New Arrival

37 views
Skip to first unread message

ZEYANA HAMID

unread,
Mar 23, 2009, 9:33:57 AM3/23/09
to the-fund...@googlegroups.com
I am writing to announce the birth of my second born Abdallah R.M Ramia he is one week old now and is doing quite fine Alhamdulillah.
 
Zeyana Abdallah Hamid
Msc Health Informatics-Candidate
University of Missouri-Columbia MO
+17853933875


Tawaqal Juma

unread,
Mar 23, 2009, 10:09:36 AM3/23/09
to the-fund...@googlegroups.com
Alhamdullah Rabil Aalamiina, May Allah make him Qurratu ghayn to you, his father and all Muslims. Amina


From: ZEYANA HAMID <zeya...@yahoo.com>
To: the-fund...@googlegroups.com
Sent: Monday, March 23, 2009 4:33:57 PM
Subject: [The Fundametals:104] New Arrival

Masoud Mahundi

unread,
Mar 23, 2009, 10:18:19 AM3/23/09
to the-fund...@googlegroups.com
MashaAllah,
hizi ni habari njema, zinaongeza faraja katika mioyo yetu.
ALLAH AMUONGOZE, AMUEPUSHE NA SHAYTAN, AWE NURU KATIKA UISLAMU
 
Masoud H. Mahundi
Department of Computer Science
University of Dar es Salaam
P.O Box 35062
Tel 255 22 410500 - 8 (or through ext 2466)
Mobile: +255 71 5258337 / +255 78 7258337
DUP Building - First Floor, Room No 206



From: ZEYANA HAMID <zeya...@yahoo.com>
To: the-fund...@googlegroups.com
Sent: Monday, March 23, 2009 4:33:57 PM
Subject: [The Fundametals:104] New Arrival

ali jabir

unread,
Mar 23, 2009, 3:19:48 PM3/23/09
to the-fund...@googlegroups.com
Assalaam alykum
bila shaka hizi ni habari njema. Allah mjaalie upole na utii kama Nabii Ismail, Ushujaa kama Sayyidna Omar... awe mja wa kheri wa kuwafaa wazazi wake na jamii ya kiislam kwa ujumla.
 
Ben Jabir

--- On Mon, 23/3/09, ZEYANA HAMID <zeya...@yahoo.com> wrote:
From: ZEYANA HAMID <zeya...@yahoo.com>
Subject: [The Fundametals:104] New Arrival

ali jabir

unread,
Mar 23, 2009, 3:23:24 PM3/23/09
to the-fund...@googlegroups.com
Assalaam Alaykum
Jamani hii group mail ilipoanzishwa mi sikuwa na habari. Naona wachache tu wanaoandika au ndio washiriki wote hawa: Sheikh Mahuni, Dada Zeyana na Sheik Tawakal.
Nipeni chimbuko la group hii nami niipe kipaumbele
 
Ali Jabir Mwadini
Addis

--- On Mon, 23/3/09, Masoud Mahundi <mmahu...@yahoo.com> wrote:
From: Masoud Mahundi <mmahu...@yahoo.com>
Subject: [The Fundametals:106] Re: New Arrival
To: the-fund...@googlegroups.com

Masoud Mahundi

unread,
Mar 24, 2009, 1:11:22 AM3/24/09
to the-fund...@googlegroups.com

Waaleykumus-salaam brother Ali Jabir

Swali lako nimelipenda sana kwani limeonesha umakini ulionao kwenye kufuatilia mambo

Kuliwahi kuwa na mijadala tu ya mambo mbali mbali ulioshirikisha baadhi ya member wa group hili ambayo kwa kiasi fulani iliwakutanisha watu tena lau ki-fikra.

Haya mambo yalipoanza kuwavuta watu kiufahamu na kihisia, pakaonekana ni vema kuanzisha discussion group, ambayo itahusisha na wengine pia, ili kupata kusikika kile ambacho muislamu angependa wenzake wakisikie. Ni kama kusema muislamu anapata e-audience.

Ingawa hii inakwenda zaidi pale ambapo kunakuwa na maswali na wengine kuchangia. Si lazima msemaji ndio ajibu ila yeyote mwenye uelewa anaweza kujibu

Kundi hili likaitwa “The Fundamentals”

Mpaka sasa mada zilizowahi kujadiliwa ni pamoja na;

  1. Umuhimu wa isti'adha

  2. Ni nani Ahmadiya, na wapi wanapotoa watu

  3. Qul-latayn ni nini

  4. Uhalali wa kuoa watu wa kitabu (ni sahihi kwa sasa, ni akina nani hao ahlulkitaab kwa mazingira yetu, nchi zetu je)

  5. Majukumu ya vijana wa kiislamu (hata pakataka kutolewa azimio la mwaka huu)

  6. Na mengine wenzangu wanaweza kukumbushia


Memba wa kundi hili ni wengi kiasi fulani, na kila mmoja kati yao ana nafasi sawa, na hadhi sawa mbele ya memba wengine. Kuchangia, kuuliza, na kusema mtu aonacho ni vizuri wenzake waislamu wakijue.

Ni kweli kwamba Sheykh Tawak-kal, Bi Zeyana, DOC Mohammed, Sheykh Kisilwa, Maalim Mdoe, Sheykh Ijumaa na mimi ndio inaonekana tumeshiriki sana, lakini nafasi ziko wazi kwa yeyote kushiriki.

Mpaka sasa kundi hili lina memba 46 ambao wote ni watumiaji wazuri wa kiswahili na kiingereza kwenye kuwasiliana (Nadhani kifaransa ni wachache kidogo)

Baada ya kusema hayo naomba nikukaribishe kwenye 'jukwaa'

Karibu sana

MM

 
Masoud H. Mahundi
Department of Computer Science
University of Dar es Salaam
P.O Box 35062
Tel 255 22 410500 - 8 (or through ext 2466)
Mobile: +255 71 5258337 / +255 78 7258337
DUP Building - First Floor, Room No 206



From: ali jabir <alja...@yahoo.co.uk>
To: the-fund...@googlegroups.com
Sent: Monday, March 23, 2009 10:23:24 PM
Subject: [The Fundametals:108] Re: New Arrival

Zaharani Kisilwa

unread,
Mar 24, 2009, 1:53:46 AM3/24/09
to the-fund...@googlegroups.com

CONGRATULATIONS SISTER. MAY ALLAH RAISE HIM TO BE THE MOST RESPONSIBLE PERSON IN HIS RELIGIOUS LIFE.

 


From: the-fund...@googlegroups.com [mailto:the-fund...@googlegroups.com] On Behalf Of ZEYANA HAMID
Sent: Monday, March 23, 2009 4:34 PM
To: the-fund...@googlegroups.com
Subject: [The Fundametals:104] New Arrival

 

I am writing to announce the birth of my second born Abdallah R.M Ramia he is one week old now and is doing quite fine Alhamdulillah.

DOC MOH

unread,
Mar 24, 2009, 2:48:14 AM3/24/09
to the-fund...@googlegroups.com
Mashallah. Alf mabrooooooooooooooooooooooook.
 
Allah Amkuze. Tunakuomba Ya Allah kwa uwezo wako umjaalie Abdallah awe mwana mwema kama lilivyo jina lake kwa kuambatishwa na LAKO. Umfungulie milango ya rizki za halali na kumtosheleza kwa rizki zake za halali mpaka awe anachukia vya haramu.
Wassalam
Aila ya Mohammed.
2009/3/23 ZEYANA HAMID <zeya...@yahoo.com>

johari hussein

unread,
Mar 24, 2009, 3:35:01 AM3/24/09
to the-fund...@googlegroups.com
ZEYABA, Allah Akukuzikie mwanao, awe msikivu na mtiifu kwa Mola wake na dini yake bila kusahau wazazi wake.



--- On Mon, 3/23/09, DOC MOH <docmo...@gmail.com> wrote:

From: DOC MOH <docmo...@gmail.com>
Subject: [The Fundametals:111] Re: New Arrival
To: the-fund...@googlegroups.com

ali jabir

unread,
Mar 24, 2009, 6:40:06 AM3/24/09
to the-fund...@googlegroups.com
Nashukuru sana Sheikh Mahundi kwa maelezo yako mwanana. Bila shaka umetumia muda kuandika yote na hiyo ni ishara ya kujali kwako. Nakuhakikishia na kuwahakikishia wengine kwamba nani nimejali.
 
Wengi uliowataja sina hakika kwamba nawajua kwa sura. Ingefaa siku moja karibuni tukakutana mahali fulani kama watu hawa wapo Dar tukabadilishana mawazo. Jambo hilo huenda litaongeza ari ya watu kuchangia katika hili Jukwaa. Kwa sasa nipo Addis hadi tarehe 27 inshaallah.
 
Mambo mengine nitasema katika mail zijazo. Kifaransa kinyamazie tu. Vyema tutumie kiswahili.
 
Asante
Ali Jabir
ADDIS

Tawaqal Juma

unread,
Mar 24, 2009, 7:12:10 AM3/24/09
to the-fund...@googlegroups.com
Assalaam Alaykum, Hii ni makala niliyokuwa nimeiandika kuhusiana na mambo muhimu ambayo watu wengi hawayajui kuhusiana na Ghaqiqa ya Mtoto. Nilipa jina hili ili kuvuta hisia za wasomaji japo kuna ukweli fulani kuhusiana na mambo hayo yanayohusiana na Ghaqiqa. Hii ni zawadi nampa Umm Zar'aa na wanafundamentals wote Allah awabariki popote mlipo. 

 

ULIYOKUWA HUYAFAHAMU KATIKA GHAQIQAH AFANYIWAYO MTOTO MCHANGA

  

  • Ghaqiqah ni jina lililopewa kichinjwa (mnyama) achinjiwacho mtoto mchanga aliyezaliwa ni mamoja awe ni wa kike au wakiume.

 

  • Ni Sunna si waajibu. Ushahidi wa hili ni uko katika maneno ya Mtume aliposema; "Atakayepata mtoto na akapenda amchinjie basi na afanye hivyo kwa mwanamume mbuzi wawili na kwa mwanamke mbuzi mmoja". Hadithi hii imepokewa na maimamu Abuu Dawuud na Annasaai kutoka kwa Abdallah bn Umar. Kauli ya Mtume; na akapenda amchinjie ni dalili kuwa Ghaqiqah si lazima bali ni jambo linalopendeza mwislamu kulifanya. Lakini kwa mwenye uwezo wa kufanya hivyo basi iliyo bora zaidi kwake ni kufanya ama yule asiye na uwezo wa kufanya hivyo basi si lazima kwake  maana M/Mungu haikalifishi nafsi yoyote ila yale yaliyo sawa na uwezo wake na pia hakufanya uzito katika dini yake.

 

  • Imethibiti kutoka kwa Mtume wa Allah kuwa yeye kasema; kila mtoto azaliwaye anafungamana na Ghaqiqa yake, anachinjiwa siku ya saba, ananyolewa kichwa chake na anaitwa jina. Wanachuoni wamelizungumzia neno kufungamana hapa kuwa linaweza kuwa linamaanisha mambo mengi, miongoni mwa mambo hayo ni;
  1. anakuwa kama mwenye kujisikia uzito na unyonge na mwenye kukosa wepesi na furaha maishani hadi achinjiwe
  2. Anazuiwa kuwaombea wazazi wake uombezi mwema wa siku ya Qiyama
  3. Ni deni lililo mithili ya Rehani ambayo hulazimiana na mtu hadi ailipe.

 

  • iliyo bora zaidi na timilifu ni kuwa wale mbuzi wawili au kondoo wawili ambao anatakiwa mtoto wa kiume achinjiwe wanatakiwa wawe ni wenye kufanana au kukaribiana kufanana kimaumbile na kiumri. Lakini kama itashindikana kuwapata mbuzi wawili wenye sifa kama hizo itafaa hata kama watatofautiana kiumbile na kiumri maadamu tu wanasifa zinazofaa kisheria kwa ajili ya ibada hii. Sifa hizo tutazitaja baadaye.

 

  • iliyo bora zaidi na timilifu ni kumchinjia mtoto wa kiume mbuzi wawili lakini ikiwa mtu atashindwa kabisa kuchinja mbuzi kama kutokana na yeye kupata mbuzi mmoja tu au kumiliki kiwango cha mbuzi mmoja tu basi huyo huyo mbuzi mmoja atatosha.

 

  • Sunnah ni kumchinjia mtoto atakapofikisha siku ya saba kama ilivyokuja katika hadithi ya Samrah, lakini ikiwa mtu hakuweza kuchinja siku ya saba basi na afanye hivyo siku ya kumi na nne na ikiwa atashindwa siku ya kumi na nne basi na afanye hivyo siku ya ishirini na moja na ikiwa atashindwa siku ya ishirini na moja basi na afanye hivyo siku yeyote.

 

  • Ibada hii ya kuchinja hufanyika hata kama mtoto kafariki maadamu tu alizaliwa hai au hata kama mimba ilitoka lakini mtoto tayari alikuwa ameviviwa roho, yaani alikuwa amefikisha miezi minne au siku mia na ishirini na kuendelea lakini kama alikuwa hajafikisha miezi minne au siku mia na ishirini hapo hatafanyiwa Ghaqiqah.

 

  • Kuna imani imeenea kwa watu wengi kuwa kichinjwa cha Ghaqiqah hakivunjwi mifupa hii ikiwa kama ishara ya kumtakia mtoto salama na asivunjike maishani mwake hili si sahihi wala halina mashiko katika Qur’an wala Sunna. Kwa hiyo ieleweke wazi kuwa mifupa ya Ghaqiqah inafaa kuvunjwa wala hii haitakuwa sababu ya kuvunjika kwa mtoto hata kama itatokea kama watu wanavyoamini. Vile vile kuna jambo jingine nalo ni kuwa nyama ya Ghaqiqah huchanganywa au hupikwa kwa maji yaliyotiwa vitu vitamu vitamu kama sukari au huchanganywa na asali wakati wa kuliwa, hii ikiwa ni kama ishara ya kumtakia mtoto tabia njema; hili nalo pia halina mashiko. Hivyo iwekwe chumvi na kupikwa kama nyama ya kawaida

 

  • Kinachotakiwa kuchinjwa katika Ghaqiqah katika wanyama ambao kisheria wanaitwa Bahiimatul An’aam ambao ni; mbuzi, kondoo, ng’ombe na ngamia. Kwa mantiki hii haifai kumchinja farasi kwa ajili hii, wala swala hata kama anafugwa na amekuwa kama mbuzi kitabia na pia haifai kuchinja kuku wala bata kwa ajili ya ibada hii

 

  • Ama kuhusiana na umri unaofaa wa kichinjwa ni miaka mitano kwa ngamia na miaka miwili kwa ng’ombe, dume la mbuzi na dume la kondoo ni mwaka mmoja na mbuzi jike na kondoo jike ni miezi sita

 

  • Ni sharti katika kichinjwa cha Ghaqiqah kiwe kimesalimika na aibu mbalimbali kwa kifupi kabisa kichinjwa hichi kinafanana na kichinjwa cha Iddil adh’haa au iddi kubwa yaani kisiwe na chongo cha wazi, kiguru cha wazi, kilichokonda sana, wala kisiwe ambacho kimetobolewa masikio yake wala kisiwe, wala kilichokatwa mkia au kukatika pembe.

 

  • Ikiwa mtu anamiliki takribani wanyama wote wanaofaa kuchinja kwa ajili ya Ghaqiqa kiasi kuwa anaweza akitaka akachinja ng’ombe au ngamia au kondoo au mbuzi, iliyo bora zaidi ni kuchinja mbuzi maana ndiyo aliyetajwa katika hadithi.

 

  • Inafaa mtu kuipika nyama ya Ghaqiqah au kuigawa pasina kuipika lakini iliyo bora zaidi ni kuipika nyama ya Ghaqiqah kuliko kuigawa kwa kuwa kwa kufanya hivyo utawarahisishia masikini na majirani gharama za kupika.

 

  • Hakuna ubaya wowote katika kula nyama ya Ghaqiqa kwa aliyechinja, kwani kwa hakika hii ni nyama kwa ajili ya kumshukuru Allah na kile ambacho ni kwa ajili ya kumshukuru Allah kinafaa kuliwa kisheria wala hapana ubaya bali hii ni kama nyama ya iddil adh’haa.

 

  • Pia inafaa kuiweka nyama ya Ghaqiqah katika jokofu pasina kuigawa lakini iliyo bora zaidi na timilifu katika ibada hii ni kuigawa kwa mafaqiri na marafiki hata kama ni kidogo.

 

  • Haifai kununua mbuzi aliyechinjwa na kumfanya kuwa ni Ghaqiqah bali ni lazima kumununua mbuzi mzima na kisha kumchinja kwa nia ya Ghaqiqah

 

  • Ikiwa baba hayuko, kama kwa mfano kafariki, mama atasimamia jukumu la kufanya Ghaqiqah

 

  • Ghaqiqa ni Sunna kwa baba kumfanyia mtoto wake lakini mtoto hakufanyiwa Ghaqiqa na akapenda ajifanyie mwenyewe inafaa hata kama ni ni kitambo kirefu kimepita na umri ukawa mkubwa.

 

  • Inafaa kumchinjia mtoto wa kiume mbuzi hao wawili kwa utaratibu wa kugawa kwa maana ya kuwa anamchinja mbuzi mmoja mwezi huu na mwingine akamchinja mwezi mwingine wala haishurutishwi wachinjwe mara moja, bali inafaa kwa mtoto akajichinjia mbuzi mwingine ikiwa baba alimchinjia mbuzi mmoja kwa sababu ya hali yake kifedha. Bali inafaa kumchinjia mbuzi mmoja sehemu moja na mwingine sehemu nyingine wala si sharti wachinjwe wote sehemu moja wala si sharti wachinjwe sehemu alipo mtoto anayefanyiwa.

 

  • Haifai kisheria kupigia thamani ya mbuzi wa Ghaqiqa na kuwapa kiwango hicho masikini bali ni lazima achinjwe mbuzi

 

  • Haifai kushirikiana watoto katika Ghaqiqah kwa mantiki ya kuwa wachangie kwa mfano mbuzi wawili watoto wawili wa kiume. Watoto wawili wa kiume wanapaswa wachinjiwe mbuzi wane hata kama ni mapacha. Kama ni mapacha wawili wa kike watachinjiwa mbuzi wawili, kama mmoja ni wa kike na mwingine ni wa kiume watachinjiwa mbuzi watatu. Bali ngamia na ukubwa wake hafai kuwachinjia watoto wawili na ikifanyika hivyo inazingatiwa ni kwa ajili ya mtoto mmoja. Bali haitofaa kwa watoto wawili ambao hawakufanyiwa Ghaqiqa kwa wao kujiamulia kuchinja ngamia mmoja ili awe ni Ghaqiqa kwa wote wawili. Bali ngamia huyo atazingatiwa kuwa ni kwa ajili ya mtoto mmoja tu.

 

  • Si lazima wakati wa kumchinja mnyama wa Ghaqiqa kusema kuwa hii ni Ghaqiqa bali inatosha mtu kunuwia moyoni mwake na kilicho lazima kutamka ni Bismillah Rahmaan Raheem

 

  • Si lazima kuwaambia waliohudhuria kuwa watakula nyama ya Ghaqiqa, lakini ni vizuri kuwaambia ili wamuombee mtoto dua njema, uongofu, uchaji, kutengenekewa na kheri za dunia na akhera.

 

Ghaqiqah ni mnyama ambaye huchinjwa kwa ajili ya mtoto mdogo kama tulivyotangulia kusema. Jambo hili ni katika mlango wa kumshukuru Allah. Kuna pia vyakula vingine ambavyo ni katika mlango huu wa kumshukuru Allah na vinafaa kuliwa kisheria navyo ni;

1.      Walima chakula au karamu ya harusi

2.      Qiraa chakula cha mgeni, kile cha mgeni njoo wenyeji tupone!

3.      Maadaba ambacho ni chakula cha mwaliko

4.      Tuhfa ambacho ni chakula cha mwenye kutembelea pahala

5.      Khiraasu ambacho ni chakula cha kujifungua

6.      Ghadiira ambacho ni chakula cha wakati wa khitaani au kutahiri wanawake au wanaume

7.      Naqiigha ambacho ni chakula cha anayekuja kutoka safari

8.      Wakiira ambacho ni chakula baada ya kumaliza kujenga

Isipokuwa chakula cha msibani au cha siku ya tatu au cha khitima au arobaini vyakula nilivyotaja hapo juu vinafaa kuliwa Kisheria. Jariri Ibn Abdillah anasema kuwa kukusanyika kwa wafiwa na kupikiwa chakula ni miongoni mwa mambo aliyokataza Mtume wetu Mtukufu.

 

Wabillah Tawfiiq

 

 

Imeandikwa na ndugu yako katika uislamu;

 

Tawaqal Juma Hussein

Chuo Kikuu cha Waislamu

P.O Box 1031

Morogoro

Tanzania

 

 


Sent: Tuesday, March 24, 2009 1:40:06 PM
Subject: [The Fundametals:113] Re: New Arrival

DOC MOH

unread,
Mar 25, 2009, 2:14:02 AM3/25/09
to the-fund...@googlegroups.com
Sh Tawaqal
 
Allah Akubarik kwa ukumbusho huu ambao naamini sote tumefaidika.
 
Ila sijui kama ni sahihi kuiandika Ghaqiqa au huandikwa Aqiqa (Akika). Naomba nisaidieni.
 
Jengine: Imeandikwa kuwa:
  • Anakuwa kama mwenye kujisikia uzito na unyonge na mwenye kukosa wepesi na furaha maishani hadi achinjiwe
  • Anazuiwa kuwaombea wazazi wake uombezi mwema wa siku ya Qiyama
  • Ni deni lililo mithili ya Rehani ambayo hulazimiana na mtu hadi ailipe.
    Nukta ya pili inanipa mashaka usahihi wake: iweje kuwa ni sunna halafu azuiwe kuombea wazazi wake na Allah kupitia Kuran anamuamrisha mtoto afanye hivyo, duniani na akhera?
     
    Kadhalika, iweje kuwa anatakiwa afanyiwe na mzazi wake (si afanye wenyewe) halafu aadhibiwe kwa kuzuiwa (kwa kosa ambalo si lake). Tukumbuke  tumeambiwa kuwa wala hatobebeshwa mtu mzigo ambao si wake?
     
    Nukta ya tatu, naelewa kuwa baadhi ya Sunnah zimekokotozwa hadi kukaribia kuwa wajibu. Ila hapa uchache wangu wa elimu unanipa mashaka kwenye kitu kiwe ni sunna halafu kiwe ni "deni lililo mithili ya Rehani ambayo hulazimiana na mtu hadi ailipe".
     
    Narudia shukran kwa jitihada mnayopitisha katika kutuelimisha na kukumbushana. Allah Akubarikini.
     
    Ahsanteni,
    Mohammed.
     
    2009/3/24 Tawaqal Juma <tawaq...@yahoo.com>

    Masoud Mahundi

    unread,
    Mar 25, 2009, 6:07:53 AM3/25/09
    to the-fund...@googlegroups.com
    Waaleykumus-salam sheykh Ali Jabir
    Nina imani siku moja tutakutana uso kwa uso, inshaAllah soon,  lau kwa wale walio Dar na maeneo karibu na Dar.
    Labda nikuarrifu tu kwamba tunao watu ambao kwa sasa wako Tanzania, Kenya, UK, US, na wengine ambao ni mobile sana. Na wengine ndio tunalinda stations zetu
    Naomba nikutakie kila la kheri huko Adis, urudi salama
    Kila la kheri

     
    Masoud H. Mahundi
    Department of Computer Science
    University of Dar es Salaam
    P.O Box 35062
    Tel 255 22 410500 - 8 (or through ext 2466)
    Mobile: +255 71 5258337 / +255 78 7258337
    DUP Building - First Floor, Room No 206

    Sent: Tuesday, March 24, 2009 1:40:06 PM
    Subject: [The Fundametals:113] Re: New Arrival

    maryam

    unread,
    Mar 25, 2009, 9:22:51 AM3/25/09
    to the-fund...@googlegroups.com
    A'ALAYKUM WARAHMATULLAH WABARAKAATUH

    Nashkuru sana, asante tutakaribia ktk uwanja

    ZEYANA HAMID

    unread,
    Mar 25, 2009, 6:16:55 PM3/25/09
    to the-fund...@googlegroups.com
    Alhamdulillah Rabbi l Alamyn
    Assalam alaykum wanafundamentals, na kaka yangu Tawaqal ibn Jumaa
    mara zote hufurahi na hujivunia juu ya Elimu uliyojaaliwa nayo mashaallah, na darsa unayotoa na haswa imenijengea mazoea kua hata nikisoma huhisi bado nipo nyabo- ssebo land chini ya miti Mungu akuweke na akupe nguvu afya na akusahilishie matakwa yako. Nashukuru kwa zawadi adhiim

    Ama baada ya shukurani ni kuwa nasubiri tu majibu juu ya maswala ya Dr Mohammed kusema ukweli na mimi nipo katika mtazamo huohuo alionao yeye including the way we name the ceremony- Akika.

    Ila ndo tumo ndani ya kujifunza na waalim ndi nyinyi
    tafadhal!


     
    Zeyana Abdallah Hamid
    Msc Health Informatics-Candidate
    University of Missouri-Columbia MO
    +17853933875



    From: DOC MOH <docmo...@gmail.com>
    To: the-fund...@googlegroups.com
    Sent: Wednesday, March 25, 2009 1:14:02 AM
    Subject: [The Fundametals:115] Re: Ghaqiqa ya New Arrival

    Tawaqal Juma

    unread,
    Mar 26, 2009, 2:39:38 AM3/26/09
    to the-fund...@googlegroups.com
    Waalaykum ssalaam Warahamatullah,
     
    Amiina kwa dua uliyoniombea ndugu yang Muhammad nami nasema Allah atubariki sote  kwa ukumbushana kwetu.
     
    Ama kuhusiana na usahihi wa kuandika Ghaqiqa /Aqiqa (Akika). Nadhani ni tatizo lilijtokeza kutokana na kubadilisha herufi za kiarabu kwenda katika lugha ya kiswahili. Hapa ni vizuri tuwe tunasaidaiana lengo likiwa ni kuboresha mambo na kuyafanya yaeleweke vizuri zaidi. Labda tuliandike neno hilo kama 'AQIQAH. Naomba tusaidiane maana inaniwia vigumu sana mara nyingine kuandika kwa usahihi wake maneno ya kiarabu kwenda katika lugha yetu ya Kiswahili.
     
    Ama kilichoandikwa kuwa:
    • Anakuwa kama mwenye kujisikia uzito na unyonge na mwenye kukosa wepesi na furaha maishani hadi achinjiwe
    • Anazuiwa kuwaombea wazazi wake uombezi mwema wa siku ya Qiyama
    • Ni deni lililo mithili ya Rehani ambayo hulazimiana na mtu hadi ailipe.
    Nukta ya pili inanipa mashaka usahihi wake: iweje kuwa ni sunna halafu azuiwe kuombea wazazi wake na Allah kupitia Kuran anamuamrisha mtoto afanye hivyo, duniani na akhera?
     
    Kadhalika, iweje kuwa anatakiwa afanyiwe na mzazi wake (si afanye wenyewe) halafu aadhibiwe kwa kuzuiwa (kwa kosa ambalo si lake). Tukumbuke  tumeambiwa kuwa wala hatobebeshwa mtu mzigo ambao si wake?
     
    Nukta ya tatu, naelewa kuwa baadhi ya Sunnah zimekokotozwa hadi kukaribia kuwa wajibu. Ila hapa uchache wangu wa elimu unanipa mashaka kwenye kitu kiwe ni sunna halafu kiwe ni "deni lililo mithili ya Rehani ambayo hulazimiana na mtu hadi ailipe".
     
    Kwa kifupi ninachoweza kusema katika nukta zote hizi ni kuwa ile hadithi: "kila mtoto azaliwaye hufungamana na 'Aqiqah yake, anachinjiwa siku ya saba, ananyolewa kichwa chake na anaitwa jina". Wanachuoni wa kiislamu kama akina Ibn Qaymul Jawziya ambaye ameandika kitabu kizima kikizungumzia 'Aqiqah walipokuwa wanaelezea makusudio ya neno "hufungamana" lililokuja katika hadithi hiyo ambayo ni sahihi walisema kuwa  linaweza kuwa linamaanisha mambo mengi, miongoni mwa mambo hayo ni hayo waliyotaja hapo juu; ila nilichosahau mimi kusema ni kuwa baada ya wao kuleta kauli hizo mwisho walisema Allahu a'alamu kwa maana ya kuwa Allah ndiyo Mjuzi zaidi.
    Nakushukuru kwa mara nyingine kwa Tanbihi hii nzuri. Allah Akubariki.
     
    Ahsanteni,
    Tawakkal.

    Sent: Wednesday, March 25, 2009 9:14:02 AM

    Subject: [The Fundametals:115] Re: Ghaqiqa ya New Arrival

    ali jabir

    unread,
    Mar 26, 2009, 4:01:12 AM3/26/09
    to the-fund...@googlegroups.com
    Asante sana Sheikh wangu
     
    Inshallah tutaonana

    Tatu Mikidadi

    unread,
    Mar 26, 2009, 10:18:05 PM3/26/09
    to the-fund...@googlegroups.com

    Salaam alaykum ndugu zangu katika emaan,
     
    Kwanza, napenda toa pongezi kwa ukhty Zeyana. Inshaallah Allah awabarik na amjaalie Abdallah awe kijana mtiifu, mwenye afya njema na Mungu ampe muongozo katika maisha yake.
     
    Kwa hakika, najifunza mengi kuhusu dini yetu kwenye jukwaa hili. Kaka Mahundi, Tawakkal na wachangiaji walopita, Jazakallahu khair.
     
    Aidha, naomba nami kuuliza kuhusu mada iliyo mezani. Niliwahi sikia kuwa nywele za mtoto mchanga anazonyolewa siku ya 'Aqiqah' shurti zipimwe uzito kwa sonara. Uzito huo huchukuliwa ili kulinganisha thamani ya dhahabu yenye uzito huo kwa wakati ule, kisha pesa hizo hutolewa sadaqa. Je, hii  ni sahihi? Naomba kuelimishwa.
     
    Maa'salaam,  
     
    Tatu Juma Mikidadi,
     
    MCom (Information Systems) - Candidate
    Curtin - University of Technology,
    Flat 4, Rotary House.
    Kurrajong Village,
    Kyle Avenue,
    BENTLEY 6102,
    PERTH,
    Western Australia.
     
    cell number: +61413631257
    landline: +618 9266 9504


     
     




     

    Date: Wed, 25 Mar 2009 23:39:38 -0700
    From: tawaq...@yahoo.com
    Subject: [The Fundametals:119] Re: Ghaqiqa ya New Arrival
    To: the-fund...@googlegroups.com

    yussuph mahundi

    unread,
    Mar 27, 2009, 2:35:45 AM3/27/09
    to the-fund...@googlegroups.com
    Congratulation Zeyana, I hope he will make you a good son, INSHA ALLAH!
     
    Yussufu Mahundi

    ZEYANA HAMID

    unread,
    Mar 28, 2009, 7:42:09 PM3/28/09
    to the-fund...@googlegroups.com
    Ameen yaa Rabbi, ahsanteni nyote dua ziwe makbul kwa sote ameen

     
    Zeyana Abdallah Hamid
    Msc Health Informatics-Candidate
    University of Missouri-Columbia MO
    +17853933875



    From: yussuph mahundi <myma...@yahoo.com>
    To: the-fund...@googlegroups.com
    Sent: Friday, March 27, 2009 1:35:45 AM
    Subject: [The Fundametals:122] Re: New Arrival

    Tawaqal Juma

    unread,
    Mar 29, 2009, 5:19:05 AM3/29/09
    to the-fund...@googlegroups.com
    Waalaykum Salaam,
    Ni kweli ulivyowahi sikia kuwa nywele za mtoto mchanga anazonyolewa siku ya 'Aqiqah' zinatakiwa zipimwe uzito kwa sonara. Uzito huo huchukuliwa ili kulinganisha thamani ya dhahabu yenye uzito huo kwa wakati ule, kisha pesa hizo hutolewa sadaqa. Hii  ni sahihi na haina mshikeli wowote. Haya pia yanategemea uwezo wa mfanyaji wa 'Aqiqah. Kwa mwenye uwezo ni vizuri zaidi kufanya hivyo maana hilo limethibiti kisheria.
     
    Wabillah Tawfiiq
    Tawakkal
     



    From: Tatu Mikidadi <bibi...@hotmail.com>
    To: the-fund...@googlegroups.com
    Sent: Friday, March 27, 2009 5:18:05 AM
    Subject: [The Fundametals:121] Re: Ghaqiqa ya New Arrival

    Tatu Mikidadi

    unread,
    Mar 29, 2009, 9:23:50 AM3/29/09
    to The Fundamentals
     
     
    Salaam alaykum,
     
    Nashkuru kwa maelezo.
     
    Regards,

     
    Tatu Juma Mikidadi,
     
    MCom (Information Systems) - Candidate
    Curtin - University of Technology,
    Flat 4, Rotary House.
    Kurrajong Village,
    Kyle Avenue,
    BENTLEY 6102,
    PERTH,
    Western Australia.
     
    cell number: +61413631257
    landline: +618 9266 9504


     
     




     

    Date: Sun, 29 Mar 2009 02:19:05 -0700
    From: tawaq...@yahoo.com
    Subject: [The Fundametals:125] Re: Ghaqiqa ya New Arrival

    ali jabir

    unread,
    Mar 31, 2009, 2:15:17 AM3/31/09
    to the-fund...@googlegroups.com, tatma celtel, nassor masoud, aisha hashim, arbit...@yahoo.co.uk, aswegen...@yahoo.com, JIANG ALIPO, bras...@hotmail.com, George Bakilana, zubeda chande, Mwesiga Baregu
    Assalaam Alaykum
     
    Jamani kijana wetu amepotea tangu Ijumaa tarehe 27 Machi 2009.
     
     
    Jina lake Khamis Haji Khamis,
    Alitoweka Ijumaa saa nne na nusu eneo la Maji Matitu, Mbagala.
    Alionekana Ijumaa hiyo maeneo ya Nzasa, Charambe. Alikuwa anaongea maneno yasiyoeleweka hivyo hakujieleza. Anaonekana kurukwa na akili. Katika hali ya kawaida anaweza kujieleza.
     
    Alivaa t-shirt ya light blue, bila shaka kama bado anayo imechafuka sana. Suruali ya kijivu, ameikaba sana tumboni, anasumbuliwa na vidonda vya tumbo. Mara nyingi anatapika na kujisongasonga. Mwembamba sana, rangi yake maji ya kunde, nywele nyeusi, umri miaka 13 hivi.
     
    Tunaomba msaada katika kufikisha taarifa hizi kwa watu wengine. Yeyote atakaepata taarifa zake tunaomba awasiliane nasi kwa simu zifuatazo:
     
    1. 0773 308863
    2. 0777 874484
    3. 0732 992616
    4. 0777 996929
    5. 0773 500238
    6. 0784 874485
    7. 0773 848014
     
    Tunatanguliza shukurani
     
    Ali Jabir Mwadini
    --- On Sun, 29/3/09, Tawaqal Juma <tawaq...@yahoo.com> wrote:

    أبو عبدالله

    unread,
    Apr 7, 2009, 6:59:47 PM4/7/09
    to the-fund...@googlegroups.com, tawaq...@yahoo.com
    Assalaamu 'Alaykum wa RahmatuLlaah wa Barakaatuh,
     
    Al-Akh Tawakkal na wana ukumbi,
     
    Nimeipitia makala yako nzuri ya 'Aqiyqah na kama nilivyokujulisha kuwa nitairekebisha; na nimefanya hivyo na kurekebisha tahajia na kuondosha yenye utata na kuacha kazi nzuri iliyomakinika na kuiweka kwenye tovuti yenu ya www.alhidaaya.com ambapo itakuwa ukurasa wa mbele Ijumaa inshaAllaah.
     
    Kama kuna jambo lolote utakaloliona kwenye makala hapo chini linahitaji tanbihi, usisite kunijulisha.
     
    Nimeituma kwenye ukumbi waweze kufaidika nayo na kuwatumia wengine baada ya hayo marekebisho.
     
    Nduguyo,
    Abu 'Abdillaah
     
    N.B. Bullets na Numbers zinaweza zisitokeze hapa kwenye Hotmail.
     

    www.alhidaaya.com

     

    ‘Aqiyqah Afanyiwayo Mtoto Mchanga

     

    Tawakkal Juma Husayn

     

    1.    ‘Aqiyqah ni jina lililopewa kichinjwa (mnyama) achinjiwacho mtoto mchanga aliyezaliwa ni mamoja awe ni wa kike au wakiume.

    2.    Ni Sunnah si waajibu. Ushahidi wa hili ni uko katika maneno ya Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) aliposema: "Atakayepata mtoto na akapenda amchinjie basi na afanye hivyo; kwa mwanamume mbuzi wawili na kwa mwanamke mbuzi mmoja". Hadiyth hii imepokewa na Maimaam Abuu Daawuud na An-Nasaaiy kutoka kwa ‘Abdullaah bin ‘Umar (Radhiya Allaahu ‘anhu). Kauli ya Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam): “na akapenda amchinjie” ni dalili kuwa ‘Aqiyqah si lazima bali ni jambo linalopendeza Muislamu kulifanya. Lakini kwa mwenye uwezo wa kufanya hivyo basi iliyo bora zaidi kwake ni kufanya ama yule asiye na uwezo wa kufanya hivyo, basi si lazima kwake  maana Mwenyeezi Mungu Haikalifishi nafsi yoyote ila yale yaliyo sawa na uwezo wake na pia Hakufanya uzito katika dini.

     

    3.    Imethibiti kutoka kwa Mtume wa Allah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kuwa yeye kasema: “Kila mtoto azaliwaye anafungamana na ‘Aqiyqah yake, anachinjiwa siku ya saba, ananyolewa kichwa chake na anapewa jina.” Wanachuoni wamelizungumzia neno ‘kufungamana’ hapa kuwa linaweza kuwa linamaanisha mambo mengi, miongoni mwa mambo hayo ni:

      1. Anakuwa kama mwenye kujisikia uzito na unyonge na mwenye kukosa wepesi na furaha maishani hadi achinjiwe
      1. Ni deni lililo mithili ya Rehani ambayo hulazimiana na mtu hadi alilipe.

       

      4.    Iliyo bora zaidi na timilifu ni kuwa wale mbuzi wawili au kondoo wawili ambao anatakiwa mtoto wa kiume achinjiwe wanatakiwa wawe ni wenye kufanana au kukaribiana kufanana kimaumbile na kiumri. Lakini kama itashindikana kuwapata mbuzi wawili wenye sifa kama hizo itafaa hata kama watatofautiana kiumbile na kiumri maadamu tu wana sifa zinazofaa kisheria kwa ajili ya ibada hii. Sifa hizo tutazitaja baadaye.

       

      5.    Iliyo bora zaidi na timilifu ni kumchinjia mtoto wa kiume mbuzi wawili lakini ikiwa mtu atashindwa kabisa kuchinja mbuzi kama kutokana na yeye kupata mbuzi mmoja tu au kumiliki kiwango cha mbuzi mmoja tu basi huyo huyo mbuzi mmoja atatosha.

       

      6.    Sunnah ni kumchinjia mtoto atakapofikisha siku ya saba kama ilivyokuja katika Hadiyth ya Samrah, lakini ikiwa mtu hakuweza kuchinja siku ya saba basi na afanye hivyo siku yoyote atakayojaaliwa.

       

      7.    Ibada hii ya kuchinja hufanyika hata kama mtoto kafariki maadamu tu alizaliwa hai au hata kama mimba ilitoka lakini mtoto tayari alikuwa ameviviwa roho, yaani alikuwa amefikisha miezi minne au siku mia na ishirini na kuendelea lakini kama alikuwa hajafikisha miezi minne au siku mia na ishirini hapo hatofanyiwa ‘Aqiyqah.

       

      8.    Kuna imani imeenea kwa watu wengi kuwa kichinjwa cha ‘Aqiyqah hakivunjwi mifupa hii ikiwa kama ishara ya kumtakia mtoto salama na asivunjike maishani mwake. Hili si sahihi wala halina mashiko katika Qur-aan wala Sunnah. Kwa hiyo ieleweke wazi kuwa mifupa ya ‘Aqiyqah inafaa kuvunjwa wala hii haitokuwa sababu ya kuvunjika kwa mtoto hata kama itatokea kama watu wanavyoamini. Vile vile kuna jambo jingine nalo ni kuwa nyama ya ‘Aqiyqah huchanganywa au hupikwa kwa maji yaliyotiwa vitu vitamu vitamu kama sukari au huchanganywa na asali wakati wa kuliwa, hii ikiwa ni kama ishara ya kumtakia mtoto tabia njema; hili nalo pia halina mashiko. Hivyo iwekwe chumvi na kupikwa kama nyama ya kawaida

       

      9.    Kinachotakiwa kuchinjwa katika ‘Aqiyqah katika wanyama ambao kishari’ah wanaitwa Bahiymatul An’aam ambao ni; mbuzi, kondoo, ng’ombe na ngamia. Kwa mantiki hii haifai kumchinja farasi kwa ajili hii, wala swala hata kama anafugwa na amekuwa kama mbuzi kitabia na pia haifai kuchinja kuku wala bata kwa ajili ya ibada hii

       

      10.                       Ama kuhusiana na umri unaofaa wa kichinjwa ni miaka mitano kwa ngamia na miaka miwili kwa ng’ombe, dume la mbuzi na dume la kondoo ni mwaka mmoja na mbuzi jike na kondoo jike ni miezi sita

       

      11.                       Ni sharti katika kichinjwa cha ‘Aqiyqah kiwe kimesalimika na aibu mbalimbali kwa kifupi kabisa kichinjwa hichi kinafanana na kichinjwa cha ‘Iydul Adhwhaa au Idi kubwa yaani kisiwe na chongo cha wazi, kiguru cha wazi, kilichokonda sana, wala kisiwe ambacho kimetobolewa masikio yake wala kisiwe kilichokatwa mkia au kukatika pembe.

       

      12.                       Ikiwa mtu anamiliki takribani wanyama wote wanaofaa kuchinja kwa ajili ya ‘Aqiyqah kiasi kuwa anaweza akitaka akachinja ng’ombe au ngamia au kondoo au mbuzi, iliyo bora zaidi ni kuchinja mbuzi maana ndiye aliyetajwa katika Hadiyth.

       

      13.                        Inafaa mtu kuipika nyama ya ‘Aqiyqah au kuigawa pasina kuipika lakini iliyo bora zaidi ni kuipika nyama ya ‘Aqiyqah kuliko kuigawa kwa kuwa kwa kufanya hivyo utawarahisishia masikini na majirani gharama za kupika.

       

      14.                       Hakuna ubaya wowote katika kula nyama ya ‘Aqiyqah kwa aliyechinja, kwani kwa hakika hii ni nyama kwa ajili ya kumshukuru Allaah na kile ambacho ni kwa ajili ya kumshukuru Allaah kinafaa kuliwa kishari’ah wala hapana ubaya bali hii ni kama nyama ya ‘Iydul Adhwhaa.

       

      15.                       Pia inafaa kuiweka nyama ya ‘Aqiyqah katika jokofu pasina kuigawa lakini iliyo bora zaidi na timilifu katika ibada hii ni kuigawa kwa mafaqiri na marafiki hata kama ni kidogo.

       

      16.                       Haifai kununua mbuzi aliyechinjwa na kumfanya kuwa ni ‘Aqiyqah bali ni lazima kumununua mbuzi mzima na kisha kumchinja kwa nia ya ‘Aqiyqah

       

      17.                       Ikiwa baba hayuko, kama kwa mfano kafariki, mama atasimamia jukumu la kufanya ‘Aqiyqah.

       

      18.                       ‘Aqiyqah ni Sunnah kwa baba kumfanyia mtoto wake lakini mtoto hakufanyiwa ‘Aqiyqah na akapenda ajifanyie mwenyewe inafaa hata kama ni ni kitambo kirefu kimepita na umri ukawa mkubwa.

       

      19.                       Inafaa kumchinjia mtoto wa kiume mbuzi hao wawili kwa utaratibu wa kugawa kwa maana ya kuwa anamchinja mbuzi mmoja mwezi huu na mwengine akamchinja mwezi mwingine wala haishurutishwi wachinjwe mara moja, bali inafaa kwa mtoto akajichinjia mbuzi mwingine ikiwa baba alimchinjia mbuzi mmoja kwa sababu ya hali yake kifedha. Bali inafaa kumchinjia mbuzi mmoja sehemu moja na mwengine sehemu nyingine wala si sharti wachinjwe wote sehemu moja wala si sharti wachinjwe sehemu alipo mtoto anayefanyiwa.

       

      20.                       Haifai kisheria kupigia thamani ya mbuzi wa ‘Aqiyqah na kuwapa kiwango hicho masikini bali ni lazima achinjwe mbuzi

       

      21.                       Haifai kushirikiana watoto katika ‘Aqiyqah kwa mantiki ya kuwa wachangie kwa mfano mbuzi wawili watoto wawili wa kiume. Watoto wawili wa kiume wanapaswa wachinjiwe mbuzi wanne hata kama ni mapacha. Kama ni mapacha wawili wa kike watachinjiwa mbuzi wawili, kama mmoja ni wa kike na mwengine ni wa kiume watachinjiwa mbuzi watatu. Bali ngamia na ukubwa wake hafai kuwachinjia watoto wawili na ikifanyika hivyo inazingatiwa ni kwa ajili ya mtoto mmoja. Bali haitofaa kwa watoto wawili ambao hawakufanyiwa ‘Aqiyqah kwa wao kujiamulia kuchinja ngamia mmoja ili awe ni ‘Aqiyqah kwa wote wawili. Bali ngamia huyo atazingatiwa kuwa ni kwa ajili ya mtoto mmoja tu.

       

      22.                       Si lazima wakati wa kumchinja mnyama wa ‘Aqiyqah kusema kuwa hii ni ‘Aqiyqah bali inatosha mtu kunuia moyoni mwake na kilicho lazima kutamka ni BismiLlaahir Rahmaanir Rahiym.

       

      23.                       Si lazima kuwaambia waliohudhuria kuwa watakula nyama ya ‘Aqiyqah, lakini ni vizuri kuwaambia ili wamuombee mtoto du’aa njema, uongofu, uchaji, kutengenekewa na kheri za dunia na Akhera.

       

      ‘Aqiyqah ni mnyama ambaye huchinjwa kwa ajili ya mtoto mdogo kama tulivyotangulia kusema. Jambo hili ni katika mlango wa kumshukuru Allaah. Kuna pia vyakula vingine ambavyo ni katika mlango huu wa kumshukuru Allaah na vinafaa kuliwa kishari’ah navyo ni:

       

      a.     Waliymah: chakula au karamu ya harusi.

      b.     Qiraa: chakula cha mgeni, kile cha mgeni njoo wenyeji tupone!

      c.      Ma-adabah: ambacho ni chakula cha mwaliko.

      d.     Tuhfah: ambacho ni chakula cha mwenye kutembelea pahala.

      e.     Khiraasu: ambacho ni chakula cha kujifungua.

      f.       Ghadiyrah: ambacho ni chakula cha wakati wa khitaani au kutahiri wanawake au wanaume

      g.     Naqiy’ah: ambacho ni chakula cha anayekuja kutoka safari.

      h.     Wakiyrah: ambacho ni chakula baada ya kumaliza kujenga.

       

      Isipokuwa chakula cha msibani au cha siku ya tatu au cha Khitmah au arobaini. Vyakula nilivyotaja hapo juu vinafaa kuliwa Kishari’ah. Jariyr bin ‘Abdillaah anasema kuwa kukusanyika kwa wafiwa na kupikiwa chakula ni miongoni mwa mambo aliyokataza Mtume wetu Mtukufu.

       

      WabiLlaahit Tawfiyq

       

       

       

       

       

      Get the New Internet Explore 8 Optimised for MSN. Download Now

      Zaharani Kisilwa

      unread,
      Apr 8, 2009, 5:47:56 AM4/8/09
      to the-fund...@googlegroups.com

          ASSALAAM ALAYKUM.   

       

           Kaka Tawakkal, naomba nianze kwa kukushukuru kwa kuutumia muda wako mwingi kutufahamisha mambo mbalimbali katika dini yetu tukufu. nakiri wazi kwa wana undamentali wote ya kwamba pamoja na kwamba sula hili lizungumziwalo hapa linaonekana la kawaida masikioni mwangu na mwa wengi, sikuwa nalifahamu kiundani hivi kabla ya kunijuza haya. waalimu wangu masheikh doctor ijumaa na mahundi hawakunifunza haya kabla, ikiwa kama adhabu kwa kuwa sikutokea darasani siku hiyo ya somo hili. hivyo hapa nafaidika sana.

       

           Baada ya utangulizi huu naomba unisaidie kidogo juu ya kifungu namba saba cha somo lako kama kinavyoonekana na kusomeka hapa chini katika maandishi ya rangi nyekundu

       

           “7.    Ibadan hii ya kuchinja hufanyika hata kama mtoto kafariki maadamu tu alizaliwa hai au hata kama mimba ilitoka lakini mtoto tayari alikuwa ameviviwa roho, yaani alikuwa amefikisha miezi minne au siku mia na ishirini na kuendelea lakini kama alikuwa hajafikisha miezi minne au siku mia na ishirini hapo hatofanyiwa ‘Aqiyqah’”

       

            SEHEMU  NIIITAKIAYO MAELEZO NI JUU YA KUTAMBUA NI MBUZI WANGAPI WA KUCHINJIWA MTOTO AMBAYE BADO NI MIMBA MAANA UTAMBUZI WA PENGINE NI WA JINSIA YA KIKE AU YA KIUME UNAKUWA MGUMU. AU KUNA IDADI MAALUMU YA VIUMBE MIMBA HIVI AMBAVYO NI TOFAUTI NA IDADI INAYOTAMBULIKA KWA WATOTO WALIOZALIWA HAI?

       

           TAFADHALI NISAIDIE JUU YA HILI ILI KIU YANGU YA KUKAMILISHA UELEWA SAHIHI USO SHAKA JUU YA SOMO HILI UKAMILIKE UKINIACHA NIKIWA NA FURAHA JUU YA NILICHOJIFUNZA. NATANGULIZA SHUKRANI ZANGU KWA MARA NYINGINE.

       

       

      KISILWA, ZAHARANI

      INSTITUTE OF ACCOUNTANCY ARUSHA

      NJIRO HILL, ARUSHA

      MOBILE: +255 715 000 635

       

       


      Reply all
      Reply to author
      Forward
      0 new messages