Salaam alaykum ndugu zangu katika emaan,
kuongezea kwenye post ya kaka Mahundi, kuhusu Scholarship za New Zealand...
Taratibu za maombi ya udhamini chini ya serikali ya New Zealand yana tofauti kidogo na Australia. Japo vipo vipengele vinavyofanana, hivyo basi nitaelezea hii ya Australia ambayo ninaifahamu. Na yenyewe karibuni itatangazwa kupitia tovuti hii: http://www.adsafrica.com.au/countryinfo/tanzania.php
Kawaida maombi ya scholarship kwa ajili ya Public (yaani, wale wanaofanyakazi serikalini au katika mashirika ya umma) hupitia Idara kuu ya Utumishi (President’s Office-Public Service Management). Baada ya Utumishi kukusanya maombi hayo, hufanya shortlist ambayo hufuatiwa na usaili. Hapa Utumishi inakuwa ni kiungo baina ya Tanzania na ofisi za Serikali dhamini ambazo kwa bara letu zipo Afrika Kusini. Na inakuwa bado hujachagua chuo tofauti na ya New Zealand, inahitaji anayetuma maombi kupata admission katika chuo kimojawapo kilichopo kwenye orodha yao na maeneo ya kusomea pia yametajwa, la kuzingatia ni tarehe ya mwisho ya kupokea maombi ya vyuo hivyo.
Nimepitia tovuti ya Utumishi kuangalia kama wameweka tangazo kuhusu Scholarship ya New Zealand, sijaliona. Tovuti yao ni: www.estabs.go.tz, tovuti hii pia huwekwa matangazo mbalimbali kama vile nafasi za kazi pamoja na scholarship za nchi tofauti tofauti. Kwahivyo pia ni vyema, tukiwa na tabia ya kupitia kila baada ya kipindi Fulani ili kupata taarifa hizi muhimu.
Aidha, kabla ya kutuma maombi ya Scholarship hii ya New Zealand ni vyema kuwasiliana na idara ya mafunzo, ofisi za utumishi kujua kama mlolongo unafanana kisha kuendelea na hatua zinazofuata. Na kama utumishi hawana taarifa na udhamini huu, basi utatuma maombi kufuatana na maelezo yaliyotumwa kwetu na bwana Mahundi.
Al muhim kuzingatia deadline na kuhakikisha vitu vilivyotajwa kwenye tangazo lao vyote vipo intact. Ikiwa ni pamoja na vyeti vyote viwe certified, pia huwa wanasisitiza matokeo ya test of English language proficiency. Ni vyema test hii ikifanywa mapema, kwenye tangazo lao wameainisha wanataka IELTS kutoka kwa watanzania. Mitihani hii hufanyika kwenye kituo cha British council, nafkiri pia wanatoa mafunzo jinsi ya kufaulu. Tafadhali pitia tovuti yao kwa maelezo zaidi: http://www.britishcouncil.org/africa-tz-ielts.htm
Natumai maelezo haya yatatoa muongozo, inshaallah kama kuna swali pia nitafurahi kulijibu likiwa lipo ndani ya uwezo wangu.
Maa’salaam,
Tatu.