Ninaomba mpenyo kwenye maisha yangu

327 views
Skip to first unread message

Mary Damian

unread,
Jun 24, 2013, 10:16:44 AM6/24/13
to strictl...@googlegroups.com, sg-kundi-...@googlegroups.com

Naitwa mama Naomi, Naomba muungane nami katika kumuomba Mungu juu ya mambo yafuatayo;
1. Mungu anipe kazi tena nzuri – wazazi wangu wanaishi katika mazingira magumu sana ninapenda niwabariki kwa kuwatunza pia kuwajengea nyumba lakini sina kabisa fedha. pia ninahitaji kumpeleka mtoto shule lakini hatuna kitu.Mungu amenibarikia elimu nimetafuta kazi tangu 2011 hadi leo sijapata
2. Mama yangu anaumwa muda mrefu sasa ninaomba uponyaji kwake lakini pia wazazi wangu wote na ndugu zangu hawajaokoka nahitaji waokoke
3. Mtoto wetu ni mkubwa sasa umri wa kusoma shule lakini hajapata mwenzake, amekuwa akituomba tumnunulie mdogo wake wa kiume tunaomba Mungu atubariki katika hilo
4. Mume wangu ni mtafutaji sana lakini si mtu wa kufanikiwa, ana miaka mitano sasa anaanzisha miradi tofauti mara duka, kilimo nk lakini vyote vinakufa .

Tunampenda Mungu na kumheshimu.

--Salome
Ndugu mwanamaombi, popote ulipo, chukua nafasi ya kuomba kwa ajili ya dada Salome, tamka kitu juu yake ili Mungu afungue milango kwenye maisha yake.

Daniel Nzali

unread,
Jun 24, 2013, 10:36:28 AM6/24/13
to strictl...@googlegroups.com, sg-kundi-...@googlegroups.com
Mungu wetu ni mwema sana dada Salome.. Nina uhakika sisi kama watoto wake tukikaa katika njia zake na kuomba katika mapenzi yake Yeye kama baba Yetu atatupa haja za mioyo yetu... Tunakuombea..!

Nzali.D.J.
 


From: Mary Damian <maryd...@aol.com>
To: strictl...@googlegroups.com
Cc: sg-kundi-...@googlegroups.com
Sent: Monday, 24 June 2013, 17:16
Subject: Ninaomba mpenyo kwenye maisha yangu

--
Tafadhali zingatia msingi wetu ni Neno la Mungu, Lengo letu Kuujenga mwili wa Kristo, kushirikiana, amani na upendo. Yeyote yuko huru kuchangia, kufundisha, kukubali kufundishwa sawasawa na Msingi wetu Mkuu Neno la Mungu. Kujiunga na Team ya Injili au Maombi wasiliana nasi kwa simu 0714 915 424. Tuma Email. strictl...@yahoo.co.uk Facebook:https://www.facebook.com/pages/Strictly-Gospel/363180289370
 
Blog: www.strictlygospel.wordpress.com
 
Kujiondoa Kwenye Kundi Hili Tuma Email:
strictlygospe...@googlegroups.com
 
 


flano mambo

unread,
Jun 25, 2013, 2:52:16 AM6/25/13
to strictl...@googlegroups.com
Bwana Yesu apewe sifa, napenda kukupa hongera sana Dada Salome kwa kuendelea kumpenda Bwana Yesu japo unaona upepo mwingi katika maisha yako. Napenda tukumbuke kuwa neno la Mungu linatufundisha kuwa" BWANA NDIYE MCHUNGAJI SITAPUNGUKIWA NA KITU, ..... KATIKA MAJANI MABICHI HUNIONGOZA, KANDO YA MAJI YA UTULIVU HUNILAZA............ NIJAPOPITA KATI YA BONDE LA UVULI WA MAUTI SITAOGOPA MABAYA MAANA WEWE U PAMOJA NAMI."

wapendwa tabia za wachungaji wa wanyama ni kuhakikisha usalama wa wanyama wake wawapo malishoni, si hivyo tu bali kuhakikisha wanapata malisho safi ndo maana wachungaji wa wanyama huhama hama leo atalisha mbagala kesho ataona no ngoja nipeleke gongolamboto maana mbagala majani yamekauka. na gongolamboto yakipungua na kukauka usishangae ukakutana na kundi la mifugo pale mizani wanaswagwa kwenda kula malisho mazuri kibaha.

Namaanisha kuwa Bwana Yesu ndiye mchungaji wetu hivyo hakika hatutapungukiwa kabisa, yeye ndiye ajuaye malisho yanayomfaa mtoto wangu SALOME yapo kibaha na si kimara, hivyo dada itakulazimu utembee hadi kibaha but ukifika pale lazima tu siku moja utarudi hapa strict kushuhudia maana hakika Bwana Yesu anayo majani mabichi kwa ajili yako. Japo unapita kwenye bonde la uvuli wa mauti linalofisha miradi na mpenyo hakika usiogope maana yeye aliye kweli na amini anasema YU PAMOJA NAWE, kwenye Isaya 43 anasema ujapopita kwenye maji mengi hutagharikishwa, na ujapopita kwenye miali ya moto hutateketea, yaani kweli mafuriko huenda yakatupata na miali ya moto ikakudondokea ila Yeye aliye Amini NA Kweli amesema HUTATEKETEA NA KUTAGHARIKISHWA.

Dada nasema hivyo bse hata mimi nimepita kwenye failures nyingi hadi kutapeliwa zaidi ya milioni13 ambazo nilizitegemea sana kwenye biashara na sijapata hata sh1, nimetapeliwa kiwanja nilichokilipia 6mil  by 2008 but wonderful Mungu amenipa nyumba modern mwezi uliopita yaani at zero cost yaani sijalipia hata shilingi moja.

Wewe endelea kusimama kwenye neno lake, hakikisha kidogo upatacho unamkumbuka Mungu (zaka aka 10%) utaona ipo siku Suprise itakuzukia maana neno la Mungu kwenye Wakorinto linasema MUNGU HUMPA MBENGU MWENYE KUPANDA NA MKATE KUWA CHAKULA........

Jitie nguvu kwa Bwana, tutazidi kumsihi Bwana Yesu kwa ajili yako

Flano


Sent: Monday, June 24, 2013 5:16 PM

Subject: Ninaomba mpenyo kwenye maisha yangu

SELELI EDWIN

unread,
Jun 25, 2013, 10:18:05 PM6/25/13
to strictl...@googlegroups.com
Salome, my dada ktk Bwana,

Jinsi nilivyokamatwa moyoni mwangu na kuguswa sana na unayopitia(Bwana ni shahidi), kwakweli ninatoa muda wangu wa kutosha kuandika na nikutie moyo,Wapendwa wanapopitia baadhi ya mambo e.g. from 2001 kutafuta kazi, todate nothing!!!!!!!!!! yaani ukijipima kwa dhati ya moyoni, unatamani sijui yangu yanaweza subiri kidogo, Bwana atenda kwako kwanza then arekebishe na yangu later ivyo nasikia moyoni kujaa huruma na kutia moyo.Nianze kwa kusema pole  mtoto wa Mungu hupendwae sana na Baba wa Mbinguni, Naweza hisi kwa kua mpaka kuchukua hatua ya kuandika kuomba maombi kwa changamoto zilizopo-ingawa ni KiBiblia kushirikishana na kuombeana but pia kibinadamu mapito au challenge zinakuwaga mzigo wa aina yake mpaka kutoweza kubeba mwenyewe ivyo kuhitajiana sisi kwa sisi kama wana wa Mungu. Nakupa pole rafiki lakini pia nakupa hongera kwakua ingawa nawiwa kukutia moyo kwa shuhuda kadhaa, Neno na some ushauri tayari wewe umetia moyo kweli kwa sentence yako hii yenye kilo za kutosha mtu wa Mungu...''Tunampenda Mungu na kumheshimu''''', nimependa sana, jinsi gani  mnapitia mambo na bado mnakua na stamina ya ajabu ya kutamka na kikiri positive(no single room to devil provided ktk mawazo/matamshi) excellent indeed mpendwa na  ina nguvu sana iyo sister Salome. What wonderful maturity in Jesus/faith is that! wow! great!( ILI ISIWE NDEFU SANA, SOMA VIPANDE VINGINE NEXT EMAIL)


USHUHUDA-UNAHUSU KUTAFUTA SANA KITU UNACHOKIHITAJI/UNACHOPENDA SANA NA UKITEGEMEA KIJE HARAKA LAKINI KINAKAWIA ILA HATIMAYE KITAKUJA.Yuko kaka mmoja, alikua na matarajio makubwa toka akiwa darasa la 4 kufika Chuo KIkuu.Kuna wakati mmoja Baba yake alimwita na watoto wenziwe na kuanza kuwauliza kila mmoja anataka kua nani maishani. To his father's surprise, yule mtoto akatamka kua anataka kua Prof wa Chuo. At the age of standard 4, bila shaka mtoto yule alikua hajui nini maana na msalaba wa kua/kufikia Chuo Kikuu/u-prof but ndicho ali-wish kua/kilichomtoka moyoni na mdomoni mtoto yule. Amekua toka shule ya msingi akiwaza/kuota ilo.Darasa la 7 akafeli na Ikabidi kuingia day( shule za kwenda na kurudi home)-njia ya kuchukua wanafunzi  to secondary waliokua na maksi ndogo( kimsingi walio-feli). Akasoma kweli na machungu na mahasira ya ku-fail-na miaka ile ilikua heshima sana ukishinda moja kwa moja kwenda boarding school-wow it was lovely. Akasoma kwa bidii sana ingawa hesabu ilikua ina msumbua kweli, Mtihani wa form 4 ukaja, kabla ya paper, aliamka sa 11 kuomba sana Bwana atende muujiza ktk Maths angalau D tu ili asipigwe penati na kisha masomo mengine afanye vema sana ili kwenda A-level shule kali za serikali za boarding kipindi kile(bado ilikua ni heshima,raha na kautukufu fulani ivi kwa mwanafunzi, wazazi na shule kua na wanafunzi walioshinda straight to A-level boarding  and never a day skuli. Matokea yakatoka, amefail na hesabu F-imesisima kama inaimba chorus! pia amepigwa penati, mbaya sana! aliumia, alilia, alizira/kupunguza speed hata mambo ya kanisa, aliona mbinguni kama sio fair-(yaani na maombi yote yale na ata walioshinda straight A-level wengine-hawakua that much serious students  na wengine not committed kwa Bwana/kanisani/ktk fellowshups).Aliona ndio mwisho hatafika Chuo Kikuu-mwanzo wa barabara ya kua Prof kwa kua ameshindwa kwenda A'level , ilikua kama ndio mwisho wa mbingu kwakwe. Wazazi wake wakafanya mipango ya kumpeleka A'level but ya private- (kipindi kile ilifahamika tu  wazi kua ukienda A'level private, wewe ulizidiwa/ulifail-kitu ambacho huyu kijana alikua anakichukia kweli.

Kijana huyu kwa jinsi alivyokua ameumia, aliwambia wazazi kua hatakwenda kusoma na labda amefail ili Bwana atukukuzwe ivyo anajikisikia kwenda kumtumikia Bwana.Ilikua kama Mungu aliokoa maisha ya Kielimu ya kijana huyo kwa kuwafanya wazazi kua wakali kama mbogo na kumwambia kwa mamlaka kua watatafuta shule na kuipata na kisha kumpa mkononi kila kitu cha shule, akatae mwenyewe na kisha kusiwepo lawama baadaye kua Wazazi hawakumsomesha na akikataa pia, atoke nyumbani na kutafuta wazazi wengine na nyumba ya kuishi!!!!!! lo! ilikua too heavy kwa kijana-form4!..atakula, lala,vaa wapi! mwishowe kwa shingo upande akenda A'level private! Huzuni zikapita, moya wa ibada na kuchangamkia mambo ya Mungu ukarudi, akarudia uhai wake wa zamani kama mpendwa moto moto. Akasoma sana  HGL akijua kwakweli lazima aende Chuo kikuu STRAIGHT na akikanyaga tu kule..ni moja kwa moja kufaulu then MA na Phd tayari Mwl. chuo na uProf huo.simple! na aliwaza pia kama amepitia dreams breaches toka Primary, O level Sasa  kwa A' Level basi zinakuja nyakati za yeye aburudishwe na Bwana kwa kushinda A'level to Chuo Kikuu bila kupoteza hata chembe ya mwaka-ni wakati wake wa kubarikiwa, aliwaza/amini kijana uyo.

Paper ikaja ya final A'Level, akafeli  kiasi kwa kua mwaka huo ndipo Chuo Kikuu walitangaza rasmi, kwanza hawahesabu pass mark ya somo la dini-hata kama umepata A ya Bible knowledge,it was good for their certificates, si kua-apply Chuo Kikuu na pia mbaya zaidi utadhani Chuo kilikua kinamtegea/kinatumiwa na devo-walitangaza hawachukui wavulana wenye Dv 2 ya point 12 aliyokua nayo! do!  sasa anaendaje ktk ndoto yake ya ya kufika Chuo? ikawa ni kama mwisho wa kila kitu.Ikabidi aingie ualimu kwa shingo upande kwa kweli-why?ametoka familia ya Ualimu-anaelewa vizuri sana  ilivyo changamoto kuishi kwa kipato cha Ualimu ktk familia kubwa ivyo hakupenda kua Mwalimu. Akiwa anasoma Ualimu kila mwaka anaomba chuo kikuu kwa kutumia matokeo ya A-level, akijua may be Utawala utabadili mawazo ya kuchukua hata wavulana wa point 12. Ikatangazwa kua wakifaulu vema kabisa Diploma hasa kwa teaching subjects watakazo enda fundisha  sekondari-si yale masomo mengine  ya Ualimu mfano saikology,Filosophia, Vielelezo nk, wataruhusiwa kuapply kwa kutumia pass mark izo. Matokeo yakaja, amefaulu sana yale ya ualimu lakini haya ya kufundisha,amefeli kiasi..badala ya kupata A, alipata B na mwaka huo wengi walipata A teachings subjects.Sasa anafikaje ktk hamu yake? Alikakata tamaa kabisa, ikabidi aendelee na maisha uku aki-appy ivyo tu hamna jinsi. Chuo Kikuu kilikua na  utaratibu wa kusaidia  walioshindwa STRAIGHT kuingia au walikaa muda bila kusoma na wanapenda kuji-upgrade(mature age-entry)..Kijana huyu  kwa hasira kabisa akona hana jinsi, ngoja ajaribu tena, akajiandikisha ila tatizo, Hesabu ikawa ni lazima kwa kila mtu kuisoma ingawa hamna penati ukifeli. Paper ikaja, amefell vibaya Hesabu lakini amefaulu kuliko kawaida masomo mengine kiaisi kwamba marks za masomo yale  zikafidia gap ya hesabu na akaweza kuvuka mstari wa ufaulu na hatimaye baada ya miaka 7 ya ku-apply akiwa A'level, Diploma na akiwa kazini, ndio kupata nafasi ya kusoma Chuo.

Conclusion:  Mungu mpaka atakapokuja kutenda kwa baadhi ya mambo ktk maisha yetu, tutakua tumepata dabo-dabo portions. Kijana huyu si tu amepata shahada yake baada ya kuapply miaka 7 na bado ataendelea na MA,PhD and Post Phdz lakini kipindi icho pia amejifunza nini maana hasa ya kumgoja Bwana(kwa experience si lecture tu), amejua na kuongeza kuomba, imebidi apende Neno maana umo alikua anatafuta ahadi kwa bidii zote, ameongezeka maarifa/ufahamu/uelewa ktk kuhusiana na Bwana, amepata Neno la ushuhuda na points za ushauri/counselings. Lakini pia maisha ya primary to Diploma-8 years...ameelewa kwa uhalisia si theories kua failure is not the final and delay is not the denial, anaweza kumhakikishia yeyote kua, kwa yale matamanio mema kabisa na ya haki, kama hayaji leo basi kesho au kesho kutwa, well,week ijayo..I mean yatakuja tu. Kwamba kwa nini yanakuja kwa wengine faster na yeye hayakuja, huyu kijana amepata ufahamu wa mbinguni kabisa kutokana na maisha yake kua kila mtu ana ratiba yake na Mungu na kusudi so specific ambalo litasababisha jinsi Mungu anavyomchuka mtu A si sawa na mtu B...kila mtu na njia,channel yake...hata kama ni mke na mume,mapacha wanaofanana waliookoka, tuliookoka nao pamoja, bado kila mtu ana njia yake..mfano ktk miaka 7 ya kutafuta Chuo..wenzake kijana huyo tayari ni Phd holders lakini haimaanisha huyu kijana hatafika na haimainishi wale Phd wenzake kila kitu chao huenda speed ivyo ivyo, nao ktk maeneo fulani kiroho na kimwili, wanamshanga na kutamani sana aliyonayo kijana uyo. Iko namna Mungu hufanya kwa kila mtu kivyake akilenga yale aliyokusudia kwayo kwa nini aliruhusu fulani kuja duniani, yawe facilited.

Press on

Edwin Seleli

2013/6/24 Daniel Nzali <nza...@yahoo.co uatarm>

SELELI EDWIN

unread,
Jun 26, 2013, 8:45:53 AM6/26/13
to strictl...@googlegroups.com
Salome, my dada ktk Bwana,

Ninaendelea....Kuhusu kutaka sana/kutarajia kitu ukipendacho sana kije haraka/vizuri bila tabu na kutafuta kazi toka 2011 todate

USHUHUDA:
Unahusu Mungu anaweza sababisha ukapata kazi usiyowahi kuwaza na tena katika njia ambayo hata chembe, usingedhani kwa iyo Bwana angekutazamisha/kuku-market kwa watoa kazi na tena unapewa kazi si kwa masomo na vyeti ulivyonavyo/somea bali kwa vipaji/vipawa Mungu alivyokuumba navyo na kusababisha/kuvi-advertise mbele ya hao watoa mkate.. ni ajabu kabisa dada Salome na SG people, Mungu huyu, acheni kabisa, ikifika wakati wake kukutendea, atafanya chochote/atatumia yeyote na kwa namna yeyote ndani ya Neno na mapenzi yake ili tu mwanae apate jibu.

Yuko Mkaka, baada ya kumaliza masomo yake ya Elimu ya Juu, alitamani sana kupata kazi immediately. Ukweli kwamba wengi wa wahitimu hupata frustrations/kusota sana mtaani muda bila kipato/kazi, ilihali vyeti vya Diploma, degree ya 1, 2, vilimfanya kua na hofu/concerned sana  na kumpelekea ktk maisha yake Chuo kikuu kua na maombi kila mara na kuombewa ili BWANA amrehemu tu, amalizapo basi moja kwa moja ni kupata  kazi/mshahara. Kwakua pia alipata kwa neema sana nafasi ya kwenda Chuo Brother huyu, alijua kwa jinis Mungu alivyohusika yeye kupata Chuoa, bila shaka Mungu huyo huyo atakua na u-urgency wa aina yake ili kama Chuo kilipatikana kwa yeye Mungu kuamua kwa njia yake basi ili heshima kwa Bwana iwepo/ ushuhuda ukae vizuri/unoge, sharti atatenda  ipatikane kwa njia yake tena haraka kweli.. Lakini pia Kaka huyo alikua na pressure zake nyingine za kumtaka sana Mungu asikawie kumpa kazi, ni kwamba anatoka familia ya kipato cha chini( maskini)  na ni mzaliwa wa kwanza kwao. Kabila lao ni moja ya yale Tz ambayo ukiwa mzaliwa wa kwanza ni baraka na 'utukufu'  mkubwa unakunao lakini pia ni msalaba na kitanzi ya aina yake kwa kua unahesabika kama mkono wa pili wa Baba yako mzazi, mtunza/mwendelezaji jina la ukoo,mlea wadogo zako pamoja na Mze wa mji na ukisha pata kazi, unasukumiwa wadogo zako kadhaa uwasomeshe pia kwa kua wanasema unajifunza majukumu au ni wakati wako kumsaidia Baba yako kulea kama alivyokulea wewe mkubwa.

PIa kabila lao wana ujamaa  sana, ni kitu chenye nguvu sana ivyo kuishi watoto wa Baba na Mama mmoja  lakini pia na watoto wa Shangazi, Mjomba, Binamu wote nyumba/family moja, mnahudumwa sawa hapa hapo, ni jambo la kawaida na custom iyo inakua held with great respect. Mzaliwa wa kwanza huyo kwa kuyaelewa yote hayo, alikua si tu anaomba amalize masomo vema na kupata kazi haraka lakini kwa kweli hata kama kungepatikana kazi nzuri akiwa bado Chuo, kutokana na pressures iliyokua ktk Ukoo na familia yake nyumbani hasa walipoelewa kua wanachuo hulipwa ela( kwao walijua ni nyingi mno), ange aidha fanya kazi uku anasoma au kuhahirisha mwaka wa masomo ili angalau akamate ela kwa mwaka kusaidia nyumbani kidogo then angeendelea tu ili mradi kwa kuhahirisha mwaka kusigeweza mfanya kufukuzwa Chuo.

Akiwa anasoma chuo, kuna somo  linaitwa Research Methods, second semester ambalo ni lazima kwa kila mwanafunzi lakini lina hesabu, mtihani wa kumaliza semester akafeli                 (''akakamatwa''/''akashikwa'' au aka-sup). Ilimliza sana na hakuona jinsi gani maombi yanajibiwa uku mawazo yanamsumbua, akijiuliza atamaliza kweli na kupata degree ktk mtihani wa mwisho kabisa wa Chuo na kupata kazi safi ikiwa ameanza na record mbaya?. Lakini pia mwaka huo huo kukaingizwa somo la Computer nalo lilikua lazima kwa kila mwanafunzi. Kutokana na background yake ya kitoka Mikoani na kuja jijini kusoma kwa kulelewa na walezi, haikua rahisi kwake kupata ela ya kusoma Computer mapema ivyo somo jipya la  Introduction to Computer, ''likamkamata pia/akafeli paper yake ya mwisho. Ilikua ni kilio tu na maswali mengi kuuliza mbinguni. Ikabidi kurudi Chuo kwa ajili ya sup 2/kurudia mitihani.Walio-sup wenziwe, walisahau aibu yao na kuanza kumshangaa kua naye kumbe alikamatwa, wakaburudika kweli na vicheko na habari zikasambaa zaidi kua fulani naye ''ndani ya nyumba'' i.e kusup.Kukawa na aibu kubwa kwakwe kwakua ni kijana aliyejihusiha na mambo mengi chuo, ktk fellowship za chuo alikua mmoja wa wanenaji Neno hodari na kanisani kwake ivyo alijulikana sana na ivyo kufell kwakwe kulivuma/peperushwa sana. Matokeo yale yalimfanya akae chumbani mabibo hostel na kuacha kwenda lecture kwa mwezi-aibu ya kukutana na watu waliomuheshimu na kumkubali sana hasa ktk masomo ya kujieleza na ku-present, hata baadhi ya ma-Prof walimpenda sana na alipata kibali cha ajabu kwao, sasa akikutana nao, anaongea nini? confidence chini kabisa..akawa anasoma kwa kuphotocopy notes na kuhudhuria group discussions kwa ungalifu sana asionekana kienyeji na kwa kweli aihamia group mpya mpya za watu wa kozi nyingine lakini wanaosoma masomo baadhi sawa na yake..yaani mahangaiko kweli.

Matokeo ya kusup yakatoka na this time akafaulu( aka-clear) ila kwa somo la hesabu              ( research), ni kimiujiza-ujiza  kama si kwa neema tu maana jinsi hesabu zinavyomtesa, ilipelekea alisahau kujaza namba yake ya mtahiniwa na pia kujaza swali moja. Dr aliyesimamia mtihani alipokua anakagua ili kupanga papers kinamba, akagundua kosa ilo, akaongea na waalimu wa idara wenzake na kama jopo, wakapiitisha maamuzi ya kumpigia simu mkaka, ivyo akaitwa ofisini na kupelekwa kwa mkuu wa idara, mbele ya jopo lile, akaelezwa kasoro iyo-ilikua kidogo a-collapse maana aliwaza sup ya mara ya 2 usipofaulu, una-disco na hakuna ndoto za kupata kazi kwa kumaliza vema ukiwa na cheti cha shahada mkononi.Jasho lilimtoka lakini Dr mmoja wapo akamuona kijana ktk hali ile na kisha akasema, ''kama idara tumeamua kua tukusamehe..jaza sasa namba na swali ulililo sahau mbele yetu wote( walifanya utaratibu wa kijopo kwa mamlaka waliyokua nayo kama idara ili isije ikoneka kama kuna rushwa kama DR mmoja tu angemuita kijana huyo kujaza namba na swali aliloruka-ni ajabu kabisa kijana alivyorehemiwa na Maprof wale maana ni kiunyume na utaratibu wa kawaida wa mitihani na utahiniwa.Hatimaye, mwisho wa Chuo ukaja, kafanya final exams na aka-clear,kisha Nov. graduation, akawa kati ya wahitimu na kupewa degree..kisha kupata cheti baadaye tena chenye neno Hon(BA)....hua haelewi mpaka leo iyo term 'hon'..yaani honorary BA imekujaje wakati ali-sup masomo 2 kwakua hua ana dhani wanaopataga vyeti vyenye Hon ni wale walikwenda straight! so haelewi mpaja leo inapatikanje iyo attachement..''Hons''. 

Akaanza kusaka kazi ili kushughulikia pressure zake binafsi, za familai na ukoo. Alikua anandika mpaka barua 50 za applications na umu unajaza barua, cv, vyeti...zilimhitaji stamp kama uzito wa bahasha ukizidi. Kwakua alikua hana ela, akawa anapiga ''mzinga' wa nauli  kwenda kupost barua na ela ya stationaries kwa ajili ya kuapply kazi nyingi mno. Hakupenda sana kuapply za kimtandaoni kwa kua alikua hajui computer vema ivyo akienda internet cafe na kukaa na mtu wa humu muda mrefu kumsaidia kuaapply on line,, mhusika anahitaji posho na pia mwingine anakereka..ivyo mkaka akajikukuta inabidi ale sambasamba na kazi za kuapply kwa hard copies tu kuondoa majaribu yale ya internet cafe na hata kukwepesha aibu ya kujulikana kijana mzima tena graduate yet hajui hata kuapply kwa online e.g. kufanya attachements nk maana kuna internet cafe nyingine alikua akimwambia taratibu mhusika amsaidie kuappy, yeye anakosa hekima na ku- shout na pia mwingine anacheka na kushangaa/hata kuuliza tena kwa sauti..''yaani hujui kuapply tu na kuattach-na watu wanasikia-baadhi  wanaacha kujali mambo yao-kuendelea kusoma ktk screen zao, wanamkodela kijana macho-aibu kweli na ikawa inamtia hasira kweli  wakati mwingine na kuna nyakati aliwahi kumfokea/mkemea vibaya sana hadharani mtu wa cafe aliyemshushia personality kwa kumshanga-shangaa na kushout kwa sauti na kijana kisha akatoka kwenda internet cafe nyingine.

Alikua anabeba barua 10,20,30 kwa mchungaji wake, fellowship za kanisani, mikesha, mifungoni,wanenaji wageni eg mitume na manabii wakija kanisani kwakwe, crusade za nje na seminar za nje jangwani na Biafla, bado kazi haikuja wala hata kua -short listed kwa interview tu. Alichoka, alikosa nauli, alikosa ela ya pango..akahamia kanisani kulala ktk benchi miazi 6. Aliwavizia kuomba ''tafu'' wapendwa na ndugu mpaka wakamchoka, aliomba hifadhi kwa ndugu na jamaa wa damu, waliishindwa kukaa na kijana hasiye changia lolote, alikopa mpaka akasau kua alishamkopa fulani  kisha kurudipo tena ndipo anakumbushwa kua hajalipa deni.Akiwa ktk hali iyo, alikumbwa na matatizo ya misiba nyumbani kwao-inabidi kukopa/kuomba tafu  ili aende, aliuguza dada yake aiyekua  na hali ngumu aliyemuombea hifadhi kwa mama yake mdogo mmoja.Alitamani sana kupata kazi kubwa na inayolingana na cheti chake cha shahada lakini, haikua ivyo mapema.Kuna wakati alipata kazi za kujishikiza kama kufundisha, kufanya tu-research, mshara ukaaishia kulipa madeni yanayotisha ya nyuma ingawa bila madeni bado yeye binafsi kuishi kwa huo mpaka mwisho wa wmezi bila kukopa, ilikua ngumu, wakti mwingine contract  za temporary kazi au day worker zinaisha.

Ilikuaje kwa mkaka uyu hatimaye? ( SOMA NEXT EMAIL)

Press on,

Edwin Seleli


2013/6/26 SELELI EDWIN <selel...@gmail.com>
Salome, my dada ktk Bwana,

Jinsi nilivyokamatwa moyoni mwangu na kuguswa sana na unayopitia(Bwana ni shahidi), kwakweli ninatoa muda wangu wa kutosha kuandika na nikutie moyo,Wapendwa wanapopitia baadhi ya mambo e.g. from 2011 kutafuta kazi, todate nothing and mtoto mkubwa kuomba ANUNULIWE MDOGO WAKE! WHAT?!!!!!!!!!! yaani ukijipima kwa dhati ya moyoni, unatamani sijui yangu yanaweza subiri kidogo, Bwana atenda kwako kwanza then arekebishe na yangu later ivyo nasikia moyoni kujaa huruma na kutia moyo.Nianze kwa kusema pole  mtoto wa Mungu hupendwae sana na Baba wa Mbinguni, Naweza hisi kwa kua mpaka kuchukua hatua ya kuandika kuomba maombi kwa changamoto zilizopo-ingawa ni KiBiblia kushirikishana na kuombeana but pia kibinadamu mapito au challenge zinakuwaga mzigo wa aina yake mpaka kutoweza kubeba mwenyewe ivyo kuhitajiana sisi kwa sisi kama wana wa Mungu. Nakupa pole rafiki lakini pia nakupa hongera kwakua ingawa nawiwa kukutia moyo kwa shuhuda kadhaa, Neno na some ushauri tayari wewe umetia moyo kweli kwa sentence yako hii yenye kilo za kutosha mtu wa Mungu...''Tunampenda Mungu na kumheshimu''''', nimependa sana, jinsi gani  mnapitia mambo na bado mnakua na stamina ya ajabu ya kutamka na kikiri positive(no single room to devil provided ktk mawazo/matamshi) excellent indeed mpendwa na  ina nguvu sana iyo sister Salome. What wonderful maturity in Jesus/faith is that! wow! great!( ILI ISIWE NDEFU SANA, SOMA VIPANDE VINGINE NEXT EMAIL)



USHUHUDA-UNAHUSU KUTAFUTA SANA KITU UNACHOKIHITAJI/UNACHOPENDA SANA NA UKITEGEMEA KIJE HARAKA LAKINI KINAKAWIA ILA HATIMAYE KITAKUJA.Yuko kaka mmoja, alikua na matarajio makubwa toka akiwa darasa la 4 kufika Chuo KIkuu.Kuna wakati mmoja Baba yake alimwita na watoto wenziwe na kuanza kuwauliza kila mmoja anataka kua nani maishani. To his father's surprise, yule mtoto akatamka kua anataka kua Prof wa Chuo. At the age of standard 4, bila shaka mtoto yule alikua hajui nini maana na msalaba wa kua/kufikia Chuo Kikuu/u-prof but ndicho ali-wish kua/kilichomtoka moyoni na mdomoni mtoto yule. Amekua toka shule ya msingi akiwaza/kuota ilo.Darasa la 7 akafeli na Ikabidi kuingia day( shule za kwenda na kurudi home)-njia ya kuchukua wanafunzi  to secondary waliokua na maksi ndogo( kimsingi walio-feli). Akasoma kweli na machungu na mahasira ya ku-fail-na miaka ile ilikua heshima sana ukishinda moja kwa moja kwenda boarding school-wow it was lovely. Akasoma kwa bidii sana ingawa hesabu ilikua ina msumbua kweli, Mtihani wa form 4 ukaja, kabla ya paper, aliamka sa 11 kuomba sana Bwana atende muujiza ktk Maths angalau D tu ili asipigwe penati na kisha masomo mengine afanye vema sana ili kwenda A-level shule kali za serikali za boarding kipindi kile(bado ilikua ni heshima,raha na kautukufu fulani ivi kwa mwanafunzi, wazazi na shule kua na wanafunzi walioshinda straight to A-level boarding  and never a day skuli. Matokea yakatoka, amefail na hesabu F-imesisima kama inaimba chorus! pia amepigwa penati, mbaya sana! aliumia, alilia, alizira/kupunguza speed hata mambo ya kanisa, aliona mbinguni kama sio fair-(yaani na maombi yote yale na ata walioshinda straight A-level wengine-hawakua that much serious students  na wengine not committed kwa Bwana/kanisani/ktk fellowshups).Aliona ndio mwisho hatafika Chuo Kikuu-mwanzo wa barabara ya kua Prof kwa kua ameshindwa kwenda A'level , ilikua kama ndio mwisho wa mbingu kwakwe. Wazazi wake wakafanya mipango ya kumpeleka A'level but ya private- (kipindi kile ilifahamika tu  wazi kua ukienda A'level private, wewe ulizidiwa/ulifail-kitu ambacho huyu kijana alikua anakichukia kweli.

Kijana huyu kwa jinsi alivyokua ameumia, aliwambia wazazi kua hatakwenda kusoma na labda amefail ili Bwana atukukuzwe ivyo anajikisikia kwenda kumtumikia Bwana.Ilikua kama Mungu aliokoa maisha ya Kielimu ya kijana huyo kwa kuwafanya wazazi kua wakali kama mbogo na kumwambia kwa mamlaka kua watatafuta shule na kuipata na kisha kumpa mkononi kila kitu cha shule, akatae mwenyewe na kisha kusiwepo lawama baadaye kua Wazazi hawakumsomesha na akikataa pia, atoke nyumbani na kutafuta wazazi wengine na nyumba ya kuishi!!!!!! lo! ilikua too heavy kwa kijana-form4!..atakula, lala,vaa wapi! mwishowe kwa shingo upande akenda A'level private! Huzuni zikapita, moya wa ibada na kuchangamkia mambo ya Mungu ukarudi, akarudia uhai wake wa zamani kama mpendwa moto moto. Akasoma sana  HGL akijua kwakweli lazima aende Chuo kikuu STRAIGHT na akikanyaga tu kule..ni moja kwa moja kufaulu then MA na Phd tayari Mwl. chuo na uProf huo.simple! na aliwaza pia kama amepitia dreams breaches toka Primary, O level Sasa  kwa A' Level basi zinakuja nyakati za yeye aburudishwe na Bwana kwa kushinda A'level to Chuo Kikuu bila kupoteza hata chembe ya mwaka-ni wakati wake wa kubarikiwa, aliwaza/amini kijana uyo.

Paper ikaja ya final A'Level, akafeli  kiasi kwa kua mwaka huo ndipo Chuo Kikuu walitangaza rasmi, kwanza hawahesabu pass mark ya somo la dini-hata kama umepata A ya Bible knowledge,it was good for their certificates, si kua-apply Chuo Kikuu na pia mbaya zaidi utadhani Chuo kilikua kinamtegea/kinatumiwa na devo-walitangaza hawachukui wavulana wenye Dv 2 ya point 12 aliyokua nayo! do!  sasa anaendaje ktk ndoto yake ya ya kufika Chuo? ikawa ni kama mwisho wa kila kitu.Ikabidi aingie ualimu kwa shingo upande kwa kweli-why?ametoka familia ya Ualimu-anaelewa vizuri sana  ilivyo changamoto kuishi kwa kipato cha Ualimu ktk familia kubwa ivyo hakupenda kua Mwalimu. Akiwa anasoma Ualimu kila mwaka anaomba chuo kikuu kwa kutumia matokeo ya A-level, akijua may be Utawala utabadili mawazo ya kuchukua hata wavulana wa point 12. Ikatangazwa kua wakifaulu vema kabisa Diploma hasa kwa teaching subjects watakazo enda fundisha  sekondari-si yale masomo mengine  ya Ualimu mfano saikology,Filosophia, Vielelezo nk, wataruhusiwa kuapply kwa kutumia pass mark izo. Matokeo yakaja, amefaulu sana yale ya ualimu lakini haya ya kufundisha,amefeli kiasi..badala ya kupata A, alipata B na mwaka huo wengi walipata A teachings subjects.Sasa anafikaje ktk hamu yake? Alikakata tamaa kabisa, ikabidi aendelee na maisha uku aki-appy ivyo tu hamna jinsi. Chuo Kikuu kilikua na  utaratibu wa kusaidia  walioshindwa STRAIGHT kuingia au walikaa muda bila kusoma na wanapenda kuji-upgrade(mature age-entry)..Kijana huyu  kwa hasira kabisa akona hana jinsi, ngoja ajaribu tena, akajiandikisha ila tatizo, Hesabu ikawa ni lazima kwa kila mtu kuisoma ingawa hamna penati ukifeli. Paper ikaja, amefell vibaya Hesabu lakini amefaulu kuliko kawaida masomo mengine kiaisi kwamba marks za masomo yale  zikafidia gap ya hesabu na akaweza kuvuka mstari wa ufaulu na hatimaye baada ya miaka 7 ya ku-apply akiwa A'level, Diploma na akiwa kazini, ndio kupata nafasi ya kusoma Chuo.

Conclusion:  Mungu mpaka atakapokuja kutenda kwa baadhi ya mambo ktk maisha yetu, tutakua tumepata dabo-dabo portions. Kijana huyu si tu amepata shahada yake baada ya kuapply miaka 7 na bado ataendelea na MA,PhD and Post Phdz lakini kipindi icho pia amejifunza nini maana hasa ya kumgoja Bwana(kwa experience si lecture tu), amejua na kuongeza kuomba, imebidi apende Neno maana umo alikua anatafuta ahadi kwa bidii zote, ameongezeka maarifa/ufahamu/uelewa ktk kuhusiana na Bwana, amepata Neno la ushuhuda na points za ushauri/counselings. Lakini pia maisha ya primary to Diploma-8 years...ameelewa kwa uhalisia si theories kua failure is not the final and delay is not the denial, anaweza kumhakikishia yeyote kua, kwa yale matamanio mema kabisa na ya haki, kama hayaji leo basi kesho au kesho kutwa, well,week ijayo..I mean yatakuja tu. Kwamba kwa nini yanakuja kwa wengine faster na yeye hayakuja, huyu kijana amepata ufahamu wa mbinguni kabisa kutokana na maisha yake kua kila mtu ana ratiba yake na Mungu na kusudi so specific ambalo litasababisha jinsi Mungu anavyomchuka mtu A si sawa na mtu B...kila mtu na njia,channel yake...hata kama ni mke na mume,mapacha wanaofanana waliookoka, tuliookoka nao pamoja, bado kila mtu ana njia yake..mfano ktk miaka 7 ya kutafuta Chuo..wenzake kijana huyo tayari ni Phd holders lakini haimaanisha huyu kijana hatafika na haimainishi wale Phd wenzake kila kitu chao huenda speed ivyo ivyo, nao ktk maeneo fulani kiroho na kimwili, wanamshanga na kutamani sana aliyonayo kijana uyo. Iko namna Mungu hufanya kwa kila mtu kivyake akilenga yale aliyokusudia kwayo kwa nini aliruhusu fulani kuja duniani, yawe facilitated.

Press on,

Edwin Seleli



2013/6/26 SELELI EDWIN <selel...@gmail.com>

SELELI EDWIN

unread,
Jun 26, 2013, 1:22:03 PM6/26/13
to strictl...@googlegroups.com
Salome,

Nimamalizia ushuuda wa kupata kazi.. kwa mpango na nyakati za Mungu hata kama tumeshafanya na kutaka kweli kazi kwa nyakati zetu na kwa namna yetu njema tu kama wanadamu wengine.

Hatimaye Mkaka alichoka kuaapply na akaamua kuacha kabisa, akamwambia Mungu ivi, ''sitaapply tena na kama jitihada za kibinadamu, nimefanya kwa uaminifu na nguvu zote ikifika wakati utaamuru mtu mmoja uko na uko maofisi mengi barua zangu zilipokwenda au utajua ufanyaje nini kama Mungu si tena jitihada zangu za kibinandamu mana nimefanya sana na nimefell''. Kweli akacha kuaaply, na akatoa muda mwingi ktk huduma kanisani na kusema kweli alishai maisha ya kubangaiza, mara wapendwa kuguswa, mara yeye kuwagusisha, mara dayworker, mara, siku nyingine anakula mlo mmoja na wakati mwingine analala ivyo mpaka kesho yake. Kukiwa na maombi ya mfungo ya siku 7 kufungua jion tu kwa uji, inakua kwakwe sherehe maana imeondoa officially bajeti rasmi ya kula na jioni ile wapendwa hawawezi kufungua kunywa uji bila kuguswa na kutoa ofa. Siku zikapita wa akiwa anaendelea na huduma ndani na nje ya kanisana. ikatokea mpendwa mmoja akamjia na kumwambia kua ''amesikia kuna NGO moja inatafuta vijana wadogo wa form 4,6 labda kidogo na Diploma kwenda kufanya survey ya mwezi Wilaya moja wapo magharibi mwa Tz, unaonaje ukajaribu tu ktk interview,hata wakikukataa, upoteze kitu''. Kwakua Mkaka alishazidiwa sana na hali ya maisha, akujali level yake ya shule/status wala umri wake kua mkubwa kwenda kujichanganya na watoto. Akaenda na cha kwanza akakutana nacho nje pale ni baadhi ya wanafunzi wake aliowafunisha wajati anajishikiza hapa na pale, wakashangaa kweli na hata kucheka kirafiki wakiuliza ...'''aah! teacher..na wewe umekuja huku kuvizia chance za madent wako, aaa teacher bwanaa'', ili kuondoa aibu, Mkaka Mwalimu akachekacheka tu na kuzugu ivi kisha  kuwapigisha story ili waachane na ile topic na alifanikiwa.

Katika interview panel..umri wake, vyeti vyake ilikua kama kituko kidogo walimwona! ni kama waikua wanasema uyu naye vipi, amekwendaje mtu mzima ivyo kwa kikazi kilicholengwa kwa watoto-anasema aliona sura zao wazi kabisa zinamwambia ujumbe huo-lakini akajikaza tu. Ajabu, hawakumfanyia usaili bali wakamwandikisha moja kwa moja na kumfanya supervisor wa surveyors/watoto wote. Kabla ya kuondoka Dar, mkaka aliitwa  na Mzee wake wa kinisa anayemfahamu mkaka vema, akamwambia statement hii. Ninasikia moyoni kukuambia kua ''si kila wakati utahitaji kusema sana kujitetea, wakati mwingine kaa kimya, usiongee kitu hata kama unaonewa, mpe Roho wa Mungu nafasi akunong'oneze nini cha kusema na kisha angalia Bwana anavyokutetea'''..Mkaka alikodoa macho na kujiuliza kwanini Mze amemwambia ivyo? akamuuliza Mzee, ''kwanini amemwambia ivyo, akajibu, ''mimi sijui lakini kwamba  Roho Mtakatifu amesema nikuambie ivyo,  ilo nina uhakikia nalo kabisa', basi mkaka akaomba maombi, akamukea mikono na Mze wa kanisa akaomba kisha waachana, mkaka akisumbuka na mafikra yake, kwanini Mze/RM aseme vile, kuna nini/maana yake nini? lakini hakuna jibu.Wakaenda Wilayani, NGO ilikua inapokea ela toka shirika kubwa la Umoja wa mataifa kufanya kazi zake( NGO iyo ilikuani implementing partner wa Shirika la umoja wa mataifa). Kabla ya kutoka Dar es Salaam, baadhi ya watoto wale, wanandugu kule shirika la UN na waliwaambia ela wanayotakiwa kupewa baada ya mwezi mmoja  kwa kazi ile ni laki 9 kila mmoja ata wakawapenyezea contract paper copy ya shirika na NGO ile.Badala ya kufanya kazi mwezi, NGO ile ikawapigisha kazi haraka-haraka, over worked mpaka usiku na kwa week 2 tu kazi ya mwezi kwisha. vIjana wale na Mkaka mkubwa wakafurahi kweli kua wamepiga kazi kwa muda mfupi hata kama walikua wanachoka na kuchukia kumbe hatimaye imekua safi kwa kua wanawahi toka porini uko na kuja Dar-wengi walikua watoto wa jijni-maisha ya pori ilkua msalaba.

Kazi imekwisha, inabidi kurudi nyumbani. Siku ya kulipwa ujira na kuagwa ikafika, Wakaitwa wote kupewa pesa na kila mmoja anajua ni fungu tamu la laki 9, kumbe ile kufanyishwa kazi week 2 ilikua ila, wakasainishwa laki 6 na nusu! Kukazuka mtikisiko mkubwa, watoto wakatoa contract copy ya UN...ilikua kazi, Mkaka mkubwa akakumbuka matatizo yake ya ukoo, familia yao, miasha Dar, akakumbuka madeni na aibu zote, akaanza kuwasha moto mkali na alipotaka kuinua simu kupiga Shirina la UN, ghafla akakumbuka..''''si kila wakati utahitaji kusema sana kujitetea, wakati mwingine kaa kimya, usiongee kitu hata kama unaonewa, mpe Roho wa Mungu nafasi akunong'oneze nini cha kusema na kisha angalia Bwana anavyokutetea''', mmh! akajizuia na kukaa kimya.Hata wale watoto wakawa wana shangaa Mkaka Mkubwa/supervisor vipi, kimya kabisa ghafla. Watoto wanitwa kusign wachukue ela ile isiyo kamilifu, wakagoma, baadaye Coordinator wa NGO akasema, anayetaka fedha akasain, asiyetaka, aache na asilaumu mtu! lo! nani aache! taratibu,mmoja bada ya mwingine kimya kimya akaenda kusign. Wakawa wamekata laki 3 nzima kila kichwa NGO ile na mashirika shirikishi mengine-NGO's i.e implementing partners wa UN, wakaamua kufanya sherehe kubwa ya kuwaaga surveyors..ilikua ni zoezi kubwa ivyo liihusisha NGO 4 na surveyors wakutosha.Surveyors wakashirikishwa katika kuandaa sherehe , kila mmoja akapewa jukumu lakini kaka mkubwa akaombwa awe MC msaidizi. Jioni ikafika, ukumbi ukawa  umejaa wakuu wote wa NGO's and Shirika la UN kati ya wageni waliokuja, walikua hawajui Kiswahili-kutoka Kenya, Uganda, Ethiopia Kazakstan. Sherehe  ikawa haianzi,  wanamtafuta MC mkuu apatikani na amezima simu. Kumbe alikua hajui Kiingereza na ilhitajita MC anayeweza lugha zote ili na wakubwa wajue kinachoendelea. Mc Msaidizi muagwa( Mkaka surpervisor)naye alichelewa kufika ukumbini na hata ivyo hakua na haraka kwa kua MC mkuu yupo,yeye aliwekwa ili mradi tu.. Ghafla Mc msaidizi akasikia sauti ya gari imekuja kasi sana na kufunga break za fujo nje ya nyumba kisha makele....Mkaka anaitwa atoke nje haraka kwenda kuendesha sherehe, nusu saa imepita , wakubwa wameshaka, kila mtu yuko tayari, MC mkuu hapatikani. Alikwenda Mkaka na akafanya u-MC kwa lugha zote Kiswahili na Kiingereza na pia  manjonjo yote( usheshi, kushawishi, changamsha, stories,kukaribisha speeches, summarization ya wanayosema wakubwa nk). Baadae wakati watu wanasherekea na ni wakati wa DJ sasa na mambo yake MC main task imekwisha, akatoka nje kupumzika kidogo kisha kwenda kupumzika. Akiwa nje, Wakuu wa Mashirka wakawa wana toka, wakimkuta MC msaidizi, wanampongeza kweli kwa furaha na kusema ana kipaji cha ajabu cha kuongea na ku-entertain, ajabu zaidi Mkuu wa Shirika la UN akaenda mbele zaidi na kuuliza Mc anafanya nini jijini Dar, ana mpango gani anapoondoka kwenda uko nk! boss yule Mkazakstan akamuomba Mc-kua kama anaweza kwenda ofisini kwake kesho yake kwa maongozi kidogo


Alipofika ofisni, Boss  akamwambia wazi..'''Ofisi yetu imekua kwa mwaka sasa inaandaa post na ofisi itakayohusu ''Taarifa kwa Umma'' na nimevutiwa sana na kipaji chako cha kuongea na kuwasilina na watu ktk sherehe ya jana, nimekuambia tu mpango huu wa ofisi kama rafiki, siyo official, usimwabie mtu.Halafu akamuuliza Mkaka, ''unajua kutumia computer? da! wakati mkaka anataka kutoka jasho ajibuje-( maana hata kuaaply on line ilkua jaribu kule internet cafe), Boss akamuuliza ile pale ni program gani? (anamuonyeshea kwenye computer yake on the screen), bahati njema Mkaka alishajua/kariri kua kunapotokea viboma-viboma/mistari mingi inayotengeneza tuvyumba kwa monitor, hua ni excell, so akajibu ni excel, Mzungu akafurahi na kusema '''aaaaa safi kumbe unajua akasema basi sawa, itakapofika wakati, utahitajika.Mkaka aliona ivi anaota, anaona maono au ni kweli! hakuamini kwanza kuingia ofisi kubwa kama ile kisha kuambiwa yeye ni rafiki wa Mzungu wakati ndio kwanza walikutana usiku tu ktk sherehe na kisha kuaminiwa kwa  kuambiwa tip/ plan ya ofisi na kana kwamba hiyo haitoshi, akachukuliwa kwenda lunch ktk mgahawa mmoja wa bei ya juu Wilayani pale. Mkaka anasema, alivyokua amechoka namely nguo, viatu, kuingia na kukaa ktk gari ile safi ya VX za UN yenye mkonga wa satellite na mitambo ya ajabu ya radio call ndani, aliona  kama anachafua vile au wataghairi ghafla na  kumshusha, watoe gari jingine kumbeba.

Baada ya mlo, wakaagana, usiku NGO ile iliyowapa kazi, ikawapigia simu surveyors wote ku-report ofisini kabla ya kuondoka kila mtu na kwao. Walipofika, wakaambiwa wamapata maagzio toka UN agency kua, wanahitaji baadhi ya surveyors wabaki kusaidia NGO ile kuingiza data na ivyo, wanataka kuwafanyia interviews ili kupata hao wachache.Kesho yake usaili ukafanyika na kwakua ela waliyolipwa ilkua inaendlea kuishia ktk guest hata kusafiri to Dar bado, ikabidi waombwe watoe matokea siku iyo iyo.Wakaitwa na yakatangwa matokeo kua ni surveyors 4 wakabakizwa kama staff wa NGO ile na Mkaka akaambiwa '''yeye amepangiwa kazi nyingie si ktk NGO ile''. Wote wakatawanyika kurudi jijini. Maisha yakaendelea, ela waliyolipwa kule ikaisha kulipia madeni, sadaka, fungu la kumi, na kutuma nyumbani kidogo. Kukapita miezi 2 na nusu, Mkaka hoi, akawaza Mzungu amedanganya au alisema tu vile kwa changamko lake la nafsi? akajiuliza pia  baada ya interview ile mbona aliambiwa kua amepangiwa kazi nyingine? kuna nini sasa tena? akaendelea na kazi ya Bwana, kanisani sana na kufanya vikazi vya hapa na pale na hata kujaribiwa kuanza tena upya kutafuta kazi. Akarusha barua tena nyingi kama mwanzo na akaedelea ivyo mara kwa mara. Sku moja anatembea pale manyanya, ghafla simu ikaingia, kuangalia ivi, akaona namba ya simu land line, kupokea, akasikia ''habari? naongea na Kaka fulani? ndio. tafadhari kuna dharura, unaweza ukafika makao makuu hapa UN agency? kama huwezi, usijali hata kesho!'' aisee! Mkaka akasema kidogo adondoshe simu(kupokea ujumbe toka UN agency)! ''sasa ivi naja''- akajibu mkaka.Alikua ana akiba ya alfu 5 mfukoni, hakaamua kuchukua taxi mara moja alfu 5 mpaka makao makuu pale na hakujali kama atarudije.. Alipofika, ofisi ya HR ofisa akaanza kwa dhati na unyeyekevu kweli kumuomba msamaha kwa kua wali-misplace email na kwamba walitakiwa wamwambie miezi miwili iliyopita kua anatakiwa awe ameshafika Wilayani kule kama staff mpya wa UN agency. Mipango ikafanyika haraka. Mkaka akafika na kuanzi kazi. Toka NGO ya nchini na U-mc to UN agency. Hakuwahi kuwaza kazi njema aliyokua anataka iwe ya viwango ivyo, wala kufikiri hata siku moja kua nagekuja kua na CV yenye History ya kufanya kazi na UN agency. Kazi ilitakiwa ifanyike kwa mkupuo mmoja ivyo ivyo alipewa miezi mitatu contract lakini kwa neema aliyompa Bwana na kwa kua post ile ilkua ndio imeundwa/mpya, ktk utendaji kazi akawa na bidii na creativities hatimaye miezi mitatu ikazaa miaka 2 na miezi 2. Mshahara aliokua anapata na mafao yake baada ya miaka 2 na miezi 2, ilifanya baraka kubwa kwa maisha ya mkaka, familia na ukoo wao pia ktk nyumba ya Mungu na watu wake sana. Aliweza kusomesha/kuchangia gahrama za Wachungaji 6, yatima mmoja toka shule ya msingi mpaka sekondari mbali na michango mingine Sehemu kubwa ya baraka hii, aliingiza ktk kazi ya Bwana na watu wake na pia watu wa nyumbani kwake..Mbaii na mshahara, safari tu nje ya kituo cha kazi kama akija DAR, kila akilala na kuamka, laki 1,50,000, Kgm laki 1,43,000, wakati mwingine unakaa nje ya kituo mwezi mzima au 2! Mungu ana njia ya kulipa yote kwa muda mfupi si lazima kufanya kazi maika 30 ndio upate  sana, Bwana anaweza fupisha

Press on,( CONTRACT NA UN AGENCY ILIPOKWISHA, kawaida watu hurudi nyumba mara moja  kuanza biashara na mafao wanayopata makubwa na kutafuta kazi nyingine na hasa ukiwa na Cv yenye kuonyesha ulishafanya na UN inaku na upako wa aina yake kama ukipenda kazi za kuajiriwa. Wakati anajiandaa kurudi, UN  agency hao hao, MbInguni wakawakamata, wakafanya kitu cha ajabu kabisa, hakijawahi tokea na ni kinyume na utaratibu wa kawaida kwa UN system kote duniani, ilikuaje? nikipata muda tena nitakushuhudia jinsi gani uyo Mkaka Mungu alivyoamua kushughulikia mambo yake hata kama alipitia njia ya kukatisha tamaaa sana toka primary to Chuo to kutafuta kazi)


Fuatilia conclusion yangu ya maneno ya Mungu-nina-share maandko machache kwa next email mpendwa, nakutia moyo sana, sana kabisa, one day, you will write a book dada Salome hata kama unaona mbinguni kuko kimya, you will be suprised, a day is on the way kama ukikomaa na Bwana mpaka mwisho.

Stephen Mabinza

unread,
Jun 26, 2013, 4:31:53 PM6/26/13
to strictl...@googlegroups.com

Mpendwa Salome,

 

SAMAHANI, MIMI SIJAKUOMBEA ILI UPATE KAZI, NIMEKUOMBEA UPEWE HEKIMA!

 

Nimepita hapa na kuyaona Mahangaiko yako, kwa kweli unashida, naweza kuhisi unavyojisikia. Uhitaji ni “UGONJWA” mbaya sana, shetani huutumia mwanya kama huo kuwa mtego wake wa kwanza kabisa katika kuwaangusha watoto wa Mungu; NAKUTAKA UWE MACHO!

 

Ukipitia habari ya Ayubu ambayo ni ya kweli kabisa, na ni mfano halisi wa kipekee juu ya msiba huu wa ‘Uhitaji’,  shetani kitu chake cha kwanza alichofanya ni kumwambia Mungu kuwa “Ayubu, ni lazima aonekane kuwa ni mcha Mungu, maana wewe (Mungu) umemzingira kila mahali” kwa Msemo rahisi, Shetani alimaanisha tu kwamba ‘Ayubu ni mcha Mungu kwa sababu anakila Kitu cha ki mwili!’

 

Na Mungu katika kumthibitishia shetani kwamba, ‘Kuwa na kila kitu’ cha kimwili si sababu ya watoto wa Mungu kudumu katika ‘Ufalme wa Mungu’ ambao ni “Amani, haki na Furaha katika Roho mtakatifu” maana mambo hayo ndiyo husababisha  Ibaada halisi moyoni mwa mwamini; shetani aliruhusiwa amjaribu Ayubu, ndipo shetani alianza kwa KUMUONDOLEA NA KUMKWAMISHA AYUBU KWAKILA KITU cha kimwili alichokuwa nacho na alichokihitaji, kimoja baada ya kimoja alimnyang’anya! 

 

Si hivyo tu, pia rafikize Ayubu na mkewe, “walimwacha” kwa maana ya kwamba, hawakumtia moyo! Walimvunja moyo, na kumhukumu kuwa ni mwovu, walimuona Ayubu si CHOCHOTE kwa Mungu na kwa wanadamu, maana, mawazo ya wanadamu,  ni juu ya Mali na huwatanguliza Mbele Matajiri! Kwa Mtazamo huo huo, rafikize na mkewe walijaribu kuingiza Akilini mwa Ayubu wazo kuwa Mungu amemwacha ndiyo maana ‘KAMNYAMALIA KIMYA!’

 

Haraka za kupata majibu ama kufunguliwa katika uhitaji wa aina yoyote ile ni hamu na tamaa ya kila Mwanadamu, maana  huo ni Ubinadamu! Tunashuka moyo na kujiona si chochote mbele ya wenye “nazo” Hatuheshimiki na hatufikiriki kuwa tuna mawazo na ushauri mzuri, kwakuwa hatuna ‘Kitu’ cha ki mwili! Kweli ki mwili mambo huwa hivyo, lakini wewe mwana wa “Kiroho” hayakuhusu yote hayo, sasa, usivunjike moyo kwa ajili hiyo!

 

Salome dada yangu, kwakuwa naamini kuwa unayajua maandiko, kwa ajili hiyo sioni haja ya kunukuu mistari toka Biblia  (ila ukinitaka kufanya hivyo nitakunukulia),  Katika swala hili la “MTU KUWA NA KAZI YA KUFANYA”  SI JAMBO LA KUMUOMBA MUNGU! Ni jambo ambalo Mtu ameumbwa nalo, kwa hiyo huwezi kuomba kitu ambacho tayari unacho!  Wewe na mme wako kazi mnayo,  na hakuna andiko linalosema watu waombewe kupata kazi, ndiyo maana sijakuombea upate Kazi!  Salome dada, unaweza kunishangaa kidogo, kwa nini nimefanya hivyo, si kwamba nina roho mbaya kiasi cha kukuonea wivu ukifanikiwa, ama ukipata kazi ile unayoamini ndiyo kazi!

 

 Tumeshauriwa kuwa, jambo lolote likitutatiza, tuyaangalie maandiko! Yesu alipoulizwa katika hoja ya mtu kuwa na wake wengi, alijibu hivi “….lakini mwanzo haikuwa hivyo…mke mmoja mme mmoja…”Hebu tuone katika swala la mtu kuwa na kazi ya kufanya mwanzo ilikuwaje? Na wote tunajua kuwa mwanzo wa Maisha ya mwanadamu ni katika Bustani ya huko Edeni.  Biblia inasema  katika kitabu cha mwanzo 2:15 kuwa, 15BWANA Mungu akamchukua huyo mtu akamweka kwenye Bustani ya Edeni ailime na kuitunza”. Tunachokiona hapo ni kwamba mtu aliumbwa na kazi yake tayari ilikuwepo! Tatizo letu, ambalo naliona na wewe Salome unalo ni ‘kupata kazi ya aina Fulani’ lakini kiukweli, wewe hapo ulipo unayo kazi, ambayo ndiyo sababu ya riziki yako ya kila siku! Sambamba na hilo hebu soma ule mstari wa 16 unasomeka hivi, 16BWANA Mungu akamwagiza huyo mtu akamwambia, ‘‘Uko huru kula matunda ya mti wo wote katika bustani.”
 
Hebu jiulize, tangu 2001 hadi unailete shida yako hiyo mbele za Mungu, hujapata kula hata siku moja? Jua unakula kwakuwa una “Itunza Bustani” ya aina Fulani ambayo katika macho ya ufahamu wako imefichwa! Neno la Mungu linasema, “…Asiyefanya kazi asile..” Sasa, jiulize tena, kwanini unakula nawe unasema, hufanyi kazi? Huoni kuwa, kama unakula na hufanyi kazi unavunja Neno la kweli la Mungu?
 
Mimi naamini huvunji Neno la Mungu katika hilo la kula, kwasababu, wewe unayo kazi Fulani, maana kula kunaambatana na kazi Fulani ambayo Mungu alikupa, lakini si “kazi Fulani uitakayo!” Kula kunambatana na Kazi, na vyote hivyo Mungu amemuumba Mtu navyo, hupaswi kuyasumbukia kiasi hicho cha kulia mbele za Mungu, kazi ni kama chakula kipo kwa ajiri yetu, wala sisi hatujaumbwa kwa ajiri ya kazi na kula; Bali vyakula na kzi viliumbwa kwa ajili yetu! Kwa hiyo kazi unayo ndiyo maana unakula; Yesu alithibitisha kwa kusema kula wala kuvaa kusiwasumbue, hata Selemani na fahari yake yote, hajapata kuvaa kama, maua ya kondeni yanavyopendezeshwa kwa mavazi ya ajabu, wala Ndege wa angani hawajapata kukosa kula licha ya kwamba wao hawana Shambba (Hawafanyi kazi) tena hawana Ghara (Hawana maarifa / si wabunifu). Sembuse wewe Mwana wa Mungu mwenye mamlaka JITAMKIE NENO MWENYEWE KWA IMANI ITAKUWA TU!
 
Pamoja na sababu hiyo hapo, mimi niliona nikuombee upate “UHEKIMA” ambayo Mtu hawi nayo isipokuwa awe na Ufahamu na Maarifa.  Ndiyo maana shetani hufunga ama kuondoa Maarifa, ndiyo maana Neno linasema, “Watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa” Sasa, bila kuwa na uwezo wa ‘UFAHAMU’ (understanding ability) huwezi kuwa na MAARIFA – ambao ndiyo ngu ya kuendeshea Hekima (Knwoledge is power!), kwa hiyo ukiwa na Uwezo wa kufahamu mambo jumlisha na Maarifa ndipo unapata Hekima! (Understanding ability + Knwoledge = Wisdom  Kwa sababu, Maarifa ndiyo “Cement” kati ya Ufahamu na Hekima; Kwa maana hiyo, hakuna mwenye Hekina asiye na Fikra na maarifa! Umaarufu wa Selemani ulitokana na kuomba kwake HEKIMA, sote tunajua alivyokuwa ni mjuzi wa kubuni Biashara (Kazi) ambayo ilimfanya awe mkuu sana kiuchumi, si hivyo tu aliweza pia kuongoza visivyo vya kawaida! Pata Hekima ili ujue kubuni na kuifanya kazi itakayompendeza Mungu, ili aibariki nawe upate Furaha na mafanikio ya moyo wako!
 
NAKUTAKIA AMANI YA BWANA MBAYO ULIMWENGU HUU PAMOJA NA FAHARI YAKE HAUWEZI KUKUPATIA!


From: SELELI EDWIN <selel...@gmail.com>
To: strictl...@googlegroups.com
Sent: Wednesday, June 26, 2013 5:18 AM
Subject: Re: Ninaomba mpenyo kwenye maisha yangu

Gladys JB

unread,
Jun 27, 2013, 6:42:00 AM6/27/13
to strictl...@googlegroups.com
Mabinza,
Ningekuwa kwenye uhitaji wa kazi km dada Salome ningeona kati ya wenye roho mbaya wewe pia umo. Lakini kwa
meseji uliyompa huyu dada, imenifungua kwanza mimi kwa sehemu fulani ambayo nilikuwa cjagundua janja ya adui.

HEKIMA, hekima hekima, JIBU la mambo yote

Dada Salome umepewa jibu la Maswali yako yote.

Wana SG Hekima ni jibu la mambo yetu yote. Lakini unatakiwa uvumilivu wa kutosha
ili Hekima Atende kwako Apendavyo.

Mithali 8:14

Gladys



From: Stephen Mabinza <stephen...@yahoo.com>
To: "strictl...@googlegroups.com" <strictl...@googlegroups.com>
Sent: Wednesday, June 26, 2013 11:31 PM

Stephen Mabinza

unread,
Jun 27, 2013, 2:09:55 PM6/27/13
to strictl...@googlegroups.com
Gladys,

Tunatakiwa kusaidiana sisi kwa sisi, kwa moyo wote na kwa upendo ule ule kama tujipendavyo! Dada yetu Salome, amekwisha tushitaki kwa Mungu, Neno linasema, kama Ndugu yako akija kwako anahitaji mkate, mpe mkate, haifai kitu kumwambia aende kwa amani! Kama Salome angekuwa ameweka Email au Namba mojawapo ya simu yake, ninahakika jambo furani lingetukia. Naamini tumebarikiwa kwa viwango mbali mbali, Salome anatakiwa kufurahi kama wengine, ili Yesu akiuliza siku moja nilikuwa Sina ADA ya mwanangu,  Mlinipa? tujibu sote kwa pamoja Tulikupaaaa! Maana kila mmoja wetu angejishika kwa kadri ya kubarikiwa kwake, mwenye ushauri haya, mweny pesa haya, mwenye Anuani ya kunako Ajira haya mwnye kumtembelea haya nk, alimladi kila mtu aje apate cha kumwambia Yesu  "Mimi nilikupa BWANA"

Gladys, Heshima, utukufu na shukrani ziwe juu ya Mungu wetu, yeye anajua kufariji watoto wake, hata katika hali hii, Dada yangu Salome mtumaini Bwana!.


From: Gladys JB <ilovejesusch...@yahoo.com>
To: "strictl...@googlegroups.com" <strictl...@googlegroups.com>
Sent: Thursday, June 27, 2013 1:42 PM
Subject: Re: Ninaomba mpenyo kwenye maisha yangu
Mabinza,
Ningekuwa kwenye uhitaji wa kazi km dada Salome ningeona kati ya wenye roho mbaya wewe pia umo. Lakini kwa
meseji uliyompa huyu dada, imenifungua kwanza mimi kwa sehemu fulani ambayo nilikuwa cjagundua janja ya adui.

HEKIMA, hekima hekima, JIBU la mambo yote

Dada Salome umepewa jibu la Maswali yako yote. ys,

flano mambo

unread,
Jun 28, 2013, 1:50:47 AM6/28/13
to strictl...@googlegroups.com
Mabinza mwana wa Mungu, Bwana Yesu akubariki sana kwa mchango wako swadakta! hakika unapendeza yaani unatupandisha kiwango cha kumuelewa Mungu katika neno lake. Binafsi nimechota kile ulichokuwa unamuelekeza dada yetu mpendwa Salome. Hakika inapendeza.

Mbarikiwe

Flano


Sent: Thursday, June 27, 2013 9:09 PM
Reply all
Reply to author
Forward
0 new messages