Tambaza Hoi Matokeo ya Kidato cha Sita
*Shule za Kata zachomoza 10 bora
*RC Iringa atoboa siri ya ufaulu mzuri

WAKATI shule zisizo na majina makubwa zikifanya vizuri katika mtihani wa taifa wa kidato cha sita, sekondari kongwe ya Tambaza, jijini Dar es Salaam, inashika mkia.
Matokeo ya mtihani huo uliofanyika Mei, mwaka huu, yalitangazwa jana na Kaimu Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA), Dk. Charles Msonde.
Katika kundi la shule 10 za mwisho, Tambaza ni ya tatu, ikitanguliwa na Ben Bella ya Unguja na Fidel Castro (Pemba), ikifuatiwa na Muheza (Tanga), Mazizini (Unguja), Mtwara Technical (Mtwara), Iyunga Technical (Mbeya), Al-Falaah Muslim (Unguja), Kaliua (Tabora) na Osward Mang’ombe (Mara).
Tambaza ni miongoni mwa shule kongwe nchini zilizokuwa zikifanya vizuri katika mitihani, ambazo hivi sasa zinakabiliwa na changamoto kadhaa zikiwemo za uchakavu wa miundombinu, uhaba wa walimu na vifaa vya maabara.
Kundi la shule 10 bora linaongozwa na shule ya kata ya Igowole (Iringa), Feza Boy’s (Dar es Salaam), Kisimiri, ambayo ni ya kata (Arusha), Iwawa nayo ya kata (Njombe), Kibaha (Pwani), Marian Girls (Pwani), Nangwa (Manyara).
Zingine ni Uwata (Mbeya), inayomilikiwa na Katibu Mkuu Uamsho wa Wakristo Tanzania, Kibondo (Kigoma) nayo ya kata na Kawawa (Iringa), inayomilikiwa na Shirika la Uzalishaji Mali JKT (Suma-JKT).
Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dk. Christine Ishengoma, akizungumza kwa simu jana, alisema matokeo hayo yanatokana na ushirikiano mkubwa kati ya uongozi wa mkoa na wa shule hizo.
“Tunamshukuru Mungu kwa matokeo mazuri. Hata mwaka jana Igowole ilifanya vizuri katika matokeo ya mtihani wa kidato cha nne,” alisema.
Dk. Msonde akizungumzia ubora wa ufaulu kwa kuangalia madaraja waliyopata watahiniwa wa shule, watahiniwa 30,225 sawa na asilimia 85.73 wamefaulu kwa madaraja la kwanza hadi la tatu, kati yao wasichana ni 9,954 (asilimia 90.59) na wavulana ni 20, 271 (asilimia 83.53).
Kwa mujibu wa jedwali, wasichana wanaongoza katika daraja la kwanza na la pili, huku wavulana wakiongoza katika madaraja ya tatu, nne na sifuri (0).
Aliwataja watahiniwa 10 bora kwa masomo ya sayansi kitaifa kuwa, Isaack Shayo (St. Joseph Cathedral), Doris Noah (Marian Girls), Innocent Yusufu (Feza Boys), Placid Pius (Moshi), Benni Shayo (Ilboru), Abubakar Juma (Mzumbe), Mwaminimungu Christopher (Tabora Boys), Chigulu Japhaly (Mzumbe), Hussein Parpia (Al-Muntazir) na Ramadhani Msangi (Feza Boys).
Watahiniwa 10 bora kwa masomo ya Biashara kitaifa ni Jovina Leonidas (Ngaza), Nestory Makendi (Kibaha), Imma Anyandwile (Umbwe), Theresia Marwa (Loyola), Grace Chelele (Loyola), Betrida Rugila (Baobab), Jacqueline Kalinga (Weruweru), Tajiel Kitojo (Arusha), Shriya Ramaiya (Shaaban Robert) na Mwanaidi Mwanzema (Weruweru).
Kwa masomo ya Lugha na Sanaa kitaifa, watahiniwa 10 bora ni Lisa Mimbi (St. Mary Goreti), Rosalyn Tandau (Marian Girls), Joseph Ngobya (St. Joseph Cathedral), Aneth Mtenga (Marian Girls), Idda Lawenja (Marian Girls), Edna Mwankenja (Kisimiri), Catherine Kiiza (St. Mary’s Mazinde Juu), Nancy Swai (Mwika), Mohamed Salmin (Mwanza) na Idrisa Hamisi (Mwembetogwa).
Alisema NECTA imezuia kutoa matokeo ya watahiniwa 150 wa shule ambao hawajalipa ada ya mtihani hadi watakapolipa, pia watahiniwa tisa wa shule walipata matatizo ya kiafya na kushindwa kufanya mtihani kwa baadhi ya masomo, ambao wamepewa fursa ya kuyafanya mwakani.
Dk. Msonde alisema watahiniwa 29 walipata matatizo ya kiafya na kushindwa kufanya mtihani kwa masomo yote, ambao wamepewa fursa ya kufanya mitihani mwakani, huku wawili wamefutiwa matokeo baada ya kubainika kufanya udanganyifu.
Alisema watahimiwa 41,968 waliandikishwa kufanya mtihani, kati yao wasichana wakiwa 12, 674 (asilimia 30.20) na wavulana 29,294 (asilimia 69.80). Hata hivyo, waliofanya mtihani walikuwa 40,695 na waliofaulu ni 38,905.
Akizungumzia kuhusu matokeo ya ualimu, alisema watahiniwa waliojisajili kufanya mtihani wa daraja A walikuwa 10,827, kati yao wasichana ni 4,093 (asilimia 37.80) na wavulana 6,734 (asilimia 62.20).
Alisema asilimia 99.62 ya waliofanya mtihani huo wamefaulu, kati yao wasichana ni 4,049 (asilimia 99.66) na wavulana ni 6,646 (asilimia 99.60).
Kwa upande wa Stashahada ya Ualimu Sekondari, alisema waliofanya mtihani ni 4,931, kati yao wasichana ni 1,698 (asilimia 34.44) na wavulana 3,223 (asilimia (65.56).
Source: RAIA MWEMA http://raiatanzania.co.tz/index.php/habari/984-tambaza-hoi-kidato-cha-sita
Other SOURCES
MAJIRA: http://www.majira.co.tz/index.php?page=read_more&name=news&id=2452
MWANANCHI: http://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/Matokeo-kidato-cha-sita-yatia-fora/-/1597296/2386998/-/11hwq0oz/-/index.html
BLOG: http://jumamtanda.blogspot.com/2014/07/matokeo-kidato-cha-sita-yatia-fora.html
HABARI LEO: http://habarileo.co.tz/index.php/habari-za-kitaifa/27318-ufaulu-kidato-6-juu
DAILY NEWS: http://www.dailynews.co.tz/index.php/local-news/33789-better-form-six-results-released
Kuna nini tambaza?
--
Tambaza1996 Facebook Group: http://www.facebook.com/groups/tambaza1996/
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Tambaza High School (1994 to 1996)" group.
To post to this group, send email to tamba...@googlegroups.com.
Visit this group at http://groups.google.com/group/tambaza1996.
Kama kuna kitu kimenikosesha raha baada ya kusikia matokeo ya shule niliyopitia, kati ya shule zilizo fanya vibaya kwenye mtihani wa kidato cha sita ni hili. Hii selection ipoje siku hizi, wanapeleka vilaza au uongozi? Tatizo nini jamani, hii sio ile Tambaza ya kutembea kifua mbele….
Mahmoud Shungu
Branch Supervisor
Tanga Branch
C&TM Operations
Tanzania Cigarette Company Ltd
A member of the JTI Group of Companies
J6 H349 Euckenford Street
P.O.Box 683, Tanga
--
Yaani nimesikitika sana, inabidi tujue tatizo liko wapi ili at least we do something. Yaani shule yenye jina kubwa kama Tambaza inakuwa mkiani?
Headmaster na walimu wrote watimuliwe! No alibi kama ya brazil kufungwa 7 ! |
Shida ni walimu au wanafunzi ? Au shida ipo kwa wote kunahaja kama kweli tumeguswa tuangalia kwa undani nini tatizo na kama inawezekana kuwasaidia wasiidiwe angalau watoke kwenye shule 10 mbovu
Inabidi tupange twende pale shule ili kujua ukweli! Au mnaonaje? Hii ni fedhea kubwa, sasa hivi kusema umesoma tambaza ni aibu!bora kata! |
Joyce ni kweli naunga mkono hoja. .. hivi kina Oluoch, Kitai wako wapi!? Namkumbuka Merchant alikuwa anajituma mwanzoni bdae naye akabwaga manyanga. .. akaita tambaza JABA |
Acheni wehu nyie mnaojadili matokeo ya Tambaza, vijijini kwenu hakuna shule ambazo matokeo ni mabaya? what have u done?? acheni kujifanya mnaumizwa fanyeni ktk familia zenu na extended family if u real want to help.
Are you serious with your idiotic comment?
Kujadili Tambaza tumekuwa wehu?
Acha kuharibu hali ya hewa.
S0347/0503 | F | 10 | III | G/STUDIES - 'D' PHYSICS - 'B' CHEMISTRY - 'C' ADV/MATHS - 'B' |
It's a systematic problem. Kuan zia wizarani kuja chini, no one cares abt hizi public schools, and wadogo zetu are quite different na sie as well. They need help, support and motivation , kutegemea govt ambayo watoto wakifeli solution ni kuongeza grading scales is a joke. So,if we really care, we should start to think abt these results, seriously. Otherwise itafika wakati we wouldn't want to mention tumesoma Tambaza. I 2nd Gesona, personal effort I think haipo kabisa. What should we do?