Ameen,barikiwa mtumishi
----------
Sent from my Nokia phone
------Original message------
From: Patrick Kamera <
pka...@gmail.com>
To: <
strictl...@googlegroups.com>
Date: Friday, June 14, 2013 4:19:56 AM GMT-0400
Subject: KUMFUATA KRISTO BILA KUJIKANA HAIWEZEKANI
34 Akawaita mkutano pamoja na wanafunzi wake, akawaambia, Mtu ye yote
akitaka kunifuata na ajikane mwenyewe, ajitwike na msalaba wake, anifuate.
35 Kwa kuwa mtu atakaye kuiponya nafsi yake, ataiangamiza, na mtu
atakayeiangamiza nafsi yake kwa ajili yangu na kwa ajili ya Injili, huyu
ataisalimisha.
36 Kwa kuwa itamfaidia mtu nini kuupata ulimwengu wote, akipata hasara ya
nafsi yake?
37 Ama mtu atoe nini badala ya nafsi yake?
38 Maana kila mtu atakayenionea haya mimi, na maneno yangu, katika kizazi
hiki cha uzinzi na dhambi, Mwana wa Adamu atamwonea haya mtu huyo,
atakapokuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika watakatifu. – *Marko
8:34 -38 SUV*
Mara zote tunaona mkutano mkuu au umati ndio unamfuata Bwana Yesu, lakini
hapa mambo yalikuwa tofauti, Bwana Yesu mwenyewe aliwaita mkutano ambao
bila shaka ulikuwa ni watu wengi tu, pamoja na wanafunzi wake kwani alikuwa
na jambo la muhimu sana, jambo la msingi kabisa la kuwaambia. Tukumbuke pia
hapo nyuma kidogo walitaka kumfanya mfalme baada ya muujiza alioufuanya wa
kulisha wale wanaume 5000 bila kuhesabu wanawake na watoto, naye alifahamu
hilo akawakwepa. (*Yohana 6:15*)
Hakutaka waendelee kumfuata huku wakiwa na agenda zao wenyewe au mategemeo
yao wenyewe ya kubweteka na kula mikate na samaki bure tu na kupokea
miujiza ya uponyaji na mahitaji yao wao tu. Hapana., alitaka kuweka wazi
lengo la kuja kwake na ya kuwa kumfuata yeye kutawagharimu vyote iwe ni
umaarufu, heshima au hadhi zao katika jamii, kupendwa na watu n.k. Mahali
pengine alisema “mtachukiwa na watu wote kwa ajili ya jina langu…”
Ni vizuri tukumbushane kuwa kumfuata Bwana Yesu ni kutangaza vita na
shetani, atafanya kila awezalo kujaribu kutukatisha tamaa lakini kama Neno
lisemavyo tunamshinda kwa Damu ya Mwana Kondoo na kwa Neno la ushuhuda
wetu, isitoshe tumepewa mamlaka ya kukanyaga nyoka na nge na nguvu zote za
yule adui na wala hakuna kitakachotudhuru. (*Luka 10:19*)
Hivyo basi kama mtu umeamua kumkiri Bwana Yesu kama Bwana na Mwokozi wako,
basi mfuate kwa moyo wako wote ukitambua ukweli huo, muda wa kujibaraguza
na kuchezacheza na dhambi haupo, usiku umeenda sana alfajiri ndio hiyo
inawadia, Bwana Yesu yuko mlangoni, amka wewe usinziaye....
Tukifanya uamuzi wa dhati kabisa wa kumwishia yeye, Mungu ni mwingi wa
neema na rehema naye ni mwaminifu, atatuwezesha na kutufanikisha kusimama
katika Kristo ila hatatulazimisha hata siku moja.
Maneno ya Bwana Yesu ni Roho tena ni Uzima, kutokuyazingatia ni
kutokujitakia mema…asomaye na afahamu!
Mbarikiwe na Bwana Yesu,
Patrick
--
Tafadhali zingatia msingi wetu ni Neno la Mungu, Lengo letu Kuujenga mwili wa Kristo, kushirikiana, amani na upendo. Yeyote yuko huru kuchangia, kufundisha, kukubali kufundishwa sawasawa na Msingi wetu Mkuu Neno la Mungu. Kujiunga na Team ya Injili au Maombi wasiliana nasi kwa simu 0714 915 424. Tuma Email.
strictl...@yahoo.co.uk Facebook:
https://www.facebook.com/pages/Strictly-Gospel/363180289370
Blog:
www.strictlygospel.wordpress.com
Kujiondoa Kwenye Kundi Hili Tuma Email:
strictlygospe...@googlegroups.com