Ajira na Watahiniwa wa vyuo vikuu.

25 views
Skip to first unread message

albert kisima

unread,
Sep 6, 2010, 10:09:09 PM9/6/10
to lux...@googlegroups.com
Baadhi ya watu wanaongea kuhusu watahiniwa wa vyuo vikuu kujiajiri pindi wamalizapo mafunzo yao vyuoni. Kwa bahati mbaya, wengi wao wamekuwa wakilielezea tu wazo hili bila hata kueleza ni kwa namna gani kundi hili litaweza kujiajiri pamoja na kuwa swala hili la namna ya kujiajiri laweza kuwa ni la muhusika mwenyewe kutegemea na mtaji alio nao na ni kipi amekusudia kufanya. Kweli, wapo wanaofikiri kujiajiri ni kurahisi na pia wapo wanafikiri kuwa kujiajiri ni kugumu na hakuwezekani. Fikra zote hizi pengine zaweza kuja kutokana na mazingira aliyonayo mtu.

Wewe walionaje hili? Kujiajiri ni kugumu au ni kurahisi? Kwa nini wasema hivyo?

Mimi binafsi naona kujiajiri baada ya kumaliza chuo ni kurahisi na pia ni kugumu, yategemea na mazingira aliyonayo mtu.

Kujiajiri ni kugumu.
Kikubwa ni mtaji wa namna ya kuanza kutekeleza mradi ambao mtu amekusudia kuuanzisha. Kuna uwezekano wa kukopa Benki. Lakini ni wote walio maliza vyuo wanauwezo wa kuyakamilisha masharti? Nadhani swala la kujiajiri, ugumu wa kwanza huja kwenye namna ya kupata mtaji wa kuanzia. Vijana wengi wanaomaliza vyuo hutegemewa kuanza kuziinua familia zao kimahitaji n.k Hali hii kiukweli husabisha vijana kutafuta ajira kwa haraka kuliko kufikiri kujiajiri kwani kujiajiri kunakuwa tena ni kibarua kingine tena ambacho nacho kinahitaji mtaji mkubwa ambao uwekezaji wake utaweza kusaidia familia na jamii baada ya kipindi fulani kifupi. Ni jamii ya watu wachache sana hususani Tanzania, wenye nia na utayari kwa hiari yao kuwasaidi wale wanaotaka kujiajiri.

Kwa upande mwingine, kujiajiri kunaweza kuwa kurahisi pia. Wapo vijana wanaotoka katika familia zenye uwezo. Kikubwa hapo kwa kijana ni kuwasilisha wazo lake la kutaka kujiajiri na mchakato wa utekelezaji utaanza mara moja. Wapo walioweza kuzitumia fursa hizi ipasavyo na pia wapo walioshindwa. Washindwao kuzitumia fursa hizi kwa namna moja ama nyingine, ni lazima watakuwa na matatizo yao binafsi kuanzia ya malezi mpaka ya kuathiriwa kimtizamo na wenzao ya kuwa kujiajiri ni kugumu ilihali wameshindwa kuitumia fursa waliojaaliwa.

Nashauri kwamba, kuajiriwa kwa kijana aliyemaliza chuo kuwe ni msingi wa yeye kujiajiri na kisha yeye pia kuchukua jukumu la kuajiri wengine wanaotaka kuajiriwa, na tena waliojiriwa na wao watengeneze ajira nyingi. Kwa hiyo utaratibu uende hivyo. Kikubwa hapa ni kuwa, tusibweteke kwa kuajiriwa kwa kuona ndio mwisho. Tulioajiriwa tutumie kipato chetu kujiendeleza kimaendeleo na miongoni mwa maendeleo, mojawapo likiwa ni la kujiajiri na kisha kutegeneza ajira kwa wengine.

Nawasilisha.


Mdoti Com-kom

unread,
Sep 7, 2010, 12:33:41 AM9/7/10
to lux...@googlegroups.com
Hoja yako kaka ni ya msingi sana.

Kujiajiri umekuwa wimbo, wa kila siku na wa kila anayetaka kura, na katika majukwaa hiyo ndio sentesi rahisi ya kufupisha mjadala.
Nasikitika kuwa japo kwa kiasi fulani mazingira hayajaandaliwa kuwawezesha wenye lengo la kujiajiri kufikia lengo, lakini ipo haja ya vijana kuwa wabunifu, kuunganisha nguvu zao na kuibua miradi yao tunachoshindwa ni kuthubutu.

Naalika wale walio tayari kuunganisha nguvu tuwasiliane ili 2weze kuibua miradi ye2.

AMINA!

JOHN MKUMBWA

unread,
Sep 7, 2010, 10:18:58 AM9/7/10
to lux...@googlegroups.com
Nafurahi sana kukutana na mada kama hii jukwaani,
Mawazo yako ni  mazuri kaka Albert japo nami ninalo la kuongeza hapo tena la msingi sana,
Yatubidi kubadili mtazamo wetu, namna tunavyowaza kuhusu mafanikio yetu na namna ya kuyafikia hayo mafanikio..
katika kujiajiri kuna mambo mengi japo nisemee mawili,
1. Elimu ya ujassiriamali
2. Mtaji
wengi tumekuwa nafikra kuwa mtaji ndio kila kitu lakini si kweli hata kidogo.. kitu chamsingi hapa ni elimu ya ujasiriamali, ujue haswa unchotakka kukifanya na namna yakukifanya kwa ufasaha. Kitakachofuata ni mtaji na wapi upatikane..
Nimeshawahi kusema katika hili jukwaa kuhusu fursa ya kujiajiri(ujasiriamali ) lakini hakun mwanajukwaa aliyetaka kunisikia katika hili.
Natamani kila aliye mwanajukwaa afahamu kile nilichotaka kuwashirikisha ndugu zangu,
THERE IS AN OPPORTUNITY, LETS SHARE TOGETHER AND REACH SOMEWHERE
 
Nawasilisha
 

albert kisima

unread,
Sep 7, 2010, 10:59:26 PM9/7/10
to lux...@googlegroups.com
Kaka John Mkubwa, usichoke kuielimisha jamii. Wapo wengi tu wanaofaidi na mafundisho yako. Nadhani kuna haja ya kuwa na NASAHA ZA KAKA MKUMBWA KUHUSU KUJIAJIRI. Weka tips muhimu na watu tutalishika somo. Hata na yeyote awezaye kutoa elimu hii ya ujasiriamali, nae aje na nasaha zake tujifunze hapa kwenye forum yetu adhimu.

Kaka, umetaja elimu ya ujasiriamali na mtaji kama miongoni mwa nguzo muhimu.

Kuhusu mtaji, huoni pengine kijana atakuwa na haja ya kuajiriwa wakati mwingine ili aweze kupata mtaji. Nataja kuajiriwa kama miongoni mwa namna za kupata mtaji. Sijui walisemeaje hili.


Mdoti Com-kom

unread,
Sep 7, 2010, 11:58:00 PM9/7/10
to lux...@googlegroups.com
Kaka kisima umenena, ipo haja ya kuajiriwa kwanza hasa uki kubaliana na mimi kuwa kwa uzembe waliönao vijana wa vyuo vikuu wa ponda mali kufa kwaja, na kuto kuwa na malengo muafaka ni lazima wafuate utaratib u huo.

Lakini tena ile dhana ya mtaji kuwa fedha ndio unaovuruga dhana nzima ya kujiajiri. Je mtaji nh lazima uwe pesa? Je umeshapita bank ili kujua kuwa unakopesheka kwa mirad unayoibuni.
Buni, uwe nao katika writings.

Amina

Reply all
Reply to author
Forward
0 new messages