Nimeachwa na mchumba

94 views
Skip to first unread message

Strictly Gospel

unread,
Apr 28, 2013, 11:12:00 PM4/28/13
to Strictly Gospel Group
mahusiano

Bwana asifiwe naitwa Ombeni, ninaishi Dar es salaam nimeachwa na mchumba wangu mwezi mmoja kabla ya harusi, nimeumia sana kiasi cha kukata tamaa kabisa na nilijipanga kuoa mwaka huu nimemuomba msamaha kwa yale niliyokosea amegoma kabisa na amesema hawezi kunisamee,wapendwa nashindwa hata kwenda pale kanisani kwa sababu yake. Nishaurini nifanyeje

--Ombeni

Stellah Maganga

unread,
Apr 29, 2013, 3:41:19 AM4/29/13
to strictl...@googlegroups.com
Mpenwa kila jambo na wakati wake huyo dada hakuwa wako na kukata tamaa ni dhambi wewe chuchumalia yajayo na huo uchungu ni wa shetani.Hebu sahau endelea na maisha yako ila yale makosa amboayo unajua ni kweli labda umefanya jaribu kuyaacha ila hakua wako na mungu anajua kinacho enndelea.
stay calm


From: Strictly Gospel <strictl...@yahoo.co.uk>
To: Strictly Gospel Group <strictl...@googlegroups.com>
Sent: Monday, April 29, 2013 6:12 AM
Subject: Nimeachwa na mchumba

--
Tafadhali zingatia msingi wetu ni Neno la Mungu, Lengo letu Kuujenga mwili wa Kristo, kushirikiana, amani na upendo. Yeyote yuko huru kuchangia, kufundisha, kukubali kufundishwa sawasawa na Msingi wetu Mkuu Neno la Mungu. Kujiunga na Team ya Injili au Maombi wasiliana nasi kwa simu 0714 915 424. Tuma Email. strictl...@yahoo.co.uk Facebook:https://www.facebook.com/pages/Strictly-Gospel/363180289370
 
Blog: www.strictlygospel.wordpress.com
 
Kujiondoa Kwenye Kundi Hili Tuma Email:
strictlygospe...@googlegroups.com
 
 


Bariki Mwasaga

unread,
Apr 29, 2013, 6:22:23 AM4/29/13
to strictlygospel
Kaka Ombeni

Je ungeachwa na mke kama alivyokuwa mtumishi wa Mungu Benny Hinn ingekuweje? jamaa aliachwa na mkewe lakini akaendelea kunyakua roho zilizopotea....kasi yake ya kumpiga mabao shetani iliongezeka. Sasa wewe amka hapo ulipo songa mbele mtazame Yesu Kristo aliyekuita ambaye amejaa uaminifu kuliko maelezo.


2013/4/29 Stellah Maganga <maganga...@yahoo.com>



--
Bariki G. Mwasaga,
P.O. Box 3021,
Dar es Salaam, Tanzania
+255 754 812 387

Mathias George

unread,
Apr 29, 2013, 6:58:05 AM4/29/13
to strictl...@googlegroups.com
Pole na hongera sana mpendwa wangu! jambo hilo ni gumu na zito kwa akili na mtazamo wa kibinadamu. Lakini katika Ulimwengu wa Roho jambo hilo linakupa hatua kubwa sana katika imani. Mshukuru Mungu kwa yote. Usiache kwenda kanisani coz haiwezekani mwanadamu akutenge na Mungu wako. Kama kweli umeokoka mimi nakusihi uendelee tena uongeze bidii zaidi ya kumtafuta Mungu, kwenda kanisani na kukaa karibu na watumishi wa Mungu. "Challenges Strengthens relationship". Maisha yetu ya wokovu hayawezi kuthibitika tusipopita kaika majaribu na changamoto mbalimbali, ndyo maana imeandikwa; "Atayevumilia mpaka mwisho ndiye atakayeokoka." Siyo atakayevumilia mpaka katikati!

--- On Mon, 4/29/13, Stellah Maganga <maganga...@yahoo.com> wrote:

Kisoma Mussa

unread,
Apr 29, 2013, 2:54:50 PM4/29/13
to strictl...@googlegroups.com
Pole sana, ni vema kujitathmini na kujua tatizo lililowafanya mkaachana ili Mungu akikujalia mchumba mwingine usifanye makosa ila cha msingi ujue hakuna cha kututenga na upendo wa Kristo, kuwa makini usije ukatafuta mwanamke yeyote tu ili uzibe pengo badala ya kutulia na kumwomba Mungu aongoze maamuzi yako! Usimlaumu huyo mchumba wako, ni bunadamu hajakamilika ukihukumu nawe utahukumiwa, kanisani nenda kwa ujasiri mwambie roho mtakatifu akupe nguvu


2013/4/29 Mathias George <gmath...@yahoo.com>

thobiasi mosha

unread,
Apr 30, 2013, 2:10:53 AM4/30/13
to strictl...@googlegroups.com
usilazimishe jambo tulia katika mikono salama ya mungu jikubali kuwa umwkataliwa na amani ya rohoni itakusaidia je ungekuwa umeathrika usingefuata ushauri ili uwe  na maisha marefu lamsingi sahau na kuachilia -msubiri Mungu
pastor thobiasi

--- On Sun, 4/28/13, Strictly Gospel <strictl...@yahoo.co.uk> wrote:

From: Strictly Gospel <strictl...@yahoo.co.uk>
Subject: Nimeachwa na mchumba
To: "Strictly Gospel Group" <strictl...@googlegroups.com>
--

Cathy Marco

unread,
Apr 30, 2013, 4:18:10 AM4/30/13
to strictl...@googlegroups.com
kaka OMBENI,  mke mwema anatoka kwa bwana usilazimishe Mungu anamakusudi na wewe huwezi jua amekuepusha nini juu ya huyo mchumba wako muombe Mungu mueleze haja ya moyo wako, naamini bwana atatenda na atakuonesha mke aliye mwema, anayejua kusamehe na mwenye upendo wa dhati kwako, usiogope kwenda kanisani mana huko ndo faraja yako ilipo be strong  nenda kaabudu,  tuliza moyo wako kwa bwana bibilia inasema mtu asye samehe wenzake makosa yao naye hata samehewa.  pole sana kwa huu wakati mgum ulio nao, ikiwa umemwomba msamaha na hataki kuku samehe usilazmishe ili isije ikakucost hapo badae,   huyo ni binadam wakawaida tu naye hajakamilika. ipo siku ataukumbuka mwema wako na atajutia lakn atakua kshachelewa nakama kuna mtu anamshaur asikusamehe ipo cku ukweli  atakuja kuufaham ni hayo tu, omba bila kukoma mpigie MUNGU magoti naye atajibu haja ya moyo wako.

from cathy marco.


2013/4/29 Kisoma Mussa <hopeminis...@gmail.com>

Doris Barnabas

unread,
May 2, 2013, 2:50:09 AM5/2/13
to strictl...@googlegroups.com
shalom!


pole sana kaka Ombeni
samahani kabla ya kukupa ushauri naomba niulize maswali machache
1. je huyo mchumba ulimpata baada ya maombi/ ulipewa na Bwana au ni kwa njia ile yetu ya kawaida ya kuangalia tabia, mwenendo wake, ukoo wake, mazoea, tunasali wote, ameokoka n.k samahani kukuuliza swali hili lina maana kubwa.na sio peke yako wanao oana kwa njia hii

2.
je hayo makosa uliyofanya ni dhambi au just hulka? nina maana kuna makosa ambayo hata mbele za Mungu ni dhambi mf uasherati, uongo n.k na kuna makosa ambayo si dhambi just hulka ya mtu kwa mwenzio inakuwa kosa mf. hujamnunulia zawadi, hujamtakia hali kwa kumpigia simu n.k na haya ni yale yaweza ikiwa kosa kwa mtu A na isiwe kosa kwa mtu B
maana yawezekana unajihukumu bure wakati hujatenda dhambi

USHAURI
1.Kwa wakati huu acha kujihukumu, kama ulitenda dhambi omba Toba kwa Mungu na jisamehe mwenyewe KWANINI TOBA ili shetani asije chukua nafasi akauangusha zaidi na asiendelee "kukusuta" kuwa u mkosji. PIA ili uendelee kujenga urafiki na uhusiano wako na Mungu maana hiki ndo kikubwa zaidi

2.kwa wakati huu usijaribu kujiingiza katika uhusiano na msichana yoyote maana shetani mjanja atakuletea binti kwa nje ni kondoo kumbe ndani ni mbwa mwitu then mkishafunga ndoa utabaki unaumizwa.

3. kwa kipindi hiki Roho yako na ifanye iamie UKURSA MPYA kabisa yaani kana kwamba hujawahi kutaka kuoa. Roho yako ihamishie katika KUTAFAKARI UKUU WA MUNGU TU zaburi 105:5 "zikumbukeni ajabu zake ALIZOZIFANYA MIUJIZA YAKE na hukumu za kinywa chake"

y
aani jitahidi muda mwingi uwe unamtakakari Mungu hasa uumbaji wake mf. mtafakari kunguru anavyo ruka kula lala nk kisha fikiri kuna mwanadamu aweza kufanya hayo? mfano mwingine eti bahari ya shamu inagawanyika kati n.k
kwanini utafakari
utakuwa umemshinda shetani anayetaka akutoe kwenye ewepo wa Mungu
PIA uatweza kurudi katika hali nzuri kisaikolojia nk
NA TENA utakuwa hujihukumu tena
ZIADI YA YOTE utatiwa nguvu kwa Upya na Roho Mtakatifu
najua sijukupa DIRECT SOLUTION but naamini kupitia hapa utapata mwanzo mpya.
barikiwa
doris

Gladys JB

unread,
May 2, 2013, 4:26:13 AM5/2/13
to strictl...@googlegroups.com
Kaka Ombeni jitie nguvu ktk Kristo.

Swali langu kwako pmj na uchungu wote ni hili,
ULITAKA KUOA ILI KUSHINDA TAMAA AU KWA KUWA NI AGIZO LA MUNGU?

Kwa nini nauliza hivi, (hili litusaidie sote)

Ukitaka kuoa au kuolewa kwa sababu ya kushindwa kudhibiti tamaa za mwili na macho (misukumo na misisimko ya mwili) bado utakuwa hujamaliza tatizo ila huenda ukawa umeliongeza kwa sababu tamaa haiko mwilini iko ktk moyo wa mtu.

Pambana kwanza na tamaa uishinde, madhabahu yako iwe sawa, kisha oa au olewa. (Ni ushauri)
Natoa angalizo hili jepesi sana kwa sababu km twaoa na kuolewa sbb ya tamaa twaweza kukosea sana tukajutia uchaguzi na maamuzi yetu, na pia yafuatayo yakitokea hatutaweza kuishinda  tamaa,

1. Magonjwa ya muda mrefu btn wanandoa
2. Mke akijifungua tena mbaya zaidi kwa operesheni
3. Uzuri wa sura na shape vinapotoweshwa na sababu yoyote
4. Mwenzi mmoja wapo anaposafiri kwa muda mrefu kikazi, kibiashara au kimasomo na mengine kadha wa kadha.

Kumbe kila mwana SG na aliye nje ya kundi anapaswa kuyajua haya kabla hajaingia ktk mkakati wa ndoa.

Hayo nayo nimeyapitia lkn nilifundishwa na mtumishi mmoja kuishinda tamaa sio kukimbilia ndoa, nilishika nikatenda, ninaendelea kumkumbusha Mungu na kumshukuru na mpk sasa ninaendelea vema ktk Yesu. Kifafa cha wokovu hakipo tena (japo sijawahi kufanya zinaa tangu nimeokoka) maana kifafa kiko hata ktk mawazo na nia zetu tena huko ni kubaya zaidi maana hakuonekani.

Paulo akasema, "Nimejifunza kuridhika na hali zote. Kuwa nacho ama kupungukiwa......"

Ukijifunza kuridhika inafaa sana kwa mtauwa. Sisemi usimwombe Mungu kwa bidii ili upewe mwenzi ama hitaji lolote utakalo, endelea kuomba tena omba bila kukoma na pia shukuru hata km hayajatokea uombayo, lakini pia uwe na tahadhari kuwa stm waweza omba kwa muda mrefu tena kwa bidii na asitokee au ucpate kile uombacho kwa wkt unaotaka ww. 

"WKT MWINGINE MUNGU HUWA HABADILISHI HALI ZETU ILA ANAJITAHIDI KUBADILI MIOYO YETU"  ndipo atupe tuombayo maana Yeye anatujua vema kuliko tujijuavyo.

Tuendelee kutiana moyo huku tukijifunza kwa bidii ili kushinda zaidi. Haya ni mawazo yangu

NAWAPENDA KWA KUWA KRISTO ALIAGIZA UPENDO

Gladys mwana wa John Simtitu





From: Strictly Gospel <strictl...@yahoo.co.uk>
To: Strictly Gospel Group <strictl...@googlegroups.com>
Sent: Monday, April 29, 2013 6:12 AM
Subject: Nimeachwa na mchumba

elia kisigila

unread,
May 2, 2013, 8:42:15 AM5/2/13
to strictl...@googlegroups.com
Shalom! Nashukuru sana dada Doris Barnaba kwa ushauri wako mzuri na wa kina kama naweza kuuita namna hiyo... Wakati mwingine tunaweza kutokujua kile Mungu atakacho juu ya maisha yetu. Mungu alipomkataa Sauli kuwa mfalme ilimchukua muda mrefu Samweli nabii kuyakubali matokeo na akabaki ku ng'ang'ana kumuombea msamaha kwa vile hakuyakubali matokeo mpaka Mungu alipoanza kumlazimisha kuchukua hatua kwa kwenda kumpaka mafuta mtumishi wa Mungu Daudi mtu apendezaye moyo wa Mungu. Ndugu Ombeni, wakati huu zifanye fahamu zako ziweze kukubali matokeo. Uzoefu unaonyesha kuwa kuachwa kwa mtindo huo ni kule kwa kumtafutia mtu sababu, inawezekana kabisa huyo binti ameshapata kile alichokua anahitaji kwako na ndio maana amefikia uamuzi huo. Yawezekana kabisa tangu mwanzo hakua na maamuzi ya kuolewa nawe aliamua kutafuta alichokihitaji kwa manufaa yake binafsi na alipoona amekipata akaanza kutafuta sababu za kuachana nawe. Piga konde moyo mtu wa Mungu, tazama mbele na mkono wa BWANA utkua juu yako. Jipe muda tu na utayajua mambo yote sio muda mrefu. Niliwahi kutokewa na hali kama hiyo nami nikang'ang'ana kumbe yule binti alikua mjamzito kwa mwanaume mwingine, nilipokubali matokeo na kuachia ngazi baada ya muda ndipo ikajulikana kua yule binti alikua mjamzito, hivyo ndugu hebu mshukuru Mungu kwa hatua hiyo na uanze kujipanga ki vingine... Mungu akutie nguvu.
Rev. Elia Kisigila


From: Doris Barnabas <ddo...@yahoo.com>
To: strictl...@googlegroups.com
Sent: Thursday, May 2, 2013 9:50 AM

Subject: Re: Nimeachwa na mchumba

Mwamfupe Anyisile

unread,
May 2, 2013, 11:36:12 AM5/2/13
to strictl...@googlegroups.com, elia kisigila

Pole sana OMBENI!
Mimi niseme ashukuriwe sana MUNGU kwa ajili ya kukuacha huyo aliyekuwa Mchumba na Mke wako Aliyekuwa Mtarajiwa!

Jicho lako limeona nje ya KUACHWA kwako na ndipo panapokuletea maumivu nafsini mwako juu ya hili!

Lakini kama ungeliona kule aonako MUNGU juu ya maisha yenu baada ya kuoana ungelishangiria sana na kumtukuza Mungu kwa ajili ya kuachwa kwako!

Unajua daima yaliyowekwa wazi ni kwa ajili yetu sisi wanadamu, na yale yaliyofichwa ni kwa ajili ya Mungu mwenyewe, lakini pamoja na hayo yale yaliyofichwa yana utukufu mkuu wenye kusudi la MUNGU! Je! Liwe baya KUSUDI la MUNGU kwako?

Jibu ni hapana! Ingawa najua umeumia juu ya tukio hili huna budi kujipa moyo na kujisamehe pale uliponung'unika kwa ajili ya hili ambao Kimwili waona umesalitiwa lakini katika roho Mpango wa MUNGU umekutoa katika chumba cha majuto makuu kwake ama yeye kwako maana nyote ni nafsi zinazoishi katika Mwili hivyo pengine kama ilivyo kawaida yetu wanadamu hatuwezi kuitambu nini hatima yenu ingekuwa huko mbeleni.

Kwa uaminifu NENDA mbele za MUNGU katika CHOMBO chake madhabahuni pale Ukalitolee SADAKA jambo hili pasi na kulihesabu kuwa ni sehemu ya hasara kwako bali lifanye kuwa ni lenye faida kwako katika maisha ya Kiroho! Amen? Amen!

Yupo Mtu mmoja akaota NDOTONI ya kwamba mkewe; amezaa mwana! Lakini kabla mwana hajakuwa akafa angali mtoto mchanga, Huyu Mtu akawa ni mwenye huzuni kuu sana katika kufiwa na mwana mchanga wake, lakini katika wiki moja baada ya kumuomboleza mwana mchanga wake alokufa, akaona maono, mbali na kufa mwana wake mchanga,

Akaona amekua na tayari kawa mtu mzima, na tazama akawa ni sehemu ya uadui mkuu sana kwa babaye, akatafuta watu wengine mbali na mji wa babaye ili wajipange na kumuua babaye na mamaye na jamaa wote wa nyumbani mwake, lakini bado akiwa ndotoni, akazidi kuona,......kundi lile pamoja na mwanae wakiwa katika harakati za kufanya mauaji, wakaangukiwa na ukuta wa uzio wa nyumba yake nao wakafa........

Yule Bwana alikupiga kele na majirani kuja wakakuta na mwana wake ni mmoja wa waliokuwa wakipanga kuwaua nyumba nzima....

Kisha yule Bwana akastuka kutoka usingizini na kutambua ya kwamba ile ilikuwa ni ndoto lakini aliyehusishwa ni mwana wake aliyekufa angali mchanga.......

kila mmoja na apate jibu
Ndipo Mungu anatwambie furahini kwa kila jambo maana hakuna ayajuaye mawazo na fikra za Mungu juu yetu isipokuwa yeye, hivyo tusilifanye kila jambo kuwa ni fitna za muovu shetani yeye mwenye kuitwa ib'lisi ..........

Nenda katoe SADAKA Madhabahuni pa Mungu, kwa hiyo ili wazo lako jipya lije pamoja na mwanzo mzuri wa MUNGU.



JHU KYALA JHO NTIMI GWANGU-----Original message-----
From: elia kisigila
Sent: 02/05/2013, 4:42 pm
To: strictl...@googlegroups.com

edwin msavangwa

unread,
May 3, 2013, 1:55:33 AM5/3/13
to strictl...@googlegroups.com
Bwana asifiwe ndugu Ombeni
 
Ondoa  SHAKA KARIBU WOTE TUMEPITIA MISUKOSUKO ya kimapenzi la msingi kwa sasa ni kujaribu kutulia na kufanya mambo ambayo yanaweza kukusahaurisha kwa kiasi fulani habari za huyu bint ila nachokushauri kwa imani yako kwa Mungu mkuu jitahidi kuomba sana tena sana bila kuchoka maana pale ambapo sisi tumeshindwa Mungu hujizihirisha tena kwa pasipotegema sisi kabisa
Kimsingi sasa tulia hudhuria semina funga na omba sana. Karibia wengi sisi tuliooa tunapitia magumu sana ktk ndoa lakini kwa kuwa mliweka nadhiri na Mungu please mrudie yeye tena ili arekebishe palipo pinda pia huu ni muda wa kutazama pale ulipokuwa unakosea mara kwa mara
2013/4/30 Cathy Marco <babypri...@gmail.com>

Pastor JCC

unread,
May 4, 2013, 11:38:28 AM5/4/13
to strictl...@googlegroups.com
Bwana Yesu apewe sifa ndugu yangu Ombeni. Nakushauri uende kwa Baba yako wa Kiroho ana uwezo wa kuwaita na kuwashauri na ikiwezekana awaite pamoja. Ukiona inashindikana tafuta mtumishi mwingine wa Mungu unayemwamini ili akusikilize na uhakikishe unamwambia kweli yote ili akusaidie. Kama ukishindwa, nakushauri uje kwngu nitakusaidia, sijui uko wapi mimi niko Dar. Analia mawasiliano yangu hapo chini.
 
Mungu akubariki sana
 
Rev. Damasus F. Mkenda
Redeemed Gospel Church Tanzania
Jesus Celebration Centre Dar es salaam
Off Morogoro Road at Kinesi (Urafiki) Football Grounds
P O BOX 55667
Dar es salaam - Tanzania
Tel: +255-754-585415/+255-712-340953/+255-787-661125/
From: thobiasi mosha <thob...@yahoo.com>
To: strictl...@googlegroups.com
Sent: Tuesday, April 30, 2013 9:10 AM

Subject: Re: Nimeachwa na mchumba
Reply all
Reply to author
Forward
0 new messages