Ipi ingekuwa hatma ya Muungano wa Tanzanyika na Zanzibar?

5 views
Skip to first unread message

albert kisima

unread,
Nov 6, 2010, 5:43:54 PM11/6/10
to lux...@googlegroups.com
Hebu fikiria, kama Tanzania Bara Chadema wangeshinda Uraisi na Visiwani CCM. Unafikiri nini ingekuwa hatma ya Tanzania hususani Muungano? Nimewaza kuhusu hili, sijaona mwafaka wake lakini nimehisi laweza kuwa na laweza kuzidi kuwa agenda nzito sana katika chaguzi za uraisi, wabunge na madiwani katika chama tawala.
Pengine vita ya hali na mali lazima ipiganwe kila wakati wa uchaguzi mkuu kuhakikisha CCM inashinda bara na visiwani.
Nasema hivi kwani nahisi muhimili mkuwa wa Muungano, nionavyo mimi ni chama tawala cha CCM.
Ni katika kuwaza tu, "nini ingekuwa hatma ya Muungano endapo Tanzania Bara Chadema ingeshinda Uraisi na Visiwani CCM"



Mdoti Com-kom

unread,
Nov 7, 2010, 3:09:59 AM11/7/10
to lux...@googlegroups.com
Kisima unafikiri sana unapaswa kuwaza pia. Iwapo chadema ingeshinda bara ingeunda serikali ya muungano. Kama ilivyokuwa sasa ccm ilishinda bara, kura alzopata kiwete zanzibar ni chache ukilinganisha na upinzani hasa Lipumba. Muungano si tatizo kubwa kama ilivyo CCM

JOHN MKUMBWA

unread,
Nov 7, 2010, 3:51:09 AM11/7/10
to lux...@googlegroups.com
Umewaza jambo ambalo ni la msingi na ukijaribu kuliwaza zaidi kwa undani utagundua sababu hasaa ya Chama tawala CCM kutumia akili ujanja na nguvu zao zoote ikiwamo nguvu ya fedha katika kutetea nafasi ya uraisi kwani kumpa nchi mtu asiye mwana CCM ni kuuangamiza muumgano. Lakini tunakoelekea CCM itakaa kambi ya upinzani ipendeisipende..hata hapo Zanzibar kwa Maalim Seif ninayemfaham kama sio kuwa na uhakika wa umakam wa rais kisingeeleweka hata kidogo, eti aachwe kwa 1%!!!!!! then akubali!!! ila ni mawazo yangu tu haya. 

2010/11/7 albert kisima <alber...@yahoo.com>

albert kisima

unread,
Nov 7, 2010, 4:35:15 AM11/7/10
to lux...@googlegroups.com
Ndugu John, kwa mtizamo wangu, ulichosema ni sahihi. Chaguzi zilizopita Maalim Seif alikuwa akiachwa kwa tofauti kubwa tu ya kura, na alikuwa hakubaliani. Sasa hii tofauti ndogo hivi ambayo pengine kura zilizoharibika zingeweza kufidia pengine na kumpa ushindi lakini kakaa kimya. Hii inaonesha, jamaa ni mbinafsi, kuna maslahi yake kayaweka mbele. Anaenda kwa kuyasoma majira ya wakati tu.



albert kisima

unread,
Nov 7, 2010, 4:35:26 AM11/7/10
to lux...@googlegroups.com
Ndugu John, kwa mtizamo wangu, ulichosema ni sahihi. Chaguzi zilizopita Maalim Seif alikuwa akiachwa kwa tofauti kubwa tu ya kura, na alikuwa hakubaliani. Sasa hii tofauti ndogo hivi ambayo pengine kura zilizoharibika zingeweza kufidia pengine na kumpa ushindi lakini kakaa kimya. Hii inaonesha, jamaa ni mbinafsi, kuna maslahi yake kayaweka mbele. Anaenda kwa kuyasoma majira ya wakati tu.

JOHN MKUMBWA

unread,
Nov 8, 2010, 2:15:09 AM11/8/10
to lux...@googlegroups.com
Kumbe niliwaza sahihi, na tunakoelekea chama tawala kitawanunua kwa gharama yeyote ile wapinzani wallioko juu, namaanisha wanaoinyima usingizi CCM, kama Zanzibar tayari huku bara ndicho kinachofuata,
kama ulimkariri Mheshmiwa Dr. Kikwete (ndivyo anavyopenda kuitwa) katika hotuba yake ya kutangazwa na kuapishwa alisema mengi ila kubwa ni kuhakikisha CCM inapata ushindi mkubwa zaidi 2015 ! !.. Hapa inaonyesha haijalishi ahadi zitatekelezwa au la.. kinachotakiwa ni ushindi tuu.. Tutafika kwa staili hii?

2010/11/7 albert kisima <alber...@yahoo.com>

albert kisima

unread,
Nov 8, 2010, 3:35:32 AM11/8/10
to lux...@googlegroups.com
Kaka Mdot, nionavyo mimi Muungano upo na unaendelea kuwepo kwa sababu ya CCM. Kikatiba, serikali ya Muungano haikwepeki, lakini binafsi naona Muungano ungekuwa hatarini sana kuvunjika.
Nyerere na Abeid Karume, walikorofishana katika swala hili la Muungano, ilifikia mahali Karume akamwambia Nyerere, kuwa huu Muungano ni kama koti tu, likimbana anaachana nalo, ndio leo Muungano uwe chini ya vyama viwili tofauti vyenye itikadi tofauti?

John, kila mwaka wa uchaguzi tutakuwa tunailalamikia tume ya uchaguzi, na itaendelea kuwa mhimili wa CCM wa kuchakachua matokeo kama tume hiyo nayo haitarekebishwa kikatiba. Wapinzani wataendelea kuambiwa wajipange tena kwa uchaguzi unaofuata, na utaratibu utazidi kuwa huo huo.
Kama usemavyo ndugu John, chama tawala kilishasema kitasaka ushindi kwa hali na mali. Kutokutoa kipaumbele katika kurekebisha katiba, hususani kwa vifungu vya uchaguzi na tume yenyewe ya uchaguzi, yaweza kuwa ni miongoni mwa matayarisho yao makubwa kwa chaguzi zijazo na upinzani utazidi kuambiwa "ujipange kwa uchaguzi ujao". Tuangalie makali ya Bunge letu, yawezekana nyingi za ndivyo sivyo zikasimamiwa ipasavyo na kuuanza ukurasa mpya wa demokrasia kwa vitendo na si zama hizi za demokrasia kwa maneno.

Reply all
Reply to author
Forward
0 new messages