Dear members,
Pale Chogo south kuna mapande mawili yanauzwa;
Pande la kwanza linapakana na shamba la Mndeme upande wa kusini,magharibi linapakana na Lukumbulu/Iso Lupembe, mashariki yupo Tobias na mimi na kaskazini ni barabara inayokwenda kwa Fox. Isso alitamani kuongeza, Mndeme alitamani kuongeza last week, akakosa shamba likachukuliwa na Lukumbulu, na Lukumbulu alitaka eka mia, lakini ana hamsini tu. Kazi kwenu, mwenye kisu kikali ndiye mla nyama.
Pande la pili liko karibu na Samweli Gideon/Mbuya/Malila upande wa magharibi,ni kaskazini kwa shamba la Tobias, ni kimlima chote. Linauzwa na bibi aliyetuuzia ile milima miwili,anamega tena mlima mwingine. Sikui Rafael kama utachemsha na hapa? Kwa waliofika kule, unapofika shambani kwa Gedion basi ni mkono wako wa kulia, kuna kimlima pale cha huyu bibi.
Malila