Watu wengi watamani kufikishwa mwezi mtukufu wa ramadhani lakini si kila mmoja anayetamani ataufikia.Kuna baadhi ya watu tulikuwa nao ramadhani iliyopita lakini mpaka hivi sasa hatupo nao tena. Kwa hiyo sie tulio ruzukiwa uhai mpaka hivi sasa yatubidi tujitahidi kumuomba Allah atufikishe mwezi huu mtukufu wa ramadhani mwezi wa fadhila.