RE:Story ya Punda

5 views
Skip to first unread message

noela njawa

unread,
Aug 5, 2013, 3:48:49 PM8/5/13
to mga...@googlegroups.com



Siku moja punda wa mkulima alianguka ndani ya kisima. Mnyama huyo alipiga kelele kinyonge kwa masaa kadhaa wakati mkulima akijaribu kufikiri nini cha kufanya.
 
Hatimaye, aliamua kwakuwa punda wake alikuwa mzee, na pia kisima hicho kilihitaji kufunikwa juu, Akaona hapakuwa na haja ya kumtoa.
 
Akaita majirani zake wote waje kumsaidia. Wao wote wakachukua makoleo na kuanza kuchota taka kwa koleo na kuzitupia ndani ya kisima.
 
Mara ya kwanza, punda aligundua nini kilikuwa kinatokea akapiga kelele kwa nguvu. Basi, ikawashanganza wale watu punda aliponyamaza ghafla!
Baada ya kutupa taka kadhaa kwenye hicho kisima. Huyo mkulima alishangazwa na kile alichokiona. Kwamba kila koleo la taka lililorushwa juu ya mgongo wa punda, punda alikuwa akifanya kitu cha kushangaza. Alikuwa akijitikisa ili taka zimwagike chini huku akipiga hatua moja kuja juu.

Kadri mkulima na majirani walivyoendelea kutupa uchafu kwa koleo juu ya punda yule, alizidi kutikisa mgongo wake na kupiga hatua moja kuja juu. Muda mfupi baadae, kila mtu alishangaa jinsi punda alivyozidi kutokeza ndani ya kisima na kuja juu.



FUNZO:
Maisha yatakutupia kila aina ya uchafu. Ili utoke nje ya kisima wahitaji kujitikisa na kuchukua hatua moja juu. Kila tatizo ulilonalo, ni jiwe la kukuwezesha kukanyaga na kupiga hatua kuja juu. Tunaweza kutoka nje ya kisima kirefu kwa kuongeza bidii ya kupiga hatua moja kuja juu bila kuacha na kutokata tamaa kamwe. Tikisa itikisa uchafu mbali na kuchukua hatua kuja juu.
Kumbuka kanuni 5 rahisi ili uwe na furaha:
1. Weka huru moyo wako mbali na chuki - Samehe.

2. Weka huru akili yako mbali na wasiwasi - Wengi hushindwa kabisa kipengele hiki.

3.Tosheka / rizika na ulichonacho.

4. Toa zaidi.

5. Tarajia vichache kutoka kwa watu lakini zaidi kutoka kwako mwenyewe.

Una uchaguzi wa aina mbili ...
i) Tabasamu na funga ujumbe huu,
ii) au tuma ujumbe huu kwa mtu mwingine ili ashiriki somo hili

Imetumwa na: Dr. Emeria A. Mugonzibwa - Mwanga.


(Nimeiona kwenye blog ya Lady Jay dee nikaipenda by Noela.)

Myanga Edwin Njawa

unread,
Aug 6, 2013, 10:59:19 PM8/6/13
to mga...@googlegroups.com
fUNDISHO


2013/8/5 noela njawa <noela...@yahoo.com>

--
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Mgaiwa" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to mgaiwa+un...@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
 
 

Saivoiye, Martha

unread,
Aug 7, 2013, 5:28:21 AM8/7/13
to mga...@googlegroups.com

Daaah uchafu kumbe dili!

 

Asante kaka Myanga!

 

Martha Saivoiye

Associate

Corporate Affairs & Communications

 

+255 22 216 6600

martha....@jti.com

                                                                                                                                                 

Tanzania Cigarette Company Ltd

A member of the JTI Group of Companies

20 Nyerere Road, P.O. Box 40114, Dar es Salaam

 

jti.com

Reply all
Reply to author
Forward
0 new messages