Ndugu wanajamvi

2 views
Skip to first unread message

emmanuel elias

unread,
Dec 29, 2010, 8:24:38 AM12/29/10
to lux...@googlegroups.com
        Binafsi, sioni umuhimu wa kubadili katiba  au kuifanyia marekebisho,  kabla ya
          kuwaelimisha wananchi kuhusu katiba iliyopo ili watambue mapungufu iwe
            rahis kwao  yaani wananchi kupendekeza marekebisho sahihi  ya hiyo
             katiba kwa manufaa ya watanzania wote.Ni vyema wahusika wahakikishe
              wananchi wanaisoma na kuielewa katiba hiyo iliyopo iwe rahisi kwao
              kufanya mapendekezo sahihi.
              
               Ahsanteh, nawasilisha.

Mdoti Com-kom

unread,
Dec 31, 2010, 5:41:45 AM12/31/10
to lux...@googlegroups.com
Asante Emanueli

Kwa mtazamo wangu utekelezwaji wa hili uliombal;o waweza kuchukua muda mrefu kuliko kawaida na inaweza kuwa ni baada ya miaka kumi. Nadhani kama uwazavyo swala la kuwaelimisha raia ni la msingi lakini si kuwaacha wao kugundua mapungufu.
Linaloweza kufanyika ni kuchumbua katiba kugundua matatizo yaliyoppo ndipo tuwaeleze wananchi mapungufu. natumai hii itakuwa njia rahisi. ipo haja pia ya kutumia wasomi wetu wa sheria, na katika hili minority rule inaweza kuchukua mkondo wake.

tahadhari wanasheria wanaonunulika kirahisi kama WEREMa wasipewe nafasi katika hili.

Amina


From: emmanuel elias <eliasem...@gmail.com>
To: lux...@googlegroups.com
Sent: Wed, December 29, 2010 4:24:38 PM
Subject: Ndugu wanajamvi

Albert Kissima

unread,
Dec 31, 2010, 10:30:37 AM12/31/10
to Lux.mund
Cha kuongeza tu ni kuwa tujaribu kuangalia wakenya walifanikiwa vipi
kuibadilisha katiba yao. Sikuufuatilia sana mchakato huu lakini kwa
ufupi, wakenya walitoa maoni yao na kisha kupiga kura katika
kuipitisha katiba mpya. Bila shaka tunalo la kujifunza hapa. Wakenya
waliwezaje kuchangia kwa kutoa maoni yao? Hii inadhihirisha kuwa
walikuwa wakiifahamu vyema, ama kwa wenyewe kuipitia na kubaini sehemu
zenye upungufu au baada ya ufafanuzi wa sehemu zinazotakiwa
marekebisho kwa kuwatumia wataalamu na kisha wakatoa maoni yao.
Reply all
Reply to author
Forward
0 new messages