TAARIFA YA NDANI: KUONGEZA MUDA WA KUCHUKUA FOMU - UCHAGUZI WA KANDA YA KASKAZINI

9 views
Skip to first unread message

Amani Golugwa

unread,
Jul 25, 2016, 6:29:50 AM7/25/16
to Amani Golugwa
TAARIFA YA NDANI YA CHAMA - KUONGEZA MUDA WA KUCHUKUA FOMU ZA KUGOMBEA UONGOZI WA KANDA YA KASKAZINI

SALAAM...!
KIkao cha Kamati KUU kilichoketi tarehe 23/24 Julai 2016, kimetoa maelekezo ya kuongeza muda wa kuchukua fomu za kugombea nafasi za uongozi wa kanda hadi tarehe 15 AGOSTI 2016, SAA KUMI NA NUSU JIONI.

HIVYO... Nichukue fursa hii kuwatangazia Wanachama Wote WA CHADEMA kuwa, kutakuwa na uchaguzi wa ndani ya chama wa nafasi za Uongozi wa Kanda ya Kaskazini. Uchaguzi huu utafanyika ili kutekeleza azimio la Baraza Kuu kuwa kanda zote nchini zifanye uchaguzi wa nafasi zifuatazo za Uongozi wa Kanda;

1. Mwenyekiti wa Kanda
2. Makamu Mwenyekiti wa Kanda
3. Mtunza Hazina wa Kanda

Mara baada ya kuwapata viongozi hawa, zitaundwa timu za wataalamu za Kanda (Timu 8).

HIvyo, Tangazo hili ni kwa wanachama wote WENYE SIFA, WENYE UWEZO, WENYE KUPATIKANA (AVAILABILITY) kujitokeza kugombea kwenye nafasi hizi.

Gharama za Fomu ni Tshs 100,000/=, fedha hii italipwa kupitia BENKI kama ifutavyo;

JINA LA AKAUNTI: CHADEMA KANDA YA KASKAZINI
BENKI: CRDB, MAPATO BRANCH, ARUSHA
AKAUNTI NAMBA: 0150280160800

Siku ya mwisho wa kurudisha Fomu itakuwa ni tarehe 15 Agosti 2016 Saa KUMI NA NUSU Jioni.

Fomu zitawasilishwa/kurudishwa Ofisi ya Kanda ya Kaskazini kwa KATIBU WA KANDA zikiwa zimeambatanishwa na uthibitisho wa Benki wa kulipa Fedha (Deposit Slip) na zikiwa zimejazwa kwa ufasaha.

KWA WALE WALIOKWISHA KUCHUKUA FOMU HAWANA HAJA YA KUCHUKUA TENA.

Kwa Maelezo zaidi wasiliana na Ofisi ya Katibu wa Kanda;

KATIBU WA KANDA - KASKAZINI
S.L.P 11325,
ARUSHA, TANZANIA
Email: gol...@gmail.com au chademak...@gmail.com
Simu: +255 754 912 914 au +255 0784 343 275

Nawatakia kila la heri,

Amani Golugwa
Katibu Kanda - Kaskazini
 

FOMU_YA_UCHAGUZI_NDANI_YA_CHAMA_KANDA.docx
Reply all
Reply to author
Forward
0 new messages