Re: Digest for luxmund@googlegroups.com - 3 Messages in 2 Topics

1 view
Skip to first unread message

emmanuel elias

unread,
Dec 29, 2010, 7:50:34 AM12/29/10
to lux...@googlegroups.com


2010/12/17 <luxmund...@googlegroups.com>

Group: http://groups.google.com/group/luxmund/topics

    albert kisima <alber...@yahoo.com> Dec 16 10:54PM -0800 ^
     
    Hii ni mada ambayo nilikutana nayo katika ukurasa wa facebook wa rafiki yangu mmoja.
     
    Yeye alidokeza kuwa, si sahihi kusema Tanzania Bara au Tanzania Visiwani kwani jina Tanzania tayari limeshajumuisha majina, Bara na Visiwani. Ulikuwa ni mtizamo wake na aliweka kigezo cha kukosolewa inapobidi, hivyo alihitaji uhalali wa alichokuwa anakiamini.
     
    Binafsi naona ni sahihi kusema Tanzania Bara ama Tanzania Visiwani, kwani kwa kutamka hivi, ni ufafanuzi tu. Yaani, kwa kusema hivi, sioni kama inaleta maana tofauti pindi mtu asemapo Tanzania upande wa Bara au Tanzania upande wa Visiwani.
     
    Wanakikundi, mwasemaje?

     

    Mohamedi Shabani Mtoi <moudd...@gmail.com> Dec 17 01:49AM -0800 ^
     
    Kisima.
    Unaposema Tanzania Bara moja kwa moja unagusa huku kwetu yaani
    Tanganyika kwa maneno megine. Na unaposema Tanzania Visiwani inagusa
    Zanzibar, Kimtazamo iko hivyo na kabal ya mabiliko ya Katiba ya Zenj
    ilikuwa hivyo lakini kwa sasa katiba ya Zenj inaitambua ZNZ kama nchi
    kamili iliyo na mipaka yake na mamlaka yake kamili.
     
    Hivyo kwa maneno mengine unaweza kusema ile dhana ya mtazamo wa Tz
    visiwani haipo tena kimebaki kiini macho. Nasema hivyo maana katiba ya
    sasa ya Muunganao haimtambui makamu wa kwanza na wa pili wa raisi wa
    ZNZ lakini pia wakati huo huo katiba mpya ya ZNZ haimtambui waziri
    mkuu wa Tanzania kwa maana ya Jamhuti ya muungano wa TZ.
     
    Tz visiwani ilishakufa kilicho baki ni dhana na hisia kuwa iko hai. Na
    ukiangalia kwa undani utaona jinsi Tanganyika inavyorudi taratibu
    taratibu maana kinachounganisha Uznzbari na Utanganyika ni katiba
    ambayo kwa sasa katiba zote mbili zina sigana ndio maana hata vuguvgu
    la kudai katiba mpya linachagizwa kila kona.
     
    Ili tuwe na Tanzania visiwani na Tanzania Bara yenye taswira ya kweli
    kwenye kioo kisicho na nyufa muungano unahitaji kufanyiwa marekebisho
    makubwa sana! Yaani kuweka mezani na kuongea upya juu ya mustakabali
    wa Jamhuri ya muungano wa TZ vinginevyo ingetokea CUF ikachukua dola
    ZNZ na CDM ikachukua Dola huku Bara naamini tungekuwa tunaongea
    mengine maana tayari nchi mbili hizi zingekuwa vipande vipande maana
    katiba zote mbili hazielezi nafasi ya vyama pinzani vinaposhika dola
    ZNZ na TZ Bara kuwa muungano unakuwa na sura gani. Pata mfano wa CUF
    na CDM bungeni kuhusu uongozi wa kambi ya upinzani.
     
    kwa sasa imebaki dhana, hisia, na maneno matupu ambayo unaweza kusema
    hayavunji mfupa. HATUNA TENA TZ VISIWANI WALA TZ BARA maneno hayo
    yamesha koma kwenye katiba mpya ya ZNZ isipokuwa yapo kwenye vinywa
    vya watawala na baadhi ya wananchi wanao amini kuwa ZNZ si nchi kamili
    yenye mamlaka yake kamili.
     
    Naomba kuwasilisha.
     
    Mtoi
    Neno la leo
    "Heri mpumbavu anayeficha uchi kuliko mwerevu anayetembea tupu wazi"
     

     

    Mohamedi Shabani Mtoi <moudd...@gmail.com> Dec 16 11:40AM -0800 ^
     
    Wanajamvi.
     
    Muugwana ni vitendo! Muungwana amelonga na ameliona jukwaa kutokuwa
    active kwa mijadala na kuegemea upandea mwingine ulioonyesha kupoteza
    muulekeo. Hili limekemewa wakati unaofaa kwa kuwa kuna changamoto
    nyingi na mambo mengi ya msingi ya kujuzana. Na mambo binafsi yenye
    harufu ya kadi za salamu kuyaonea kinyaa.
     
    Inabidi wale wenye hoja zenye mashiko kama alivyosema msemaji hapo juu
    waje kimashiko zaidi na mbolea ya kukuzia hoja hapa jukwaani maana
    tayari ujumbe umeshafika na unahitaji kufanyiwa kazi ili kuondoka
    kwenye uegemezi wa mambo binafsi kama wingi za salaam na kuanza
    kujadili mambo yenye mashiko.
     
    Kukiri kuwa kuna wenye hoja zisizo na mashiko ni hatua kubwa ya
    ukomavu wa kupima hoja ya kila mtu hii inaonyesha jukwaa lina vichujo
    vya kutosha kung'amua hoja nyepesi na nzito; Mfano anayetoa salamu na
    anaye shauri kupunguza mfumo wa salamu na kujadili mambo ya msingi.
    Hapa hapahitaji kuwa na shahada ya uzamivu kung'amua mwenye mashiko na
    mwenye ukame wa fikra.
     
    Kisima ametupa courage na kuturudisha kwenye mstari ameona kama
    aliyemtangulia alivyoona! Nami nikupongeze HONGERA KISIMA KWA KUONA!
    umetupa courage. kuna kakitabu niliwahi kukasoma kana msemo "No matter
    how far the wrong way you have gone! Turn back! hata hapa jukwaani
    "Hata kama tumeingia chaka kwa kiwango cha kukatisha tamaa! tutafute
    uchochoro wa kutokea tusizidi kupotea" Hii ni courage laini lenye
    ladha ya vitendo zaidi kuliko maneno yaliyozoeleka. na Courage is not
    the absence of fear, but rather the judgement that something else is
    more important than fear.
     
    "Heri wale wenye hoja zenye mashiko maana wasio nazo wanachakujifunza
    kutoka kwao"
    Naomba kuwasilisha.
     

     


Reply all
Reply to author
Forward
0 new messages