Asante sana Comrade GS kwa salaam zako, Mungu akupe maisha marefu ili uendelee kuyaona matunda ya chama unachokitumikia kwa moyo wako wote na akili yako yote.
Ni furaha kuona wafanyakazi wa Migodi na Nishati sasa wana chama chao huru, kilichoanzishwa na wao wenyewe kwa manufaa yao wenyewe, vizazi vyao na taifa kwa ujumla.
NUMET ni alama ya ukombozi na uhakikisho kuwa sisi wafanyakazi wa Migodi na Nishati tunao uwezo wa kuunda chombo cha kutusaidia kuzisimamia haki zetu bila kujali vikwazo vilivyopo mbele yetu. Hii ni alama pia ya ushindi wa harakati zetu za kudai haki zetu na maslahi bora kazini mwetu.
Tumwombe Mungu atupe nguvu na hekima ya kuifanya NUMET kuwa chama kikubwa, sio hapa nchini mwetu peke yake bali Afrika nzima na Duniani. Tuzidi pia kumwomba Mungu na kufanya kazi sana ili NUMET liwe kimbilio la wanyonge mahali popote walipo.
Mungu atubariki sote ili tuweze kuuona mwaka mpya wa 2015 tukiwa na matumaini ya kusonga mbele zaidi ili kuyatimiza malengo yaliyopo mbele yetu na wafanyakazi wenzetu.
Shigela.
--
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "NUMET Media Release" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to numet-media-rel...@googlegroups.com.
To post to this group, send email to numet-med...@googlegroups.com.
Visit this group at http://groups.google.com/group/numet-media-release.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
Amina.
Field Marshal