Amani ya Bwana iwe daima nanyi enyi nyote,
Hapa SG kuna Neema/Karama/Vipaji/ Akili/ Huduma/Uzoefu/ Ufunuo na NENO KWELI KWELI toka kwa Bwana ndani ya Washirika wa Kanisa hili, nina hakika umekua unajifunza mengi na hata nawe kufundisha mengi na hata leo pia utadaka matamu sana na pia hata kufurahi na kuchekeshwa unapo fellowship sana hapa, raha kweli humu Watu tulio nao, vipaji vya ajabu kuchekesha wenzao-tehe!
Maswali ya kuchangia/Muongozo wa Speaker ni huu….
…..Je, mtu anaweza kutubu dhambi zake
kimya kimya au ni lazima aje hadharani kuzisema na kukiri kwa majuto? ?
…….Je, toba ipi yenye nguvu, ile ya kutaja na dhambi ulizofanya aidha ukiwa mwenyewe chumbani au hadharani unatubu au hata kusema tu '' umekuja kwa kua unataka kutengeneza na MUNGU'' anaona NIA yako, yatosha?
……. Je Ni lazima uende kwa Kiongozi wa kanisa ili kutubu dhambi? Au maliza mwenyewe kivyako-vyako kama Mwana wa Mungu sawa tu na Kiongozi yoyote maana wote tu Wana, hakuna aliye Mwana zaidi au kupendwa kiuspesheli?
..... Au ni ile ambayo ukishatubu, iwe kivyako chumbani au umeenda kwa Kiongozi wa Imani/Dini, uwe umetaja au la, bali muhimu ni utakavyoiishi baada ya Toba?
......Kama ni ivyo, basi inakuaje Toba kweli kweli unafanya kisha siku nyingine lazima kufanya/jitakasa tena na kila leo kujitakasa/kutubu kadri tuinapo SIKU ILEE yaja upesi maaan imeandikwa..'''Mtakatifu ana azidi kua Mtakatifu-simply means-kujitakasa.....
Karibuni mlete shule na kwa kweli hii mada ni sawa kweli kwamba yataka mawazo na michango huru kwa kadri ujuavyo uwe huru tu kushare, haina shaka lakini pia kwa jinsi ilivyo, hasa nondo za Neno na Ufafanuzi wake itasaidia sana kujua Ki-Biblia TOBA YA KWELI ni ipi haswa.
Press on,
Edwin Seleli
![]() |
|
"Mathayo 5: 23 Basi ukileta sadaka yako madhabahuni, na huku ukikumbuka ya kuwa ndugu yako ana neno juu yako, 24 iache sadaka yako mbele ya madhabahu, uende zako, upatane kwanza na ndugu yako, kisha urudi uitoe sadaka yako."
Hili ni Neno la Mungu.
Kupatana na kutengeneza ni pamoja na yule unaye neno juu yake. Ukiwa na neno juu ya Mchungaji utaenda kwake. Ukiwa na neno juu ya Mungu, unaongea naye . Ukiwa na neno juu ya kanisa lote unaongea na kanisa lote.
Ubarikiwe. Alphonse Ziragora ![]() -------Message original-------
|
-- Tafadhali zingatia msingi wetu ni Neno la Mungu, Lengo letu Kuujenga mwili wa Kristo, kushirikiana, amani na upendo. Yeyote yuko huru kuchangia, kufundisha, kukubali kufundishwa sawasawa na Msingi wetu Mkuu Neno la Mungu. Kujiunga na Team ya Injili au Maombi wasiliana nasi kwa simu 0714 915 424. Tuma Email. strictl...@yahoo.co.uk Facebook:https://www.facebook.com/pages/Strictly-Gospel/363180289370 Blog: www.strictlygospel.wordpress.com Kujiondoa Kwenye Kundi Hili Tuma Email: strictlygospe...@googlegroups.com |
![]() |