Amani ya Bwana iwe pamoja nanyi enyi nyote,
Tunafanyaje kuhusu yafautayo…
MOJA: Ukoo/Jamii/Familia yako inafanya harusi au sherehe za Ukoo kuhusu
aliyekufa, Dada yako anaolewa na wote hawajaokoka ila wanataka mchango
wako na unajua kabisa mchango wako utahusika sana kununua vileo, mbuzi
ya kuchinja ktk vichaka vya maBabu na Ma-Bibi walikolala huku
maneno-maneno yakisemwa ya ibada fulani,
Je uchangia harusi izo za ndugu zako na sherehe za Ukoo na family au
kamwe usichangie hata kama ni Ndugu wa kuzaliwa tumbo mmoja?
PILI: Umejaa Roho lakini wewe ni Rais, Waziri, Mbunge, Speaker, Jaji,
RC, DC, WEO, VEO na kuna shughuli za Mwenge-‘ibada ya Kisasa’ ya Miaka
Nchi TZ au siku ya kuwakumbuka Mashujaa waliokufa kwa kusimama na kutoa
heshima kwa Wafu waliolifia Taifa ktk Mapigano ya Uhuru au Kiongozi
Mkuu alikufa juzi, week ijayo tunaanza kikao lakini kabla wote kusimama
kwanza kwa dk chache kumkumbuka/ombea nk? Kwa nafasi/cheo chako,
ufanyeje? Usishiriki/ususie/uombe udhuru? na ni mpaka lini utaomba
excuse ukiwa ni Kiongozi Msimamizi au mhusika sana wa jambo hilo mfano
liko Chini ya Wizara au eneo lako la Utawala?
Tafakari yangu
Kibinadamu: Isije ikawa Mungu haturuhusu wengi wetu kupanda juu na kua
ktk mamlaka za maamuzi au uwajibikaji Mkubwa maana anajua itakua ngumu
sana kuwa wasafi 24/7 na siku ile ikatukuta kama mwivi ajapo bila
taarifa ivyo kwa kua anatupenda na hataki kutupoteza Jehanum basi
atahakikisha hata kama utaomba na kutaka sana, itabaunsi tu,mmh! Ila
sijui ni kweli? Maana mbona tumehaidiwa kua vichwa and mbona tuna akina
Yusufu, Daudi, Daniel na wenzake? ILA, twende mbele turudi nyuma tena,
kua mbona pia ni kweli uko juu kuna unajisi Nje nje?-Daniel aligomea
hata aina ya vyakula sembuse kusaini mikataba, kuachia pesa kwa shughuli
tokana na shinikizo la Wakubwa kwa haya ma-sherehe na sikukuuu ukiwa
kama Wewe Waziri wa Fedha, Gavana wa BOT aliyejaa Roho?
Tutafakari na kuelimishana kwa Neno pia Akili/Ufahamu Bwana amekupa na hata Uzoefu nao, sawa kabisa.
Press on.
Edwin Seleli