KESI YA UPUNGUZWAJI WAFANYAKAZI WA NORTH MARA KATIKA TUME YA USULUHISHI NA UAMUZI MUSOMA.

5 views
Skip to first unread message

National Union Of Mine and Energy Workers of Tanzania

unread,
Oct 5, 2013, 10:02:24 AM10/5/13
to numet-media-release

Ndugu zangu wanachama wa NUME, wafanyakazi na wadau wenzetu.

Mtakumbuka kuwa NUMET Ilikuwa na majadilino ya muda mrefu na mwajiri katika kampuni ya dhahabu ya North Mara juu ya dhamira yake ya kupunguza wafanyakazi.

Kwa bahati mbaya katika majadiiano hayo hatukufikia muafaka, na hivyo tulikataa kwa mujibu wa sheria zoezi hilo kufanyika. Sababu kubwa ya kukataa ni kwasababu mwajiri hakuwa na sababu za msingi za kupunguza wafanyakazi, na pia taratibu zingine muhimu za kisheria alizikiuka.

Mwajiri alitufungulia kesi tarehe 25.09.2013 akiomba Tume ya Usuluhishi na Uamuzi, impe kibali cha kuendelea na zoezi la kupunguza wafanyakazi kwa vigezo vyake alivyoviweka

Tulipata wito wa kwenda mahakamani tarehe 30.09.2013, na tulipofika tulianisha mapungufu mbali mbali ya kisheria na kuitaka tume iifutilie mbali kesi hiyo.

Mwajiri aliomba aiondoe kwenye tume ili aweze kuileta tena upya, ombi lake lilikubaliwa. Na tarehe hiyo hiyo mwajiri alifungua kesi upya.

Tuliitwa jana tarehe 04.10.2013 (yaani siku 4 baada ya kesi kufunguliwa badala ya siku 14) kwenye tume (CMA) kwa ajili ya usuluhishi, na kwa bahati mbaya usuluhishi ulishindikana.

Kesi imeishapangiwa tarehe 23.10.2013 kwa ajili ya kuanza hatua ya kusikiizwa kati ngazi ya uamuzi (Arbitration).

naendelea kuwaomba wadau kutusaidia kwa hali na mali, hasa kwa wanasheria wanaoweza kujitolea katika hatua hii ya Arbitration tutawashukuru sana.

"AN INJURY TO ONE, IS AN INJURY TO ALL!"

SOLIDARITY FOREVER.


___________________________________________________________________________
Nicomedes M. Kajungu
General Secretary
National  Union of Mine &  Energy Workers of Tanzania (NUMET)
P.O.Box 7733
MWANZA.
+255782315688, +255767483271

_________________________________________________________________

Leila Sheikh

unread,
Oct 5, 2013, 11:04:58 AM10/5/13
to numet-med...@googlegroups.com
Kila la kheri.
Haki ya mtu haipotei.
 
Leila Sheikh

--
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "NUMET Media Release" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to numet-media-rel...@googlegroups.com.
To post to this group, send email to numet-med...@googlegroups.com.
Visit this group at http://groups.google.com/group/numet-media-release.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.


National Union Of Mine and Energy Workers of Tanzania

unread,
Oct 5, 2013, 11:25:29 AM10/5/13
to numet-media-release

Leila

Ahsante.



___________________________________________________________________________
Nicomedes M. Kajungu
General Secretary
National  Union of Mine &  Energy Workers of Tanzania (NUMET)
P.O.Box 7733
MWANZA.
+255782315688, +255767483271

_________________________________________________________________


2013/10/5 Leila Sheikh <calaba...@yahoo.com>
Reply all
Reply to author
Forward
0 new messages