Fw: [ludewa] Tumuulize Mbunge Wetu.

3 views
Skip to first unread message

Edgar Lugome

unread,
Dec 2, 2016, 6:47:54 AM12/2/16
to lud...@googlegroups.com



----- Forwarded Message -----
From: Domy Haule <domini...@gmail.com>
To: lud...@yahoogroups.com
Sent: Tuesday, October 2, 2012 6:28 PM
Subject: Re: [ludewa] Tumuulize Mbunge Wetu.

 
Bonna, Labda nichangie tu kwa kuwa sasahivi ninapita Lukuyusi nikielekea Ukenju kwa utalii wa ndani. Nimelipita jiwe moja kubwa mbele ya nkaranga, naambiwa na nahodha, eti juu ya jiwe lile kuna maandishi 'BORDER', Ninajiuliza sana, ni nini maana ya mwingereza kuandika neno hilo katika jiwe kubwa lililopo mita 200 hivi kutoka ufukweni?

Hayo tuyaache kwani mada za ziwa nyasa zimejadiliwa sana. Jambo la msingi ni wakati natoka ludewa nakwenda Lupingu, nimepishana na .'Excavator' mtambo ambao waswahili wengi hudhani unaitwa kijiko, ninamuuliza operator ananiambia jitihada za mbunge zimempatia kazi kupitia kampuni ya boimanda. Barabara ni pana sana kuweza pitisha kila aina ya gari hadi walipofikia. Lengo ni kupasua milima na kufikisha upana huo Lupingu. Asante sana Mh Deo.

Nimekuta mabadiliko pia ya uongozi, Kolimba ni Mwenyekiti mpya wa CCM Ludewa na Dada Mmoja Mjasiriamali, Anaitwa Eliza, nimepata jina lake moja tu, ni mjasiriamali pia, ni binti mdogo, yeye ataiwakilisha Ludewa NEC CCM Taifa. Hongera sana Binti, NEC Inamajukumu makubwa ikiwa ni pamoja na kutunga na kusimamia ILANI ya CCM, ambayo mwoshoni baada ya ushindi kichama, jina hubadilika na badala ya ilani, huwa Sera ambayo itaendelea hadi kuwa sheria na kutekelezeka, Ni jukumu kubwa sana na ni imani yangu wana Ludewa watawaunga mkono viongozi wote wapya wa CCM bila kujali itikadi bali utaifa.

Mengine nitayaandika baadae


Domy

2012/10/2 bonaventura ngalawa <chri...@yahoo.com>
 
Amani iwe kwenu.
 
Ni muda sasa tangu kusitishwa kwa vikao vya bunge ambalo mbunge wetu,Mh. Deo Filikunjombe ni muwakilishi wetu huko.
 
Kumekuwa na ukimya,pengine kuna yanayofanyika jimboni kwetu,lakini mimi sijui maana sipo Ludewa na wala sijafika huko muda mrefu kidogo.Naomba "update" mheshimiwa.
 
Mimi najua kimya kingi kina mshindo mkuu, ila hofu yangu ni kuwa ngoja ngoja nayo yaumiza matumbo,nakukumbusha tu kuwa,mimi nahitaji kujua KUTOKA KWAKO,tupo wapi,ZILE JITIHADA zimefikia wapi.
 
Nataka kujua ili kwa umoja wetu WAPENDA MANDELEO wa Ludewa tushiriki,kama ni kwenye kukosoa na iwe hivyo,na kama kwenye kupongezana basi tufanye vivyo ili kutiana moyo.
 
Kutujuza kutatuamsha na kukufanya nawe pia kuyakumbuka kwa urahisi na kukuepusha na KUJISAHAU katika yale yaliyo ya vipaumbele kwako,sikuzuii KUVUKA LENGO.Wewe tekeleza tu,hata na yale ambayo hayakuwa katika mipango yako,kasi ikiwa kubwa si lazima kuipunguza ili tu malengo yaende sambamba na wakati.
 
Si kwamba nakuunga mkono kwa JITIHADA ZAKO pekee,bali nataka hata kwa maneno matupu kuwa sehemu ya mabadiliko makubwa ya Ludewa ninayoyaona mbele yako.
 
Naomba pia nikukumbushe kuwa sitabakia kwenye kuunga mkono tu!bali nitakosoa nikiona waenda tofauti.
 
Naomba sasa Mheshimiwa unijuze/utujuze tumefikia wapi katika yote muhimu kwa Ludewa,na hapa sitaki kuorodhesha maana inawezekana nikayataja machache na kwako yakawa mengi.
 
Mimi nakuunga mkono,
Na wewe usiniangushe.
 
Ngalawa Bonaventura.



--
Dominick Francis Haule
Managing Director
Dokaman International Ltd
Part of
Sophist Tanzania College & Dokaman High School
P.O.BOX 2426,
Tel. +255 26 270 2688, CELL: +255-767 11 1173, +255 718 19 4606
IRINGA MUNICIPAL





__._,_.___
Reply via web post Reply to sender Reply to group Start a New Topic Messages in this topic (2)
Recent Activity:
.

__,_._,___


Reply all
Reply to author
Forward
0 new messages