Novena Ya Huruma Ya Mungu Siku Ya Sita

0 views
Skip to first unread message

Beatrix Gerke

unread,
Aug 5, 2024, 2:23:35 PM8/5/24
to saynasitro
Kusudila kitabu hiki ni kutoa kitabu rahisi kwa kutumia Wenyeji katika Sala zao za kanuni. Wengi hawawezi kununua Kitabu cha Sala kizima, na kwa hiyo hawawezi kuabudu vizuri. Kitabu hiki kitawasaidia sana kuabudu na akili zaidi na kusali vizuri.

"Anitoleae sifa mimi hunitukuza."


The purpose of this book is to provide a book at low cost for the use of African congregations at the ordinary services of the Church. Many cannot afford the complete Book of Common Prayer and a Hymn Book. They are therefore not able to take their proper part in worship. This book should help them to a more sincere and intelligent worship.

"Whoso offereth me praise, glorifieth me".




As can be seen from the introduction, it was intended to be a 'low-cost alternative' which Africans could afford. As such it omits many services and the ones it does include are heavily abridged, omitting many of the parts not spoken by the people. The Common Prayer portion of this book, in fact, occupies only about 1/8 of the pages, with another 1/8 for a selection of Psalms; the remaining 3/4 of the book is devoted to a words-only hymnal of mostly familiar English hymns translated into Swahili.


This book appears as 167:2 in David Griffiths' Bibliography of the Book of Common Prayer. The text has been spell-checked, but, as the author knows no Swahili, there still may be errors. Please let us know if you find any.


BABA Mwenyiezi na mwenye rehema; Tumekosa kwa kutokufuata njia zako takatifu. Tumekuwa kama kondoo waliopotea, Tumefuata mno mawazo na tamaa zetu. Tumezihalifu sharia zako takatifu. Tumeyaacha yaliyotupasa kutenda. Tumeyatenda yasiyotupasa kutenda; Wala uzima hatunao. Uturehemu Wewe Bwana, sisi maskini wenye dhambi. Uwaachilie, Mungu, wanaoungama dhambi zao. Uwarudishe wanaotubu; Kwa ahadi zako ulizowaahidia wana Adamu kwa Kristo Yesu Bwana wetu. Na kwa ajili yake, Baba wa rehema, Utujalie tuyatende tangu leo mambo ya kitawa, ya haki, na ya kiasi. Jina lako takatifu litukuke. Amin.


BABA yetu, uliye mbinguni, Jina lako liwe takatifu. Ufalme wako uje. Mapenzi yako yatimizwe duniani, Kama yatimizwavyo mbinguni. Utupe leo riziki zetu. Utusamehe makosa yetu, Kama sisi tunavyowasamehe waliotukosa. Usitutie majaribuni; Lakini utuokoe maovuni; Kwani ufalme, na nguvu na utukufu ni wako milele. Amin.


NJONI, tumwimbie Bwana: tufanyie shangwe mwamba wa wokofu wetu.

Tuje mbele zake kwa shukrani: tumfanyie shangwe kwa zaburi.

Kwani Bwana ni Mungu mkuu: na Mfalme mkuu juu ya miungu wote.

Mkononi mwake zimo bonde za dunia: hata vilele vya milima ni vyake.

Bahari ni yake, ndiye aliyeifanya : na mikono yake iliiumba nchi kavu.

Njoni, tuabudu, tusujudu: tupige magoti mbele za Bwana aliyetuumba.

Kwani ndiye Mungu wetu: na sisi watu wa malisho yake, na kondoo za mkono wake.

Ingekuwa heri leo msikie sauti yake! Msifanye migumu mioyo yenu: kama vile Meribah, kama siku ya Massah jangwani;

Kama vile walivyonijaribu baba zenu: wakanipima, wakayaona matendo yangu.

Miaka arubaini nalihuzunika nacho kizazi hiki nikasema: watu waliopotoka mioyo hawa, hawakujua njia zangu.

Nikaapa kwa hasira yangu: wasiingie rahani mwangu.

Utukufu una Baba, na Mwana: na Roho Mtakatifu;

Ulivyokuwa mwanzo: ulivyo sasa, utakavyokuwa milele. Amin.


WEWE, Mungu, twaskusifu: wewe, Bwana, twakukiri.

Wewe Baba wa milele: ulimwengu wote unakuabudu.

Wewe Malaika zote: nazo Mbingu na Nguvu zote,

Nao Makerubi na Maserafi: wakuimbia hawakomi,

Mtakatifu, Mtakatifu, Mtakatifu: Mungu Bwana wa majeshi.

Mbingu na nchi zimejaa: enzi ya utukufu wako.

Wakusifu wewe; jamii tukufu ya Mitume.

Wakusifu wewe: shirika lenye sifa la Manabii.

Wakusifu wewe: jeshi la Mashahidi waliovaa mavazi meupe.

Kanisa takatifu katika nchi zote: lakukiri wewe.

Baba mwenye enzi: isiyo na kiasi.

Mwana wako pekee: wa kweli, wa kuabudiwa.

Na Mfariji: Roho Mtakatifu.

Wewe Kristo: ndiwe Mfalme wa utukufu.

Wewe Mwana wa milele: wa Baba.

Wewe ulipotaka kujifanya mtu, ili umwokoe Mwana Adamu: hukuchukizwa na tumbo lake Bikira.

Wewe ulipoushinda uchungu wa mauti: uliwafunulia waaminio Ufalme wa Mbingu.

Wewe unakaa mkono wa kuume wa Mungu: katika utukufu wake Baba.

Tunasadiki : utakuja kuwa Mwamuzi.

Kwa hiyo, twakuomba uwasaidie watumwa wako: uliowakomboa kwa damu yako ya thamani.

Uwajalie pamoja na Watakatifu wako: utukufu wa milele.

Uwaokoe watu wako, Bwana: uubarikie urithi wako.

Uwatawale: uwainue hata makao ya milele.

Sisi kila siku: twakutukuza.

Twalisifu Jina lako: zamani hizi na za milele.

Ukubali, Bwana, kutulinda leo: tusipate dhambi.

Uturehemu, Bwana: uturehemu sisi.

Utuonee huruma, Bwana: kwani sisi twakutumaini wewe.

Nimekutumaini wewe, Bwana: nisipotee milele.


MFANYIENI shangwe Bwana, dunia yote: mtumikieni Bwana kwa furaha, njoni mbele zake kwa kuimba.

Jueni kwamba Bwana ndiye Mungu: ndiye aliyetuumba, na sisi tu watu wake, na kondoo za malisho yake.

Ingieni milangoni mwake kwa kushukuru, nyuani mwake kwa kusifu: mshukuruni, lihimidini Jina lake.

Kwani Bwana ndiye mwema, rehema zake za milele: na uaminifu wake vizazi na vizazi.

Utukufu una Baba, na Mwana: na Roho Mtakatifu;

Ulivyokuwa mwanzo, ulivyo sasa: utakavyokuwa milele. Amin.


NAMWAMINI Mungu Baba Mwenyiezi, Muumba mbingu na nchi;

Na Yesu Kristo Mwana wake pekee Bwana wetu, Aliyechukuliwa mimba kwa uweza wa Roho Mtakatifu, Akazaliwa na Bikira Mariamu, Akateswa zamani za Pontio Pilato, Akasulibiwa, Akafa, Akazikwa, Akashuka pahali pa wafu; Siku ya tatu akafufuka, Akapaa mbinguni, Anaketi mkono wa kuume wa Mungu Baba Mwenyiezi ; Kutoka huko atakuja kuwahukumu watu wahai na wafu.

Namwamini Roho Mtakatifu; Kanisa Takatifu, Katholiko; Ushirika wa Watakatifu; Ondoleo la dhambi; Kiyama ya mwili, Na uzima wa milele. Amin.


BABA yetu, uliye mbinguni, Jina lako liwe takatifu. Ufalme wako uje. Mapenzi yako yatimizwe duniani, Kama yatimizwavyo mbinguni. Utupe leo riziki zetu. Utusamehe makosa yetu, Kama sisi tunavyowasamehe waliotukosa. Usitutie majaribuni; Lakini utuokoe maovuni. Amin.


Bwana, utuonyeshe rehema yako.

Watu. Utupe wokofu wako.

Mhudumu. Bwana, umwokoe Mfalme.

Watu. Utusikie kwa rehema tukuombapo.

Mhudumu. Wahudumu wako uwavike haki.

Watu. Uwafurahishe wateule wako.

Mhudumu. Uwaokoe watu wako, Bwana.

Watu. Uubariki urithi wako.

Mhudumu. Utupe amani, Bwana, siku zetu.

Watu. Kwani hatuna mwingine wa kutupigania, ila wewe Mungu wetu.

Mhudumu. Mungu, utuumbie ndani mioyo safi.

Watu. Wala Roho yako Mtakatifu usituondolee.


EE Baba Mweyiezi, ndiwe uliyetuumba na kutukomboa kwa damu ya Mwana wako Mpenzi, ili tutangaze sifa zako. Utusaidie tukushuhudie kwa mawazo na maneno na matendo, ili tukutukuze na kuonyesha imani yetu kwa wengine, kwa Yesu Kristo Bwana wetu. Amin.


MWENYJEZI Mungu, Baba wa rehema zote,sisi watumwa wako wanyonge twakushukuru kwa unyenyekevu na kwa moyo kwa wema wako wote na pendo lako kwetu sisi, na kwa watu wote. Twakutukuza kwa ajili ya kuumbwa kwetu, na kuhifadhika kwetu, na kwa baraka zote za maisha haya; lakini zaidi ya yote, kwa pendo lako lisilopitika la kukombolewa ulimwengu na Bwana wetu Yesu Kristo; kwa njia za neema, na tumaini la utukufu. Utupe, twakusihi, fahamu itupasayo ya rehema zako zote, mioyo yetu ikushukuru pasipo hila, nasi tuonyeshe sifa zako, si kwa midomo yetu tu, ila na kwa maisha yetu: tukijitia kabisa katika utumwa wako, tukienda mbele yako katika utakatifu na haki siku zetu zote; kwa Yesu Kristo Bwana wetu, kwa huyo pamoja na wewe na Roho Mtakatifu iwe heshima yote na utukufu, maisha na milele. Amin.


MOYO wangu wamwadhimisha Bwana: roho yangu yamfurahia Mungu, Mwokozi wangu.

Kwani ameutazama: unyonge wa mjakazi wake.

Kwani hakika, tokea leo: vizazi vyote wataniita heri.

Kwani aliye hodari amenitendea makuu: na Jina lake ni takatifu.

Na rehema zake vizazi hata vizazi: kwao wanaomcha.

Ametenda nguvu kwa mkono wake: amewatawanya walio na kiburi katika mioyo yao.

Amewashusha wakuu katika viti: amewakweza wanyonge.

Wenye njaa amewashibisha mema: wenye mali amewaondoa mikono mitupu.

Kwa kukumbuka rehema amemsaidia Israeli mtumishi wake: kwa jinsi alivyowaambia baba zetu, Ibrahimu na uzao wake, hata milele.

Utukufu una Baba, na Mwana: na Roho Mtakatifu;

Ulivyokuwa mwanzo; ulivyo sasa, utukavyokuwa milele. Amin.


SASA wamruhusu, Bwana, mtumwa wako kwa amani: kama ulivyosema.

Kwani macho yangu: yameuona wokofu wako.

Ulioweka tayari: machoni pa watu wote.

Nuru ya kuwaangaza mataifa; na kuwa utukufu wa watu wako Israeli.

Utukufu una Baba, na Mwana; na Roho Mtakatifu;

Ulivyokuwa mwanzo: ulivyo sasa, utakavyokuwa milele. Amin.




MUNGU Baba, wa mbinguni: uturehemu maskini wenye dhambi.

Mungu Baba, wa mbinguni: uturehemu maskini wenye dhambi.

Mungu Mwana, Mkomboa ulimwengu: uturehemu maskini wenye dhambi.

Mungu Mwana, Mkomboa ulimwengu: uturehemu maskini wenye dhambi.

Mungu Roho Mtakatifu, utokae katika Baba na Mwana; uturehemu maskini wenye dhambi.

Mungu Roho Mtakatifu, utokae katika Baba na Mwana: uturehemu maskini wenye dhambi.

Utatu Mtakatifu, Mhimidiwa, Mtukufu, Nafsi tatu na Mungu mmoja; uturehemu maskini wenye dhambi.

Utatu Mtakatifu, Mhimidiwa, Mtukufu, Nafsi tatu na Mungu mmoja: uturehemu maskini wenye dhambi.

Usiyakumbuke, Bwana, makosa yetu; wala makosa ya baba zetu; wala usitupatilize kwa dhambi zetu; utuachilie, Bwana mwema, waachilie watu wako, uliowakomboa kwa damu yako ya thamani, wala usituonee hasira milele,

Utuachilie, Bwana mwema.

Na mabaya yote na madhara; na dhambi, na hila na jeuri za Shetani; na ghadhabu yako na laana la milele,

Utuokoe, Bwana mwema.

Na upofu wote wa moyo; na kiburi, majisifu, na unafiki; na husuda, chuki, na uovu, na kutopendana kwote,

Utuokoe, Bwana mwema.

Na uasharati na dhambi zingine zote za kufisha; na madanganya yote ya dunia, ya mwili, na ya Shetani,

Utuokoe, Bwana mwema.

Na umeme na tufani; na tauni, maradhi, nzige na njaa; na vita na uaji, na na mauti ya ghafula,

Utuokoe, Bwana mwema.

Na maafikano ya fitina ya siri, na kuasi; na elimu ya uwongo, uzushi, na kufarakana kwa dini; na kuwa na moyo mgumu, na kulidharau Neno na amri zako.

Utuokoe, Bwana mwema.

Kwa siri ya Kufanyika mwili kwako kutakatifu; kwa Kuzaliwa kwako kutakatifu, na Kutahiriwa; kwa Kubatizwa kwako, Kutunga, na Kujaribiwa,

Utuokoe, Bwana mwema.

Kwa huzuni yako, na Hari ya damu; kwa Msalaba wako na Kuteswa; kwa Kufa kwako kwa thamani, na Kuzikwa; kwa Kufufuka kwako kutukufu na Kupaa; na kwa kuja kwake Roho Mtakatifu,

Utuokoe, Bwana mwema.

Wakati wote wa kutaabika kwetu; wakati wote wa kufanikiwa; saa ya kufa, na siku ya kuhukumiwa,

Utuokoe, Bwana mwema.

Sisi wenye dhambi twakusihi utusikie, Bwana Mungu: upende kulitawala na kuliongoza Kanisa lako takatifu Katholiko, lishike njia njema;

Twakusihi utusikie, Bwana mwema.

[Upende kumbariki mfalme wa inchi hii, na kuuongoa moyo wake aikubali kweli yako;

Twakusihi utusikie, Bwana mwema.]

Upende kuwaangaza Maaskofu wote, Makasisi, na Mashemasi, wajue na kufahamu kwa kweli Neno lako; wakalieneze kwa mafundisho na kwa mwenendo wao;

Twakusihi utusikie, Bwana mwema.

Upende kuwavika watu wakuu wa Serkali na wazee wote neema, hekima, na akili;

Twakusihi utusikie, Bwana mwema.

Upende kuwabariki na kuwalinda makadhi, [maliwali, na maakida,] na watu wote wenye mamlaka; ukiwajalia neema ya kutenda haki, na kuihakikia kweli ;

Twakusihi utusikie, Bwana mwema.

Upende kuwabariki na kuwalinda watu wako wote;

Twakusihi utusikie, Bwana mwema.

Upende kuwapa mataifa yote umoja, amani, na urafiki;

Twakusihi utusikie, Bwana mwema.

Upende kutujalia moyo wa kukupenda na kukucha, na kufuata kwa bidii amri zako;

Twakusihi utusikie, Bwana mwema.

Upende kuwazidishia neema watu wako wote, illi kwa unyenyekevu walisikie Neno lako, walikubali kwa moyo safi, na kuzaa matunda ya Roho;

Twakusihi utusikie, Bwana mwema.

Upende kuwaleta katika njia ya kweli Washenzi na Waislamu na wote waliopotea na kudanganyika;

Twakusihi utusikie, Bwana mwema.

Upende kuwaimarisha wasimamao; kuwafariji na kuwasaidia walio na moyo dhaifu; kuwainua waangukao ; na hatima kumkanyaga Shetani chini ya miguu yetu;

Twakusihi utusikie, Bwana mwema.

Upende kuwatunza, kuwasaidia, na kuwafariji wote walio katika hatari, shidda, na taabu;

Twakusihi utusikie, Bwana mwema.

Upende kuwahifadhi wote wanaosafiri katika inchi au baharini, wanawake wote walio na utungu wa kuzaa, wagonjwa wote, na watoto wote wachanga, na kuwahurumia wafungwa wote;

Twakusihi utusikie, Bwana mwema.

Upende kuwalinda na kuwaruzuku watoto wote wasio na baba, wanawake waliofiwa na waume zao, na wote wasio na msaada, na wanaoonewa;

Twakusihi utusikie, Bwana mwema.

Upende kuwarehemu watu wote;

Twakusihi utusikie, Bwana mwema.

Upende kuwasamehe adui zetu, nao watufukuzao na watusingiziao, uwageuze mioyo;

Twakusihi utusikie, Bwana mwema.

Upende kutupa na kutuhifadhia mazao ya inchi kwa jinsi yake, tupate kuyatumia wakati wake;

Twakusihi utusikie, Bwana mwema.

Upende kutujalia tutubu kwa kweli; kutusamehe dhambi zetu zote, za ulegevu na ujinga, na utuvike neema ya Roho yako Mtakatifu, tutengeneze mwenendo wetu kwa Neno lako takatifu ;

Twakusihi utusikie, Bwana mwema.

Mwana wa Mungu: twakusihi, utusikie.

Mwana wa Mungu: twakusihi, utusikie.

Mwana Kondoo wa Mungu: uzichukuae dhambi za ulimwengu;

Utupe amani yako.

Mwana Kondoo wa Mungu: uzichukuae dhambi za ulimwengu;

Uturehemu sisi.

3a8082e126
Reply all
Reply to author
Forward
0 new messages