Je kuna mahali na namna ktk Neno tunawezapata KWELI ili kupinga na kukosoa tabia hii kua ni mbovu sana na haifai kwa Mtu SERIOUS anayekwenda Mbinguni? hasa inavyoshamiri ktk baadhi ya Nchi zilizoendelea na hata zinazoendelea ktk Miji na Majiji Makubwa ya Kibiashara na yenye Watu wenye mishe-mishe mingi?
Kama kuna ubaya au kosa, madhara yake nini haswa kiroho na kitumishi hata ki-imani? Je mnaweza fundisha/rekebisha/onyesha kitu gani so SERIOUS ikiwa kuna tatizo kubwa ili Kanisa lipone?
Je Kitu gani anayekwenda LIVE ibadani anapata Zaidi kuliko anayekwenda Ibadani ELECTRONICALLY/KIDIGITALI? Yaani wa Kijitari akishiriki kila kitu kama kutoa sadaka-kwa mpesa/Bank Ac ya Kanisa, Fungu la ten au twenty au mbili au M23,kuimba na kusifu kwa kufuata hao hao waliopo LIVE Kanisani pale, kusikiliza Neno na kuitikia ya madhabahuni, kutumika kwa yale yatatangazwa kua kuna hiki na kile kinahitaji kiki kile nk? Nini tofauti yake na yule wa LIVE ibadani pale?
Kwa hoja zipi haswa tunaweza kumfundisha huyu wa kushiriki Ki-TV/RADIO/LINK/MEDIA NYINGINE za Ki-internet na satellites kua ana matatizo tena makubwa sana kiroho?
Upande wa PILI, vipi yule anayeshiriki kwa kutumia IBADA YOTE lakini ILIYOREKODIWA akaja kusikiliza na kuona baadaye si LIVE kama mwenziwe nambari one juu pale wa kidijitari pia? Kuna mambo atakosa kwa kua ni recorded Ibada?
Jaribu au Jibu maswali yote au lolote unapenda na kuweza na kama una kitu unataka kufundisha/shirikisha Watu hapa.
Press on,
Edwin Seleli