Nyimbo nyingine alizofanya akiwa peke yake ni pamoja na Demu Wangu aliofanya na marehemu Albert Magwea, pamoja na Chupa Nyingine. Akiwa na Wateule, wamefanya ngoma nyingi pia ambazo ni Msela, Nipende Nichukie na wimbo wao wa mwisho kutoa ni Vile Vile waliotoa mwaka 2011 wakiwa wamemshirikisha Solo Thang, huku video yake wakifanyia Afrika Kusini na Ireland alikokuwa anaishi Solo Thang!