Hellow SG,
Kidogo inauma lakini inabidi iwe ivyo, interesting indeed, kindly read to the end .Nawaza kua ingawa generally speaking as rule of the Bible,
twapaswa kutoa, lakini ni hekima ku-apply ukweli mwingine wa kuongozwa na Roho Mt
SPECIFICALLY ktk occasions fulani kabla
hujatoa hasa utoaji kama changizo, au wa kuwapa watu vitu, msaada, ku-sponsor
mambo ya Mungu, watu/watumishi wake, kutenda wema au kusaidia jambo. Kuongozwa
specifically kutamuacha mtoaji salama kiroho(moyo wako wa ukarimu na kujali
watu husigeuke kua mtego au wengine wenye nia zao kukuingiza matatizoni na pia
kimwili kubaki salama( watu wakijua unazo- ziwe nyingi au ndogo ili mradi
unaweza ukafanya jambo, wanaweza kula njama kukufanyizia au hawataisha kukufuata-fuata
kila mara kwa mahitaji yao ya kweli na
wa uwongo mpaka inakua kero/karaha
na makwazo.
Kuna Mkaka mmoja, anapenda sana kujali, hurumia ivyo, akutanapo na mhitaji au akifuatwa na mhitaji, hata kama hana jinsi wakati huo kusaidia, huweza hata kuji-sacrifice kukopa mahala kutatua tatizo la mpendwa au ndugu tu wa damu, jirani, kisha kulipa baadae, raha yake yeye ni kuona ishu iliyokua ina mbana mpendwa, jamaa imekwisha na yeye kafanyika kua sehemu ya suluhisho. Mkaka huyo anajijua ivyo kwa hakika ndani yake jinsi Mungu alivyomuwekea software iyo ya kutoa iwe mali, pesa, muda,moyo, vitu, ushauri yaani utoaji wa aina yoyote ili mradi mhitaji apate ahueni. Siku moja, aka-spot watoto wawili wa mpendwa ambao kila mara akiwaona ibadani, mikeshani, mifungo, seminar, wana nguo zile zile, watu wakikaa kunywa chai, soda baada ya ibada ya kwanza, wao wako pembeni tu, wanatamani kunywa chai,soda kama watoto wa wengine but no money na mama yao, hubaki kanisani tu maana aende nje kufanya nini ilihali hana ela ya kuwanunulia watoto wake na yeye mwenyewe.Mkaka yule akawaita siku moja na kuwapa ofa.Namna mtoto mdogo kati ya hao wawili alivyokamata chupa ya soda ya fanta baridi na kuipeleka mdomoni na kuanza kuimimina kwa throat, huhitaji ufunuo KUONA kua something has been terribly wrong or missing maskini. Wakanywa, kula na kufurahi kweli. Siku nyingine Mkaka huyo akawapa tena ofa na sasa kila j2 almost huwapa ofa ya chai na soda au juice, simple breakfast tu (chai ya strungi na maandazi au sconzi au chapati na wanashushia na soda u juice. Siku nyingine Mkaka akawachukua kwa mitumba market kule Karume na akawaambia wachangue kila wanachopenda kuanzia viatu,mashati, bukta, flana, jeans,makoti, kofia nk, walijimwaga kweli kuchagua, hawakuamini hayo yalikua yanatokea kweli. Siku izi wana-shine, wanabadilisha nguo na viatu, wana raha na furaha kweli na wamuonapo Mkaka uyo, wanasikia kupendwa kweli na wamependa sana mambo ya kanisa, huduma na bila shaka love yao kwa Bwana wao/wetu imeongezeka kama siyo kua revived greatly.
Siku moja Mkaka akapata sms toka kwa Mama yao ambaye ni single mother, aliyewahi kuolewa mara mbili, kua anataka kumuona, wakakutana na baada ya kushukuru na kubariki yote Mkaka aliyofanya, akasema jambo ambalo ilimchukua dk kadhaa kulitamka uku akitoa machozi, ‘TOKA NIZALIWE NA BAADA YA KUOKOKA, SIJAWAHI KUKUTANA NA MWANAUME ALIYENIONYESHA UPENDO KWA KINA HIKI, SIKUWAHI KUWAZA KATIKA KANISA KUBWA KAMA HILI NA LENYE WAHITAJI WENGI PAMOJA NA YATIMA,ANGETOKEA, MTU WA KUFANYA ALICHOWANYIA WANANGU, NIMEKUA NAKUOMBE SANA KWA MUNGU KWA UTOAJI WAKO NA UPENDO NA AMBAO WANANGU WAMENIAMBIA KWA MACHOZI, NA KILA MARA LAZIMA WANIPE HABARI ZAKO. HATIMAYE MOYONI NIMESIKIA KUKUPENDA NA KWA KWELI NASHUHUDIWA WEWE SASA UTAKUA BABA WA WATOTO WANGU. MIMI NIMEKUPENDA SANA NA NIMESHINDWA KUJIZUIA, IMEBIDI NIMUOMBE MUNGU KISHA NIKUAMBIE KUA NATAMANI TUISHI PAMOJA KAMA MUME NA MKE’’, alimaliza kusema uku akitetemeka na kuangalia chini. Mkaka alimshukuru kwa kumpeda na kumwambia anaheshimu sana upendo wake ila apewe nafasi kuuuliza Mungu. Wakaomba na kuachana.
Mkaka alifika home, akawa anawaza mengi mfano, mdada yule ni single mother, umri wake mkubwa kumzidi, pia alishawahi kua ktk ndoa ingawa waume walishakufa, ana wana wawili. Yote hayo yakamfanya hata hasiingie maombini kwa kua aliona ni maombi yasiyo na tija na hata akawa anapotezea kumjibu Singe Mother baada ya ‘maombi’ yake. Single mother akakumbushia kwa sms, call kila mara hata kuwatumia wanae, Mkaka akaendelea kupotezea mwishowe sms mpaka saa 7usiku kila leo, zikazidi, akaamua kumpa audience kwa nia moja tu..kumwambia ukweli!. Siku ikafika na baada ya maombi ya kufungua ibada ya wawili, Mkaka ‘expected Baba watoto wa Single mother akafungua kinywa, NINAONA KWA VIGEZO VYOTE, SI MPANGO WA MUNGU MIMI NA WEWE TUWE MWILI MMOJA NA NILIFANYA WEMA KWA WANAO KAMA MKAKA WA VIJANA WENGI KANISANI NA KAMA NAVYOFANYA KWA WENGINE WENGI’’ alisema. Single Mother alitetemeka, kisha machozi.
Mkaka alikaa kimya akimwangalia analia mpaka huruma kweli zikamwingia then alipomaliza kulia, akamwambia, ‘Mungu wa mbinguni anajua haja yako, husipozimia moyo, atakudhibitishia kua anakupenda, tusonge mbele na mambo haya ya mimi na wewe kua mwili mmoja, yasiwepo tena baada ya leo maana kwa hakika hakutakuwepo ndoa iyo ila itakuwepo nyingine ambayo BWANA atakupa wewe mume bora na mimi, mke mwema’, kisha akaomba na wakaachana. Kuanzia hapo, Mkaka akapunguza utoaji wake kwa watoto na mwisho akaacha kabisa kwa miezi na mambo yakawa yamekwisha. Ghafla mwezi uliopita, Single mother akamtumia sms Mkaka kua anahitaji msaada kwa watoto wake wapate tuition na pia mtoto wa dada yake anahitaji shule ivyo anaomba aunganishwe na yeyote kanisani atakayeweza saidia ilo.Mkaka akikumbuka yaliyo tokea meizi kadhaa kwa yeye kujali maisha ya wanae, hakujibu sms na akachuna kabisa hata kuhakikisha hakuna kukutana kamwe iwe kanisani au hudumani. Mwishowe single mother akatuma sms ya kua amefanya uamuzi wa kutafuta appointment na Mke wa Mchungaji Kiongozi ili akaeleze yote yanayomsibu moyoni kuhusu yeye Mkaka na kwamba haoni kabisa kua kuna mume mwingine zaidi ya Mkaka uyo. Sasa Mkaka anawaza ivi, single mother ataongea nini kule, je ya ukweli au ulongo? Na itakuaje shock ya kwanza atakayopata Mama Mchungaji maana anamfahamu sana Mkaka uyo na huduma na moyo wake? Yote haya yalimpata na yako njiani kumpata Mkaka, kisa wema/utoaji, out of his loving heart ya kusaidia/kuwapa watu vitu. Kweli utoajji mwingine, unamajaribu yake sometimes.
Pia Mkaka alishapata
fedha nzuri miaka ya nyuma akiwa Wilayani. Kukatokea michango mingi kanisani kwa
ajili ya maendeleo ya kanisa ilo mfano kununua vyombo vya kusifu na kuabudu na
kuhubiria mikutano ya nje, watu wakawa wanaitwa na BWANA ivyo wakahitaji
kuchangiwa karo kwenda vyuo vya Biblia, ujenzi wa kanisa na mikutano ya injili.
Mkaka alikua anachukua nusu ya gharama ya mkutano, aliamua kuwasomesha wachungaji
wanne na kuchangia gharama za vyombo robo ya thamani yote. Ikatokea hata baada
ya kuhama uko, wapendwa wale wanakua wanataka sana kuja kwakwe Dar, kila
wachungaji wajapo Dar, wanataka kufikia kwake, kila anayetaka kusoma Bible
college, anamtumia Mkaka ombi, kanisa la kule kila likifanya shughuli, Mkaka
anahusihushwa, vijana wakitaka kuoa na kuolewa, lazima wamfafute Mkaka wa Dar sasa
aliyekua kwao uko Wilayani na inafika mahali Mkaka huyu amelemewa kwa kua
kanisani kwakwe pia kwa Dar sasa, ana
husika na mambo mengi, yakiwemo pia ya kutoa
Maswali ya kutafakari
Unamshauri nini Mkaka
ktk kikao kijacho ambacho kwa kweli hakipendi kwa heshima aliyo nayo kanisani,
anajisikia kama atashusha P?
Au unadhani pengine Mkaka anakosea sana mpango/target kamili ya Mungu kwa kumkatalia singe mother pengine angeomba seriously, kweli single mother angethibitishwa kua ndiye wife?
Mkaka afanye
nini/ali-relate vipi na watoto waliokwisha kua na raha sana, kupenda sana
kanisa, kua na uhakika kila jumapili baada ya ibada wana breakfast na bila shaka
wakampenda sana Yesu kwa jinsi Mkaka alivyowa-care lakini ameacha kwa kua Mama
yao ameingiza agenda nyingine na anawatumia kama chambo au point of contactig Mkaka?
Akikataa kutohusika kwa lolote kihuduma za kutoa/ku-care for uko Wilayani, akiwapangua wapendwa wote wa uko na kubaki na wa Dar including kuwakwepa vibaya sana kwa kutojibu sms, call zao wanapokuja Dar ili wasifikie kwakwe la sivyo watapafanya a permanent centre kila wajapo jijini tena na ndugu na jamaa zao au hata Kwaya nzima inapokuja kurekodi, je amepungukiwa upendo?
Kwakua ktk changizo, ni mazoea siyo Bible, watu hutaja hadharani viwango(si kama sadaka), wale wapendwa wenye nazo, wanapotaja halafu kila likitokea jambo la idara za kanisa, binafsi, wapendwa huenda kuomba msaada kwao, mpaka wanalemewa na wengine walishafanyiziwa kwa kukabwa baada ya kutoka ibadani, je watoeje changizo? Kimya kimya kwa kuogopa kuombwa na wapendwa mikopo, kupigwa mizinga/kubom-iwa na kwa usalama wao pia?
Press on,
Edwin Seleli
Shalom SG,
Kabla ya kushauri ni nini Mkaka huyo afanye, naomba nitoe maelezo yafuatayo. Kila kupenda kuna maudhi yake na maudhi mengine ni endelevu. Biblia inatoa angalizo kuwa “Naam, na wote wapendao kuishi maisha ya utauwa katika Kristo Yesu wataudhiwa.” – 2TIMOTHEO 3:12 (SUV msistizo added). Na kama kusingekuwa na taabu katika kutenda mema Bwana asingetoa angalizo hili “Tena tusichoke katika kutenda mema; maana tutavuna kwa wakati wake, tusipozimia roho.” – GALATIA 6:9. (SUV msisitizo) Kuna kuchoka, kuna kuzimia roho. Ndiyo kusema kuna tatizo, ndiyo maana watu wanachoka na kuna ugumu ndiyo maana watu wanazimia njiani? Na haya yote yana chanzo chake – WAPENDWA (hapa nina maanisha Watumishi na Washirika kwa ujumla), hili ni TATIZO KUU.
Nina ujasiri katika hili, ninaandika haya kutokana na yale niliyoyaona katika muda wangu mfupi ktk wokovu. Hayo ambayo ‘mkaka’ huyu anayapitia, yapo katika makanisa mengi. Wapendwa wengine wamewafanya wenzao kuwa ng’ombe wa maziwa. Tumekosa kiasi na busara, tunaonyeshwa onyeshwa tu, lakini ukiangalia kunatokana na mtu kutaka sana msaada wa mhusika. Tuwaache watu watoe kwa moyo wa kupenda (KUTOKA 35:29) na kama alivyokusudia moyoni mwao (2KOR 9:7). Tusiwatolee nabii nyingi za kuwafanya watoe au kuwaona wao ndiyo mahala pa sisi kuponeapo, maana kwa kufanya hivyo tunawatwika mizigo ambayo mwisho itawalemea. Tabia kama hizi zinapaswa zikemewe kwa nguvu zote katika makanisa yetu. TATIZO jingine ni uchache wa wapendwa design ya ‘Mkaka’ huyu. Hivyo anapotokea mtu kama huyo, kila mpendwa hujikuta ‘anafukuzia’ hapo hapo na kumfanya mtoaji kukosa nafasi ya kupumua.
Sasa nitoe ushauri na kujibu maswali yaliyoulizwa kwa ujumla. Kwanza mkaka yule amshukuru Mungu kwamba kaguswa na kuwasaidia watoto wa mmama. Tatizo lingekuwa kubwa zaidi kama yule mmama angekuwa binti (anayempenda Mungu na mwenye uhitaji wa mme) na watoto wale ni wadogo zake wanaomtegemea mdada huyo, issue yake ingekuwa TOUGH kweli kweli. Kwa maana hilo lililomtokea mama wa wototo wale ni jambo la kawaida kabisa katika maisha haya, ni swala la kuchukuliwa kikawaida tu. Hisia zake zimeguswa mpaka akafikia kumdodokea kijna wa watu, huo ndiyo muono wangu. Kuna matukio mengi sana ya namna hii yamatokea, na hata watu wengine wameitumia hii kama njia ya kupata wanachokita – kugusa hisia za mtu. Kuna wadada wengi tu wamekubali kuolewa kwa kulipa fadhila walizofanyiwa!!! Hivyo tendo la mama huyo kutaka kumwona Mama Mchungaji lisimhuzunishe Mkaka yule. Hizo ni reaction baada ya mama yule kuguswa hisia zake. Ni vema likifika haraka kwa Mama Mchungaji, ili Mkaka awe huru kuwasaidia watoto wale wanaokosa msaada kwa sababu ya hisia za mama yao. Pia mama yule aelezwe ukweli huu kwamba, hisia zake azizuie kwa maana zinafanya watoto wake wakose msaada, asiwe mbinafsi kiasi hicho.
Kuhusu wingi wa wapendwa kutaka msaada kwa Mkaka huyu, Biblia inasema “Kwa hiyo kadiri tupatavyo nafasi na tuwatendee watu wote mema; na hasa jamaa ya waaminio.” – GALATIA 6:10 (SUV msisitizo added). Haijalishi ni wangapi na mara ngapi (frequency), Mkaka wewe angalia ni kwa kadiri utakavyopata nafasi. Usifanye kwa kulazimika au huzuni bali kwa moyo mkunjufu. Wakati nafasi hairuhusu waambie wapendwa ukweli huo na simamia usimamo huo. Nionavyo mimi sio vizuri kutojibu sms zao, badala yake ajivike ujasiri na kuwajibu sasa hivi sina nafasi ya kuwasaidia. Anapotaka kutoa, afanye kana kwamba yeye ndiye aliyeona mtu fulani ana tatizo hilo na ndipo achukue hatua ya kutoa.
Na hili la kuchangia kwa kutaja kiwango kwenye Public ya wapendwa, linaweza kutatuliwa na yule anayehamasisha michango kwa kuwaeleza KUSANYIKO mapema, atoe angalizo la maneno kama watakao ahadi hapo hamaanishi kuwa wao ndiyo wenye kipato kikubwa, au ahadi hizi zisichukuliwe na wapendwa kuwa watakaoahidi hapa ndiyo tiketi ya watu kwenda kuwaomba misaada mbali mbali kwao.
Naona nimeandika sana, niishie hapa.
Keep on watching,
Mathew.