Pendwa Seleli na wote
wengine,
Naona nisipoteze muda
nianzie hapa, ili kujibu kama alivyonitaka Seleli aliposema,
“Eva alipomsikiliza
shetani, tunaona aina ya mtoto aliyempata! ...dah!
a big question my friend aiseeee!”
Kwa upande wangu
sioni kama kuna swali kuu hapa, sote tunajua kuwa Shetani ni Muuaji, na Biblia
inasema hivyo, lakini pia Biblia inasema katika Yohana kuwa, “Mwana hufanya
ambayo alimuona Baba yake akifanya” Sasa kama Tunaliamini Neno la Mungu, basi
tunakubali kuwa anayeua ni mwana wa shetani, kwakuwa inasemwa kuwa shetani alikuwa
ni muuaji tangu mwanzo, kwa maana hiyo, hiyo ndiyo iliyokuwa kazi yake na
anaendelea nayo hadi leo, kwa hiyo nategemea pia na watoto wake wafanye uuaji
kama kzi ya nyumbani mwao, kazi ya Baba yao; Kwa hiyo, na Kaini mtoto wa kwanza wa Eva ni mtoto wa
shetani, muuaji, maana alimuua nduguye!
Zaidi sana, hata
katika wana wa Adamu, ukoo ule, Kaini hayumo! Basi, kwakuwa kila mwanamme hapa
Duniani alizaliwa na Mwanamke, labda kama hatuliamini Neno, tumuulize Eva,
alimpata wapi Kaini, mbona hafanani na Adamu ambaye hata Bwana Yesu aliona ni
sifa njema kujiita “Mwana wa Adamu!”? (Lakini, Bwana Seleli, hivi hakuna sehemu
katika SG blog tulipata kulisemea jambo hili la uzao wa nyoka, au linalofanana
na hilo?! – hebu tukumbushe mkubwa, ili tupate kupaangalia tena.)
Jambo jingine ‘jirani yangu’ mwema Seleli alisema,
“Ila kali mwenzangu,
fafanua '''''Mpango wa kukusanya mbegu ili "KUZIZINISHA" ni
mpango wa kimapepo'''.....Nini maana ya kuzini? huwezi zini na vyombo vya
hospitali bwanaaa au? tehe tehe apo Kaka lete nondo za uhakika, sijakupata
kabisa.”
Iko siku, Yesu ali
fanya Kikoto cha kamba na kuwatimua mbio watu waliojaribu kubadirisha matumizi
ya Hekaru, liwe Soko huru! Tunajifunza nini tunapotaka kubadili matumizi ya
hekaru ambalo ni Bibi Harusi wa Kristo kwa kupandikiza mbegu za uzazi ambazo
hazitokani na Mme halali wa mhusika? Je, hujapata kusoma pale ambapo Mwanamme
mmoja alipotakiwa kumuinulia uzao nduguye, ambaye alifariki bila kuwa na uzao,
yeye alipofanya tendo la ndoa akazimwaga chini zile mbegu badala ya kuziacha
zipenye ndani ya lile tumbo la Yule mama,
kilichompata ulikiona? Alikufa palepale! Sasa huoni pia waliotoa mbegu
zao na kuziweka Benki badala ya kuzipenyeza katika matumbo ya wake zao, isiwe
nao tayari walisha kufa?!
Mwili wa mtoto wa Mungu ni Hekalu
takatifu, na hekalu hilo ni Bibi harusi
wa Kristo, sasa unaonaje, ikiwa Bibi harusi hafanyi ambavyo Bwana harusi
atakavyo, je, Bibi harusi huyo anafaa kuwa mke wa Bwana harusi mtarajiwa? Bibi
harusi akiingiza mbegu zisizotokana na huyo Bwana harusi, na Bwana Harusi
akamuona Yule Bibi harusi wake ni mjamzito, huku Bwana harusi Yule anayo hakika
kabisa kuwa hajawahi kumuingilia mkewe mtalajiwa huyo, Bwana harusi Yule
hatomwacha? Hebu isome ile habari ya Yusufu na Mariamu kwanza; inatufundisha
nini, kuhusiana na Kristo na Kanisa?
Mwisho , Seleli
kasema huku akichekacheka kuwa,
“Ufahamu ni chembe ya
Uhai!" tehe tehe Mabinza bwanaa ako kakibwagizo kako ako sijui ulikatoa
wapi? ka aina yakeee eeee? tehe, safiiiiii”
Nikwamba kibwagizo
kile ni Neno la Mungu, kinatoka na Zab.
119:104, ukiuchukia uongo, utaupenda ukweli na ukiupata ukweli unakuwa huru
kweli kweli, na aliye huru ni mtu hai! upo seleli?
“Ufahamu ni chembe ya
uhai!”
MABINZA LS.