KUTOA ZAKA kila mwezi au kila upatapo kipato.

2,824 views
Skip to first unread message

Mary Damian

unread,
Jul 11, 2013, 7:44:01 AM7/11/13
to strictl...@googlegroups.com
Wana SG, mafundisho ya kutoa zaka kila upatapo kipato ni SAHIHI, sio mafundisho potofu hata kidogo. Naomba ninukuu maandiko ambayo tunayafahamu sote kisha nitayafafanua. "Yakobo akaweka nadhiri akisema, Mungu akiwa pamoja nami, akinilinda katika njia niiendeayo, na kunipa chakula nile, na nguo nivae; nami nikirudi kwa amani nyumbani kwa baba yangu, ndipo Bwana atakuwa Mungu wangu. Na jiwe hili nililolisimamisha kama nguzo litakuwa nyumba ya Mungu; na katika kila utakalonipa hakika nitakutolea wewe sehemu ya kumi". - Mwanzo 28:22. Hebu ongezea na andiko hili "Lakini, ole wenu, Mafarisayo, kwa kuwa mwatoa zaka za mnanaa na mchicha na kila mboga, na huku mwaacha mambo ya adili, na upendo wa Mungu; iliwapasa kuyafanya hayo ya kwanza, bila kuyaacha hayo ya pili". - LUKA 11:42 (SUV msisitizo added).

Utoaji wa Zaka/Fungu la kumi/Sehemu ya kumi ni jambo lilikuwepo hata kabla na baada ya sheria. Yakobo anasemakatika kila utakalonipa hakika .......... Bwana Yesu anawaambia mafarisayo wasiache kutoa zaka za mnanaa na mchicha na kila mboga. Swali ni kwamba ni wakati gani mboga mboga hizi zinapatikana? Je si wakati wa kuzivuna? Lakini jambo la kuzingatia ni kuwa kila atoae zaka yampasa kuleta ZAKA KAMILI ( Malaki 3:10). Logical thinking rahisi ni zipi, kuleta zaka kamili kwa mtu wa kawaida ambaye uwekaji wa kumbu kumbu sio kivile? Hivi Mungu huagiza wanawe na kisha kuweka ugumu wa kuyatekeleza. ukikaa na zka muda mrefu hakuna uwezekano wa kusahau, na ukisahau itakuwa umetoa zaka kamili? Kwa nini mambo yasiwe rahisi kwa kutoa kila unapopata? Hebu chukulia mfanyakazi akae na zaka kisha baada ya mwaka ndipo atoe, Je, ataweza kutoa mapato ya 120% (yaani 10% mara miezi 12)?

Ninajua tunakubaliana kuwa kutoa Zaka ni wajibu wa kila mwamini. Sasa frequency (mara ngapi kwa kipindi gani) isiwe issue. Huenda mpendwa Milinga unatatizwa na andiko lifuatalo; nanukuu "Usiache kutoa zaka ya fungu la kumi katika maongeo yote ya mbegu zako, yatokayo shamba mwaka baada ya mwaka".  - KUMB 14:22. Kama ndiyo andiko hili, basi naomba uangalie tafasiri zingine zinasema nini kuhusu maongeo. Hebu angalia ya KJV - neno maongeo limetafsiri ni "increase", yaani ongezeko. Hawa ndugu zetu walikuwa na aina mbali mbali za Zaka katika kitu kimoja. Wote tunajua kuwa zaka zinatolewa nyumbani mwa Bwana lakini hebu ona hii "Kila mwaka wa tatu, mwisho wake, toa fungu la kumi lote la maongeo yako ya mwaka huo, uliweke ndani ya malango yako;". - KUMB 14:28(SUV - msisitizo added). Agizo hapa ni kuiweka zaka ndani ya malango yako sio nyumbani mwa Bwana!!!

Pia kuhusu ile zaka ya kila mwaka inawezekana walikuwa wanavuna mara moja kwa mwaka. Ona tafasiri hii  “You shall tithe all the yield of your seed, which comes forth from the field year by year". - Deut 14: 22 - RSV. Hivyo mavuno ya shamba ni tofauti na mambo ya msharaha au faida katika biashara ambayo mpendwa anapata mapato kila mwezi, wiki n.k. Nimalizie kwa kusema, Zaka ya kila mwaka iliyoonyeshwa hapo juu, ilikuwa inatolewa nyumbani mwa Bwana lakini inaliwa na mtoaji pamoja na mlawi. Swali ni hili Je, Zaka unazotoa huwa unakula mwenyewe? Zaka ya kila baada ya miaka mitatu ilikuwa inatolewa na kuwekwa malangoni ili mlawi, mjane, watima na mgeni wakiiona waweze kuchangamkia (Soma mwenyewe KUMB 14:22-29 uthibitishe).
 
Ninaona kuwa nimejibu hoja hii na kuthibitisha kuwa kutoa zaka kila unapopata mapato ni mafundisho sahihi na inawezekana pia nimekuongezea na aina nyingine ya Zaka.

Keep on digging.
Mathew.
 

lev...@ymail.com

unread,
Jul 11, 2013, 11:53:30 AM7/11/13
to strictl...@googlegroups.com, strictl...@googlegroups.com
Kutoa dhaka kila mwezi ni fundisho sahihi kabisa, 

Sent from my iPhone
--
Tafadhali zingatia msingi wetu ni Neno la Mungu, Lengo letu Kuujenga mwili wa Kristo, kushirikiana, amani na upendo. Yeyote yuko huru kuchangia, kufundisha, kukubali kufundishwa sawasawa na Msingi wetu Mkuu Neno la Mungu. Kujiunga na Team ya Injili au Maombi wasiliana nasi kwa simu 0714 915 424. Tuma Email. strictl...@yahoo.co.uk Facebook:https://www.facebook.com/pages/Strictly-Gospel/363180289370
 
Blog: www.strictlygospel.wordpress.com
 
Kujiondoa Kwenye Kundi Hili Tuma Email:
strictlygospe...@googlegroups.com
 
 

Mathew Maduhu

unread,
Jul 15, 2013, 7:01:49 AM7/15/13
to strictl...@googlegroups.com
Shalom SG,
Napenda kufafanua baadhi ya mambo yahusuyo Zaka na kujibu maswali ya mpendwa Flano aliyoyauliza kwenye mada ya  Mafundisho potofu lakini yakilenga mambo yahusuyo Zaka.
 
Kabla ya kutoa mchango huo, naomba ninukuu baadhi ya maneno yaliyotolewa katika michango ya mada zilizopita. Tarehe 8-Mei-2013, wakati akidadavua mada iliyohusu UJUMBE KWA KILA MTU KWA WANA WA ISRAEL iliyotolewa na Dada yetu Doris, Mtumishi wa Mungu Kamera ya Bwana Yesu (Patrick) alisema "Njia mojawapo nzuri ya kujifunza kila kitu kwenye Neno la Mungu ni kwa kutumia ile Kanuni ya "Imetajwa wapi kwanza", yaani the Principle of First Mention". Sasa basi tuuangalie mwanzo wa taifa la israeli na favor ya Mungu juu yao ilikuwaje. ......... Agano la Ibrahimu lilikuwa ni Agano la neema ya Mungu, Mungu alijiapia mwenyewe na Ibrahimu na uzao wake walikuwa beneficiaries."
 
Mpendwa Flano umesema vema kuwa kutoa Zaka kulianza wakati wa Ibrahimu - umeenda kwenye kanuni ya imetajwa wapi kwanza. Isipokuwa siamini kama Yakobo ali-propose au kujitolea yeye mwenyewe kutoa zaka. Ninaamini kuwa alifundishwa kufanya hivyo na wazazi wake. Hebu tuangalie maandiko haya. "Kwa maana nimemjua ya kwamba atawaamuru wanawe, na nyumba yake baada yake waishike njia ya Bwana, wafanye haki na hukumu, ili kwamba Bwana naye akamtimizie Ibrahimu ahadi zake". - MWANZO 18:19. (SUV- msisitizo added).
 
Sasa kwa kutumia nukuu ya mpendwa Patrick hapo juu; Ibrahimu alikuwa na agano na Mungu, kwa hiyo mambo yaliyotendeka kabla ya Sheria (Agano la Sinai) yalifanyika chini ya Agano la neema. Agano la neema huusisha imani. Na palipo na Imani pana kusikia Neno la Mungu (RUMI 10:17). Hivyo tendo la Ibrahimu kumpa Melkezedeck fungu la kumi halikuibuka ghafla tu, ni jambo lilokuwepo moyoni mwake, lililotokana na kusika. Huenda issueni nani ampe hilo fungu la kumi - alipojitokeza kuhani huyo na kumbariki ndipo Ibrahimu akatoa zaka yake kwake. Kwa upande mwingine wakati Yesu anazungumza na mafarisayo kama nilivyoeleza hapo kwanza; Yesu aliwaambia wamche Mungu na kuendelea kutoa Zaka za mboga mboga kama walivyokuwa wakitoa hapo awali - LUKU 11:42. Hii ilimaanisha (kwa mtazamo wangu); Bwana Yesu alikubaliana na utoaji wa zaka zile kama watazitoa wakiwa wamezingatia mambo ya adili, rehema na upendo.
 
Hivyo Flano swali linalohusu kutoa Zaka aidha tufuate torati ama mfano wa Ibrahimu na Yakobo, linajibika kwa kuangalia chanzo na mwendelezo wa kutoa Zaka pamoja na kufahamu maana na faida ya kutoa Zaka na madhara ya kutotoa. Kwa maoni yangu na kwa kuzingatia mtiririko wa maandiko kuhusu Zaka/Fungu la kumi/Sehemu ya kumi, utoaji wake umeendelezwa kutoka Agano la Ibrahimu kisha Agano la Sinai (torati) na mpaka agano jipya (EBRANIA 7:4-10). Hivyo maagizo yaliyopo katika nyakati zote yanatakiwa kuzingatiwa. Yaani 1) kutoa kwa sababu Mungu amekubariki 2) kutoa zaka kamili 3) Nyumbani wa Mungu 4) ukiwa unampenda Mungu na kushika maagizo yake.
Naishia hapa kwa sasa. Keep on digging.
Mathew.
 


2013/7/11 <lev...@ymail.com>

flano mambo

unread,
Jul 15, 2013, 7:20:13 AM7/15/13
to strictl...@googlegroups.com
thats great contribution Mathew, Be blessed my Brother


From: Mathew Maduhu <mdma...@gmail.com>
To: strictl...@googlegroups.com
Sent: Monday, July 15, 2013 2:01 PM
Subject: Re: KUTOA ZAKA kila mwezi au kila upatapo kipato.

SELELI EDWIN

unread,
Jul 17, 2013, 5:54:23 PM7/17/13
to strictl...@googlegroups.com

HOJA YA PILI YA MR.MILINGA NA MAONI YANGU


Milinga:Mafundisho kuhusu kutoa ZAKA kila mwezi au kila upatapo kipato


Maoni: Ni ajabu kweli kuona jinsi gani watu/wapendwa wanavyoweza kukazana kweli kutafuta mipenyo ili tu kutotoa fungu la kumi TENA KWA AJILI YA MAMBO YA MUNGU LAKINI KODI KWA SERIKALI AMBAYO NYINGINE ZINAKWENDA KUTUMIKA KWA UFISADI WA KILA AINA, HAWAKAZANI KUIKWEPA AU HATA KUICHUKIA BASI. Si kwamba ni ajabu tu lakini kwa kua Biblia inasema yaujazayo moyo ndio yanamtoka mtu yaani kwa maneno yangu, ile ‘software’ yenyewe kabisa ya mtu/mpendwa akiwa mwenyewe halisi, ile/yule ‘yeye’ haswaaa, hata akifanya pretedence awapo kati ya watu wa Mungu wenziwe, hua haifichiki ndipo sa unaona mtu kabisa anampenda Mungu na kufahamu tabia zake kuu, moja wapo kubwa sana mbali na ile ya Utakatifu  ni hii ya utoaji, nevertheless, bado mtu au mtoto wa Mungu anakomaa kutafuta kamlango ka kuzibania noti zake izo tena chache kweli wakati wako wana wa Mungu wameshavuka pingu za mateso ya roho za ubinafsi na kujipenda nafsi wenyewe kuliko Mungu na sasa hawaongelei fungu la kumi kwa kua hayo ni mambo basics kwa  faith beginners! bali wanaongelea fungu la 15,20,30 na wengine 50! Napenda kuchangia hoja hii kwa ku-estabish solid ground ya tabia hii ya Mungu ya Utoaji na mapenzi yake kwetu kwa ujumla kisha nita-conclude kwa nguvu nyingi sana in Jesus name kuhimiza na kutia moyo utoaji wa aina ZOTE na kwa frequencies ZOZOTE, ziwe short or long waves because we love Him and all what we have and mpaka sisi wenyewe ni mali yake, we got nothing we own for real on serious note!



Katika Yoh.3:16 Mungu aliupenda Ulimwengu kisha AKAMTOA mwanae wa pekee. Yesu alisema ktk Yoh.15:13 hakuna love kubwa kama hii ya mtu KUUTOA uhai wake kwa ajli ya rafiki zake na Paul anamnukuu Bwana ktk Mdo.20:35 kua ni baraka zaidi au Heri (ni bora/furaha/yafaa/njema nk) KUTOA kuliko kupokea, hapa tabia njema ya kupenda kutoa/kujitolea inatiliwa maanani/mkazo kati ya wanadamu



UTOAJI ulipelekea mpaka mtu ambaye hajaokoka akasikilizwa mbinguni na kumbukumbu ya utoaji wake ikawa smartly and correctly recorded na some ‘’Bill Gates tools users angels’ in heaven-Mdo.10:1-4. Si tu yeye bali wokovu uliwapata hata majirani, housemaids, marafiki, ndugu na jamaa zake..Mdo.10:24,44-48! can you imagine that for a second! Jinsi gani nguvu ya Utoaji ilivyo? Japokua ni plan ya Mungu toka hakujawekwa misingi ya dunia sisi tuokolewe lakini kwa hapa naona Bwana alifanya ‘emergency strategy’ ku-manifest iyo plan iliyokuwepo tu toka mwanzo.



UTOAJI ulipelekea Mungu kujisikia raha mpaka ku-confirm na ku re-affirm commitment yake kuhakikisha Ibrahimu ana pata uzao mwingi ambamo humo humo Masiya angetokea pale alipomtoa mwanae wa pekee bila utani wala maigizo au danganya toto game, kumchinja kama sadaka ya kuteketezwa. Na kwakua Mungu huona mioyo, alijua dizani ya wapendwa kama Ibrahimu means business inapokuja swala la kumwamini na kumuishia Mola kwa kuachilia kila alichonacho kwakwe ivyo ilibidi Mungu aweke malaika mmoja awe on standby. Ndiposa aliponyanyua/nyoosha tu mkono wenye kisu kushusha kwa koo la innocent son Isack, rocketfully an angel on duty/guard akafanya hima kumwita mpendwa maridadi kabisa yule kwenye utoaji tena wa zaidi ya fungu la kumi…your own ONLY loving son,da! iyo kitu ikawa tamu sana mbele za Mungu, ikamshinda kuvumilia/kujikausha ndipo akatoa appreciations( inapendeza kuona kua Mungu ana-appreciate pia a well done job ya mtu,hapuuzi au kujifanya hai-feel!),moyo wake ukayatoa yalioujaza au yaliyobubujishwa na tendo la Utoaji la senior brother…Mwanzo.22:1-19 hasa mistari ya 12,15,16,17..Mungu anasema ‘’Sasa NIMEJUA wamcha Mungu wala HUKUNIZUILIA MWANAO, MWANA WAKO WA PEKEE( interesting arrangement ya maneno hapo , Mungu anasisitiza admiration yake hapo…see this again..’’mwanao…mwana wako wa pekee’’)


Halafu inakua kama bado Mungu hakukata kiu sawa sawa(unajua utoaji ule ulimgusa/mshangaza sana) ivyo basi.. ‘’Malaika akamwita tena mara ya PILI toka mbinguni kusema     ( unaona hapo, anaitwa tena) halafu Mungu anaona ili kukata kiu ya furaha yake na kuridhia/kuappreciate kazi njema/ tendo la Utoaji la brother, anasema maneno mazito haya.. ‘’KWA NAFSI YANGU NIMEAPA KWA KUA UMEFANYA JAMBO HILI NA HUKUNIZUILIA MWANAO, MWANA WAKO WA PEKEE! Kisha anafanya ile nilidokeza juu..Confirming na Affirming… anasema..’’Kukubaliki nitakubaliki na kukuzidisha nitauzidisha uzao wako kama nyota na mchanga wa beach baharani. Ulishawahi fikiri vipi kama Ibrahimu angembania-bania Isack ingekuaje kuhusu Yesu kuja kutokea? Ofcoz angekujaga tu Mwokozi but kubania kwa Ibrahimu kungemkosesha yeye mwenyewe hadhi aliyonayo leo ktk mambo ya Imani na mbele za Mungu. Unaonaje/utajisikiaje wewe Rais Obama au JK akupeti-peti kwenye bega a kusema..’’aisee kwakweli sasa nimejua wewe ni rafiki yangu na unanipenda’’! mwe! Nakwambia hata kama sina pesa, ghafla BOT yote nitaona ni yangu saa iyo iyo! Sasa wandugu,why tunambania bania vinoti vyetu vya Tanzania na kuyaacha mambo ya kanisa kusota na watumishi wa Mungu/walawi wetu wa ukweli ku-sweat, wanalala njaa wakati mwingine, suti hawana, watoto wao skuli wanatimuliwa, wanakaa nyumba ya kupanga tena sebule na chumba,watoto wanalala sebuleni nk wakati nje hapo wapendwa wamebaki benzi, prado, terekta,katapilla,saloon, wana majumba Mbezi, Msasani, Bunju, Boko, Madale,Kitunda,Pugu halafu sadaka na fungu la kumi kufacilitate mambo ya ufalme na daily activities/uses ktk nyumba ya Bwana, tunakua kila mtu ni financial management experts! hata kama ulisomea kufundisha maigizo, nyimbo, ngonjera,mashairi, vyuma vya magari na tureni,siasa, idara za chama cha CCM na Chadema, human resources, kuchoma sindano ngombe na pusi or watu au kuchoma moto sodium kwa bansen burner kule lab lakini inapokuja swala la kutoa sadaka na mafungu ya kumi, suddenly tunakua Financial, Budgeting, Philosophy and critical thinking and argumentation experts!



Kuna watu wanaompenda Mungu bila kujisaza mpaka wanatoa sadaka ya utakaso kwa familia zao kwa MAMBO YA KUFIKIRIKA! Can you imagine that? Mpendwa anavyompenda Mungu na kujua kila alichonacho si chake na kwakwe cha kwanza ni kumpendeza Mungu kwanza nasi kubania-bania mali, anatoa sadaka ya kutisha kwa kua-assume tu may be mmoja wa wana familia yake anaweza kua amemkosa Mungu-Ayubu.1:1-5 see mstari wa 5.. anatoa sadaka ya kuteketeza kwa KILA mtoto(alikua nao kumi), so kama ni kondoo au ng’ombe  10 wana uwawa kwa ajili yao just because yeye kudhani tu wenda ktk kuenenda kwao, watoto wakawa  wameharibu somewhere- think about this once again-ng’ombe, kondoo au hata mbuzi 10 kuuwawa kila majira ya ibada baada ya feasting! Leo hapa Dar bei ya mbuzi/ng’ombe/kondoo mmoja ni sh ngapi? Halafu bado tunatafuta kutoroka na kuingia mitini kutotoa fungu la kumi kama moja wapo ya matoleo mengi tu ktk Bible?



Pia kuna mpendwa hapa anampenda Mungu kiasi kwamba hata kama alipewa chance ya kutoroka kutoa, opportunity ambazo tunazisaka kweli mechanically na si God given lakini kaka Daudi hakuchangamkia iyo chance ya kuingia mitini bali aliamua kuweka akiba ya matolea yenye thamani zaidi ya fungu la kumi kwa ajili ya mwanae kuja kujenga nyumba ya Bwana- angalia madini na vito vya thamani vinatisha sana alivyoweka/toa huyu brother hapa-1Nyakati.29:2-5



The fact that Abraham na Jacob gave tenth/tithe Gen.14:18-20, 28:22 before even specific Moses Laws or clear/popular prophets’ utterances, that by its self-cements the fact that, God loved from the past, when his people honour Him with their possessions-Proverbs.3:9



Yesu mwenyewe ametia moyo swala zima la kua na moyo wa kutoa aliposema tutoe ili nasi tupewe kipimo cha kushindiliwa..Luka.6:38



Nimeongelea Utoaji kwa ujumla ktk mifano hapo juu kuonyesha jinsi gani hii ni moja ya tabia kuu za Mungu na watu wake wanaomfuta kwa dhati. Na tunaposema utoaji, umo twakuta aina nyingi mifano zaka, malimbuko, changizo, sadaka za kuteketeza nk. Kwa kweli iyo hapo juu, jitihada yoyote ya kupangua /ku-adjust/ ku-harmonise /kubalance balance/kutwist focus ili watu wawe na second thought kuhusu kumtolea Mungu na hasa kwa maana hii ya zaka, ni msukumo wa kibinadamu zaidi kuliko Roho Mtakatifu na si moyo wa dhati wa kutaka kumpendeza Mungu kwa kufundisha jambo  la kimbinguni la kikweliii. Pia jitihada izo zinatoa picha ya nature mbaya ya mwanadamu ambayo aidha viongozi wa mhusika kiroho au yeye mwenyewe hawajaishughulikia. Ni indicator ya madhara ya shibe kwa mtu kuanza kumsahau Mungu kwa ku-less prioritize mambo yake, ni roho ya ubinafsi na kujipenda/kujihurumia kupita kiasi.



Mtu akimpenda Mungu, hajisazi, si tu fungu la Kumi hata Isack kabisa ambaye ni zaidi ya fungu la kumi, hatatoka tu maana kwakwe yeye twaishi na kuenenda na kupata uhai. Yaani hata kua na wazo la kua kutoa zaka kila mwezi ni upotofu! Ilo wazo on serious note, linatokana na nini au ni kitu gani kimeki-inspire icho kiwazo au kuzaa thinking/wazo ilo? Ni Roho Mtakatifu? The opposite can be very true!!!!!!!! Ukitaka kujua kua something is wrong, tujipime tu tulikuaje kabla ya kuzikamata noti? Uko nyuma? mbona tulitoa tu fresh tena kwa raha hata ubongo kama vile haukufanya kazi? leo imekuaje? Kumetokea nini? au ndio Roho anasema more clearer than the past days nini? eti eee?  Mh! hamna lolote ni kiburi cha uzima/maisha ndicho kinatusumbua, heri tuwe kama zamani, vitoto vizuriiii vya Yesu kufanya na kutenda mambo yote ya Ufalme na kanisa, Mungu nisaidie mie kwanza na kisha wenzangu.



KAMA kutoa KILA MWEZI fungu la kumi ndio kuna leta upotofu, kwangu hii ni minor issue, in fact this query is dismissed! Wajua kuna vitu so simple and minor ambavyo when are mechanically given huge weight to artificially make them sound voluminous and are made sweatingly climb the ladder, still their simplicity/lightness is vivid! Why monthly giving frequencies? Kwakua many members wa mijini na majijini wana income kupitia salary nazo hutoka mwisho wa mwezi, then logically it is easily and peacefully follows that kanisa kuweka utaratibu kwa upendo tu si kimabavu ili wawe wanatoa kila au mwisho wa mwezi, it is logical, right? kuna tabu gani hapo? Mbona wapo pia kuna members wengine ambao si wafanyakazi, wanatoa kila baada ya week, wengine siku? Kama kipato kinaingia kila week, mwisho wa mwezi, siku na mtu anaweza na anampenda Mungu wake na mambo ya kanisa/ufalme na Wachungaji wake wa KWELI( Walawi wa uhakika), si anatoa tu kwa raha na furaha zake!



Mantiki nyingine ya kutoa kila mwezi ni kua kuna watu wengine hapo kanisani, wanahitaji kula,kulala, kusomesha watoto, kama staff wa kila siku kanisani namely walinzi, wafanya usafi wa mazingira, viti/benchi na vyoo vya kanisa ili ujapo kanisani , usianze kutukana live au moyoni ukutapo vyoo/viti vichafu mbaya, wahasibu wa kanisa, housemaids wa nyumba ya kuhani, sasa hawa wote wanatuhudumia/hudumia madhabahu na kanisa/jengo kwa ujumla, wale wapi? wanaendaje home? kodi je? Ingawa fungu la Kumi ni kwa Makuhani but kwa upendo wa baadhi ya watumishi na care zao, hasa pale washirika wanaompenda Mungu ambao hawatoi fungu la kumi bali la 15, 20, 50, basi baraka iyo hua extended kuhudumia wengine/mambo mengine pia. Isingekua kuna mahitaji ya kila siku/monthly ya mjengoni kanisani hapo na watumikao humo, well, mnaweza kukaa na fungu zenu za kumi toka jan na dec mkazitoa but hawa watumishi mtakua mmewatendea haki? Mungu alijua nyumba yake itakua na shughuli na washughulikaji ivyo anahimiza kuhakikisha iwe full kwa chakula(‘’chakula’…a symbolic language kumaanisha kuwepo na majibu ya mahitaji yake na wakaao/watumiko hapo kwa ajili yetu)-Malaki.3:10.



Na sijui why kila mwezi iwe bonge la issue wakati wako wanapokea/ earn kila week na kutoa out of their willingness ? That is why nasema hapa hamna serious stuff for serious mind/spirit to discuss hence this case, is therefore once again dismissed mercilessly. Sana sana ni kibinadamu zaidi ndio kinachotusumbua tu wanadamu, hakuna Roho wala sincerity kua kuna kitu cha kiMungu VERY CRITICAL tunakosea/ kinamiss/tumepotoka! Mmh! kiko wapi? show us/ me here boldly! bring that substance here and we will discuss/chew it together to help/bless each other in love- which does not mean failing to speak straight to one another the truth/fact.



Halafu embu pia tutumie common au spiritual senses/reasoning kidogo, why would God in the whole Bible, only here allows people to TEST Him ktk eneo hilo la kuleta zaka kamili uku akiwahaidi /akiwavutia/tia hamu kwa baraka za kutisha sana atakazoachia? Majibu ni hoja 3…kwanza anajua ‘much know nature’’ za wanadamu inapokuja swala la kuachilia mali/ fedha kwa Mungu( mambo ya imani kumpa/kutoa kwa Mungu aliyeko eti ndani ya  Pastor/Kuhani wako na uyo kuhani azitafune izo noti kwa raha kabisa maana ana ruksa toka JUU kisha wewe uamini/ujue kwa hakika amekula Mungu halafu same same man of God wako mnakutana naye sokoni kununua bamia na sangara au na yeye anabamizwa kama wewe na ‘anopheles’ na ku-suffer badly malaria due to unfriendly parasites’ job in his body, iyo ‘much know nature’ ikishawaza ivyo kwakweli itakataa/kataza/wagomesha wanadamu wasitoe.



Pili, Mungu anajali na yuko fair! hawezi ona Watumishi wake alio watwaa kati yetu kumtumikia kwa ajili yetu, wafe njaa, wasote usiku na mchana kuomba na kufunga wakati tuna koroma, walie na kung’ang’ana na Mungu kila mara kupata nguvu, upako na Neno la kusema ili tukija tukute/tujue kweli Bwana amesema, halafu watu hao hao wa thamani, wawe frustrated na tabia zetu mbovu za unyimivu na kubania vinoti na vishiringi mpaka wengine inapelekea wanajuta kwanini walikubali mwito na mbaya zaidi wengine wanachoka kabisa na kurudi village kulima kwakua hali ngumu, wapendwa stiff-necked wanakomoa, wamegoma kutoa zaka na hata sadaka nyingine. Thus, Bwana inabidi afanye attractions/divine tempting if you like ili wale wagumu nao wakunjue mioyo na mikono hatari iyo inayo bajeti kuzidi waliosomea class kabisaa mambo ya budgeting!



Tatu, basi tu Mungu kama Baba, wakati mwingine pamoja na matatizo yetu e.g. ya kutotoa ili tubarikiwe, atalazimika kutusaidia tu ivyo ivyo. Unajua tena dad na watoto wake awapendae sana, so inabidi ‘kama alazimishie vile’ baraka, maana anazo nyingi lakini tunagoma kuzitwaa kwa kutoa, sasa naye anataka sana na ni raha yake kuwabariki wanae so inabdi tu sasa atushitue kidogo…’Hey! You guys/children, why are you too slow/hard, come on I have plenty in the store, give, give, give to my house or if you think I am making a joke (after all I never joke), well, test me/put me on test for this…give exact tithe then see/prove me wrong yaani if I will not do what I promised’’



Conclusively, Kwakua Mungu mwenyewe ni Mtoaji number 1 na kwakua Watu wazito ktk Bible/imani yetu walitoa sana hata wengine mafungu ya kumi kwa vipato vyao na hata ktk kila maongezeko na vilevile Yesu mwenyewe kuhimiza moyo wa kutoa  ( mafungu ya kumi yakiwemo- Matayo.23:23) na kwakua mtu akishampenda Mungu au mtu/kitu, atafanya zaidi hata ya utaratibu ili tu kukukamilisha kiu ya pendo lake kwakwe ampendaye( iwe kutoa au kutumika kila sec,saa,dk,day,week mwezi nk basi swala la kutoa zaka kila mwezi ni jema sana na ashukuriwe Mungu kwakua, wakati wengine wanaona frequencies za kila mwezi ni tabu, wengine walishatoka uko kwa beginners struggles to an advanced eagle! Ni utukufu hata utukufu, alisema, ‘’kazi nizifanyazo mie mtazifanya naam na kubwa kuliko izo( Utoaji wa zero to hero pia included hapa)

.

Nitaendelea na hoja ya 3 kuhusu ''wanawake kukatazwa mambo kadhaa, hapa nina interests binafsi pia  kwakua when a woman is mistreated, nina tatizo kubwa na mwanaume yoyote wa aina iyo kuanzia Baba yangu mzazi, thank God ameookoka sasa. So kwa kua nilikua na background spesheli na my no more mom, expect me to be on the side of the women sana tena kwa raha na confidence zote kabisa na hoja maridhawa hasa.


Press on,


Edwin Seleli



2013/7/15 flano mambo <fle...@yahoo.com>

Anthony Athanas

unread,
Jul 18, 2013, 2:57:53 PM7/18/13
to strictl...@googlegroups.com

Ahsante brother Seleli!

 

Umenigusa sana na maelezo haya hapa chini kuhusu kutolea serikali sehemu ya kodi kwa lazima si hiari na TENA NI 30% YA MAPATO YAKO KWA MWAKA INAITWA COOPERATE TAX NDIO HIYO WANAFANYA MPANGO ILI KILA MWENYE TIN namba na anafanya biashara ataza  KULIPA MWISHO WA MWAKA BILA KUKWEPA.

 

BARIKIWA SAANA

 

 AHSANTE SANA Maduhu Mathew kwa mafundisho yako mazuri sana.

 

Ahsanteni woooote wenye nia nzuri kimaandiko kuelekeza watu ktk neema ya Kumjua KRISTO.

Barikiweni woote

Amen

Anthony

Mathew Maduhu

unread,
Jul 19, 2013, 5:58:04 AM7/19/13
to strictl...@googlegroups.com
Shalom Edwin,
Nimekupata vilivyo mpendwa, hasa kwa jinisi ulivyodadavua "namna mpya ya wapendwa" ya kutafuta unafuu ili wasitoe Zaka. Lakini haya yanajitokeza kwa sababu wapendwa wanatoa Zaka kwa lazima badala ya kutoa kwa sababu WANAMPENDA MUNGU aliyewapenda kwanza HATA akamtoa mwanae kwa ajili yetu (YOH 3:16). Utukufu na sifa ni kwake Bwana anayetupa nafasi ya kuumega mkate kwa uwazi na upendo.
Mathew.
 


2013/7/18 SELELI EDWIN <selel...@gmail.com>

Stephen Mabinza

unread,
Jul 21, 2013, 3:31:16 PM7/21/13
to strictl...@googlegroups.com
Wapendwa,
 
Mimi nimefuatilia kwa ukaribu wa kutosha mjadala huu juu ya swala hili la zaka, bado sijafunguka vya kutosha, ningali bado natatanika sana juu ya swala hili la zaka. Torati ni sheria iliyosimama kimwili, Biblia inasema kuwa Torati ni kivuri cha mambo ya Rohoni, na inaendelea kuweka wazi kuwa Bwana wetu kristo alikuja kuitimiliza kweli hiyo na kuifanya Torati kuwa ya Rohoni sawasawa na Neno la Mungu kusema, “Nitaiweka sheria yangu katika mioyo yao” nikisoma ile Lk. 11:42 naona inasema hivi, 42Lakini ole wenu, Mafarisayo, kwa maana mnampa Mungu zaka za mnanaa, mchicha na kila aina ya mboga, lakini mnapuza haki na upendo wa Mungu. Iliwapasa kutoa matoleo hayo, wala msisahau kufanya hayo mengine.  Kwa mstari huu naendelea kuelewa kwamba zaka ilitolewa kwa mjibu wa Torati, ambayo pia Yesu alipokuja alikubaliana nayo lakini sioni popote kama naye alitoa Zaka, licha ya kunukuliwa akimwambia Yohana mbatizaji kwamba, “tunapaswa kuitekeleza haki yote”!. Katika agano la jipya kiuwazi sijaona fundisho lolote linalo onyesha kama Mitume walipata kutoa zaka wakati wote walipokuwa na Yesu ama baadaye. Luka.6:38. Iliyonukuliwa na mchangiaji mmoja, nayo haizungumzii Zaka! Inasema, “38Wapeni watu vitu, nanyi mtapewa. Kipimo cha kujaa na kushindiliwa na kusukwasukwa hata kumwagika, ndicho watu watakachowapa vifuani mwenu. Kwa kuwa kipimo kile kile mpimacho, ndicho mtakachopimiwa.”  Hapo napo hapana neno  Zaka pale!
 
Naamini Biblia, napenda kujifunza, naomba kusaidiwa ni wapi kunasomeka kuwa Mitume walitoa Zaka wakati wa Yesu na baada ya yeye kupaa mbinguni? Mbili, ikiwa tunasimama kwa misingi ya Mitume na Manabii, ambapo mitume wameonya kuwa “Sisi (mitume), malaika ama mtu mwingine akifundisha, mafundisho kinyume na haya tunayoyafundisha na alaaniwe!” na kwakuwa Neno la Mungu ni toshelevu, Agano la kale linapatana na Agano jipya, ni wapi katika mafundisho ya Mitume wana fundisha utoaji wa Zaka?
 
                 
Wapendwa,
 
Mimi nimefuatilia kwa ukaribu wa kutosha mjadala huu juu ya swala hili la zaka, bado sijafunguka vya kutosha, ningali bado natatanika sana juu ya swala hili la zaka. Torati ni sheria iliyosimama kimwili, Biblia inasema kuwa Torati ni kivuri cha mambo ya Rohoni, na inaendelea kuweka wazi kuwa Bwana wetu kristo alikuja kuitimiliza kweli hiyo na kuifanya Torati kuwa ya Rohoni sawasawa na Neno la Mungu kusema, “Nitaiweka sheria yangu katika mioyo yao” nikisoma ile Lk. 11:42 naona inasema hivi, 42Lakini ole wenu, Mafarisayo, kwa maana mnampa Mungu zaka za mnanaa, mchicha na kila aina ya mboga, lakini mnapuza haki na upendo wa Mungu. Iliwapasa kutoa matoleo hayo, wala msisahau kufanya hayo mengine.  Kwa mstari huu naendelea kuelewa kwamba zaka ilitolewa kwa mjibu wa Torati, ambayo pia Yesu alipokuja alikubaliana nayo lakini sioni popote kama naye alitoa Zaka, licha ya kunukuliwa akimwambia Yohana mbatizaji kwamba, “tunapaswa kuitekeleza haki yote”!. Katika agano la jipya kiuwazi sijaona fundisho lolote linalo onyesha kama Mitume walipata kutoa zaka wakati wote walipokuwa na Yesu ama baadaye. Luka.6:38. Iliyonukuliwa na mchangiaji mmoja, nayo haizungumzii Zaka! Inasema, “38Wapeni watu vitu, nanyi mtapewa. Kipimo cha kujaa na kushindiliwa na kusukwasukwa hata kumwagika, ndicho watu watakachowapa vifuani mwenu. Kwa kuwa kipimo kile kile mpimacho, ndicho mtakachopimiwa.”  Hapo napo hapana neno  Zaka pale!
 
Naamini Biblia, napenda kujifunza, naomba kusaidiwa ni wapi kunasomeka kuwa Mitume walitoa Zaka wakati wa Yesu na baada ya yeye kupaa mbinguni? Mbili, ikiwa tunasimama kwa misingi ya Mitume na Manabii, ambapo mitume wameonya kuwa “Sisi (mitume), malaika ama mtu mwingine akifundisha, mafundisho kinyume na haya tunayoyafundisha na alaaniwe!” na kwakuwa Neno la Mungu ni toshelevu, Agano la kale linapatana na Agano jipya, ni wapi katika mafundisho ya Mitume wana fundisha utoaji wa Zaka?
 
                  
Wapendwa,
 
Mimi nimefuatilia kwa ukaribu wa kutosha mjadala huu juu ya swala hili la zaka, bado sijafunguka vya kutosha, ningali bado natatanika sana juu ya swala hili la zaka. Torati ni sheria iliyosimama kimwili, Biblia inasema kuwa Torati ni kivuri cha mambo ya Rohoni, na inaendelea kuweka wazi kuwa Bwana wetu kristo alikuja kuitimiliza kweli hiyo na kuifanya Torati kuwa ya Rohoni sawasawa na Neno la Mungu kusema, “Nitaiweka sheria yangu katika mioyo yao” nikisoma ile Lk. 11:42 naona inasema hivi, 42Lakini ole wenu, Mafarisayo, kwa maana mnampa Mungu zaka za mnanaa, mchicha na kila aina ya mboga, lakini mnapuza haki na upendo wa Mungu. Iliwapasa kutoa matoleo hayo, wala msisahau kufanya hayo mengine.  Kwa mstari huu naendelea kuelewa kwamba zaka ilitolewa kwa mjibu wa Torati, ambayo pia Yesu alipokuja alikubaliana nayo lakini sioni popote kama naye alitoa Zaka, licha ya kunukuliwa akimwambia Yohana mbatizaji kwamba, “tunapaswa kuitekeleza haki yote”!. Katika agano la jipya kiuwazi sijaona fundisho lolote linalo onyesha kama Mitume walipata kutoa zaka wakati wote walipokuwa na Yesu ama baadaye. Luka.6:38. Iliyonukuliwa na mchangiaji mmoja, nayo haizungumzii Zaka! Inasema, “38Wapeni watu vitu, nanyi mtapewa. Kipimo cha kujaa na kushindiliwa na kusukwasukwa hata kumwagika, ndicho watu watakachowapa vifuani mwenu. Kwa kuwa kipimo kile kile mpimacho, ndicho mtakachopimiwa.”  Hapo napo hapana neno  Zaka pale!
 
Naamini Biblia, napenda kujifunza, naomba kusaidiwa ni wapi kunasomeka kuwa Mitume walitoa Zaka wakati wa Yesu na baada ya yeye kupaa mbinguni? Mbili, ikiwa tunasimama kwa misingi ya Mitume na Manabii, ambapo mitume wameonya kuwa “Sisi (mitume), malaika ama mtu mwingine akifundisha, mafundisho kinyume na haya tunayoyafundisha na alaaniwe!” na kwakuwa Neno la Mungu ni toshelevu, Agano la kale linapatana na Agano jipya, ni wapi katika mafundisho ya Mitume wana fundisha utoaji wa Zaka?
 
                   “Ufahamu ni chembe ya uhai!”
 
                                   Mabinza LS.
 


filbert mwanga

unread,
Jul 21, 2013, 10:51:55 PM7/21/13
to Gospel Strictly, stephen...@yahoo.com

Kuna mambo yanahitaji mjadala ni yale yote ambayo Maandiko hayatamka lolote juu ya jambo hilo. Wengi wamekaririshwa neno torati bila kujua maana yake. Hivyo kila jambo lolote linalogusa nafsi zao ni torati. Wengi wanahitaji cheap grace.
Swala la zaka na sadaka imetolewa na watakatifu wa Mungu kama Ibrahim, Isaka, na Yakobo kabla ya Waisraeli kuwepo duniani. Tena kama ni swala la zaka kwamba imezungumzwa ktk agano jipya jawabu ni ndio kwa herufi kubwa. Jifunze kwa makini habari za Melkezid
eki mfalme wa Salemu ukielewa vyema hasa katka Waebrania na Mwanzo tutaacha dhambi ya wizi wa makusudi na sio wizi bali unyanganyi (robbery). Tena ni laana.

Sent from Yahoo! Mail on Android

Subject: Re: KUTOA ZAKA kila mwezi au kila upatapo kipato.
Sent: Sun, Jul 21, 2013 7:31:16 PM

Janeth mmari

unread,
Aug 5, 2013, 3:06:49 AM8/5/13
to strictl...@googlegroups.com
Seleli Shaloom!!!!
Nafurahi kusoma hoja zako zinanifundisha sana sana kuliko kawaida, please nangoja ulete hiyo hoja ya wanawake na mavazi nasubiri kwa hamu kubwa

2013/7/15 flano mambo <fle...@yahoo.com>

 
Kujiondoa Kwenye Kundi Hili Tuma Email:
--
Tafadhali zingatia msingi wetu ni Neno la Mungu, Lengo letu Kuujenga mwili wa Kristo, kushirikiana, amani na upendo. Yeyote yuko huru kuchangia, kufundisha, kukubali kufundishwa sawasawa na Msingi wetu Mkuu Neno la Mungu. Kujiunga na Team ya Injili au Maombi wasiliana nasi kwa simu 0714 915 424. Tuma Email. strictl...@yahoo.co.uk Facebook:https://www.facebook.com/pages/Strictly-Gospel/363180289370
 

 
Kujiondoa Kwenye Kundi Hili Tuma Email:

SELELI EDWIN

unread,
Aug 7, 2013, 3:48:06 AM8/7/13
to strictl...@googlegroups.com

Janeth Mmari  Shalom too,


Ubarikiwe kwa kutia moyo, nayo ni huduma na kitu cha KiMungu kabisa, feedback yako inatia moyo Mtu kuendelea kufanya huduma humu ukijua aisee! kumbe Mwandishi hajiandikii mwenyewe bali Watu kwa kua wanasoma na kuongea back! great! ni sawa sawa na Mhubiri yuko Madhabahuni, amechachamaa halafu anasema ''Bwana Asifiwe?'' au ''Amen? au ''Alleluyaa'' watu wote kimyaa au itikia yao ni ile ya ''plz maliza haraka twende home!  Preacher mmoja kanisani kwetu alishawahi kutufokea mbaya na mwingine kwetu kule kwenye ng'ombe wengi alijifungia Biblia akakatisha mahubiri-!!!!Kweli mwitikio(positive or negative) makes the fellowship in here more lively,Amen and Amen.


Hoja Kuhusu Wanawake nilishamaliza siku sasa kama week ya 2 sasa, ziko ktk kichwa cha habari kile original cha Milinga kilichosema..''Je Mafundisho haya ni Potofu'' ndani ya subject hiyo iiliyoko humu humu, nilijibu hoja kuhusu Wanawake kwa kuzijumuisha 3 kwa mpigo kwa kichwa cha bhabari kidogo hiki..''WANAWAKE NA MAKATAZO KTK BIBLIA'' kilichokua na hoja 3 kuhusu wanawake  hizi hapa chini.


HOJA NO. 3-Mafundisho ya kukataza wanawake kuvaa suruali ili hali zinafunika uchi na mwili wao kwa usahihi zaidi kuliko hata siketi na gauni.

 

HOJA NO. 9-Mafundisho ya kuzuia wanawake wasiwe viongozi wa kanisa au wasiruhusiwe kufundisha


HOJA NO. 10- Mafundisho ya kuzuia wanawake kufanya kazi zenye kipato kwa misingi ya dini au mafundisho



Lakini pia chini ya kichwa kile kile original-''Je Mafundisho haya ni potofu?''. nilijibu Hoja nyingine 2 izi hapa chini.


''NYOTA ZILIZOIBIWA ZA WALIO NDANI YA YESU''' na ''MAFUTA NDIO UPAKO''?


 

Therefore, plz tafuta iyo Subject original, fungua then barikiwa mfulurizo Mtumishi. Kama unashindwa kui-trace iyo subject tokea upande wako, ask help toka kwa Mchungaji Mary Damian au hata mie ninaweza take trouble kuzikopi na kuzituma tena  as separate subjects! Let us/me know. Amen.


Press on,


Edwin Seleli




2013/8/5 Janeth mmari <jane...@yahoo.com>

imani moshy

unread,
Aug 10, 2013, 10:38:04 AM8/10/13
to strictl...@googlegroups.com
Wana strictly nasukuru sana kwa michango yenu juu ya utoaji wa zaka mana nilikuwa nahitaji kujua undani wa zaka kamili,nashukuruni sana kwa michango na mawazo yenu mazuri mliyoongozwa na Roho Mtakatifu
leo,naomba mnisaidie kujua myumishi wa kweli ni yupi mana mwenzenu nimechanganyikiwa kutokana na ushauri aliyoniomba rafiki yangu wa karibu juu ya maswahibu yanayompata
kifupi ni kwamba nina rafiki yangu mmoja anataka kumchumbia dada mmoja huko tabora na tayari ameshaenda kumfahamu dada wa msichana na mama alimchangamkia sana na kumwomba kila anapopata muda asiache kwenda kumsalimia mana jamaa huwa anasafiri sana kwenda tabora.sasa jana msichana kamweleza jamaa kwamba mama yake amemwambia amdanganye jamaa ampe hela na kununua kiwanja na kisha wajenge na wakimaliza amwache,pili alimwambia ahakikishe msichana anafanya lolote mpaka jamaa awe tasa
kilichonichanganya zaidi mama huyo aliokoka miaka kama nane iliyopita na ni kiongozi kwenye kanisa moja kubwa sana la kiroho
hubu  nisaidieni nimshaurije huyu rafiki yangu




Sent: Wednesday, August 7, 2013 10:48 AM

jwmsella .

unread,
Aug 12, 2013, 2:41:07 AM8/12/13
to strictl...@googlegroups.com
Imani,

Kwamba umeombwa ushauri inaonyesha kuwa Mungu amekujalia kibali kwa rafiki yako hadi akaona kuwa wewe waweza kumpa ushauri ufaao. Neema ya Mungu iwe juu yako ufanyapo hilo.

Yangu ni machache sana:

Kama msichana amemfahamisha rafiki yako kuhusu hila za mama yake (msichana), inaashiria kuwa msichana ana upendo wa dhati vinginevyo angetekeleza halafu rafiki yako angelizwa. Hivyo, rafiki yako anaweza kuendelea na uchumba, ila kama ninavyowashauri walio katika uchumba siku zote, asifanye mambo mengi kupita hatua ambayo uhusiano umefikia. Kwa mfano, katika hatua ya uchumba sidhani kama ni busara kufanya investments (uwekezaji) mkubwa au kuingia katika gharama kubwa kama kupeana pesa za kujenga nyumba na mtu ambaye bado hajawa mwenzi (mme/mke) wako.

Pili rafiki yako awe makini zaidi na mama mkwe wake mtarajiwa - awe mwangalifu lakini asionyeshe wazi wazi kuwa ametambua hila zake. Kwa mfano, awe mwangalifu anapokaribishwa nyumbani kwao - yaani, kwa mfano asiende pale kama mchumba wake hayupo, nk.

Tatu, amwombee; na huwezi kumwombea kwa dhati mtu ambaye hujamsamehe.

Kwamba huyo mama ni kiongozi wa kanisa lakini ana hila za namna hiyo (ambazo mimi naziona hazina tofauti na mtu ambaye ni mchawi), tukumbuke kuwa naye ni mwanadamu, na si kila ambaye ni kiongozi wa kanisa ni kweli amekutana na Mwanzilishi wa Kanisa (yaani Yesu Kristo).

Niishie hapo kwa sasa.

JWM


2013/8/10 imani moshy <imani...@yahoo.com>



--
Love, the sum of whole law.

SELELI EDWIN

unread,
Aug 12, 2013, 7:52:17 AM8/12/13
to strictl...@googlegroups.com
Imani Moshy,

Kua.... ''Mama wa Msichana amemwambia amdanganye jamaa ampe hela na kununua kiwanja na kisha wajenge na wakimaliza amwache'''

Maoni: Nakubaliana na Joel, that girl ooh meen, ana TRUE LOVE-kwakwe Kiwanja na pesa hazina value kuzidi Mume mtarajiwa ndio maana kumwaga siri hadharani-na imagine ni MAMA YAKE MZAZI-si BABA na mtoto ni wa KIKE  yet anaamua ku-expose deal/plot mbaya nje nje..nimependa iyo na nimpenda huyo dada ktk Bwana,safi sana.


Pia....''Mama mzazi wa msichana alimwambia ahakikishe msichana anafanya lolote mpaka jamaa awe tasa''

Maoni: Aisee hii kali na hatari sana!..kufanywa TASA! wakati umetoka JUU uko fully, completely equipped  and blessed kisha a human anafanye kazi yake mbaya! Sasa kwakua Mchumba Kike ana akili na tayari ameonyesha TRUE LOVE na kwa vile kama mwanamke atapenda kuzaa Mitume, Manabii, Wachungaji, Waalimu, Wainjilist, Waombaji, Watoaji, Wanakwaya, Wazee, Mashemasi, Wahudumu, Madaktari, Waalimu,Wanajeshi nk, bila shaka HATAKUBALI kumfanya tasa Mchumba wake  na kwa kua Mama mtu ni muovu, atataka kufanya yeye mwenyewe atakapo note/mbana mwanae na kujua hajafanya icho, then ningekua mie uyo kaka.SIENDE HOME UKO KWA UYO MAMA MKWE TO BE WA AJABU AJABU KWELI-kwani lazima!!!!!!! Maana anaweza nipa maji ya kunywa, chakula, mkono,kiti cha kukalia  vyote ivyo vikiwa na madude tayari ya kunishughulikia- ingawa tutakula vya kufisha, havitatudhuru na tutakamata nyoka na kusigina ngeee BUT SI kilive-live wakti Bwana ameshafunua na umeshajua kabsaaaaaa!


Na ni Kiongozi wa Kanisa uyo Mama Mkwe to be:

Maoni: Mada ya Joel inaitwa ''Kanisa Tumekosea wapi''.inajibu kwa sehemu kubwa inakuaje tunakua na BAADHI ya Viongozi kwa BAADHI ya Makanisa/huduma wabovu..plz soma yote na bila shaka na michango iliyopo na  itakayokuja, LAKINI swali lako hasa, UTAMJUAJE MTUMISH WA KWELI? NI NJIA 2 TU MAIN...Moja: Kwa Matunda yao- kama yako kinyume au sawa na Bible HATA IVYO, WATAKAPOKUA Wanafafana na Bible-Biblia imekubali devo anaweza kujifanya Malaika wa nuru then, Pili: njia PEKEE NA BORA SANA NA SMART MNO ni ROHO MTAKATIFU ndani yetu-hua anatutonya/bip/call/ashiria/sema/fichua/shitua/indicate/nong'oneza hata akiwa NJE KILA KITU SAFI! ndio maana kwa kweli kwa kizazi cha leo na vurugu izi ni gravely/deadly/lively TUNAMUHITAJI RM kujazwa naye na kisha kujaa kila mara na kujenga/kutuza urafika naye kila mara

Press on,

Edwin Seleli

2013/8/12 jwmsella . <joel....@gmail.com>

imani moshy

unread,
Aug 18, 2013, 7:03:09 AM8/18/13
to strictl...@googlegroups.com
shalom,nashkuru sana kwa ushauri wako mungu akubariki mtumishi



From: jwmsella . <joel....@gmail.com>
To: strictl...@googlegroups.com
Sent: Monday, August 12, 2013 9:41 AM
Subject: Re: NITAMTAMBUAJE MTUMISHI WA MUNGU
Reply all
Reply to author
Forward
0 new messages