Hata mwenyewe amewahi kusema kwamba Ray C ndiye role model wake, kwa maana ndiye aliyemvutia mpaka kuingia kwenye gemu la muziki Bongo! Mpaka leo ninapoandika makala haya, Recho na Ray C ni kama mtu na mdogo wake, wameshafanya baadhi ya shoo pamoja na kuwakonga vilivyo mashabiki wao.
Kila mmoja aliamini kwamba Recho ataliziba pengo la mwanadada Ray C na kweli aliweza kufanya hivyo ipasavyo. Mwaka mmoja uliofuatia, akatoka na ngoma nyingine kali iliyomake headline, Upepo, jina lake likazidi kupaa. Hatujakaa sawa, akatoka na Nashukuru Umerudi, akathibitisha kwamba hakuwa amebahatisha kwenye gemu!
Kwa hiyo Recho ulipogundua kwamba unafanana na Ray C, na ukaona viatu vyake kwenye muziki vimekutosha na umejipatia mashabiki wengi na mafanikio makubwa, umeona haitoshi mpaka ukataka kuiga hata yale yasiyofaa kutoka kwake? Kama madai hayo ni ya kweli, bado hujachelewa, muda wa kujirekebisha unao kwa sababu kiumri bado wewe ni mdogo! Iga yale mazuri tu kutoka kwa Ray C, hakika utafika mbali lakini ukianza na hayo mengine, msemo wa umesifiwa kukimbia ukapitiliza kwenu, utakuwa unakuhusu!
8d45195817