MUNGU ANAWASILIANAJE/ONGEAJE/ZUNGUMZAJE NA MWANADAMU?

77 views
Skip to first unread message

Seleli Edwin

unread,
Jun 18, 2014, 9:06:57 PM6/18/14
to strictlygospel

Amani ya Bwana iwe pamoja nanyi enyi nyote.


Hili ni somo siyo mada na nimekusudia kupitia ninyi wote Watu wa Mungu wa Kanisa letu jema sana lililotupa faida kubwa na ambalo wa kwanza wao kusaidiwa na kupewa faida na ufahamu wa ajabu na mtamu mno wa mambo ktk NENO LA MUNGU, ni mimi. Yako mambo nilikua sijui kabisa yaani completely zero na pia mengine nilikua najua vibaya na mengine nilijua kwa ufahamu mdogo sana, na mengine nilijua vema sana ila nikaongezewa kitu kingine bora zaidi hivyo hakika Kanisa letu ni baraka na ninyi ndio wenye kubeba baraka izo mnaposaidia Watu kujua mambo ya Mungu zaidi na ziadi, I BLESS U ALL.


Sasa turudia kazini/hudumani….. HILI NI SOMO MUHIMU SANA, SANA KABISA KWA MTU WA MUNGU ILI TUWEZE KUA SALAMA, TUFANYE MAAMUZI SAHIHI, TUFANYE HUDUMA BORA SANA, TUENENDA KTK RAMANI YA MUNGU NA HATA KUJUA MAPENZI YA MUNGU KWA HAKIKA KWA YALE AMBAYO HAYAJAANDIKWA WAZI WAZI KTK NENO


Sitafundisha hili somo lote A-Z ila nitachokoza kwa kuweka skeleton, ninyi nyote jazeni nyama. Kwa kusoma Maandiko, vitabu kadhaa na uzoefu kiasi tu wa misha yangu mwenyewe na wa kihuduma na ibada, nimefahamu kua Mungu huzungumza/ongea/wasiliana na Watu tena pia hufanya ivyo kwa wote wawe wameokoka-wamejaa Roho Mtakatifu au la, wanaomjua au la na njia anazotumia ni kama izi(waweza ongezea nyingine…)


MOJA: Neno-Matendo na Maneno ya Mungu yaliyoandikwa ktk Bible, usomapo, unasoma taarifa/maneno yake hivyo ndivyo anawasiliana nawe


PILI:Sauti ya Wazi-masikio ya kibidamu yanasikia kabisaaa au Sauti ya Ndani-masikio ya kiroho ndio yanasikia, Roho Mtakatifu ananema ndani yako


TATU: Kukiwapo Amani,ushwari na utulivu ndani ya Moyo-kwamba ukihisi iyo hali basi unachowaza/panga Mungu amekitiki, endelea nacho


NNE:  Kutokuwepo kwa Amani, Ushwari na Utulivu ndani ya Moyo- kwamba ukihisi iyo hali basi unachowaza/panga Mungu hajakitiki, usiendelea nacho, acha mara moja


TANO: Msukumo, msisitizo, muhamasisho au mzigo wa moyoni- unapata kitu moyo halisi kweli juu ya jambo fulani na hakikuachi hadi unajua kabisa kua una jambo moyoni si la kawaida


SITA: Ndoto- ukiwa umelala-unaona vitu/picha/sikia sauti


SABA: Maono ya wazi-kuona kama TV both ukiwa umelala au hujalala au ya ndani-rohoni/moyoni kitu/jambo linakua la uhakika sana


NANE: Kwa ishara ktk mazingira ya Nje-Mungu anafanya jambo ktk mazingira yako


TISA: Watu- Wanaongea mazungumzo ya kawaida tu au Mtu ana hubiri/fundisha Neno, kupitia hayo, mambo fulani yananatishwa/kua na nguvu na maalumu sana na binafsi kweli kwako


KUMI: Wanyama-Mungu kutumia Mnyama mfano Punda kusema na Mwanadamu


KUMI NA MOJA: Wazo-Mungu kukuingizia/angushia Wazo ndani yako au hata ktk akili/ufahamu wako

Karibu ulete Ushuhuda, Maandiko au ufafanuzi kwa njia izo juu pia uzoefu wako wa kutembea na Mungu na uliyosikia kwa wengine, lini na namna gani Bwana alisemaga/anaongeaga nawe/nao?


Press on,

Edwin Seleli

flano mambo

unread,
Jun 25, 2014, 8:30:14 PM6/25/14
to strictl...@googlegroups.com
Sure Kaka Seleli,
Nimeipenda hiyo article yako. unajua kuna shidakubwa kanisani kwa wana wa Mungu kujua namna Mungu anavyowasiliana na wanadamu. Hata kuna kipindi mimi nilikua nikimsikia mtu akisema Mungu akasema nami au akaniambia yaani nilikua namuona mwongo, mzushi na mtu anayejitafutia masifa tu. 

Lakini baada ya kujifunza, Mungu husema nasi tena yu mwepesi wala si mzito ishu ni sisi na ving'amuzi vyetu vya kiroho. Barikiwa sana mtu wa Mungu

Flano


--
Tafadhali zingatia msingi wetu ni Neno la Mungu, Lengo letu Kuujenga mwili wa Kristo, kushirikiana, amani na upendo. Yeyote yuko huru kuchangia, kufundisha, kukubali kufundishwa sawasawa na Msingi wetu Mkuu Neno la Mungu. Kujiunga na Team ya Injili au Maombi wasiliana nasi kwa simu 0714 915 424. Tuma Email. strictl...@yahoo.co.uk Facebook:https://www.facebook.com/pages/Strictly-Gospel/363180289370
 
Blog: www.strictlygospel.wordpress.com
 
Kujiondoa Kwenye Kundi Hili Tuma Email:
strictlygospe...@googlegroups.com


Emmanuel Nshimirimana

unread,
Jun 25, 2014, 8:30:15 PM6/25/14
to strictl...@googlegroups.com

Amen and Amen



--
Reply all
Reply to author
Forward
0 new messages