MJADALA JUU YA MISHAHARA YA WABUNGE

0 views
Skip to first unread message

khadija moh'd

unread,
May 3, 2011, 12:55:22 PM5/3/11
to stephen msechu, regional-forum-for-researchers-and-journalists

Ndugu wanaharakati,

Kwa kifupi nadhani nami pia nitoe walau  kero ambayo kwangu naona imekuwa ikinisumbua sana, pamoja na majibu ya WM, mimi naomba tujadili hoja yangu hii.

Wabunge  wetu wakati wanapoomba  sisi wananchi tuwachague, hupenda kutumia kauli kuwa wanaomba tuwatume Bungeni ili watutumike, kwa lugha hii, nadhani mwajiri wa Mbunge ni Mwananchi yaani mimi na wewe.

Sasa hoja yangu inakuja hivi, hivi wewe kama umeomba nafsi ya kazi ili utumikie Umma, kupitia Taasisi  X au B, je wewe mwomba kazi unauwezo wa kujipangia mshahara na posho?

Hivi hawa wabunge ambao sisi wananchi tunawachagu inakuwaje wao wakiwa Bungeni wanajipangia mishahara na posho halafu ajira yao ya kipindi cha Miaka mitano inapoisha, hurudi tena kwetu na kusema naomba ndugu wananchi mnitume  Bungeni ili niweze kuwatumikia  na sisi bila kuhoji mambo mhimu kama haya tunawarudisha tena Bungeni,

Unajua kwangu haiingii akilini kabisa, yapo mambo ambayo ukiyatazama utaona kabisa hayaingii akilini, leo Mbunge anapokea   mamilioni ya shilingi, Madiwani nao wanapokea kiduchu tu, huku watendaji wa Kata na Vijiji wakiwa hawana ofisi kabisa, kuna sehemu moja nilimtembelea Afisa Mtendaji wa Kijiji nikakuta mbele ya Meza yake kuna kichuguu kikubwa nikamwuliza hivi kweli Bosi wako yaani Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya anaweza akdiriki kuja kukutembelea na akaingia katika ofisi hii akakaa na kutia sahihi kitabu cha wageni?

Hivi, leo, tumekuwa na pupa ya kuwachagua vijana ambao wametoka chuo Kikuu  ati hao ndio wanaofaa kuwa wabunge,  ( katika hili sina maana ya kupinga wasomi ati wasipewe nafasi) ila hapa najaribu kujiuliza mnipe majibu kabisa, Kijana leo amemaliza chuo kikuu na kupta shahadaa yake ya kwanza, hicho kinakuwa kigezo kikubwa cha kupata ubunge wakati kijana huyu, kwanza akiingia Bungeni, laizma hesabu yake ya kwanza itakuwa kupigania maslahi ya posho na mishahara mikubwa ili alipe gharama zote ambazo wazazi wake walitumia katika kumsomesha yeye, pili atakuwa na hesbau za kuanza kujenga nyumba nzuri na kusaidia familia yake. Ndio maana Watanzania wengi wamekuwa na tabia ya kulalamika kuhusu hali ya maisha mara tu baada ya uchaguzi kumalizika, ikifika wakati wa upigaji kura tunakwenda likizo  kimaamuzi.

Kwa ndugu zetu Waamerika, wao wana taratibu nzuri, elimu haiwi kigezo cha cha kwanza cha kupata madaraka, bali kwanza hujifunza  huyu anayengombea madaraka tabia yake ilikuwa yanamna gani wakati alipokuwa yungali mtoto, alipokuwa pre-school, primary school na hata chuo Kikuu, iwapo itaonekana kwamba tabia na mwenendo wake vilikuwa  ovyo, basi kwa hali hiyo hawezi kufikiriwa hata kidogo, pia hali ya uwezo wa kiuchumi huangaliwa na   mwisho ndipo elimu yake hufuata baada ya mchakato wa hayo yote mawili  kuonekana kuwa amekidhi vigezo.


Pamoja na utamaduni tulionao kwamba  tujenge taifa ambalo linalenga kuweka usawa  kati ya wenye nacho  na wasio nacho tuwe sawa nadhani  hali hii ndio hupelekea  kuwepo kwa ufisadi ambao hautaondoka kamwe.

Ndugu wanaharakati wenzangu, nadhani ipo haja kwamba katika siku zijazo na hata sasa, Waziri Mkuu ambaye ndiye Mkuu wa shughuri za Serikali Bungeni pamoja na  waziri wa Uratibu Sera na Bunge, waweke utaratibu kuwa Kila Wabunge anapohitaji kuongezewa Posho na mishahara yao, basi iandaliwe White Paper ipitishwe kwa waajiri wao ambao ni sisi wapiga kura,  na wanapiga kura ( wananchi) ndio watoe  uamuzi wa ni kiasi gani ambaocho wabunge walipwe. Kwa kweli  kwangu naona wabunge wengi hawana uzalendo kabisa haswa unapoona mbunge analipwa mamilioni ya shilingi huku Polisi, Hospitali zetu, Walimu, watoto wa shule za msingi na hata Vyuo vikuu wakiwa katika mazingira mabaya  na hata watoto wetu kuishia kukaa mavumbini katika karne hii, nawaapia hao wabunge siku ya mwisho Mungu atawaulizia kama waliwatendea haki wale waliowachagua,  msijifuahishe kwa kutinga katika mashangingi mazuri mazuri mkadhani huo ndio mwisho siku ya Mungu inakuja mtajibu hata kama raia hawatachuku hatua.

Naomba Mwaka 2015, wananchi mchukue hatua  na hasa katika kipindi hiki tunapoelekea kufanya mabadiliko makubwa  ya katiba ya Nchi. Mbunge au Wabunge wasijipangie mishahara au posho. Vinginevyo nafasi ya Ubunge itakangazwe kama nafasi ya ajira.


Nawatakia mjadala mwema katika hili.

Asante



William Daudi
Program  Office
TWSEDHRO
Kigoma Tanzania



 
 
 
 

stephen msechu

unread,
May 4, 2011, 5:06:36 AM5/4/11
to khadija moh'd, regional-forum-for-researchers-and-journalists
Ndugu Wanaharakati,
 
Unajua kunavitu (vingine vidogo vingine vikubwa) ambavyo madhara yake ni makubwa ila yamejificha.
 
Nakubaliana na kamaradi kuhusu mishahara ya wabunge kuwa ni mikubwa sana na inabidi mwananchi ndiye aseme ni kiwango gani walipwe.
 
Kwanza nianze na madogo, suala la kuwaita wabunge na viongozi WAHESHIMIWA kwangu mimi sio sahihi, kwa haraka haraka halina tabu ila ukiliangalia kwa undani linaleta hofu na woga kwa mwananchi juu ya kiongozi wake. Linaleta matabaka ya viongozi na waongozwa, kiongozi juu na mwananchi chini dhana ambayo ni potofu kwani kinyume ndio sahihi.
 
Kwanini tusiitana NDUGU? hii inaleta usawa na ukaribu ni rahisi kumhoji au kumpa taarifa mtu uliyekaribu naye!
 
Kuhusu mishahara, vile vile, japo ni vyema watu kulipwa sawa kwa kazi sawa, pia si vyema kuwepo na tofauti kubwa kati ya kazi moja na nyingine kwani itaibua tabaka la wenye nacho na wasionacho, wenye kumuliki njia za uzalishaji na wasionanjia za uzalishaji. Baada ya muda matabaka haya hukuwa na kudhuriana hivyo ni vyema tukaiangalia upya mishahara ya wabunge.....mbona wa Rais sio mkubwa hivyo ukilinganisha na cheo chake?
 
Hata hivyo suala la kuwabeza vijana wanaotoka chuo kikuu kuwa sio sahihi kuchaguliwa kwa kigezo watahujumu rasilimali kwa lengo la kunufaika mapema, bado ni mapema kulisema hilo kwani ndio kwanza wameingia bungeni na pia tusisahau  mafisadi wanaotajwa wamekuwa kwenye siasa kwa muda mreefu na wanamabilioni ila bado wanaiba left right and centre! Hivyo tuwape muda na ufisadi unatokana na hulka ya mtu mwenyewe pamoja na uwepo wa mianya ya kuiba.
 
Nawasilisha! 

2011/5/3 khadija moh'd <ded...@yahoo.com>



--
Stephen W. Msechu,
Program Officer,
Agenda Participation 2000
P. O. Box 55756,
Dar es Salaam, Tanzania.
+255 713 282263.


www.msechustephen.blogspot.com

"Happiness is belonging, not belongings."


ELLY KIMBWEREZA

unread,
May 5, 2011, 12:51:09 PM5/5/11
to regional-forum-for-rese...@googlegroups.com
Wapendwa Wanaharakati
Napenda nichangie hoja ya mishahara na masihara  ya baadhi  ya wabunge.Mimi ni mmoja wa wahanga wa hoja kama hiyo  mnamo mwaka 1978 nikiwa mwanafunzi  wa mwaka wa pili chuo kikuu Daresalam ambapo   nilifukuzwa chuoni baada ya kushiriki maandamano ya kupinga wabunge kuongezewa mishahara  wakati huo  hayati Mwalimu Nyerere  akiwa mkuu wa chuo  hicho.
Nakumbuka kama vile jana jinsi umma wa watanazania ulivyotangaziwa kwamba eti tulikuwa tunapinga mipango ya  kutupeleka wasomi vijjijini mara tutakapomaliza masomo.Enzi hizo za ujamaa- radio na magazeti machache yaliyokuwako yalikuwa vyombo vya  propaganda na hapakuwa  na nafasi ya  kuhoji hoji maamuzi  ya serikali.
Nakumbuka kikao hicho cha Bunge kilifanyikia  Pemba na kulikuweko picha  ya wabunge wakicheza kwenye  bembea.
Nakumbuka nchi ilikuwa imekumbwa na mlipoko wa kipindupindu karibu  kila sehemu lakini wabunge hawakuliona hilo  la  muhimu zaidi ya  kujadlili  wao kuongezewa mishahara.
Nafikiri Mwalimu Nyerere aligundua  baadae kwamba aliongopewa na wasaidizi wake na ndio baada ya miezi kadhaa alituondolea adhabu ile tukarudi kumalizia masomo yetu.
Nina hadithi ndefu ya kusimulia kwani nimetumia sehemu kubwa ya maisha yangu kule kijijini nilikopelekwa kama adhabu lakini sasa niko  huko kwa hiari yangu mwenyewe.
Nimeshiriki mambo mengi ya uongozi huko kijijini hata kuwahi kuwa Diwani.Hata Ubunge nilishawahi kuuomba  lakini moyo wangu umeteseka sana kwa yale niliyoyaona na kushuhudia nyakati za uchaguzi.Kweli kama yuko kiongozi anayejali maslahi ya watanzania wenzake kuliko yeye mwenyewe  hivi sasa basi huyo ni malaika katika mazingira yetu.
Kuna  unafiki  wa kutisha  wakati wa uchaguzi na kiburi kinacholetwa na ushindi hata unaopatikana kwa rushwa  tupu.
Kiburi hicho ndiyo nguvu ya wabunge kudai mishahara minono bila hata chembe  ya aibu.
Labda tujiulize swali kwamba hiyo serikali inayoambiwa ilipe hiyo mishahara unafikiri haioni kwamba kuna kulia na kusaga meno kwa watu wake.Kama inaona unafikiri kwanini inakubaliana na hoja hiyo.
Naweza kusema tu kwamba sisi waafrika ni watu wa  ajabu sana .Na ndani ya hayo maajabu ndiko jibu liliko.
Biashara ya utumwa haingepata nafasi kama  sio wenyewe kwa wenyewe kuuzana.Ukoloni hivyo hivyo.Na sasa katika uhuru wachache  wanapora raslimali za  taifa  na tunabaki kuchekeana.
Sina uhakika kama kuna mahali utumwa  na baadae ukoloni uliisha kwa hiari.Machukizo haya ya sasa hayawezi kuisha kwa hiari.Nafikiri tukae kwenye  meza ya mazungumzo ili yakishindikana tusije kujilaumu kwamba tuliruka njia za kistaarabu kulinda maslahi yetu wote.
Nawaombeni mtakaopata nafasi ya kusoma mchango wangu huu msome vitabu viwili ambavyo kwa mtazamo  wangu ni  muhimu  kwetu wakati huu. Vitabu hivyo ni 1. Viumbe Waliolaaniwa mtunzi Franz Fanon 2.Afrika  inakwenda Kombo mtunzi ni
Professa Rene  Dumont.
Nawatakia harakati njema
Kim
 
 
 


Date: Tue, 3 May 2011 09:55:22 -0700
From: ded...@yahoo.com
Subject: MJADALA JUU YA MISHAHARA YA WABUNGE
To: steve8...@gmail.com; regional-forum-for-rese...@googlegroups.com

stephen msechu

unread,
May 9, 2011, 3:55:36 AM5/9/11
to regional-forum-for-rese...@googlegroups.com
Mpendwa Elly,
 
Ndugu yangu na mzee wangu, Kimbwereza, tumefurahi sana kupokea mchango wako haswa kwa kuwa unaonesha uzoefu na kutoa historia ambayo wengi hatukuijua.
 
Kwa kweli mjadala huu wapaswa kuendelea na hata ikiwezekana kupata njia kuingia kwenye vyombo vya habari haswa magazeti.
 
Nawakaribisha wanaharakati wengine.

2011/5/5 ELLY KIMBWEREZA <tona_...@hotmail.com>

beda msimbe

unread,
May 9, 2011, 4:31:13 AM5/9/11
to regional-forum-for-rese...@googlegroups.com
Kwa muda kitambo kidogo nimekuwa nasita kuchangia hoja, nikawa kila kukicha nasoma halafu naguna tu naendelea na kusoma kinachofuata.
Lakini kuna kitu ambacho nilipenda tuamue kwa kuangalia si umaskinbi tulionao bali dhiki inayoambatana na kazi tuliyonayo.
Ama hakika watu hudhani kwamba wabunge wanalipwa fedha nyingi bila sababu. Huenda ni kweli kabisa lakini tuone maana halisi ya malipo kwa watu.
Mzigo wa kazi ya kutunga sheria, kupitia mapato, kuhoji na kupanga allocation ya mapato akipewa mwenye njaa kama beda msimbe kuna kijijambo kitazuka. Najipa mfano mwenyewe kwa kuwa sitaki kufarikiana na jamaa zangu.
Naam, mzigo mkubwa lazima uambatane na ulaji bomba ambao utawezesha kuihimili mikikimikiki ya mzigo huo.
Sitarajii hata kidogo kwamba hata kama umewajiri ndio umfanye afanyekazi kwa mateso na badala ya kufikiria kitu anafikiria namna ya kuratibu maisha yake.
Kiumbe mwenye mashaka hujazwa na shauku ya kudhulumu kimya kimya, si ajabu vijisenti kidogo vikabadilisha msimamo.
Mimi nasema mshahara unatosha hautoshi kwa wabunge kutokana na kazi waliyonayo. Suala la msingi ni kuuliza kama mshahara huo unathamani inayostahili? Je anawajibika?
Unapowania mkataba unaulizwa swali unataka nini katika mkataba au unatarajia nini? Kama kila mwananchi ataulizwa swali kwa mfumo wa demokrasia ya Kigiriki ya wanaume kumi na wawili inawezekana lakini kwa mfumo  wa Magharibi wa uwakilishi unatazama maslahi na sababu.
Nisiwachoshe kwani mimi katika falsafa ya maisha naamini kwamba  ujamaa ni upuuzi na kila mtu alipwe kutokana na mzigo mkubwa anaoubeba katika maslahi ya binadamu.
Msimbe beda


2011/5/3 khadija moh'd <ded...@yahoo.com>

Ndugu wanaharakati,



 
 
 
 




--
 It is my pleasure to work with you, please visit http//lukwangule.blogspot.com

stephen msechu

unread,
May 9, 2011, 4:52:57 AM5/9/11
to regional-forum-for-rese...@googlegroups.com
Ndugu wanaharakati,
 
Beda pia umenena, ila mimi nadhani tusisahau kuwa ujira unategemea kipato cha mwajiri wako na majukumu yake mengine sio kuangalia kazi unayoifanya tu.
 
Tanzania tunashindwa kujisimamia hata budget ya kuiendesha serikali (Recurrent budget) je, ni sahihi kulipa mishahara mikubwa?
 
Watoto na mama zao wanakufa kila siku kwa kutokuwepo vifaa bora vya kuzalishia, je ni sahihi kumkopesha mbunge fedha ya kununulia gari (Kila kipindi arudipo bungeni) wakati inaweza tumika kununulia vifaa vya kusaidia uzazi salama?
 
Wabunge wangefanya kazi vizuri usingesikia kelele hizi, unavyoona hivi ujue watu wanahoji uwajibikaji wao ambao unaonekana ni washaka!
 
Msechu.

2011/5/9 beda msimbe <msimb...@gmail.com>

beda msimbe

unread,
May 9, 2011, 5:08:05 AM5/9/11
to regional-forum-for-rese...@googlegroups.com
Msechu
ha ha ha ha
Nimetembea karibu robo tatu ya nchi hii, mbunge ni mtu ambaye hakika ana shida kubwa si katika mjengo tu bali hata huko porini wanakowakilisha watu wao.
Wao ndio ambulance, wao ndio watengeneza uhai, kijijini Mbunge ni mtu muhimu sana ni kama mtemi watu wanapokosa chakula wanaenda kw amtemi kutaka ghala zifunguliwe. Mbunge anaenda shule mbovu kabisa anatakiwa kutoa mchango ha ha ha yaani we acha tu.
Lakini ni kweli kuwa hatuwezi kulisha  mbwa vizuri na kutupa makoko kwa watoto wetu wayale tafauti ya msemo huu ni imo ndani ya kiwango cha tija wka taifa, kiwango cha uzalishaji. Kelele zote hizi zinatokana na uduni katika uzalishaji vinginevyo sioni  sababu ya kelele za mshahara naona kelele za wanawajibika kiasi gani?Suala la bajeti ni suala la wabana bajeti mimi simo, natazama maisha nayaangalia si kwa namna inayochanganya ila kw aupeo mpana zaidi kwanini mtu anataka fedha nyingi.Mila na utamaduni unaponza, maisha ya kujidekeza ni dhiki pia lakini kwa jinsi tunavyosonga mbele kuna uwezekano wa kuangalia maslahi kwa upana. Usishangae! lakini kila anayetawala ana haki ya kulipwa kutokana na thamani ya kazi yake ya kutawala na kila aokoae maisha ana haki ya kufanya na kulipwa namna hiyo hiyo lakini la msingi asiyefanyakazi na asile.
Msimbe

2011/5/9 stephen msechu <steve8...@gmail.com>
Reply all
Reply to author
Forward
0 new messages