mob:   +255 755 067594/ 784 596444
Email:maor...@gmail.com



Yonah Samo

unread,
Apr 30, 2015, 10:12:39 PM4/30/15
to wanat...@googlegroups.com
Kuongezea maoni mazuri ya Salome, kuna jambo linanishangaza 'kukua kwa uchumi  na kuporomoka kwa thamani ya shilingi. Very strange! Wazalendo tubuni uzalishaji wa bidhaa za ndani kuleta equilibrium balance of trade. Nionavyo, law of demand and supply ndio inayoididimiza thamani ya currency yetu. Tunaagiza sana toka china na sehemu zingine kwa sana kuliko kuuza nje....so shilingi inafukuza dola dollar. Serikali peke yake haiweza kufanya kitu, kumbukeni hata vikao tumeshindwa kufanya itakuwa serikali yenye mambo mengi?

Sent from my iPhone

On Apr 30, 2015, at 22:27, Dr Yassin Mshana <ymsha...@gmail.com> wrote:

Mwalimu alisema, "It can be done, play your part".

Nakubaliana na mtaalam Salome..

Tuko wote jamani?

Tuokoe Shillingi yetu kwa namna mbali mbali....kuanzia hapo mtu ulipo..

Shukrani.

Yassin

On 30 Apr 2015 19:41, "Salome Mallamia" <salomem...@gmail.com> wrote:

Habari zenu?

Mimi naona shilingi inaporomoka kwasababu tuna Viongozi wenye mamlaka ya kuleta mabadiliko lakini HAWAJITAMBUI na KUTEKELEZA wajibu wao. Tuna wataaluma waliosoma lakini HAWAJITAMBUI na KUTEKELEZA wajibu wao.

Nchi ni kama familia haina tofauti na Mzazi anaezaa tu watoto alafu ANAZEMBEA kutimiza wajibu wake kama Baba au Mama.

Nchi ni kama kuendelea gari highway na inaendeshwa na dereva mwenye DHARAU MJUAJI HASHAURIKI lazima utaokotwa korongoni tuu. 

Hata uwe na team nzuri kiasi gani kama HUTOI FURSA  watu kufanya mambo ya kisomi na wewe kiongozi UKAYASIMAMIA kwa maendeleo ya taifa you are doomed.

Kiongozi MBINAFSI lazima ataua uchumi kwasababu anawaza TUMBO lake tuuuu wakati kiongozi anatakiwa KUJIKANA NAFSI YAKE na KUSIMAMIA MASLAHI YA UMMA.

Kinachoendelea kwenye uchumi wetu hakijitaji rocket science Hali ya uchumi au shilingi itaimarika sio kwaajili ya kwenda seminar na makongamano bali kwa MIMI na WEWE kuacha UBINAFSI na kutenda  na kusimamia HAKI na UWAJIBIKAJI kwa manufaa ya Watanzania.

Wasalaam
Salome

On 30 Apr 2015 18:43, "mwitondi via Wanataaluma wa Tanzania" <wanat...@googlegroups.com> wrote:
I was just about to make an online remittance to Tanzania only to realise that our currency is not listed. Anyone knows why?



Sent from my iPhone

On 29 Apr 2015, at 20:53, Bubelwa E. Kaiza <bubelw...@fordia.org> wrote:

Mrema,

Umeongea kiasi fulani ila sababu zakushuka kwa Tzs. dhidi ya dola yakimarekani ni hizi zifuatazo:-

1.  Kuvuja kwa uchumi (economcleakage)/matumizi holela ya dolakwenye mzunguko wa ndani ya nchiwa fedha. Duniani kote, kuendeshauchumi imara kunahitaji mikakati nataasisi imara za kusimamia sera,sheria na kanuni za fedha. NchiniUfaransa, kwa mfano, hairuhusiwikubadilisha/kununua Euro taslimzenye thamani ya zaidi ya dola1000! Afrika ya Kusini hairuhusiwikutumia dola/euro isipokuwa randtu unaponunua mali au hudumayoyote (hotelini, ticket za ndagen.k). Hapa nchini kwetu hali nishaghala baghala – mamlakazinazopaswa kusimamia uchumi wanchi hazifanyi chochote; bureaux de change zinahamisha mauzo ya kilasiku ya madukani kwenda nje yanchi.

 

2.  Watu, hasa mafisadi, kutorosha/kuhodhi dola nje ya nchikutokana na hofu ya uchuguzimkuu. Hali hii inasababisha uhabawa dola hivyo kutengeneza artificial appreciation ya dola kutokana namsingi mkuu wa uchumi wademand vs. supply.

 

3.  Tanzania kutokuwa na dhahabuya kuuza nje ya nchi (dhahabuinayochimbwa siyo ya kwetu bali niya makampuni yanayochimba(wawekezaji) na zaidi ya 90% yamauzo ya dhahabu na madinimengine nje ya nchi hairudishwinchini bali yanabaki huko (clauses za MDAs zinatoa fursa hizo kwamakampuniya madini) nyumbanikwao na wawekezaji. Kwa kifupiTanzania siyo gold mining countrybali ni source of gold, hivyo haimilikimadini yanayochimbwa nchinikwake bali madini husika humilikiwana nchi mama wa makampuni yawawekezaji.

 

4.  Kuwa na weak manufacturing, construction and professional services industries hivyo nchikutegemea imports zaidi kulikouwezo wa kuuza huduma na bidhaanje ya nchi. Aidha mauzo ya mazaoya kahawa, pamba, katani na chainje ya nchi yamepungua kufikianegligible value. Nchi isipouzabidhaa na huduma za kutosha njeya nchi haiwezi kuwa na akiba yakutosha ya fedha ya kigeni. Na kwamukhtadha huu, thamani ya fedhaya nchi haiwezi kuimarishwa napesa ya misaada au mikopo kutokakwa wafadhali au mashirika yaBretton Woods.

 

5.  Impact ya wizi wa pesa yaakaunti ya Tegeta Escrow (wafadhilikuzuia pesa ya misaada ya kibajeti). Zipo sababu nyingine piazinazoathiri uchumi wa nchi (kuwawa hovyo) kama Tanzania ambazowatu wake wengi badohawategemei maarifa na ujuzi, baliardhi na bidhaa, hususan kutokanana tasnia ya uziduaji.

 

Najua MNEC-CCM Magesaanatafuta hoja za ku-pacify halimbaya inayokikabili chama chakeila ukweli ndio huo (free consultancy).

wanabidii+...@googlegroups.comUtapata Email ya kudhibitisha ukishatuma


Sent from my iPhone

Yonah Samo

unread,
Apr 30, 2015, 10:20:06 PM4/30/15
to wanat...@googlegroups.com
Janet, maoni yako ningeyasoma mapema nisingetuma ya kwangu, umesema yote! Wenzangu tuyafanye kuwa dira kwa kila moja wetu...within no time mabadiko tutayaona, waliofanyikiwa walianza kwa kujitambua!

Sent from my iPhone

Janet Mbene

unread,
May 1, 2015, 12:21:35 AM5/1/15
to wanat...@googlegroups.com

Yahya Ipuge

unread,
May 1, 2015, 1:58:07 AM5/1/15
to wanat...@googlegroups.com

Phares,

Asante sana kwa kuanzisha mjadala mzuri na pia shukrani kwa wataalam waliotufungua macho. Nadhani sasa tinahitaji kuweka mkazo kwenye nini kifanyike. Kama walivyoeleza wataalamu kila mmoja wetu anapaswa kuchukua hatua pale alipo. Pia nimefurahi hakuna ushabiki wa kisiasa wa waziwazi.

Nashauri wewe Phares ukiwa kama "moderator" wa mjadala au uchague mmoja mwenye ujuzi wa masuala haya ili atusaidie kukokotoa maoni yaliyotolewa na kuandaa andiko (paper) ambayo itaisaidia serikali na sisi wote. Kuna mmoja alisema "free consultancy"  mimi naita mchango wa wataalam kwa nchi yao.

Kwa mfano, mimi ni mpenzi wa kahawa ya kupikwa kwa mashine (brewed coffee) na juzi nilipita kununua paketi yangu ya kila mwezi. Nikashangaa imeongezeka bei kwa sh elfu mbili.  Nikauliza kwa nini imepanda bei maana haihusiki na dola ya marekani.  Kahawa ni ya Rift Valey Mbeya na Zanzibar. Nikaambiwa mwenye duka la kahawa (Coffee Shop) ni mtu wa nje hivyo bei inategemea dola. Ila sidhani bei itapungua shilingi ikiimarika.

Swali: hapo mimi kama mlaji nitachukua hatua gani? Je ni nani anapaswa kulinda walaji kutokana na wafanya biashara  nyemelezi (opportunists) kama hawa. Nadhani mifano mingi ipo ya kitaalam kwa wachumi au ki muma kama niliotoa mimi.

Hilo andiko ninalopendekeza liainishe hatua za kila mtu na kila taasisi za kuchukukua ili kuinusuru shilingi yetu. Na baada ya miezi mitatu tufanye mjadala kama huu kuangalia kama mapendekezo yetu yatakuwa yamefanyiwa kazi.

Naomba kuwasilisha,

Ipuge
------------------
Dr. Yahya A. Ipuge M.D., MMed.
Senior Health Specialist
Wazo Hill,Tegeta
P.O. Box 66764
14130 Dar es Salaam
   

Ngwisa Mpembe

unread,
May 1, 2015, 2:24:36 AM5/1/15
to wanat...@googlegroups.com
Wandugu

Kwenye mjadala huu najaribu kutafuta majibu. Nimeona mawazo machache sana yenye reference za uchumi kidunia na kikanda. Nimeweza kuona kuwa Mporomoko wa fedha umezikumba nchi zote za Africa Mashariki kwa kiwango karibu kile kile. Je majibu yanaongelewa humu kuhusu uongozi wa taifa letu yanatukingaje na jambo hili linaloonekana na msokumo wa kimataifa. Shouldn't we talk more of mitigation strategies. Do we have any controls? Wachumi please

Ngwisa

otieno igogo

unread,
May 1, 2015, 4:25:54 AM5/1/15
to wanat...@googlegroups.com
Kwa,
 Wadu wote wa Mada tajwa hapo juu,

Nimewiwa radhi kujiunga kwenye mjadala huu ili name nipate kuwasilisha fikra zangu ambazo naamini yaweza kuongozea upanuzi wa uwigo wa dhana ya waliotangulia pia na kuwatonya wahusika wakuu na maswala ya sera hususan Dr. Janet Mbene, Mh. Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, kuhusu tunayoyaona yakitendeka ndani ya soko la biashara na uuzaji wa bidhaa za nchini dhidi ya bidhaa zinazoingizwa ndani ya nchi toka nchi za nje, kama changamoto kuu zenye kuleta udhaifu dhidi ya sarafu yetu shillingi ikilinganishwa na za nchi zingine.

Mh. Naibu waziri hebu jiulize na uweze kutufafanulia kwamba maduka ya kununua na kuuza fedha za kigeni wanafanya biashara au la, na iwapo ni wanafanya biashara, je sera  inayosimamia utoaji wa liseni na udhibiti wa huduma wanazotoa kama wafanyi biashara zipo? Kama zipo naomba utuelimishe na iwapo hazipo basi elewa kuwa Wizara yako ndiyo chanzo cha udhaifu uliopo, hivyo yakupasa kusaidiana na wadau ili upate hoja zenye mashiko zikuwezeshe kutengeneza sera ya biashara hiyo. kwani hao n iwafanyi biashara ya kununua na kuuza sarafu mbali mabali, hivyo bidha wanayouza ina mdhibiti wake lakini huduma wanayotoa ni biashara ya uchuuzi wa bidhaa ya sarafu, mtakapobainisha hicho kitendawili na kuitunguia sera madhubuti,
Hivyo Sarafu yetu shillingi itapata mzunguko mpana katika matumizi dhidi ya sarafu za kigeni hapa nchini, pia mianya ya manunuzi na kwani kwa sasa mengi ya maduka hayo ya uchuuzi wa sarafu ni mifereji ya wazi yenye kutoa sarafu za nje nchini kwa ajili ya manunuzi ya bidhaa na utoroshwaji wa mapato yenye stahaiki ya utozwaji kodi ya ndani na kupelekea udhaifu mkubwa wa shillingi yetu mara wanapoamua kwa kuwa kuna usiri miongoni mwai nahisi.

Mdhibiti wa mzunguko wa fedha yaani, BENKI KUU YA TANZANIA, amefunga tundu na kufungulia geti, ni jambo la kushangaza  tena kutia aibu kuona kwamba sheria za zao inakataza kulipiana kwa hundi za benki kiasi kinachozidi shillingi millionI KUMI, lakini inaruhusu kutoa fedha taslimu benki na kufanyia malipo kwa kiasi chochote hata kama ni mabilioni. Huu ndiyo mwanya wa manunuzi na uuzwaji holela ya sarafu za kigeni, ukwepaji wa kulipa kodi za nchi, uwezesho wa kulipiana mapato haramu na udhoofishwaji wa sarafu yetu, kwani aliyekuwa na shillingi za kitanzania miezi miwili iliyopita na akanunulia dola za merekani, kwa sasa ana ongezeko la thamani kwa kiasi cha asilimia 25% ambapo riba ya benki ni asilimia takriban 2%, kwanini dola isiwe na nguvu kwa jinsi hii.

Kwani kila mmoja anapenda apate faida, wenye maduka ya sarafu wananunua dola Benki kuu kwa bei poa, wanawauzia wateja wao kwa faida kubwa, nao wateja wanapata shillingi taslimu bila ya masharti  na kununulia dola za merekani kwa bei ya majadiliano. Huku mdhibiti akiwa amelala fofofo akidhani kwamba kafunga geti la matumizi mabaya ya hundi, kumbe lango kuu lipo wazi bila ulinzi .Ni mpaka hapo matumizi ya malipo taslimu yatakapodhibitiwa na kulazimisha matumizi ya kimtandao na hundi kushika hatamu ndipo shillingi yetu itakapopata heshima na utambuzi stahiki, ili kuimarisha utozwaji kodi kwenye mizunguko ya kibiashara, faida itokanayo na mitaji, pia kuwesha upatikanaji sahihi za mapato na matumizi ya kila mmoja wetu hapa nchini, kwani tuna wajibu wa kwa pamoja ya kuchangaia gharama za huduma za pamoja na uendeshaji wa serikali yetu kwa njia ya kodi.


Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) haijapewa jukumu la kuhakikisha kwamba kila mtu aishiye na kupata kipato hapa nchini analipa kodi itokanayo na kipato chake halali na hata isiyo halali kama itabainika,ukitizama sekta ya ujenzi nchini mwetu utakubaliana name kwamba kwa kweli watanzania siyo kam wakenye na wanyarwanda kwa kujijengea makazi, kila mmoja anajitahidi ama kuwa na kibanda chake, wapo wenye mahekalu na ma esteti, lakini ukienda kwa undani Zaidi wengi wao ni ama watumishi wa kuduma kwenye sekta rasmi na serekali kuu pamoja na vyombo vyake, pia wafanyi biashara, hayo mahekalu ama ma esteti na vibanda kwa asilimia kubwa thamani yake hailingani na mapato yanayotozwa na kulipia kodi TRA, ya wahusika. ndiyo maana hatujaweza na wala hatutaweza kuacha kuwategemea wenye kufadhili bajeti ya uendeshaji wa serikali yetu na miradi ya maendeleo, na ndiyo wenye dola na sarufu zinginezo zenye thamani kubwa dhidi ya shillingi yetu, mpaka hapo kila mtanzania mwenye kipato atakapolipa kodi na kuongezeka kwa uwigo wa walipa kodi huku ikienda sambamba na kupunguzwa kwa viwango vya kodi ambavyo kwa sasa ni ipo juu mno.

Viwango vikubwa vya kodi ni kichocheo cha ukwepaji kodi, nayo inadhoofisha makusanyo ya mapato ya kodi na kupelekea nakisi ya bajeti ya serikali, huku wenye kukwepa kodi na wanaowawezesha ndani ya mifumo rasmi wakineemeka na faida ya biashara ya ukwepaji kodi.Huu pia ni mwanya inayosababisha kudhoofika kwa shillingi yetu. Ni wakati muafaka wa kuangalia upya uundwaji wa uongozi wa juu kama Bodi za mamlaka mbali mbali ilitutokane na dhana kwamba ni nafasi za wansiasa kuwazawadi ama marafiki kama siyo ndugu au wapambe wao, kila sekta iongozwe kwa mchanganyiko wa wana taaluma husika kwa sifa stahiki za uadilifu, ubunifu na ustadi pamoja na wadau wakuu wa sekta husika ukiwakilishwa. nasema hivyo kwa kuwa naamini kwamba  wacheza mpira ni wajuuzi na muhimu kama walivyo makocha wao, bila ya ushirikiano baina ya wataalamu na wadau hatutoweza kufanikisha maswala ya udhibiti na uboreshaji wa uchumi wa nchi yetu.

Kwa hayo machache natumai kwamba nimeweza kuibua Nyanja mpya ya majadiliano kuhusu mada tajwa hapo juu, natarajia maoni chanya isiyogusa maswala ya kisiasa na wala itikadi ya aina yeyote, na kuzuia kabisa kuwajadili watu au mtu mmoja mmoja.

Wenu katika utafutaji ufumbuzu wa kuimarisha sarafu yetu,

OTIENO OLUNG'A IGOGO
MWENYEKITI,
CHAMA CHA WALIPA KODITANZANIA.



 
Box 2259, Dar es Salaam.
Mob:  +255 723 766077/ 784 760088  
Email: oig...@yahoo.com   
Website:  www.ute-tech.net
 
 


From: Yahya Ipuge <yip...@gmail.com>
To: wanat...@googlegroups.com
Sent: Friday, May 1, 2015 8:58 AM
Subject: Re: Fwd: [TPN] Kushuka kwa thamani ya Shilingi ya Tanzania

Bubelwa E. Kaiza

unread,
May 1, 2015, 6:31:49 AM5/1/15
to wanat...@googlegroups.com

...............lakini ili mapendekezo haya yaweze kutekelezeka, kila mmoja wetu ajiangalie na kujitathmini juu ya mahali alipo na majukumu yake, halafu ajiulize, Je, nimefikia hapa nilipo kwa professional competence merit na kwa kupitia a due process?

 

Ni wale tu watakojijibu, NDIYO tunaoweza kutekeleza au kuwawajibisha wahusika kutekeleza mapendekezo yaliyainishwa hapa chini.

 

Kaiza

 

From: wanat...@googlegroups.com [mailto:wanat...@googlegroups.com] On Behalf Of Janet Mbene


Sent: 01 May 2015 01:09
To: wanat...@googlegroups.com

Phares Magesa

unread,
May 1, 2015, 7:01:39 AM5/1/15
to wanat...@googlegroups.com
Wazalendo wenzetu Awadh Salum, Rosemary Mwakitwange , Camilius Kassala, Dr.Yahaya Ipuge, Buberwa Kaiza na mwingine yoyote atakaejitolea.

Kwa niaba yetu wote naomba mtusaidie kuandaa andiko hilo (draft) ili lipitiwe na wadau na baadae kutolewa rasmi kwa umma.

Naomba kutoa hoja

Phares Magesa
Rais - TPN



Sent from Samsung Mobile



-------- Original message --------
From: Yahya Ipuge <yip...@gmail.com>
Date: 01/05/2015 08:58 (GMT+03:00)
To: wanat...@googlegroups.com
Subject: Re: Fwd: [TPN] Kushuka kwa thamani ya Shilingi ya Tanzania


Phares,

Asante sana kwa kuanzisha mjadala mzuri na pia shukrani kwa wataalam waliotufungua macho. Nadhani sasa tinahitaji kuweka mkazo kwenye nini kifanyike. Kama walivyoeleza wataalamu kila mmoja wetu anapaswa kuchukua hatua pale alipo. Pia nimefurahi hakuna ushabiki wa kisiasa wa waziwazi.

Nashauri wewe Phares ukiwa kama "moderator" wa mjadala au uchague mmoja mwenye ujuzi wa masuala haya ili atusaidie kukokotoa maoni yaliyotolewa na kuandaa andiko (paper) ambayo itaisaidia serikali na sisi wote. Kuna mmoja alisema "free consultancy"  mimi naita mchango wa wataalam kwa nchi yao.

Kwa mfano, mimi ni mpenzi wa kahawa ya kupikwa kwa mashine (brewed coffee) na juzi nilipita kununua paketi yangu ya kila mwezi. Nikashangaa imeongezeka bei kwa sh elfu mbili.  Nikauliza kwa nini imepanda bei maana haihusiki na dola ya marekani.  Kahawa ni ya Rift Valey Mbeya na Zanzibar. Nikaambiwa mwenye duka la kahawa (Coffee Shop) ni mtu wa nje hivyo bei inategemea dola. Ila sidhani bei itapungua shilingi ikiimarika.

Swali: hapo mimi kama mlaji nitachukua hatua gani? Je ni nani anapaswa kulinda walaji kutokana na wafanya biashara  nyemelezi (opportunists) kama hawa. Nadhani mifano mingi ipo ya kitaalam kwa wachumi au ki muma kama niliotoa mimi.

Hilo andiko ninalopendekeza liainishe hatua za kila mtu na kila taasisi za kuchukukua ili kuinusuru shilingi yetu. Na baada ya miezi mitatu tufanye mjadala kama huu kuangalia kama mapendekezo yetu yatakuwa yamefanyiwa kazi.

Naomba kuwasilisha,

Ipuge
------------------
Dr. Yahya A. Ipuge M.D., MMed.
Senior Health Specialist
Wazo Hill,Tegeta
P.O. Box 66764
14130 Dar es Salaam
   

On 1 May 2015 07:21, "Janet Mbene" <maor...@gmail.com> wrote:


---------- Forwarded message ----------
From: Janet Mbene <maor...@gmail.com>
Date: Friday, May 1, 2015

Ngwisa Mpembe

unread,
May 1, 2015, 8:11:57 AM5/1/15
to wanat...@googlegroups.com
Wanataaluma wenzangu na Mh Rais.

Naunga mkono hoja ya Andiko. Baada ya kupitia hoja mbalimbali kama zilivyotolewa, nashauri kuwepo na hadidu za rejea fupi kuwaongoza hawa wenzetu kutoa andiko litakalokidhi haja kwa maana ya kutoa majibu/ mapendekezo kwa swala hili. 

Naomba sana pia Mwl wangu Dr C.Kasalla amalizie hoja yake.

Ngwisa Mpembe


shakir msangi

unread,
May 1, 2015, 9:26:24 AM5/1/15
to wanat...@googlegroups.com
Na kweli ni soga tuu hizi za siasa!Magesa mambo mangapi serikali imeshauriwa ushauri mzuri ukabaki katika makabrasha?Nchi inaendeshwa kwa utashi wa kisiasa!Tahir usiseme Furniture tuu, serikali iliyoshindwa kusimamia hata kutengeneza madawati ya wanafunzi wake huku miti ikikatwa hovyo kuchoma mikaa kisa ni wapiga kura

Sent from my HTC

Neema Machege <ikom...@gmail.com> wrote:

Duuh Tahir 
Hiyo ni Kali 
Hata furniture tunaagiza toka nje Na mbao zimejaa nchini 
Hili tatizo limekua sugu 

On Friday, May 1, 2015, Tahir Othman <kufak...@gmail.com> wrote:
Kuna rafiki yangu alichaguliwa Uwaziri nikamuuliza je kuna fanicha yeyote ndani ya wizara yenu made in Tanzania? Akanijibu kuwa mostly zote ni imported. Two months ago nikamuuliza swali lile lile, akanijibu kuwa kashindwa kupambana na 10% za procurement. Tuendelee kupiga soga tu labda Mungu atatusikia atusaidie! 
t.

Sent from my iTochi powered by UhuruOne

On May 1, 2015, at 11:37 AM, ymshana2003 <ymsha...@gmail.com> wrote:

Wapendwa wapenda maendeleo wenzangu.

Naona tumelifungumzia na kulizungusha hili janga vya kutosha. Sasa tuingie mitamboni tufanye kazi zetu kwa bidii kama alivyoshauri NW Janet Mbene....

Ni sawa lakini sijapata kusoma taarifa rasmi kwamba, hili janga lilitokeaje kwa ghafla? Na kuna viona mbali vya namna gani vipo au vitawekwa ili  kuepusha kugonga mwamba tena?

Ndio Tsh itatulia baada ya mikopo...lakini, hiyo itakua kama kutuliza maumivu tu. Inabidi kuwe na mbinu tofauti zilizokuwepo hapo zamani....

Tufufue Sector ya uzalishaji ...yaani  ni kuanzia shughuli za SIDO vijijini hado vikubwa kama NECO badala ya kuwa na Showrooms along Nyerere Road kwa Dar na miji mingine. Kwa fani yangu ya uhandisi naumiza kuona wahitimu wakibakia jufura vifaa vumbi kwenye showrooms ambavyo angeviteneza laiti angeajiriwa kiwandani...nk. Tumegeuka soko kirahisi by 100%....Eti kwa sababu bidhaa zetu hazifikii kiwango cha soko la kimataifa? Tutavitumia wenyewe kwani tuna TBS yetu ya kuangalia Ubora na Viwango.....

Kama dada Mbene alivyoshauri, ....."Tujitambue"  ...

Tusonge mbele

Yassin

Sent from Samsung Mobile

--
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanataaluma wa Tanzania" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanataaluma...@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

--
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanataaluma wa Tanzania" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanataaluma...@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

Eng. Bundaqa

unread,
May 2, 2015, 5:40:55 AM5/2/15
to wanat...@googlegroups.com

?

Sent from my Xperia™ S

Camillus Kassala

unread,
May 2, 2015, 12:47:07 PM5/2/15
to wanat...@googlegroups.com
Ili andiko hilo, kwa Kiswahili, liwe na maana na ufumbuzi wa kudumu, napendekeza hadidu za rejea zifuatazo:

1. Dhana ya sarafu ya taifa iainishwe.
2. Nafasi na thamani ya sarafu ya taifa katika biashara ya kimataifa ielezwe.
3. Athari, kwa thamani ya sarafu ya taifa, za manunuzi ya ndani kwa kutumia sarafu za kigeni zionshwe.
4. Athari ya kushuka kwa thamani ya sarafu ya taifa kwa uwezo wa wananchi kujikimu kimaisha ikaziwe.
5. Jukumu la Benki Kuu kusimamia mfumo wa fedha, kodi na biashara ya fedha za kigeni lifafanuliwe.
6. Kuinua kiwango cha ubora wa bidhaa na huduma za ki-Tanzania katika soko la kimataifa kupewe mkazo.
7. Athari hasi, kwa uchumi wa nchi, wa sera za uchumi wa soko huria ambao umekuwa holela zisisitizwe.
8. Athari za misaada na mikopo kutoka nje 'inyomwaga' dola (USD) katika uchumi wanchi ziwekwe bayana.
9. Athari za kuifanya nchi yetu kuwa 'koloni' la dola (=sarafu) ya Kimarekani ziwekwe wazi.
10. Sarafu ya Tanzania (= shilingi) kuwa ni nembo, kigezo, kitambulisho, na nyenzo rasmi ya utamaduni wa kiuchumi wa Tanzania, ndani na nje ya nchi ijengewe hoja ya kizalendo.

CDNKassala

Yahya Ipuge

unread,
May 2, 2015, 11:03:58 PM5/2/15
to wanat...@googlegroups.com

Phares,

Naona hadidu za rejea ziko tayari. Mimi ni mtaalam wa afya hivyo itakuwa vigumu kuandika vizuri andiko la kiuchumi. Ñashauri wenzangu waanze mimi ntakuwa mmoja kati ya wapitiaji (reviewer )wenye ''layman's lens".

Nashauri  Buberwa Kaiza atusaidie rasimu ya kwanza kutumia hizo hadidu za rejea

Ipuge
------------------

ymshana2003

unread,
May 3, 2015, 4:43:46 AM5/3/15
to wanat...@googlegroups.com
Wenzangu,

Kwa kuunga mkono mapendekeza endekefu ya ndugu Ipuge na Kasalla, ningependa kuongezea kwamba andiko likiandikwa katika lugha ya kitaalam litaleta utata katika kulitafsiti na kueleweka wa wadau wote. 

Hivyo napendekeza kwamba, wataalam wakishaandika sisi wadau tulipitie ili kulilainisha liekewe na wadau wote (sisi common-people). La sivyo litakua andiko la kitaaluma tu.

Heri na baraka.

Tusonge mbele.

Wenu, Yassin Mshana.

Phares Magesa

unread,
May 5, 2015, 2:19:07 AM5/5/15
to wanat...@googlegroups.com
Wenye maoni yoyote kuhusu suala hili sasa wapeleke kwa kamati ndogo tuliyopendekeza ili yaunganishwe katika andiko ambalo tumewaomba wenzetu watusaidie kuliandika ili lije litolewe rasmi kwa umma kama kauli yetu wote.

Kamati inaundwa na:

Ndg. Buberwa Kaiza
Ndg. Rosemary Mwakitwange,
Ndg. Dk. Yassin Mshana
Ndg. Dk. Yahya Ipuge
Ndg. Salum Awadh
Ndh. Camillius Kasalla

Hivyo basi kwa sasa majadiliano kwenye mada hii tutasitisha ili kuwapa wenzetu muda wa kuandaa andiko na sasa tutaelekeza majadiliano kwenye mada nyingine zilizopo au zitakazofuata kwenye jukwaa ili tusaidiane kutatua changamoto zilizopo kwenye jamii yetu.

Tunawashukuru wote waliotoa maoni ambayo yatasaidia kuandaa andiko hilo ambalo tunaamini watunga sera wetu na wanananchi kwa ujumla kila mmoja amepata ufahamu na watafaidika zaidi tukitoa andiko hilo kwa hiyo tuendelee kutumia utaalamu, ujuzi na ufahamu tuliaonao kuelimishana kwa faidia ya yetu na Taifa letu.

Wasalaam

Phares Magesa
Sent from my BlackBerry® smartphone provided by Airtel Tanzania.

From: ymshana2003 <ymsha...@gmail.com>
Date: Sun, 03 May 2015 10:43:32 +0200

paul masatu

unread,
May 5, 2015, 4:59:06 AM5/5/15
to wanat...@googlegroups.com

At May 5, 2015, 9:19:07 AM, Phares Magesa<'pma...@gmail.com'> wrote:Wenye maoni yoyote kuhusu suala hili sasa wapeleke kwa kamati ndogo tuliyopendekeza ili yaunganishwe katika andiko ambalo tumewaomba wenzetu watusaidie kuliandika ili lije litolewe rasmi kwa umma kama kauli yetu wote.


Kamati inaundwa na:

Ndg. Buberwa Kaiza
Ndg. Rosemary Mwakitwange,
Ndg. Dk. Yassin Mshana
Ndg. Dk. Yahya Ipuge
Ndg. Salum Awadh
Ndh. Camillius Kasalla

Hivyo basi kwa sasa majadiliano kwenye mada hii tutasitisha ili kuwapa wenzetu muda wa kuandaa andiko na sasa tutaelekeza majadiliano kwenye mada nyingine zilizopo au zitakazofuata kwenye jukwaa ili tusaidiane kutatua changamoto zilizopo kwenye jamii yetu.

Tunawashukuru wote waliotoa maoni ambayo yatasaidia kuandaa andiko hilo ambalo tunaamini watunga sera wetu na wanananchi kwa ujumla kila mmoja amepata ufahamu na watafaidika zaidi tukitoa andiko hilo kwa hiyo tuendelee kutumia utaalamu, ujuzi na ufahamu tuliaonao kuelimishana kwa faidia ya yetu na Taifa letu.

Wasalaam

Phares Magesa
Sent from my BlackBerry® smartphone provided by Airtel Tanzania.

From: ymshana2003
Date: Sun, 03 May 2015 10:43:32 +0200

paul masatu

unread,
May 5, 2015, 5:01:46 AM5/5/15
to samb...@yahoo.co.uk, wanat...@googlegroups.com
Mr President naomba usajili wa email yangu ubadilike kwenda kwenye email ya pmasa...@gmail.com

Asante

Donath R.Olomi

unread,
Jul 24, 2015, 6:24:30 AM7/24/15
to wanat...@googlegroups.com
Dear Sir,

IMED, a leading training and consulting firm will conduct a four-day
course on entrepreneurship, financial literacy and retirement planning in
17th – 21st August at Kingsway Hotel Morogoro.

The training is conducted by highly experienced facilitators, using
participatory competency based learning methodologies. Participants are
guided to identify their assets and liabilities, opportunities and threats
and plan for streams of income and socially fulfilling lives after
retirement. They will also develop life, personal finance, and investment
and management skills. Financial institutions will present options
available for supporting participant’s investments.

Topics are carefully selected to address the targeted issues and they
include:
• Entrepreneurial approach to life
• Personal balance sheet
• Physical, psychological, economic and social adjustment to a retirement’
life
• Pitfalls and good practice in retirement planning (including case studies)
• Alternative post-retirement “careers” and activities
• Identifying and selecting investment opportunities/options
• Financing investments: sources of finance and how to access them
• Developing a winning simple business plan
• Business management essentials
• Financial literacy (including retirement benefits)


The programme will run from March 9.00 am to 4.00 pm, at Kingsway Hotel,
Morogoro. Fee is Tshs 500,000/- to cover tuition, materials, refreshments,
lunch and certificate. The purpose of this letter is to invite your
organisation to send participants to this important course.
Correspondences should be directed to the above address to the undersigned
or mobile numbers shown above.

Sincerely,

Dr. Donath R.Olomi
CEO

--
“Give your energy to things that give you energy.”,

“Learn enough to begin and then learn as you go.”


Dr. Donath R.Olomi
Chief Executive Officer
Institute of Management and Entrepreneurship Development (IMED)
Baraka Plaza 3rd Floor, Mikocheni, Old Bagamoyo Road
P.O. Box 35036 Dar es Salaam, Tanzania E-mail: in...@imedtz.org, website:
www.imedtz.org
Mobile +255-754-296660

Publications available on the Internet

http://www.repoa.or.tz/documents/RR_12-2.pdf

http://www.businessenvironment.org/dyn/be/docs/31/BETanzania02.pdf

http://www.tanzaniagateway.org/docs/EnhancingSMEcontributiontoempandpovertyreduction.pdf

http://econpapers.repec.org/article/wsijecxxx/v_3a17_3ay_3a2009_3ai_3a01_3ap_3a103-125.htm

http://www.fek.umu.se/forskning/pub/Business.Studies/babsonpaperversion.pdf

http://www.sbaer.uca.edu/research/icsb/2011/763.pdf

http://fusionmx.babson.edu/entrep/fer/babson2001/I/I-R/I-R/i-r.htm

http://www.theigc.org/sites/default/files/EnterpriseMapofTanzania.pdf

Donath R.Olomi

unread,
Feb 11, 2016, 7:45:55 AM2/11/16
to wanat...@googlegroups.com
: Jamie Phillips Oxford HR on behalf of the Gatsby Foundation
[mailto:gatsby=oxfordh...@mail194.atl61.mcsv.net] On Behalf Of Jamie
Phillips
Oxford HR on behalf of the Gatsby Foundation
Sent: Thursday, February 11, 2016 2:14 PM
To: olive
Subject: Gatsby Foundation Opportunities - Please forward


Gatsby Africa is growing. We’re looking for exceptional candidates for a
number of
leadership and M&E posts. We’d be very grateful if you would have a quick
look and
forward this email to anyone whose name pops up as you read the job notice.


Many thanks in advance for your help.

Warm best wishes,
Jamie

Jamie Phillips
Oxford HR on behalf of the Gatsby Foundation
email: gat...@oxfordhr.co.uk


Strategic leadership roles in economic development with the Gatsby Foundation

Based: London or Nairobi or Dar es Salaam Closing date: 7th March 2015


Are you a private sector development/M4P specialist passionate about
promoting
sustainable economic development in Africa? Or are you from the private
sector, with
a track record supporting industry-wide initiatives? Do you have
strategic vision,
a sharp analytical mind, and proven leadership skills, along with in-depth
exposure
to market systems approaches and operational experience leading sector
development
programmes? Would you like to work for an independent and innovative
funder-implementer with big ambitions to transform key sectors, creating
jobs and
raising incomes for people across East Africa?

Gatsby is the private foundation of Lord David Sainsbury, with over £1billion
already committed to charitable causes. In East Africa Gatsby focuses on
driving
sustainable economic growth through ambitious programmes that seek to
transform
economic sectors. We work in the Tanzanian cotton and textiles sectors,
tea sectors
in Tanzania and Rwanda, and the Kenyan and Tanzanian forestry sectors. We
also fund
and support two independent institutions dedicated to sector
transformation: Msingi
and Kenya Markets Trust. Msingi - a new organisation with an East Africa wide
mandate - is in the early stages of being set-up, with a management team
to be
recruited during 2016.

We take an analytical and business-like approach, seeking to effect change
in market
systems. As a private foundation and funder-implementer we have the
freedom to
innovate and take risks, using grants, technical support, loans or equity as
appropriate. We adopt a patient and pragmatic approach, recognising that
change can
take time. We draw on industry experts, engage the private sector and
work with
governments where needed to secure effective regulatory frameworks.

Gatsby is now looking to fill several positions to strengthen our senior
team.

* Africa Programmes Directors: overseeing and setting the strategy
of one or more
large sector programmes. Minimum 12 years’ relevant experience.
* Deputy Director/Senior Manager Monitoring, Evaluation & Learning:
providing
technical support to programme teams and responsible for the quality of
monitoring
and learning across the portfolio. Minimum 8 years’ relevant experience.
* Programme Manager/Senior Programme Managers: responsible for
significant
components of sector programmes, delivering functions to support multiple
sector
programmes, and/or supporting Directors in programme leadership. Minimum
5 years’
relevant experience.

The ideal candidates will be strategic thinkers with sound judgement,
private sector
DNA and strategy consulting skills likely honed from a strategy consultancy
background. Experience and understanding of working within the private
sector and
with governments is highly desirable.

Applicants must demonstrate:

* An ability to understand sector dynamics and approaches to
transform entire
sectors, with a detailed understanding of private sector actors
* Strategic leadership – an ability to think ambitiously with a
keenness to learn
and innovate and an ability to combine thinking and analysis with
programme delivery
* An ability to influence change – with a record of building
relationships at senior
levels across the private sector, governments and donors

To find out more, please go to
<http://oxfordhr.us5.list-manage.com/track/click?u=009976a19bbff12a3b4a4d612&id=a855d3d38d&e=4b228cb27f>
http://oxfordhr.co.uk/jobs where you can download the Candidate Packs and
apply
online. Applications are welcome until the deadline of 7th March 2016 (by
midnight
GMT).


If you know anyone who fits the bill, please forward this email to them.
Many thanks!

East African candidates are particularly encouraged to apply. Candidates
who wish to
be based in London must have the existing right to work in the UK.

Gatsby Africa will be recruiting more posts in 2016 so eligible candidates
may also
be considered for forthcoming posts.

More information is available from
<http://oxfordhr.us5.list-manage.com/track/click?u=009976a19bbff12a3b4a4d612&id=466ef757da&e=4b228cb27f>
http://www.gatsby.org.uk/africa


We’re sending you this email as someone who knows about PSD/M4P/M&E/MRM
and/or
Economic Development in East Africa.

If you would like to receive weekly job alerts from Oxford HR, you can
subscribe at
<http://oxfordhr.us5.list-manage.com/track/click?u=009976a19bbff12a3b4a4d612&id=859c88e8a7&e=4b228cb27f>
http://oxfordhr.co.uk/speculative/.You can also register your CV using the
same
address.








<https://gallery.mailchimp.com/009976a19bbff12a3b4a4d612/images/3edc684b-564f-48d4-a0b7-8edddd0566ab.png>







Copyright © 2016 Oxford HR, All rights reserved.
You are receiving this email because of your links with Oxford HR and/or
the Gatsby
Foundation.

Our mailing address is:

Oxford HR

The Old Music Hall

106-108 Cowley Road

Oxford, Oxfordshire OX4 1JE

United Kingdom


<http://oxfordhr.us5.list-manage1.com/vcard?u=009976a19bbff12a3b4a4d612&id=b17bcd470f>
Add us to your address book



<http://oxfordhr.us5.list-manage.com/unsubscribe?u=009976a19bbff12a3b4a4d612&id=b17bcd470f&e=4b228cb27f&c=2e405c27ea>
unsubscribe from this list
<http://oxfordhr.us5.list-manage.com/profile?u=009976a19bbff12a3b4a4d612&id=b17bcd470f&e=4b228cb27f>
update subscription preferences

<http://oxfordhr.us5.list-manage.com/track/open.php?u=009976a19bbff12a3b4a4d612&id=2e405c27ea&e=4b228cb27f>


On Tue, May 5, 2015 00:19, Phares Magesa wrote:
% Wenye maoni yoyote kuhusu suala hili sasa wapeleke kwa kamati ndogo
tuliyopendekeza ili yaunganishwe katika andiko ambalo tumewaomba wenzetu
watusaidie kuliandika ili lije litolewe rasmi kwa umma kama kauli yetu
wote.
%
% Kamati inaundwa na:
%
% Ndg. Buberwa Kaiza
% Ndg. Rosemary Mwakitwange,
% Ndg. Dk. Yassin Mshana
% Ndg. Dk. Yahya Ipuge
% Ndg. Salum Awadh
% Ndh. Camillius Kasalla
%
% Hivyo basi kwa sasa majadiliano kwenye mada hii tutasitisha ili kuwapa
wenzetu muda wa kuandaa andiko na sasa tutaelekeza majadiliano kwenye mada
nyingine zilizopo au zitakazofuata kwenye jukwaa ili tusaidiane kutatua
changamoto zilizopo kwenye jamii yetu.
%
% Tunawashukuru wote waliotoa maoni ambayo yatasaidia kuandaa andiko hilo
ambalo tunaamini watunga sera wetu na wanananchi kwa ujumla kila mmoja
amepata ufahamu na watafaidika zaidi tukitoa andiko hilo kwa hiyo
tuendelee kutumia utaalamu, ujuzi na ufahamu tuliaonao kuelimishana kwa
faidia ya yetu na Taifa letu.
%
% Wasalaam
%
% Phares Magesa
%
% Sent from my BlackBerry® smartphone provided by Airtel Tanzania.
%
% -----Original Message-----
% From: ymshana2003 <ymsha...@gmail.com>
% Sender: wanat...@googlegroups.com
% Date: Sun, 03 May 2015 10:43:32
% To: wanat...@googlegroups.com<wanat...@googlegroups.com>
% Reply-To: wanat...@googlegroups.com
% Subject: Re: [TPN] Kushuka kwa thamani ya Shilingi ya Tanzania
%
% Wenzangu,
%
% Kwa kuunga mkono mapendekeza endekefu ya ndugu Ipuge na Kasalla,
ningependa kuongezea kwamba andiko likiandikwa katika lugha ya kitaalam
litaleta utata katika kulitafsiti na kueleweka wa wadau wote. 
%
% Hivyo napendekeza kwamba, wataalam wakishaandika sisi wadau tulipitie
ili kulilainisha liekewe na wadau wote (sisi common-people). La sivyo
litakua andiko la kitaaluma tu.
%
% Heri na baraka.
%
% Tusonge mbele.
%
% Wenu, Yassin Mshana.
%
%
% Sent from Samsung Mobile
%
% -------- Original message --------
% From: Yahya Ipuge <yip...@gmail.com>
% Date:03/05/2015 05:03 (GMT+02:00)
% To: wanat...@googlegroups.com
% Subject: Re: [TPN] Kushuka kwa thamani ya Shilingi ya Tanzania
%
% Phares,
%
% Naona hadidu za rejea ziko tayari. Mimi ni mtaalam wa afya hivyo itakuwa
vigumu kuandika vizuri andiko la kiuchumi. Ñashauri wenzangu waanze mimi
ntakuwa mmoja kati ya wapitiaji (reviewer )wenye ''layman's lens".
%
% Nashauri  Buberwa Kaiza atusaidie rasimu ya kwanza kutumia hizo hadidu
za rejea
%
% Ipuge
% ------------------
%
%    
%
% On 2 May 2015 19:47, "'Camillus Kassala' via Wanataaluma wa Tanzania"
<wanat...@googlegroups.com> wrote:
% Ili andiko hilo, kwa Kiswahili, liwe na maana na ufumbuzi wa kudumu,
napendekeza hadidu za rejea zifuatazo:
%
% 1. Dhana ya sarafu ya taifa iainishwe.
% 2. Nafasi na thamani ya sarafu ya taifa katika biashara ya kimataifa
ielezwe.
% 3. Athari, kwa thamani ya sarafu ya taifa, za manunuzi ya ndani kwa
kutumia sarafu za kigeni zionshwe.
% 4. Athari ya kushuka kwa thamani ya sarafu ya taifa kwa uwezo wa
wananchi kujikimu kimaisha ikaziwe.
% 5. Jukumu la Benki Kuu kusimamia mfumo wa fedha, kodi na biashara ya
fedha za kigeni lifafanuliwe.
% 6. Kuinua kiwango cha ubora wa bidhaa na huduma za ki-Tanzania katika
soko la kimataifa kupewe mkazo.
% 7. Athari hasi, kwa uchumi wa nchi, wa sera za uchumi wa soko huria
ambao umekuwa holela zisisitizwe.
% 8. Athari za misaada na mikopo kutoka nje 'inyomwaga' dola (USD) katika
uchumi wanchi ziwekwe bayana.
% 9. Athari za kuifanya nchi yetu kuwa 'koloni' la dola (=sarafu) ya
Kimarekani ziwekwe wazi.
% 10. Sarafu ya Tanzania (= shilingi) kuwa ni nembo, kigezo, kitambulisho,
na nyenzo rasmi ya utamaduni wa kiuchumi wa Tanzania, ndani na nje ya nchi
ijengewe hoja ya kizalendo.
%
% CDNKassala
%
%
%
% On Friday, 1 May 2015, 15:11, 'Ngwisa Mpembe' via Wanataaluma wa
Tanzania <wanat...@googlegroups.com> wrote:
%
%
% Wanataaluma wenzangu na Mh Rais.
%
% Naunga mkono hoja ya Andiko. Baada ya kupitia hoja mbalimbali kama
zilivyotolewa, nashauri kuwepo na hadidu za rejea fupi kuwaongoza hawa
wenzetu kutoa andiko litakalokidhi haja kwa maana ya kutoa majibu/
mapendekezo kwa swala hili. 
%
% Naomba sana pia Mwl wangu Dr C.Kasalla amalizie hoja yake.
%
% Ngwisa Mpembe
%
%
%
% On May 1, 2015, at 2:01 PM, Phares Magesa <pma...@gmail.com> wrote:
%
% Wazalendo wenzetu Awadh Salum, Rosemary Mwakitwange , Camilius Kassala,
Dr.Yahaya Ipuge, Buberwa Kaiza na mwingine yoyote atakaejitolea.
%
% Kwa niaba yetu wote naomba mtusaidie kuandaa andiko hilo (draft) ili
lipitiwe na wadau na baadae kutolewa rasmi kwa umma.
%
% Naomba kutoa hoja
%
% Phares Magesa
% Rais - TPN
% +255784618320
%
%
%
% Sent from Samsung Mobile
%
%
%
% -------- Original message --------
% From: Yahya Ipuge <yip...@gmail.com>
% Date: 01/05/2015 08:58 (GMT+03:00)
% To: wanat...@googlegroups.com
% Subject: Re: Fwd: [TPN] Kushuka kwa thamani ya Shilingi ya Tanzania
%
%
% Phares,
% Asante sana kwa kuanzisha mjadala mzuri na pia shukrani kwa wataalam
waliotufungua macho. Nadhani sasa tinahitaji kuweka mkazo kwenye nini
kifanyike. Kama walivyoeleza wataalamu kila mmoja wetu anapaswa kuchukua
hatua pale alipo. Pia nimefurahi hakuna ushabiki wa kisiasa wa waziwazi.
% Nashauri wewe Phares ukiwa kama "moderator" wa mjadala au uchague mmoja
mwenye ujuzi wa masuala haya ili atusaidie kukokotoa maoni yaliyotolewa na
kuandaa andiko (paper) ambayo itaisaidia serikali na sisi wote. Kuna mmoja
alisema "free consultancy"  mimi naita mchango wa wataalam kwa nchi yao.
% Kwa mfano, mimi ni mpenzi wa kahawa ya kupikwa kwa mashine (brewed
coffee) na juzi nilipita kununua paketi yangu ya kila mwezi. Nikashangaa
imeongezeka bei kwa sh elfu mbili.  Nikauliza kwa nini imepanda bei maana
haihusiki na dola ya marekani.  Kahawa ni ya Rift Valey Mbeya na
Zanzibar. Nikaambiwa mwenye duka la kahawa (Coffee Shop) ni mtu wa nje
hivyo bei inategemea dola. Ila sidhani bei itapungua shilingi ikiimarika.
% Swali: hapo mimi kama mlaji nitachukua hatua gani? Je ni nani anapaswa
kulinda walaji kutokana na wafanya biashara  nyemelezi (opportunists)
kama hawa. Nadhani mifano mingi ipo ya kitaalam kwa wachumi au ki muma
kama niliotoa mimi.
% Hilo andiko ninalopendekeza liainishe hatua za kila mtu na kila taasisi
za kuchukukua ili kuinusuru shilingi yetu. Na baada ya miezi mitatu
tufanye mjadala kama huu kuangalia kama mapendekezo yetu yatakuwa
yamefanyiwa kazi.
% Naomba kuwasilisha,
% Ipuge
% ------------------
% Dr. Yahya A. Ipuge M.D., MMed.
% Senior Health Specialist
% Wazo Hill,Tegeta
% P.O. Box 66764
% 14130 Dar es Salaam
%    
% On 1 May 2015 07:21, "Janet Mbene" <maor...@gmail.com> wrote:
%
%
% ---------- Forwarded message ----------
% From: Janet Mbene <maor...@gmail.com>
% Date: Friday, May 1, 2015
% Subject: [TPN] Kushuka kwa thamani ya Shilingi ya Tanzania
% To: "wanat...@googlegroups.com" <wanat...@googlegroups.com>
%
%
% Neema asante lakini naona na wewe umelalamika bila kutoa pendekezo nini
kifanyike?
% Hili jambo linachangiwa na factors nyingi. lakini tuanze hapo tulipo
kila mmoja azalishe kitu, kama ni ajira yake mwenyewe kama ni bidhaa ya
shambani uvuvi ufugaji nk,  tulioajiririwa tutumie muda wetu kufanya kazi
kuongeza tija na ufanisi na kuongeza pato la ndani. pili tuongeze thamani
ya mauzo yetu ya nje ili kupata fedha ya kigeni zaidi. tatu tulegeze
masharti ya uwekezaji katika viwanda vinavyoajiri watu wengi na kuchangia
zaidi kwenye pato la taifa mfano nguo? ngozi maziwa na bidhaa zake, agro
processing.uvuvi na ufugaji wa samaki nk. nne tuhamasishe matumizi ya
bidhaa zetu hii itakuza soko la ndani na kukuza savings zitakazotumika
kupanua uwekezaji na akiba na hi itawezesha kupunguza uagizaji wa bidhaa
nje na kuinua thamani ya fedha yetu, mwisho tuache rushwa ili kuwe na
ufanisi wa soko na kupunguza gharama za uzalishaji na kufanya bidhaa
kufikika kwa wengi na kuinua maisha ya watanzania wengi.
% Mwisho wasomi tuwe wa kwanza kuonyesha mfano katika yote hayo badala ya
kulalama na kunyooshea wengine vidole.
%
% MWISHO WATANZANIA TUCHUKIE MEDIOCRITY! KURIDHIKA NA SUB-STANDARD
PERFORMANCE KWENYE KILA JAMBO!
%
%
% TUAMKE  TUANZE KULITUMHLIA TAIFA LETU NA KUJIFM
% On Thursday, April 30, 2015, Neema Machege <ikom...@gmail.com> wrote:
% Asalaam alleikoum wapendwa..
% Mbona miaka iliyopita wenzetu kenya thamani vya pesa yao Ilikua sawa tu
Na yetu? 
% Inasikitisha kuona pesa yetu binashuka kila siku. 
% Ila nafikiri tatizo ni sisi wenyewe , we're not productive enough. 
Kenya wana produce Sana Na wana export sana, 
% Imagine huku Europe ukienda supermarket kuna avocado , green beans ,
tea, coffee etc kutoka Kenya,  these guys are ambitious and hard working
.. 
% Hata Viatu vya ngozi vya kimasai hizo tunaita za culture just a simple
thing,, ukienda kununua mtaani wauzaji wanasifia zinazotoka Kenya ni poa
zaidi, 
% That's a nonessential , watanzania tumezidi. Only fewer people are
creative the rest ni maneno mengi, 
% It's for us to wake up, make a move , be creative, and use our natural
resources to backup our money. 
% Na Sasa Chinese Na neighbours countries  wanavamia , tusipoangalia
we'll wake up one day to find out that we're foreigners in our own
country.. 
% And that day will be the end of the end .. 
%
% Let's save whatever is left before the whole ship sank completely.. 
% God bless our beautiful country , and may he bring us the courage to
bring some changes,
% Amen ðŸ™
%
% Neema Ezekiely 
%
% On Thursday, April 30, 2015, Alex Nguluma <a.ng...@rexattorneys.co.tz>
wrote:
% Hi Yasin,
% Naona Kali zako.
% Alex  Nguluma
%
% Sent from my iPhone
%
% On Apr 30, 2015, at 11:11 AM, ymshana2003 <ymsha...@gmail.com> wrote:
%
% Kwa kuongezea tu...
% Ile Sera ya "kujitegemea" imeloweshwa maji....basda ya wito wa "Ruksa"
kujichanganya katika biashara tukasahau kujichanganya katika mambo
ya"uchumi"....
% BoT haitoshi katika shughuli ya "Economic Intelligence" ili kuzuia
shughuli za 'Ecomic Hitmen' wanaoweza kuangusha uchumi wa nchi kirahisi
tu.....hasa hasa baada ya kupata mnuso wa gas....kuna wataalam wataendelea
kuja 'kutusaidia' na "kujisaidia zaidi" kwani kuna soko Tz. Usimamizi wa
hao "wataalam" ingebidi uwe wa karibu zaidi kwani tunao wataalam wetu
ambao Mfumo uliopo hauwahusishi vilivyo....
%
% Naishia hapo.
%
% Yassin Mshana
%
% Ni hayo tu kwa leo.
% Sent from Samsung Mobile
%
%
% -------- Original message --------
% From: "Bubelwa E. Kaiza"
% Date:29/04/2015 21:53 (GMT+02:00)
% To: wanat...@googlegroups.com,wana...@googlegroups.com
% Subject: [TPN] RE: Kushuka kwa thamani ya Shilingi ya Tanzania
%
% Mrema,
% Umeongea kiasi fulani ila sababu za kushuka kwa Tzs. dhidi ya dola ya
kimarekani ni hizi zifuatazo:-
% 1.  Kuvuja kwa uchumi (economc leakage)/matumizi holela ya dola kwenye
mzunguko wa ndani ya nchi wa fedha. Duniani kote, kuendesha uchumi imara
kunahitaji mikakati na taasisi imara za kusimamia sera, sheria na kanuni
za fedha. Nchini Ufaransa, kwa mfano, hairuhusiwi kubadilisha/kununua Euro
taslim zenye thamani ya zaidi ya dola 1000! Afrika ya Kusini hairuhusiwi
kutumia dola/euro isipokuwa rand tu unaponunua mali au huduma yoyote
(hotelini, ticket za ndage n.k). Hapa nchini kwetu hali ni shaghala
baghala – mamlaka zinazopaswa kusimamia uchumi wa nchi hazifanyi
chochote; bureaux de change zinahamisha mauzo ya kila siku ya madukani
kwenda nje ya nchi.
%  
% 2.  Watu, hasa mafisadi, kutorosha/kuhodhi dola nje ya nchi kutokana na
hofu ya uchuguzi mkuu. Hali hii inasababisha uhaba wa dola hivyo
kutengeneza artificial appreciation ya dola kutokana na msingi mkuu wa
uchumi wa demand vs. supply.
%  
% 3.  Tanzania kutokuwa na dhahabu ya kuuza nje ya nchi (dhahabu
inayochimbwa siyo ya kwetu bali ni ya makampuni yanayochimba (wawekezaji)
na zaidi ya 90% ya mauzo ya dhahabu na madini mengine nje ya nchi
hairudishwi nchini bali yanabaki huko (clauses za MDAs zinatoa fursa hizo
kwa makampuniya madini) nyumbani kwao na wawekezaji. Kwa kifupi Tanzania
siyo gold mining country bali ni source of gold, hivyo haimiliki madini
yanayochimbwa nchini kwake bali madini husika humilikiwa na nchi mama wa
makampuni ya wawekezaji.
%  
% 4.  Kuwa na weak manufacturing, construction and professional services
industries hivyo nchi kutegemea imports zaidi kuliko uwezo wa kuuza huduma
na bidhaa nje ya nchi. Aidha mauzo ya mazao ya kahawa, pamba, katani na
chai nje ya nchi yamepungua kufikia negligible value. Nchi isipouza bidhaa
na huduma za kutosha nje ya nchi haiwezi kuwa na akiba ya kutosha ya fedha
ya kigeni. Na kwa mukhtadha huu, thamani ya fedha ya nchi haiwezi
kuimarishwa na pesa ya misaada au mikopo kutoka kwa wafadhali au mashirika
ya Bretton Woods.
%  
% --
% You received this message because you are subscribed to the Google
Groups "Wanataaluma wa Tanzania" group.
% To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send
an email to wanataaluma...@googlegroups.com.
% For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
% --
% You received this message because you are subscribed to the Google
Groups "Wanataaluma wa Tanzania" group.
% To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send
an email to wanataaluma...@googlegroups.com.
% For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
%
%
% --
% Janet Z.Mbene (MP)
% Deputy Minister for Industry and trade
% P O BOX 9503 Dar Es Salaam
% Tel:     +255 22 2127873
% Mob:   +255 755 067594/ 784 596444
% Email:maor...@gmail.com
%
%
%
%
%
%
% --
% Janet Z.Mbene (MP)
% Deputy Minister for Industry and trade
% P O BOX 9503 Dar Es Salaam
% Tel:     +255 22 2127873
% Mob:   +255 755 067594/ 784 596444
% Email:maor...@gmail.com
%
%
%
% --
% You received this message because you are subscribed to the Google
Groups "Wanataaluma wa Tanzania" group.
% To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send
an email to wanataaluma...@googlegroups.com.
% For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
% --
% You received this message because you are subscribed to the Google
Groups "Wanataaluma wa Tanzania" group.
% To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send
an email to wanataaluma...@googlegroups.com.
% For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
% --
% You received this message because you are subscribed to the Google
Groups "Wanataaluma wa Tanzania" group.
% To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send
an email to wanataaluma...@googlegroups.com.
% For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
% --
% You received this message because you are subscribed to the Google
Groups "Wanataaluma wa Tanzania" group.
% To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send
an email to wanataaluma...@googlegroups.com.
% For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
%
%
% --
% You received this message because you are subscribed to the Google
Groups "Wanataaluma wa Tanzania" group.
% To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send
an email to wanataaluma...@googlegroups.com.
% For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
% --
% You received this message because you are subscribed to the Google
Groups "Wanataaluma wa Tanzania" group.
% To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send
an email to wanataaluma...@googlegroups.com.
% For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
%
% --
% You received this message because you are subscribed to the Google
Groups "Wanataaluma wa Tanzania" group.
% To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send
an email to wanataaluma...@googlegroups.com.
% For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
%
% --
% You received this message because you are subscribed to the Google
Groups "Wanataaluma wa Tanzania" group.
% To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send
an email to wanataaluma...@googlegroups.com.
% For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
%

Donath R.Olomi

unread,
Feb 12, 2016, 4:26:44 AM2/12/16
to wanat...@googlegroups.com


Dear Potential Applicant,
Stanford Seed is very exited to announce that it’s successful leadership
and management training program, the *Seed Transformation Program* will be
delivered for the first time in Nairobi, Kenya in May 2016. The
Transformation Program recruits companies throughout East Africa to
participate in 4 intensive learning sessions, over a period of 6 months to
support the growth and scale of Small and Medium size Enterprises (SMEs) in
the region.

At the bottom of this email, I have included further information about the
structure and design on the program.

For more information (and videos!) about the Transformation Program please
visit our website through the link below:

https://seed.stanford.edu/seed-transformation-program/stanford-seed-east-africa


If you meet the eligibilty requirements and are interested in applying,
please use the link here:

https://stanfordgsb.qualtrics.com/jfe1/form/SV_dhWtdy1Gl0XmFqR


*Information about the Stanford Seed Program*

*The Stanford Institute for Innovation in Developing Economies (Seed) seeks
innovative and growth-oriented leaders of small and medium-sized
enterprises (SMEs) based in East Africa.*


*Seed's highly interactive six-month Transformation Program challenges SME
leaders to assess their vision, redefine their strategies, and make
ambitious changes toward exponential growth.*

*Led by prominent Stanford University faculty and industry experts, the
program is designed to expose SME leaders to:*

- *Core business skills such as accounting, finance, marketing,
operations, corporate governance, organizational design, strategy, and
more*
- *Applied skills such as negotiation, teamwork, leadership, and
pitching*
- *Approaches to product design and prototyping*
- *Prominent executives and corporate, venture, and angel investors who
participate as guest speakers, expert panelists, and business mentors *

*Additional program benefits include: *

- *Local and regional peer networks—designed to enrich the educational
experience and build relationships across borders and industries*
- *Eligibility to apply for a Stanford Seed coach upon completion of the
program*

*Program Eligibility:*

*Applicants must demonstrate commitment and potential to grow and scale
their companies, thereby creating jobs, products, or services that benefit
those living in poverty.*

- *Applicants must be founders/senior leaders of for-profit companies.*
- *Applicants must lead organizations with an annual revenue range
between $150,000 USD and $15 million USD.*
- *Applicant's company must be headquartered, legally registered, and
currently operating within East Africa.*
- *Applicant must have English language proficiency.*
- *Previously, SME leaders working in the following sectors have
participated: agriculture/food processing, construction, civil
engineering,
real estate, education, energy, financial services, healthcare,
information
and communications technologies (ICT), retail/product manufacturing,
transportation/logistics, and water and sanitation. Other sectors can
qualify for admittance. *


*Program FeesThe Program fee for the May 2016 cohort is $1,500 USD.*



***********************************************************************************

Best wishes,
Rita
*_________________________________________*
*Rita Lonhart, MSc*
Associate Director, Global Operations

*Stanford *| *Seed*
Stanford Institute for Innovation in Developing Economies
Knight Management Center, 2nd floor, Class of '68 Building Visit Us!
<http://www.gsb.stanford.edu/visit>
*Stanford** Graduate School of Business*
655 Knight Way
Stanford, CA 94305-7298
+1 650 736 1117 (USA)
+254 (0) 790 489 344 (Kenya)
+250 (0) 784 083 724 (Rwanda)
+255 (0) 742 023 878 (Tanzania)
Skype ID: ritalonhartseed

On Tue, May 5, 2015 00:19, Phares Magesa wrote:
% Wenye maoni yoyote kuhusu suala hili sasa wapeleke kwa kamati ndogo
tuliyopendekeza ili yaunganishwe katika andiko ambalo tumewaomba wenzetu
watusaidie kuliandika ili lije litolewe rasmi kwa umma kama kauli yetu
wote.
%
% Kamati inaundwa na:
%
% Ndg. Buberwa Kaiza
% Ndg. Rosemary Mwakitwange,
% Ndg. Dk. Yassin Mshana
% Ndg. Dk. Yahya Ipuge
% Ndg. Salum Awadh
% Ndh. Camillius Kasalla
%
% Hivyo basi kwa sasa majadiliano kwenye mada hii tutasitisha ili kuwapa
wenzetu muda wa kuandaa andiko na sasa tutaelekeza majadiliano kwenye mada
nyingine zilizopo au zitakazofuata kwenye jukwaa ili tusaidiane kutatua
changamoto zilizopo kwenye jamii yetu.
%
% Tunawashukuru wote waliotoa maoni ambayo yatasaidia kuandaa andiko hilo
ambalo tunaamini watunga sera wetu na wanananchi kwa ujumla kila mmoja
amepata ufahamu na watafaidika zaidi tukitoa andiko hilo kwa hiyo
tuendelee kutumia utaalamu, ujuzi na ufahamu tuliaonao kuelimishana kwa
faidia ya yetu na Taifa letu.
%
% Wasalaam
%
% Phares Magesa
%
% Sent from my BlackBerry® smartphone provided by Airtel Tanzania.
%
% -----Original Message-----
% From: ymshana2003 <ymsha...@gmail.com>
% Sender: wanat...@googlegroups.com
% Date: Sun, 03 May 2015 10:43:32
% To: wanat...@googlegroups.com<wanat...@googlegroups.com>
% Reply-To: wanat...@googlegroups.com
% Subject: Re: [TPN] Kushuka kwa thamani ya Shilingi ya Tanzania
%
% Wenzangu,
%
% Kwa kuunga mkono mapendekeza endekefu ya ndugu Ipuge na Kasalla,
ningependa kuongezea kwamba andiko likiandikwa katika lugha ya kitaalam
litaleta utata katika kulitafsiti na kueleweka wa wadau wote. 
%
% Hivyo napendekeza kwamba, wataalam wakishaandika sisi wadau tulipitie
ili kulilainisha liekewe na wadau wote (sisi common-people). La sivyo
litakua andiko la kitaaluma tu.
%
% Heri na baraka.
%
% Tusonge mbele.
%
% Wenu, Yassin Mshana.
%
%
% Sent from Samsung Mobile
%
% -------- Original message --------
% From: Yahya Ipuge <yip...@gmail.com>
% Date:03/05/2015 05:03 (GMT+02:00)
% To: wanat...@googlegroups.com
% Subject: Re: [TPN] Kushuka kwa thamani ya Shilingi ya Tanzania
%
% Phares,
%
% Naona hadidu za rejea ziko tayari. Mimi ni mtaalam wa afya hivyo itakuwa
vigumu kuandika vizuri andiko la kiuchumi. Ñashauri wenzangu waanze mimi
ntakuwa mmoja kati ya wapitiaji (reviewer )wenye ''layman's lens".
%
% Nashauri  Buberwa Kaiza atusaidie rasimu ya kwanza kutumia hizo hadidu
za rejea
%
% Ipuge
% ------------------
%
%    
%
% On 2 May 2015 19:47, "'Camillus Kassala' via Wanataaluma wa Tanzania"
<wanat...@googlegroups.com> wrote:
% Ili andiko hilo, kwa Kiswahili, liwe na maana na ufumbuzi wa kudumu,
napendekeza hadidu za rejea zifuatazo:
%
% 1. Dhana ya sarafu ya taifa iainishwe.
% 2. Nafasi na thamani ya sarafu ya taifa katika biashara ya kimataifa
ielezwe.
% 3. Athari, kwa thamani ya sarafu ya taifa, za manunuzi ya ndani kwa
kutumia sarafu za kigeni zionshwe.
% 4. Athari ya kushuka kwa thamani ya sarafu ya taifa kwa uwezo wa
wananchi kujikimu kimaisha ikaziwe.
% 5. Jukumu la Benki Kuu kusimamia mfumo wa fedha, kodi na biashara ya
fedha za kigeni lifafanuliwe.
% 6. Kuinua kiwango cha ubora wa bidhaa na huduma za ki-Tanzania katika
soko la kimataifa kupewe mkazo.
% 7. Athari hasi, kwa uchumi wa nchi, wa sera za uchumi wa soko huria
ambao umekuwa holela zisisitizwe.
% 8. Athari za misaada na mikopo kutoka nje 'inyomwaga' dola (USD) katika
uchumi wanchi ziwekwe bayana.
% 9. Athari za kuifanya nchi yetu kuwa 'koloni' la dola (=sarafu) ya
Kimarekani ziwekwe wazi.
% 10. Sarafu ya Tanzania (= shilingi) kuwa ni nembo, kigezo, kitambulisho,
na nyenzo rasmi ya utamaduni wa kiuchumi wa Tanzania, ndani na nje ya nchi
ijengewe hoja ya kizalendo.
%
% CDNKassala
%
%
%
% On Friday, 1 May 2015, 15:11, 'Ngwisa Mpembe' via Wanataaluma wa
Tanzania <wanat...@googlegroups.com> wrote:
%
%
% Wanataaluma wenzangu na Mh Rais.
%
% Naunga mkono hoja ya Andiko. Baada ya kupitia hoja mbalimbali kama
zilivyotolewa, nashauri kuwepo na hadidu za rejea fupi kuwaongoza hawa
wenzetu kutoa andiko litakalokidhi haja kwa maana ya kutoa majibu/
mapendekezo kwa swala hili. 
%
% Naomba sana pia Mwl wangu Dr C.Kasalla amalizie hoja yake.
%
% Ngwisa Mpembe
%
%
%
% On May 1, 2015, at 2:01 PM, Phares Magesa <pma...@gmail.com> wrote:
%
% Wazalendo wenzetu Awadh Salum, Rosemary Mwakitwange , Camilius Kassala,
Dr.Yahaya Ipuge, Buberwa Kaiza na mwingine yoyote atakaejitolea.
%
% Kwa niaba yetu wote naomba mtusaidie kuandaa andiko hilo (draft) ili
lipitiwe na wadau na baadae kutolewa rasmi kwa umma.
%
% Naomba kutoa hoja
%
% Phares Magesa
% Rais - TPN
% +255784618320
%
%
%
% Sent from Samsung Mobile
%
%
%
% -------- Original message --------
% From: Yahya Ipuge <yip...@gmail.com>
% Date: 01/05/2015 08:58 (GMT+03:00)
% To: wanat...@googlegroups.com
% Subject: Re: Fwd: [TPN] Kushuka kwa thamani ya Shilingi ya Tanzania
%
%
% Phares,
% Asante sana kwa kuanzisha mjadala mzuri na pia shukrani kwa wataalam
waliotufungua macho. Nadhani sasa tinahitaji kuweka mkazo kwenye nini
kifanyike. Kama walivyoeleza wataalamu kila mmoja wetu anapaswa kuchukua
hatua pale alipo. Pia nimefurahi hakuna ushabiki wa kisiasa wa waziwazi.
% Nashauri wewe Phares ukiwa kama "moderator" wa mjadala au uchague mmoja
mwenye ujuzi wa masuala haya ili atusaidie kukokotoa maoni yaliyotolewa na
kuandaa andiko (paper) ambayo itaisaidia serikali na sisi wote. Kuna mmoja
alisema "free consultancy"  mimi naita mchango wa wataalam kwa nchi yao.
% Kwa mfano, mimi ni mpenzi wa kahawa ya kupikwa kwa mashine (brewed
coffee) na juzi nilipita kununua paketi yangu ya kila mwezi. Nikashangaa
imeongezeka bei kwa sh elfu mbili.  Nikauliza kwa nini imepanda bei maana
haihusiki na dola ya marekani.  Kahawa ni ya Rift Valey Mbeya na
Zanzibar. Nikaambiwa mwenye duka la kahawa (Coffee Shop) ni mtu wa nje
hivyo bei inategemea dola. Ila sidhani bei itapungua shilingi ikiimarika.
% Swali: hapo mimi kama mlaji nitachukua hatua gani? Je ni nani anapaswa
kulinda walaji kutokana na wafanya biashara  nyemelezi (opportunists)
kama hawa. Nadhani mifano mingi ipo ya kitaalam kwa wachumi au ki muma
kama niliotoa mimi.
% Hilo andiko ninalopendekeza liainishe hatua za kila mtu na kila taasisi
za kuchukukua ili kuinusuru shilingi yetu. Na baada ya miezi mitatu
tufanye mjadala kama huu kuangalia kama mapendekezo yetu yatakuwa
yamefanyiwa kazi.
% Naomba kuwasilisha,
% Ipuge
% ------------------
% Dr. Yahya A. Ipuge M.D., MMed.
% Senior Health Specialist
% Wazo Hill,Tegeta
% P.O. Box 66764
% 14130 Dar es Salaam
%    
% On 1 May 2015 07:21, "Janet Mbene" <maor...@gmail.com> wrote:
%
%
% ---------- Forwarded message ----------
% From: Janet Mbene <maor...@gmail.com>
% Date: Friday, May 1, 2015
% Subject: [TPN] Kushuka kwa thamani ya Shilingi ya Tanzania
% To: "wanat...@googlegroups.com" <wanat...@googlegroups.com>
%
%
% Neema asante lakini naona na wewe umelalamika bila kutoa pendekezo nini
kifanyike?
% Hili jambo linachangiwa na factors nyingi. lakini tuanze hapo tulipo
kila mmoja azalishe kitu, kama ni ajira yake mwenyewe kama ni bidhaa ya
shambani uvuvi ufugaji nk,  tulioajiririwa tutumie muda wetu kufanya kazi
kuongeza tija na ufanisi na kuongeza pato la ndani. pili tuongeze thamani
ya mauzo yetu ya nje ili kupata fedha ya kigeni zaidi. tatu tulegeze
masharti ya uwekezaji katika viwanda vinavyoajiri watu wengi na kuchangia
zaidi kwenye pato la taifa mfano nguo? ngozi maziwa na bidhaa zake, agro
processing.uvuvi na ufugaji wa samaki nk. nne tuhamasishe matumizi ya
bidhaa zetu hii itakuza soko la ndani na kukuza savings zitakazotumika
kupanua uwekezaji na akiba na hi itawezesha kupunguza uagizaji wa bidhaa
nje na kuinua thamani ya fedha yetu, mwisho tuache rushwa ili kuwe na
ufanisi wa soko na kupunguza gharama za uzalishaji na kufanya bidhaa
kufikika kwa wengi na kuinua maisha ya watanzania wengi.
% Mwisho wasomi tuwe wa kwanza kuonyesha mfano katika yote hayo badala ya
kulalama na kunyooshea wengine vidole.
%
% MWISHO WATANZANIA TUCHUKIE MEDIOCRITY! KURIDHIKA NA SUB-STANDARD
PERFORMANCE KWENYE KILA JAMBO!
%
%
% TUAMKE  TUANZE KULITUMHLIA TAIFA LETU NA KUJIFM
% On Thursday, April 30, 2015, Neema Machege <ikom...@gmail.com> wrote:
% Asalaam alleikoum wapendwa..
% Mbona miaka iliyopita wenzetu kenya thamani vya pesa yao Ilikua sawa tu
Na yetu? 
% Inasikitisha kuona pesa yetu binashuka kila siku. 
% Ila nafikiri tatizo ni sisi wenyewe , we're not productive enough. 
Kenya wana produce Sana Na wana export sana, 
% Imagine huku Europe ukienda supermarket kuna avocado , green beans ,
tea, coffee etc kutoka Kenya,  these guys are ambitious and hard working
.. 
% Hata Viatu vya ngozi vya kimasai hizo tunaita za culture just a simple
thing,, ukienda kununua mtaani wauzaji wanasifia zinazotoka Kenya ni poa
zaidi, 
% That's a nonessential , watanzania tumezidi. Only fewer people are
creative the rest ni maneno mengi, 
% It's for us to wake up, make a move , be creative, and use our natural
resources to backup our money. 
% Na Sasa Chinese Na neighbours countries  wanavamia , tusipoangalia
we'll wake up one day to find out that we're foreigners in our own
country.. 
% And that day will be the end of the end .. 
%
% Let's save whatever is left before the whole ship sank completely.. 
% God bless our beautiful country , and may he bring us the courage to
bring some changes,
% Amen 🙏
%
% Neema Ezekiely 
%
% On Thursday, April 30, 2015, Alex Nguluma <a.ng...@rexattorneys.co.tz>
wrote:
% Hi Yasin,
% Naona Kali zako.
% Alex  Nguluma
%
% Sent from my iPhone
%
% On Apr 30, 2015, at 11:11 AM, ymshana2003 <ymsha...@gmail.com> wrote:
%
% Kwa kuongezea tu...
% Ile Sera ya "kujitegemea" imeloweshwa maji....basda ya wito wa "Ruksa"
kujichanganya katika biashara tukasahau kujichanganya katika mambo
ya"uchumi"....
% BoT haitoshi katika shughuli ya "Economic Intelligence" ili kuzuia
shughuli za 'Ecomic Hitmen' wanaoweza kuangusha uchumi wa nchi kirahisi
tu.....hasa hasa baada ya kupata mnuso wa gas....kuna wataalam wataendelea
kuja 'kutusaidia' na "kujisaidia zaidi" kwani kuna soko Tz. Usimamizi wa
hao "wataalam" ingebidi uwe wa karibu zaidi kwani tunao wataalam wetu
ambao Mfumo uliopo hauwahusishi vilivyo....
%
% Naishia hapo.
%
% Yassin Mshana
%
% Ni hayo tu kwa leo.
% Sent from Samsung Mobile
%
%
% -------- Original message --------
% From: "Bubelwa E. Kaiza"
% Date:29/04/2015 21:53 (GMT+02:00)
% To: wanat...@googlegroups.com,wana...@googlegroups.com
% Subject: [TPN] RE: Kushuka kwa thamani ya Shilingi ya Tanzania
%
% Mrema,
% Umeongea kiasi fulani ila sababu za kushuka kwa Tzs. dhidi ya dola ya
kimarekani ni hizi zifuatazo:-
% 1.  Kuvuja kwa uchumi (economc leakage)/matumizi holela ya dola kwenye
mzunguko wa ndani ya nchi wa fedha. Duniani kote, kuendesha uchumi imara
kunahitaji mikakati na taasisi imara za kusimamia sera, sheria na kanuni
za fedha. Nchini Ufaransa, kwa mfano, hairuhusiwi kubadilisha/kununua Euro
taslim zenye thamani ya zaidi ya dola 1000! Afrika ya Kusini hairuhusiwi
kutumia dola/euro isipokuwa rand tu unaponunua mali au huduma yoyote
(hotelini, ticket za ndage n.k). Hapa nchini kwetu hali ni shaghala
baghala – mamlaka zinazopaswa kusimamia uchumi wa nchi hazifanyi
chochote; bureaux de change zinahamisha mauzo ya kila siku ya madukani
kwenda nje ya nchi.
%  
% 2.  Watu, hasa mafisadi, kutorosha/kuhodhi dola nje ya nchi kutokana na
hofu ya uchuguzi mkuu. Hali hii inasababisha uhaba wa dola hivyo
kutengeneza artificial appreciation ya dola kutokana na msingi mkuu wa
uchumi wa demand vs. supply.
%  
% 3.  Tanzania kutokuwa na dhahabu ya kuuza nje ya nchi (dhahabu
inayochimbwa siyo ya kwetu bali ni ya makampuni yanayochimba (wawekezaji)
na zaidi ya 90% ya mauzo ya dhahabu na madini mengine nje ya nchi
hairudishwi nchini bali yanabaki huko (clauses za MDAs zinatoa fursa hizo
kwa makampuniya madini) nyumbani kwao na wawekezaji. Kwa kifupi Tanzania
siyo gold mining country bali ni source of gold, hivyo haimiliki madini
yanayochimbwa nchini kwake bali madini husika humilikiwa na nchi mama wa
makampuni ya wawekezaji.
%  
% 4.  Kuwa na weak manufacturing, construction and professional services
industries hivyo nchi kutegemea imports zaidi kuliko uwezo wa kuuza huduma
na bidhaa nje ya nchi. Aidha mauzo ya mazao ya kahawa, pamba, katani na
chai nje ya nchi yamepungua kufikia negligible value. Nchi isipouza bidhaa
na huduma za kutosha nje ya nchi haiwezi kuwa na akiba ya kutosha ya fedha
ya kigeni. Na kwa mukhtadha huu, thamani ya fedha ya nchi haiwezi
kuimarishwa na pesa ya misaada au mikopo kutoka kwa wafadhali au mashirika
ya Bretton Woods.
%  
% --
% You received this message because you are subscribed to the Google
Groups "Wanataaluma wa Tanzania" group.
% To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send
an email to wanataaluma...@googlegroups.com.
% For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
% --
% You received this message because you are subscribed to the Google
Groups "Wanataaluma wa Tanzania" group.
% To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send
an email to wanataaluma...@googlegroups.com.
% For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
%
%
% --
% Janet Z.Mbene (MP)
% Deputy Minister for Industry and trade
% P O BOX 9503 Dar Es Salaam
% Tel:     +255 22 2127873
% Mob:   +255 755 067594/ 784 596444
% Email:maor...@gmail.com
%
%
%
%
%
%
% --
% Janet Z.Mbene (MP)
% Deputy Minister for Industry and trade
% P O BOX 9503 Dar Es Salaam
% Tel:     +255 22 2127873
% Mob:   +255 755 067594/ 784 596444
% You received this message because you are subscribed to the Google
Groups "Wanataaluma wa Tanzania" group.
% To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send
an email to wanataaluma...@googlegroups.com.
% For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
% --
% You received this message because you are subscribed to the Google
Groups "Wanataaluma wa Tanzania" group.
% To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send
an email to wanataaluma...@googlegroups.com.
% For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
% --
% You received this message because you are subscribed to the Google
Groups "Wanataaluma wa Tanzania" group.
% To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send
an email to wanataaluma...@googlegroups.com.
% For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
% --
% You received this message because you are subscribed to the Google
Groups "Wanataaluma wa Tanzania" group.
% To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send
an email to wanataaluma...@googlegroups.com.
% For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
%
%
% --
% You received this message because you are subscribed to the Google
Groups "Wanataaluma wa Tanzania" group.
% To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send
an email to wanataaluma...@googlegroups.com.
% For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
% --
% You received this message because you are subscribed to the Google
Groups "Wanataaluma wa Tanzania" group.
% To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send
an email to wanataaluma...@googlegroups.com.
% For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
%
% --
% You received this message because you are subscribed to the Google
Groups "Wanataaluma wa Tanzania" group.
% To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send
an email to wanataaluma...@googlegroups.com.
% For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
%
% --
% You received this message because you are subscribed to the Google
Groups "Wanataaluma wa Tanzania" group.
% To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send
an email to wanataaluma...@googlegroups.com.

Donath R.Olomi

unread,
May 25, 2016, 9:50:40 AM5/25/16
to wanat...@googlegroups.com, roti...@imedtz.org

IMED is looking for marketing interns

The primary responsibility is field selling in Dar es Salaam.

Preferably marketing graduates, but may also be graduates from other
fields with the passion and energy required to sell and ability to learn
fast.

Benefits include training, coaching and networking.

Send motivation letter and CVs to in...@imedtz.org with heading:
MARKETING INTERN
Reply all
Reply to author
Forward
0 new messages