Amani ya Bwana iwe nanyi enyi nyote,
MANENO-MANENO, HISIA, USENGENYAJI, KUSITUKIANA-SITUKIANA, KUMEUA KIROHO CHA MTU HATA KUTOKA KANISANI NA LEO HII YUKO FULL KUJIACHIA KWA DEVO
Inauma sana niliposikia story yake uso kwa uso na machozi yalinitoka moyoni nikasema ''eee Mungu mkumbuke Binti huyu, asife kabla hajaamka tena kukurudia na kuamini kua wako Wateule wanaoweza mpenda na kumtunza hata kufikia kimo na kina Yesu alichomtayarishia.
Kama alikua anakupenda ivi ktk UCHANGA WAKE KIROHO na akapenda kutumika kisha ''akauwawa-killed- kiroho'' na ''Waliokomaa Kiroho'' waliopaswa kumlea na kupalilia alichokua nacho yaani Wokovu kisha Huduma/Karama, basi nasikia machozi hata sana kiutumishi kwa dada huyu rafiki yangu
Nilimsitukia wenda alikua na wokovu kwa ku kila tunapoongea, anaongelea mambo ya Mungu kidogo na kila akisikia gospel song, anakua kama anazama-zama ivi na kuimba pia, lakini hapo hapo jana yake ametoka kujirusha nk- anasemaga na kupiga mastory hayo pia wakati mwingine, mmmh! nikasema hapana, let me show love ya Kiutumishi na moyo wa Bwana, nikae naye, nikataka kujua historia yake, sasa baada ya kumsosho sana, akafunguka, dah!, aliyonieleza, nilitoa machozi moyoni, sikuamini!
Story yake ni ndefu lakini in summary, aliokoka kisha kupenda sana huduma ya kuimba na akaanza kuimba baadaye kwa kipaji chake akapendwa sana ana Mtumishi msaidizi aliyekua ni Kiongozi wa Praise and Worship nazungunzia upendo wa-KITAKATIFU.
Wapendwa wakanza kumsema kua anataka kumuangusha Mtumishi, yakakolea maneno hata akaaitishwa vikao vizito, Anasema huyu dada kua alishituka sana kwa kua hakuwahi hata siku moja kuwaza hayo, yeye alihudumu na akapendwa tu na Kaka yake kiroho huyo Mchungaji Msaidizi. Aliumia sana, akalia sana kikaoni na kusema hana hila, hawamkusikiliza. Wakamsema kweli na maneno yakazagaa Kanisani ktkt ya Wamama na Wadada, akashindwa kua anasimama maana anaona kila mtu anamuona agent. Akataka kumuona Kiongozi Mkuu wa Kanisa hilo-Maarufu sana TZ kueleza ukweli kua hana shida kabisa, hakupewa nafasi
Wako walimuhisi kua alishatembea na Mtumishi yule mdogo, alililia anasema hadi kusikia kuzirahi.Akasema yuko tayari hata akina Mama kwenda kumpima kienyeji-kikicheni part au hospitali watakuta hana hila yaani hajawahii hata siku moja kufanya mambo- alikua bikira-anasema mwenyewe ivyo, lakini wakamuona ni kahaba tu hapo kanisani na ana agenda, wala hawakumsikiliza, aliumia na akalia mno ananiambia kisha, hatimaye akaamua kukaa tu nyumbani hata hamu ya kusali na kujumuika ikafa na leo, bahati mbaya sana, anapiga laga na kuruka majoka kwa DJ kama kawaida.
Nisaidieni ushauri na maombi-tumia initials zake dada EJ kumuombea, tamka na omba kwa imani na mzigo wa uzazi wa kiroho na kukasirika rohoni kua asife au devo asimkate hewa kabla hajarudi kwa Bwana, plz hepl me in this mzigo wa kuombea huyu dada, Amen
ONYO/OMBI: Tusiwe wepesi kuwahisi-hisi au dhania-dhania wenzetu KWA JINSI WALIVYO, WANAVYOFANYA HUDUMA, URAFIKI WAKO NA UKARIBU MZURI TU kisha haraka haraka tunahitimisha kua ni makahaba, wahuni, watafuta wadada na wanaume, ma-agent hata kusambaza mahisia hayo kwa Wengine, utaua Wengi Kanisani-PLZ SHUT UP KAMA HUNA UHAKIKA labda kama mazingira yatoe ushahidi mkubwa mno pasi na kuacha shaka.
Press on ktk kupata uchungu kwa kila Kondoo/kiungo chenzetu kinapokatika na kufa kiroho.
Edwin Seleli