Amani ya Bwana iwe nanyi enyi nyote,
Mambo
mengine ukisoma ktk Neno ni kama ya kawaida
na unapita kwa haraka shwaap! lakini siku nyingine ukisoma hapo hapo, ghafla
unasimamishwa taap! Halafu unaangalia/tafakari kisehemu cha Neno/sentensi au sentence
nzima kama si nusu au sura nzima then ghafla inakua kama inafunuka kwa upya au inakusitua/kubip
upaangalie kwa upya na kisha ukitekeleza, unashangaa sana kua ivi icho kisehemu
kilikuwepo hapo kila siku unasoma au kimewekwa jana!
Imeandikwa:
Waebrabia: 12:1- Sisi tunalo kundi hili kubwa la mashahidi mbele yetu. Kwa hiyo tuondoe kila kizuizi kinachotuzuia, NA DHAMBI ILE INAYOTUNG’ANG’ANIA. Tupige mbio kwa uvumilivu katika mashindano yaliyowekwa mbele yetu
Hebrews: 12:1..Therefore then, since we are surrounded by so great a cloud of witnesses [who have borne testimony to the Truth], let us strip off and throw aside every encumbrance (unnecessary weight) and that SIN WHICH SO READILY (deftly and cleverly) CLINGS TO AND ENTANGLES, and let us run with patient endurance and steady and active persistence the appointed course of the race that is set before us, …AMP-Bible
Hebrews: 12:1: Therefore, since we are surrounded by such a great cloud of witnesses, let us throw off everything that hinders and the SIN THAT SO EASILY ENTANGLES US. And let us run with perseverance the race marked out for us-NIV-Bible
MASWALI: ( Yako A hadi F, mengine yanajitegemea na mengine yanajirudia ili kufafanua mengine au angaliza issue zingine/interested)
A: Ni ipi iyo dhambi inayotu au taka kututait/kamata/suffocate so easily/sharply/faster?
B: Kila mmoja anayo yake spesheli inayomuwinda/nyemelea nini au zipo na tuna-share kwa kua wote tu Wanadamu?
C: Kwani iyo dhambi inatoka wapi jamani wakati tulisha takaswa na kusamehewa? Kwa devo, dunia hii au tunazalishaga wenyewe?
D: Kama inayotokana na sisi Wanadamu, source yake ni yale ma-file na ma-folder ya Misri nini? Kwani Misri softwares si zilishagavunjiliwa mbali siku ile tulipoamua kutwaa softwares za Canaan au?
E: Kwanini ni kweli kabisa kama Mtu akitaka kua mkweli wa nafsi yake kwamba, zile dhambi za zamani kabla ya kuja nuruni, ndizo izo izo waga sometimes zinakuja kusabahi na ku-cross-cross by your side? Why? Kwani utakaso haukufuta hata iyo memory card/experience ya kidevo na kimwili cha kale?
Zingatia maandiko haya pia
Mwanzo: 4: 1-7:1 Adamu akamjua Hawa mkewe; naye akapata mimba, akamzaa Kaini, akasema, Nimepata mtoto mwanamume kwa Bwana. 2 Akaongeza akamzaa ndugu yake, Habili. Habili alikuwa mchunga kondoo, na Kaini alikuwa mkulima ardhi. 3 Ikawa hatimaye Kaini akaleta mazao ya ardhi, sadaka kwa Bwana. 4 Habili naye akaleta wazao wa kwanza wa wanyama wake na sehemu zilizonona za wanyama. Bwana akamtakabali Habili na sadaka yake; 5 bali Kaini hakumtakabali, wala sadaka yake. Kaini akaghadhibika sana, uso wake ukakunjamana. 6 Bwana akamwambia Kaini, Kwa nini una ghadhabu? Na kwa nini uso wako umekunjamana? 7 Kama ukitenda vyema, hutapata kibali? Usipotenda vyema dhambi iko, inakuotea mlangoni, nayo inakutamani wewe, walakini yapasa uishinde.
Notice: Mungu anamwambia Kaini kua kuna dhambi inamuotea!(sin is crouching at your door; it desires to have you)
Warumi: 7:13-23: 13Kwa maana twajua ya kuwa torati asili yake ni ya rohoni; bali mimi ni mtu wa mwilini, nimeuzwa chini ya dhambi. 14 Maana sijui nifanyalo, kwa sababu lile nilipendalo, silitendi; bali lile nilichukialo ndilo ninalolitenda. 15 Lakini kama nikilitenda lile nisilolipenda, naikiri ile sheria ya kuwa ni njema. 16 Basi sasa si mimi nafsi yangu ninayetenda hilo, bali ni ile dhambi ikaayo ndani yangu 17 Kwa maana najua ya kuwa ndani yangu, yaani, ndani ya mwili wangu, halikai neno jema; kwa kuwa kutaka nataka, bali kutenda lililo jema sipati. 18 Kwa maana lile jema nilipendalo, silitendi; bali lile baya nisilolipenda ndilo nilitendalo. 19 Basi kama lile nisilolipenda ndilo nilitendalo, si mimi nafsi yangu nilitendaye, bali ni ile dhambi ikaayo ndani yangu. 20 Basi nimeona sheria hii, ya kuwa kwangu mimi nitakaye kutenda lililo jema, lipo lililo baya. 21 Kwa maana naifurahia sheria ya Mungu kwa utu wa ndani, 22 lakini katika viungo vyangu naona sheria iliyo mbali, inapiga vita na ile sheria ya akili zangu, na kunifanya mateka ya ile sheria ya dhambi iliyo katika viungo vyangu. 23 Ole wangu, maskini mimi! Ni nani atakayeniokoa na mwili huu wa mauti?
Notice: Paul analalamika/analia kua anatumikia dhambi na mwili wa mauti, kizuri anachotaka kufanya chema, hakifanyi na kibaya ambacho hataki kufanya, anakifanya!
F: Dah! Tunabalance vipi KWELI moja kua sisi ni VIUMBE VIPYA NA TUMESHATAKASWA na equally KWELI nyingine kua KUNA DHAMBI au UMAUTI ndani ya MWILI huu ambao pia ni Hekalu la Roho Mtakatifu, unatamaniwa na DHAMBI inayokua beneti-beneti na sisi? Aisee! dah!
Press on,
Edwin Seleli
--
Tafadhali zingatia msingi wetu ni Neno la Mungu, Lengo letu Kuujenga mwili wa Kristo, kushirikiana, amani na upendo. Yeyote yuko huru kuchangia, kufundisha, kukubali kufundishwa sawasawa na Msingi wetu Mkuu Neno la Mungu. Kujiunga na Team ya Injili au Maombi wasiliana nasi kwa simu 0714 915 424. Tuma Email. strictl...@yahoo.co.uk Facebook:https://www.facebook.com/pages/Strictly-Gospel/363180289370
Blog: www.strictlygospel.wordpress.com
Kujiondoa Kwenye Kundi Hili Tuma Email:
strictlygospe...@googlegroups.com
|
Mpendwa Seleli,
Topic yako ni ya maana sana ndugu yangu kwani ni wengi wanaojiswali , pengine hawapati jibu.
Nalipoitafakari, niliona mambo yote yamefungwa katika kifungo kile ulichotutolea cha Warumi: 7:13-23.
Pia Paulo akasema: "2Timotheo 4: 6-7: Kwa maana, mimi sasa namiminwa, na wakati wa kufariki kwangu umefika.
Nimevipiga vita vilivyo vizuri, mwendo nimeumaliza, Imani nimeilinda;"
Hivi Paulo, pamoja na imani aliyokuwa nayo na upako mwingi kutoka RM, ilihitajika apige vita. Hiyo vita ni ya kulinda imani ya roho wakati mwili inampeleka dhambini. Alipiga vita yake kwani ana mwili wake, nasi imetupasa kuipiga yetu kwani tunayo miili. Hence, kila mtu ana vita yake; inayo maana hiyo dhambi inayozinga iko mlangoni mwa kila nafsi kwa namna ya kipekee, kwani Paulo anasema yeye amepiga vita wala hasemi tumepiga vita. Roho itakayopiga vita vizuri ndiyo itapata ushindi.
Mbarikiwe. |
![]() |
