Wapendwa Wana-Azaki
Napenda kuchukua nafasi hii kuwajulisha kwamba Muungano wa Asasi za Kiraia wa TAFII (Tanzania Alliance For Immunisation Initiatives) unapenda kuzikaribisha Asasi za Kiraia ambazo zingependa kujiunga na Muungano huu.
Mungano huu wa Asasi za Kiraia (TAFII) Ni muungano (Network) wa Asasi zinazojishugulisha au kujihusisha na Miradi inayolenga katika Ustawi wa Afya ya Mtoto na Mama hasa katika kusisitiza upatikanaji wa Afya Kinga katika makundi haya ya kijamii hapa Tanzania, Hususani upatikanaji wa Chanjo na dawa za kinga kwa magonjwa mbalimbali yanayoweza kuzuilika kwa kinga badala ya kusubiri tiba. Muungano huu kwa sasa una wanachama (Asasi) 28.
Mwaka huu 2014 Muungano huu umejiunga na Muungano wa Asasi za Kimataifa wa Uhamisishaji katika upatikanji wa Chanjo na huduma ya Chanjo wa GAVI CSO-Global Alliance for Vaccine Initiatives – Civil Society Constituency ) Unaohamasisha upatikinaji wa Chanjo hasa kwa nchi zinazoendelea na kufanya utetezi wa kupunguza vifo vya watoto vinavyotokana na magonjwa yanaoweza kuzuilika.
Ili kuweza kufanikisha utetezi wa haki ya Afya kwa mtoto na upatikanaji wa Chanjo kwa watoto wote. Tunakukaribisha kujiunga na Umoja huu.
Kama utapenda kujiunga na umoja huu basi tuma taarifa fupi za awali za za mawasiliano ya Asasi yako/ yeny ambazo ni
Taarifa zaidi za Kiutendaji na Vikao tarajiwa zitatumwa kwa Asasi ambazo zitatuma mawasiliano yao ya awali kwa kuonyesha nia ya kujiunga na TAFII.
Kwa taarifa zaidi juu ya GAVI (Unaweza kusoma pia katika - http://www.gavialliance.org/ na http://www.gavicso.org/
Ahsante
Alphonce Mgunde
Network Coordinator