Ndugu wanajamvi.

7 views
Skip to first unread message

albert kisima

unread,
Dec 13, 2010, 1:48:42 AM12/13/10
to lux...@googlegroups.com
Baraza linakosa
msisimko kabisa.
Sijaelewa tatizo ni
nini.
Tuna kila haja ya
kuliendeleza jamvi
hili. Njia pekee ni
ya kuleta
mada
zitakazogusa hisia
za watu. Moja kwa
mtu aone kuwa
atakuwa na
deni asipotoa
mchango wake.
Kila mmoja wetu
atambue kuwa
anao wajibu wa
kulikuza jamvi hili.
Kila
kukicha hatuna
budi kuumiza
kichwa katika
harakati za
kutafuta cha
kushirikishana. Hii
iwe ni tabia yetu
wanajamvi, tuone
kuwa tuna
wajibika na jamvi
hili. Hebu tulifanye
liwe chanzo cha
maarifa.
Nimeamua
kuandika hivi
kwani, nimekuwa
nikipita hapa mara
kwa mara
kuangalia kama
kuna mada,
pongezi, shukrani,
matangazo (hapa
tungeweza
kuweka taarifa za
mahafali ya
wahitimu wa
Mwenge
2007-2010
mathalani)
na kadhalika na
kadhalika.
Pia, kwa wale
waliopo Mwenge
University,
wajaribu
kuwahamasisha
watu
wajiunge na jamvi
hili. Wahadhiri na
wanafunzi, wote
wanahusika.
Uwepo
wa wahadhiri
utatupa
changamoto zaidi.
Cha muhimu tu ni
kuwa, tusiache
jamvi likaa bila ya
chochote kiasi cha
kuwafanya watu
walione jamvi hili
kuwa halina
maana wala
msaada.

Mwisho, tuhamasishane katika ushiriki wa hali na mali, kuleta mada na hata uchangiaji wa mada husika.



Mohamedi Shabani Mtoi

unread,
Dec 14, 2010, 3:42:36 PM12/14/10
to lux...@googlegroups.com
Kaka umenena nilishawahi kusema kuwa malengo ya jukwaa hili si kupeana salamu na kujuzana kiwango cha mahaba kutoka kwa wake na wapenzi wetu tunahiaji kwenda mbali zaidi kuchangia maswala muhimu yenye tija na kumgusa kila mtu. Mimi nilipo ona ombwe hilo nikajiweka pembeni kuepusha mzozano usiokuwa na msingi kwa kuwa mtazamaji. Leo nimeshawishika kusoma mchango wako nikaona umegusa kule kule niliko wahi kukugusa.

Tunahitaji zaidi ya jukwaa la kujadili mambo ya msingi si salamu na pongezi kwa kutembeleana! nakumbuka niliwahi kuandika kuwa itafika hatua kila anayelala vizuri na mkewe au mpenzi wake atakuja andika hapa siku moja maana anaona jukwaa limekosa muelekeo! ukiingia mara leo nimeenda kwa X nikala ugali na nyama. Juzi nimetoka kwa Y ana mke na mtoto mzuri n.k haya kwa kweli nayasema kutoka skafu ya Moyo wangu kuwa hayajengi na sidhani kama ndio ilikuwa malengo ya jukwaa hili.

Asante Albert kwa kuliona hilo.

Naomba kuwasilisha.

Mtoi

2010/12/12 albert kisima <alber...@yahoo.com>

Mdoti Com-kom

unread,
Dec 16, 2010, 3:06:58 AM12/16/10
to lux...@googlegroups.com
Asante kwani kukosoa ni kutenda tofauti. Namshukuru sana Kisima kwa kujali na kusema kwani analinena analilipenda na amekuwa akitwanda hivyo. Asante sana ndugu Kisima. Labda kuna haja yakutenda zaidi kuliko kunena. Mimi nasikitishwa sana na watu wasiokuwa na hoja enye mashiko je watu waige lipi onesha linalotakiwa kuigwa. Ni kwali kuna haja ya kuamka na kuleta hoja zenye mashiko lakini kutoka sakafu ya moyo wangu sitaacha kuopingeza na naomba wengine watuambie yanayojiri.

Amina


From: Mohamedi Shabani Mtoi <moudd...@gmail.com>
To: lux...@googlegroups.com
Sent: Tue, December 14, 2010 11:42:36 PM
Subject: Re: Ndugu wanajamvi.

Mohamedi Shabani Mtoi

unread,
Dec 16, 2010, 2:40:20 PM12/16/10
to lux...@googlegroups.com
Wanajamvi.

Muugwana ni vitendo! Muungwana amelonga na ameliona jukwaa kutokuwa
active kwa mijadala na kuegemea upandea mwingine ulioonyesha kupoteza
muulekeo. Hili limekemewa wakati unaofaa kwa kuwa kuna changamoto
nyingi na mambo mengi ya msingi ya kujuzana. Na mambo binafsi yenye
harufu ya kadi za salamu kuyaonea kinyaa.

Inabidi wale wenye hoja zenye mashiko kama alivyosema msemaji hapo juu
waje kimashiko zaidi na mbolea ya kukuzia hoja hapa jukwaani maana
tayari ujumbe umeshafika na unahitaji kufanyiwa kazi ili kuondoka
kwenye uegemezi wa mambo binafsi kama wingi za salaam na kuanza
kujadili mambo yenye mashiko.

Kukiri kuwa kuna wenye hoja zisizo na mashiko ni hatua kubwa ya
ukomavu wa kupima hoja ya kila mtu hii inaonyesha jukwaa lina vichujo
vya kutosha kung'amua hoja nyepesi na nzito; Mfano anayetoa salamu na
anaye shauri kupunguza mfumo wa salamu na kujadili mambo ya msingi.
Hapa hapahitaji kuwa na shahada ya uzamivu kung'amua mwenye mashiko na
mwenye ukame wa fikra.

Kisima ametupa courage na kuturudisha kwenye mstari ameona kama
aliyemtangulia alivyoona! Nami nikupongeze HONGERA KISIMA KWA KUONA!
umetupa courage. kuna kakitabu niliwahi kukasoma kana msemo "No matter
how far the wrong way you have gone! Turn back! hata hapa jukwaani
"Hata kama tumeingia chaka kwa kiwango cha kukatisha tamaa! tutafute
uchochoro wa kutokea tusizidi kupotea" Hii ni courage laini lenye
ladha ya vitendo zaidi kuliko maneno yaliyozoeleka. na Courage is not
the absence of fear, but rather the judgement that something else is
more important than fear.

"Heri wale wenye hoja zenye mashiko maana wasio nazo wanachakujifunza
kutoka kwao"
Naomba kuwasilisha.

JOHN MKUMBWA

unread,
Dec 18, 2010, 9:15:05 AM12/18/10
to lux...@googlegroups.com
Nafurahi kulisikia hili likisemwa hapa, kwasababu ki ukweli kabisa
tumekuwa kimya na hata pale inapotokea hoja za msingi wanajukwaa
tumekuwa wavivu kujadili, ni kama vile mtu anazisoma na akimaliza
labda haoni ile sehemu iliyoandikwa - reply- au tumetekwa na facebook?
kwasababu katika facebook (kitabu cha uso ) watu wako active kuliko
kawaida, sijui tuna nini sisi vijana wa leo!!


--
John M. Mkumbwa.

Reply all
Reply to author
Forward
0 new messages