MTU WA MOYONI MWAKE AU AMPENDAYE MUNGU YUKOJE-KOJE?

65 views
Skip to first unread message

Seleli Edwin

unread,
Jul 14, 2014, 9:04:00 PM7/14/14
to strictlygospel
Amani ya Mungu Baba iwe pamoja nanyi enyi nyote,

Ni kusudi la Somo/Mada hii TUWE MATAJIRI WA MAANDIKO/MANENO YA MUNGU NA UFAHAMU SAHIHI WA KWELI ZA MUNGU ivyo tule Neno hadi tushibe tikitiki. Uwe huru kwa raha zako kuleta majibu ya jumla, Akili za kawaida, Ujuzi, Uzoefu, Ushuhuda, Ki-huduma na Karama ila ZAIDI SANA, leta NENO.

Tusome Maandiko kwanza!1 Samuel 13:13-14: 13 And Samuel said to Saul, You have done foolishly! You have not kept the commandment of the Lord your God which He commanded you; for the Lord would have established your kingdom over Israel forever;14 But now your kingdom shall not continue; the Lord has sought out [David] A MAN AFTER HIS OWN HEART and the Lord has commanded him to be prince and ruler over His people, because you have not kept what the Lord commanded you.NOTICE: ‘’A MAN AFTER HIS OWN HEART’’

Mdo. 13:22...Na alipokwisha kumwondoa huyo, akamwinua Daudi awe mfalme wao ambaye alimshuhudia, akisema, Nimemwona DAUDI, mwana wa Yese, mtu  ANAYEUPENDEZA MOYO WANGU, atakayefanya mapenzi yangu yote. NOTICE: ‘’ANAYEUPENDEZA MOYO WANGU,’’

MASWALI YA MUONGOZO KTK KULA MKATE HUU:


Maelezo: Daudi aliua sana hata Mungu akamkatalia kumjengea Nyumba maana mikono yake imejaa damu-yaani una nia njema mno ya kufanya kitu cha Mungu lakini unakataliwa kwa sababu ume KILL mno/wengi- (1 Nyakati.22:8) na pia alichukua Mke wa Mtu kikatili sana kwa kumsakizia Mume-Uria Askari wake apangwe mstari wa mbele vitani ili auwawe na kisha Rais Daudi awe naye 24/7 Wife wa Mtu-Askari wake wa nguvu ila marehemu mtarajiwa/msakiziwa- 2 Samweli: 11 sura yote. Alisuka mpango huo wa kuua Askari wake baada Mfalme kufeli mara 2 kuficha mimba aliyompachika Mke wa Askari wake. Alimuondoa Askari huyo uwanja wa vita ili arudi nyumbani na akalale na Mkewe ili amsakizie ‘’bebi to be born’, lakini kajamaa-Kaaskari kalikua very committed na Kazi ya U-soja, akataa kwenda kwa starehe kwakua wenziwe wako vitani-ktk huduma VERY SERIOUS YA KULINDA/KUTUNZA USALAMA WA NCHI UHAI WA WATU WAKE


Rais hakuchoka, akaandaa bonge la menyu ili Uria anywe haswa na Biblia inasema kwa Kiingereza… ‘’HE MADE HIM TO DRINK-yaani akakusudia Askari wake huyo ‘agonge ‘Kilimanjaro Premier Lagaa’ za enzi zile nyingi ili imulaghai na akate net works kichwani, apoteze usmart wa kuwaza na kuamua vema kwa  vipao mbele vipi vianze na vipi vingoje, iyo impelekee aende kulala na kufanya mapenzi na Mkwewe. Ingawa kweli inaonekana alizigonga chupa vema lakini, usoja- discipline na kutetea Nchi yake ilikua ni huduma ya moyo wake haswaaa na ivyo akakwepa kwenda nyumbani aliko Wife wake. Sasa Daudi kwa kupanic siri kumbuluka, kwa ukatili mwingine akaandika barua spesheli na kumpa Uriah-huyo huyo mume wa Mtu-Askari wake ili kuipeleka kwa Jemandari wa Vita uwanja wa mapambano-kumbe ndani ya hiyo barua ya Ikulu ndio kuna mpango mzima wa kumkata oxgen for real and forever.


Maswali:


MOJA: Upendezeshwaji wa Daudi kwa moyo wa Mungu,  Je, ulikua wakati kako kadogo-kadogo kakijana mwororo kanachunga Kondoo za Baba yake na hakajajua hata ..‘I love u gal kwa maneno na kitandani’’ yaani  wakati ule kanaua dubu na Goliati kwa Jina la Bwana au ni maisha yake yote hata wakati ameshakua Rais  na kupiga faulu nyingi tu za kufa Mtu?


PILI: Mungu aliposema ‘Mtu aupendazaye Moyo wangu’ na kwa kua Mungu anaona na kuhitimisha mambo tokea Mwanzo kwa hivyo si kwamba anajua jambo wakati tukio limetokea, inakuaje au ni kwa nini amuite Mtu wa dizaini hii kua ni Wa Moyoni/anayependeza Moyo wake?  Kuna siri gani? Nin spesheli yake huyu Rais?


TATU: Toa maandiko yanayoonyesha History njema-CV yake upande mzuri wa Daudi ili labda kwa hicho ndio tuone Mungu alimaanisha nini kusema huyu jamaa na mafualu yake ya hatari, imekuaje awe kipenzi ‘kyake kya moyo?’


NNE:  Kuna Mtu yoyote ktk Biblia ambaye Mungu ameshawahi mtamkia kua ni ‘’Mpendwa/Mpenzi wa Moyo wake?’’ Au ‘’Anapendwaza naye?’’, Mtaje na tupia andiko ili tuwe matajiri wa kuyajua maandiko mengi kwa mambo mbalimbali


TANO: Unawalinganishaje( similarities and differences) hao Watu Wengine namba 4 na maisha ya Daudi upande wake mwema si ule wa mafaulu ya kutisha?

 

Press on eating and drinking the Bible, Amen.


Edwin Seleli

Gladys Simtitu

unread,
Jul 24, 2014, 8:19:14 PM7/24/14
to strictl...@googlegroups.com
Mpendwa Seleli,
Nataka nipite kwa haraka ila kwa wasomaji wazuri wa Biblia watanielewa.

Kilichoupendeza moyo wa Mungu kwa Saudi ni ule wepesi wa moyo wake kuiendea toba bila kujali watu, aina ya kosa wala wadhifa wake.
Mfano: Sauli alipokosea kutii agizo la MUNGU JUU ya kuwaua Amaleki wote alipoulizwa alisema niliogopa hawa watu. Alipoamua kutoa sadaka kabla Samwel hajafika alipoulizwa alisema niliogopa hawaoi watu wasije wakatawanyika wakaniacha, Hata Samwel alipokataa kushiriki sadaka yake,
Alimshika joho na kumwambia rudi uombe nami usiniaibishe b4 hawa watu etc. So utaona kwa sehemu kubwa Sauli alitenda huduma yake kwa kuwaangalia watu na kujali heshima yake b4 men. Kinyume chake, Daudi alipozini na kuua alipoanbiwa kwa jinsi ya hekima kuwa aliyetenda Kisha like alistahili mauti am aye ni yeye, pale pale alianguka magotini b4 nabii ( ambaye kwa cheo David was his King) na kusema nimemtenda Mungu dhambi. Hata alipofanya sensa ya watu wake Mungu akaamuru tauni, Daudi alipopewa msg na malaika alisema, gari niangukie mikononi kwa Mungu kwa ni kwake niko rehema na gari BWANA aiadhibu nyumba ya baba yangu than Israel hawa Wa sio na hatia kwani nimetenda kwa upumbavu.Mungu akaghairi adhabu ile. Kumbe kwa uchache utaona makosa ya Saudi Ulikuwa ni mengi naakubwa than Sauli lkn Daudi alijaa moyo wa toba. Ndio sbb Mungu alipendezwa naye. Daudi haakufanya jambo for men but for God. Saul alifanya for men not for God.
Nimejaribu tu.

Gladys
--
Tafadhali zingatia msingi wetu ni Neno la Mungu, Lengo letu Kuujenga mwili wa Kristo, kushirikiana, amani na upendo. Yeyote yuko huru kuchangia, kufundisha, kukubali kufundishwa sawasawa na Msingi wetu Mkuu Neno la Mungu. Kujiunga na Team ya Injili au Maombi wasiliana nasi kwa simu 0714 915 424. Tuma Email. strictl...@yahoo.co.uk Facebook:https://www.facebook.com/pages/Strictly-Gospel/363180289370
 
Blog: www.strictlygospel.wordpress.com
 
Kujiondoa Kwenye Kundi Hili Tuma Email:
strictlygospe...@googlegroups.com

Siaka Nyanchiwa

unread,
Jul 28, 2014, 10:23:08 PM7/28/14
to strictl...@googlegroups.com
Seleli kaka,
  ubarikiwe kwa changamoto unazotoa maana ni kweli na za kusisimua kufanya mtu asome biblia mara mbilimbili kujibu hoja kwa umakini.
ubarikiwe sana. na kuzidi
 
Siaka S. Nyanchiwa
   Internet cafe and
College Controller
P.o Box  70 Serengeti, Mara, Tanzania.
P.o Box 417 Tarime,Mara, Tanzania.
Contacts: sian...@yahoo.com/sian...@gmail.com.
Mobile:+255755527476.

Seleli Edwin

unread,
Jul 28, 2014, 10:23:08 PM7/28/14
to strictlygospel
Gladys,

Kwakua umesema umepita haraka, Nakuhamasisha, ukipata muda tulia hapa kwa huduma/Kanisani, toa moyo na yale Mungu amekujaza KWA KADRI YA MADA NA FLOW YAKE-maswali yake. Kindly isome tena kwa utulivu utakapoamua kuja na muda wako Ibadani hapa. Na labda kusaidia baadhi ya Wasomaji wa comment yako wasipoteze point yake, wajue ivi kua kila ulipotumia neno ''Saidi''- ulimaanisha ''Daudi''  na si ''Sauli''

Just to make this discussion wide and very educative  making you do a little extra mile job, nauliza hili

Kama moyo wa Toba na Kunuia kumpendeza Mungu tu/kwanza ndio kitu kilimfanya Mungu kupendezwa na Daudi au yeye kua Mtu wa moyoni mwake Mungu, mbona hiyo quality hata sisi wengi wetu leo,  Waliookoka tunayo? mbona Wafalme wengine walikua na toba haswaa, yuko hata Kornelio aliyekua hajaokoka yet sadaka na maombi yake Mbingu iliguswa hata kusababisha emergency plan ya kumuokoa kabisa tu sasa kieleweke moja, kwa mantiki hii, NINI USPESHELI WA DAUDI aise ON VERY SERIOUS NOTE? More job is needed hapo

Press on,
Edwin Seleli

Seleli Edwin

unread,
Aug 6, 2014, 12:16:37 AM8/6/14
to strictlygospel
Siaka,

Yes my friend, God bless u and ashukuriwe Yeye atuwezeshaye kwa kweli. Nimependa hiki umesema hikiiiiiiiiiiiiii..''''changamoto unazotoa maana ni kweli na za kusisimua kufanya mtu asome biblia mara mbilimbili kujibu hoja kwa umakini''', aiseeee wewe kwa kujua au la, umeona Nia ya Utumishi na kuhudumiana nakokufanya humu kwa kupenda na moyo mwaka wa  2 sasa na zaidi kwa juhudi nyingi bila kuchoka kwa heshima ya BWANA aliyetukusanya hapa, na love tu niliyonayo kwenu kama Ndugu ambao yote yatapita halafu one day, tutakaa mbingu na Maskani moja na Baba.

Ndio maana hata chini ya mada nimetoa maswali na moja wapo ni hili..'''

NNE:  Kuna Watu/Mtu/ yoyote ktk Biblia ambaye Mungu ameshawahi mtamkia kua ni ‘’Mpendwa/Mpenzi wa Moyo wake?’’ Au ‘’Anapendwaza naye?’’, Mtaje na tupia andiko ili tuwe matajiri wa kuyajua maandiko mengi kwa mambo mbalimbali''. Sasa best embu gonga mzigo hapo kisha leta jibu, amen? good, nina/tunakungoja utulishe Mtumishi


Press on,


Seleli

Emmanuel Nshimirimana

unread,
Aug 18, 2014, 12:14:14 AM8/18/14
to strictl...@googlegroups.com
Ndugu mpendwa Seleli Edwin Bwana Ysu akubariki sana. Sasa sipatikani sana nimehamishiwa mbari na mji wa Bujumbura sasa siyo rahisi kupatikana na kupokea michango yenu ktk maisha yangu ya kiroho. Sasa ninadokowa dokowa tu!

Sasa ninapenda nichangiye kwa mada hii.na ninaamina Roho wa Mungu atatuongoza kuelewa.
Swali 1.Upendezeshaji wa Daudi kwa moyo wa Mungu, hawukusimama juu ya utakatifu wa Daudi. Kipindi kile Sauli hakutimiza maagizo ya Mungu basi Mungu hakupendezwa na uasi wa Sauli. Basi kama Mungu akasema anajipatia mwengina anaeweza kuyatimiza maagizo yake katika kazi ile ya kuongoza Israel na kuwapiga makafiri (adui wa Mungu) sasa kwa kuwa Daudi alikuwa na moyo wa uchungaji( ukiona jisi gani alifatalisha maisha yake kwa kupigana na dubu na simba kwa ajili ya wana kondoo) unaona kweli kwamba yeye alikuwa tiyari kupigania taifa la Mungu. Kwahiyo Daudi amependeza moyo wa Mungu sababu alikuwa muaminifu kwa kazi yake.
Kama angegeuka tu! naye Mungu angemuacha. Kumbuka na mwanae Sulemani alipendwa na Mungu sana tangu kuzaliwa kwake mpaka akamuita jina la kuyadhibitisha (Yedidiya).2 Sam.12:24-25. Alipoacha maagizo yake Mungu amemuacha.

2. Kwa maoni yangu kitu special cha Rais huu ni kwamba amezingatia wito wake.

3.Ninaandi baadhi ya maisha yake ya kiroho, lakini haimaanishe kwamba yeye alikuwa mtakatifu kuliko wengine, maana na mengi yake mabaya yaliandikwa.
- Daudi Alimutegemea Mungu tu. 1 samuel17:45-47 Zab.27:1-6
- DaudiAlimutumainia Mungu tu. Zab.25:2
- Dudi Alijuwa kumusifu  Mungu 1 Mambo ya nyakati 16 2 Samuel 6:18-22
- Daudi aliheshimu aliheshimu upako wa Mungu 1 Samuel 24:5-6; 26:9-11
- Daudi alikuwa na moyo wa kutubu 2 Samuel 12:13 Zab.32:1-5 ZAb.51.
Kwa Zaburi hii ya 51 mwenyewe anakiri kuwa alizaliwa na dhambi sawa sawa na kila mtu.

4. watu wengi Mungu ameongea nawo maneno ya kuonyesha jisi moyo wake ulivyo juu yao. kwanza kuna wengi ukichunguza maneno ya Mungu juu yao ni mazito sana kuliko ya Daudi. kwanza Daudi hajaambiwa na Mungu bado; ni Samuel alimuambia Sauri.
Mufano: Nabii MUSA . Huu ni mtu Mungu amemuteteya sana na kuonyesha yeye ni nani kwake. Kumb.34:10 wala hajainuka tena katika Israel nabii kama Musa  ambaye Bwana alimujuwa USA kwa USO.

Hesabu 12:8 kwake nitanena mdomo kwa mdomo maana wazi wazi wala si kwa mafumbo; na umbo la Bwana  yeye ataliona. Mbona basi ninyi hamkuogopa kimnenea mtumishi wangu huu Musa?
 Kutoka 33:11 naye Bwana akasema na Musa USO kwa USO kama vile mtu asemavyo na rafiki yake...

Tumuone Daniel.
Daniel 9: 23 Mwanzo wa maombi yako ilitolewa amri ;nami nimekuja kukupasha habari; maana wewe UNAPENDWA SANA
Daniel 10:11 Aka niambia Ee Daniel MTU UPENDWAE SANA.
 Ninaposoma maneno haya, ninamuona mmaraika akimuambiya Daniel akihakikisha upendo aupendwao. Upendo wa Mungu maana ujumbe amepewa na Mungu Mwenyewe siyo nabi ao mtu mwengine. ninaona uzito kuliko maneno yale ya Samuel.
Tulisoma sana habari za Ibrahimu babu wetu nazo zinasisimuwa mpaka Bwana akakubari kula ugali wake!!!!


Tuone Agani jipya
Yesu alisema Directly " nimewaita Rafiki zangu.." Yoh.15:15 "...Baba anawapenda.." yoh.16:27 na maandiko mengine.

5. katika maisha ya kiroho na huduma;  hatuwezi kumulinganisha huu na huu maana kila mtu ni specil katika maisha ya wito wake. Akkiwa mwaminifutui yatosha.
Mwana muziki anaweza kuwa wa kusifika sana lakini huwezi kumuita raisi, na raisi akifanya kazi yake kwa sifa nzuri huwezi kumuita Doctor na Doctor hawezi kuwa fundi wa mbaho. lakini wote tunawahitaji kwa maisha na maendeleo ya nchi.
Na kwa kiroho kila mtu akiwa mwaminifu kwa wito wake atakuwa na sifa nzuri. nina mufano mudogo tu katika kitabu ca Hesabu 25:10-13 mtu huu Fenehansi ukisoma utaona jinsi gani Mungu amemusifu kwa kazi alifanya kwa dakika ndogo tu.
Tuone ginsi gani tena Yesu amekataa mambo ya kulinganisha. Yoh.21:21-22 Petro alitaka ajuwe habari za Yohana na Yesu alimukemea.
Basi sehemu yangu ya kuchangia ni hii na ninakuhitaji tena.

Shukrani zangu kwako mpendwa kwa njia gani utapokea uchangiaji huu. na Bwana akubariki sana.
Reply all
Reply to author
Forward
0 new messages